Monday, October 25, 2021

ROHO YA KUCHELEWA ( THE SPIRIT OF DELAY) EP 1.

Bwana asifiwe mtu wa Mungu
Nipende kumshukuru Mungu kwa nafasi ya pekee ambayo ametupa tena kwa neema ambayo ni upendeleo wa Kimungu kwetu.
Leo tutajifunza neno la Mungu lenye kichwa cha somo ROHO YA KUCHELEWA ( SPIRIT OF DELAY).
Katika somo hili tutaona mambo kadhaa ambayo yamekuwa chanzo cha watu wengi kuchelewa kufikia hatima zao na bado wanachukulia kawaida bila kujali muda wa nyakati za kutimiza baadhi ya mambo katika wakati uliokusudiwa.
Note
Sio kila jambo linalochelewa ni mpango wa Mungu hapana ndivyo ilivyo hata kwa upande wa kuwahi kuwa sio kila jambo linalowahi ni mpango wa Mungu. 
➡️Mambo mengine yanachelewa kwa sababu za michezo anayoicheza shetani katika ulimwengu wa Roho bila watu wengi kujua na hivyo kuchukulia kawaida.
➡️ Mambo mengine pia yanawahi sio kwa mpango wa Mungu bali shetani anaweza kuwa amechungulia mbali na kuiona baraka yako iliyo kuu hivyo anapenyeza baraka feki kwa haraka ili kukupishanisha na Baraka ya Mungu.
Lakini hapa tutazungumzia somo lenye kichwa cha somo la Roho ya kuchelewa ( Spirit of delay).
Daniel 10:13-21
Habari ya Daniel aliyejulikana kama Belteshaza ambae majibu ya maombi yake yalishikiliwa na mkuu wa uajemi.
Hapa tunaona pamoja na Daniel kuomba na kufunga kwa majuma matatu lakini bado malaika aliyeagizwa na Mungu kuleta majibu ya Daniel alishikiliwa kwa kwa siku 21 sawa na majumaa matatu ya ambayo Daniel pia alitumia kumwomba Mungu wake.
Hapa nataka uone ni kwa kiasi gani shetani yupo kwa ajili ya kupambana kuhakikisha kwamba hupati kuwa sehemu unayopaswa kwa wakati sahihi uliokusudiwa na Mungu.
Tunayo mifano mingi ambayo imekuwa kama maisha ya kawaida kwa vijana wengi, mfano mtu anamaliza shule badala ya kutafuta kazi hata ndogo kutwa anatembea na vyeti kuomba kazi maofsini, anashindwa kutambua kwamba uzima, elimu na afya aliyo nayo ni mtaji namba moja kwenye maisha.
Mwaka 2016 wakati natoka chuo, nilikuwa na akili nyingi sana kwa sababu nilikubali kuanzia kwenye kiwango nilichokuwa nacho nikaanzisha biashara ndogo ndogo ya chakula mkoani kwangu singida na biashara ilikuwa inakwenda vyema sana na kipato changu ilifikia ikawa inaanzia laki tatu kwa mwezi na mtaji wa kwanza ilikuwa Tsh 30000 tu nilianza na miwa, miwa akaadimika nakaingia kwenye uji, chai na hatimae niliifikia hatua ya kuuza chakula cha mchana na ukuajia wake ulikuwa mkubwa sana.
Wakati naanza kufikiria kufungua mgahawa wakimataifa nikapata tangazo la kazi ambalo lilinifanya kuomba kazi kwa kweli kati ya makosa nimewahi kufanya nikuacha kazi zangu kwenda kwenye kazi ambayo nilifikiri ingenipa zaidi kumbe nilikuwa narudi hatua kadhaa nyuma.

Usiku wa juzi ndio Mungu alinipa mafunuo kwamba watu wengi wanachelewa kufikia malengo kwa sababu shetani amejiingiza katikati ya fikra za watu nakuanzisha mission ambayo imekuwa ni chanzo cha kuchelewesha baadhi ya mambo hasa kwa vijana.

Kijana unakuta anapambana kutafuta ajira na umri unakwenda mwisho wa siku alikuwa na maono makubwa anakuja kuishi kwenye robo ya maono yake kisa alishindwa kutambua kwamba mtaji wa kwanza sio fedha bali ile akili ambayo amepewa na Mungu inaweza kuwa mtaji mkubwa wa kumfanya kuishi kwenye maisha aliyokusudiwa kwenye wakati sahihi.

Wengine wameondolewa shauku ya kuoa, fedha anayo, maisha ambayo yanaweza kuendesha familia vyema anayo lakini, hataki kuoa anaona kama wakati bado kumbe ndani yake shetani ameishaingia maana anajua kwamba kijana huyu akipata mke atakuwa amejipatia kibali kwa Bwana, na maana ya kibali ni upendeleo mkuu kutoka kwa Mungu na kuwa kwenye ndoa mtu anaweza kufanya vizuri zaidi kuliko akiwa pekee yake.
Wengine wamepandikizwa roho yakujiona bado ni watoto hasa vijana wa kiume, na mabinti nao Roho ya kuchaguachagua katika ule wakati sahihi ambao mtu alipaswa kuolewa hapa shetani anacheza na ufahamu wa binti mwisho wa siku umri unakwenda anaamua kuolewa na yeyote atakae kuja ili mradi amepata mume kumbe mtu sahihi alishakuja lakini kwa sababu ya kufungwa ufahamu binti alijiona bado au yule kijana alimwona sio hadhi yake.
Shetani pia amekamata kwenye eneo la elimu, kila jambo huwa linapaswa kuwa ndani ya muda fulani ndio maana kuna umri wa kuanza shule ya msingi na kuna umri mtu anapswa kuwa amemaliza chuo kikuu lakini unaweza anafeli masomo bila sababu za msingi na anakosa ufahamu hata wakuendelea na hatua ya cheti anarudia tena kidato cha nne anafeli tena, anarudia umri unakwenda na mtu anachukulia kawaida kumbe shetani amejiweka kwenye nafasi ambayo ni ngumu kuelewa isipokuwa uwepo wa Roho mtakatifu ndani yake ambayo itamfunulia vizingiti vilivyowekwa na shetani.
Magonjwa na changamoto zingine, ni kweli mtu amepata kazi lakini shida na matatizo ni chungu nzma kila wakati wa mshahara ukifika unasikia shangazi anaumwa, mama anaumwa, au misiba hivyo kumalizia fedha yote kwenye kutatua changamoto za kifamilia badala ya kupiga hatua ya maendeleo yako, hivyo unakuwa unazunguzunguka tua hapo.
Ndugu zangu inatupasa kumkatibia sana Mungu ili kuweza kutambua vita vya kiroho ambazo shetani amekuwa akizipigana dhidi ya ndoto na maono ya vijana wengi.
Biblia inasema katika kitabu cha Yak 4:7-10
Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. 
Ukiishi karibu na Mungu ni rahisi sana kujua makusudi na malengo mabaya ya shetani hivyo ni rahisi kupigana vita hivyo maana unajua njia anazotumia shetani kuharibu au kukuchelewesha 
usikubali kupiga makitaimu sehemu moja kwa muda mrefu yawezekana sio wewe bali yupo adui amejipenyeza katika safari yakuelekea maono yako.
Na ili uweze kutambua haya yote ni vyema kuishi maisha yakumpendeza Mungu na shetani hawezi kupata mwanya wa kupenyeza roho zisizokuwa na ubora ambazo ni chanzo cha kukufanya kuishi maisha yasikusudiwa na Mungu.
Usifurahie na kuridhika na maisha yako ya kawaida jaribu kuishi maisha yenye kujitathmini kila wakati na kuishi kwenye maisha ya kuomba na kusoma neno la Mungu hapo ndipo utangudua kama unatembea kwenye njia sahihi au umehamishwa na ibilisi unasafiri kwenye njia isiyo yako.
Usione kawaida kutokuwa kwenye ndoa au kwenye mchakato wa kufunga ndoa waakati umri umefika na Mungu ameshakubariki una kazi nzuri na uwezo mzuri tu wa kuendesha maisha pamoja na mwenza wako.
Ukiona changamoto ni uchumi.au kikwazo fulani, ikatar hiyo hali kwa vitendo chukua hatua na Mungu atakuonekania kwenye hatua yako lakini usipoanza hatua fulani kila mwaka utaisha uko pale pale mambo hayaendi kumbe njiani shetani amekaa na wewe unaona kawaida.
Kushinda yote haya mwombe sana Mungu, mkaribie Mungu, mruhusu Roho mtakatifu aweke makao ndani yako ili kuweza kukupa maarifa ya kujua kila mtego na kuutegua. 
Somo hili litapatikana Youtube kuanzia wiki ijayo kwa njia ya video
Kuanzia ijumaa subscribe channeli ya ngu Ms Tv kwa maarifa ya kimungu na maisha ya kila siku
Moses Mgema
0755632375
0715366003
mgemamoses@gmail.com
God bless you so much





Friday, October 22, 2021

HUDUMA YA UIMBAJI NDANI YA KANISA

Mwalimu: Musa (Moses) Zephania Mgema
Ijumaa tarehe 22/10/2021
FPCT -Singida town centre church.
Uimbaji ni nini ?
Ni sanaa ambayo inatumika kuwasilisha ujumbe kwa njia ya lahani (chord) na mpangilio wa sauti wenye kutengeneza ladha yenye mvuto kusikiliza.
➡️Uimbaji asili yake ni mbinguni. Huduma hii ilianzia mbinguni na kiongozi wa huduma hii huko mbinguni alikuwa anaitwa lusifa kabla ya kuasi.
Ezekieli 28:13-15
➡️Huduma ya uimbaji ni moja kati ya huduma muhimu ndani ya kanisa kwa sababu imefanyika chumvi nzuri kwa ustawi wa kanisa na hata huduma nje ya kanisa.
Uimbaji katika mfumo wa injili kwa maana ya nyimbo za kiroho sio burudani bali ni huduma nyeti na ya msingi wala sio burudani au huduma ya ziada ndani ya kanisa.
➡️Huduma ya uimbaji ni huduma ambayo haina mwisho maana hata baada ya unyakuo kazi pekee tutakayoifanya huko mbinguni ni kuimba tu.
Ufunuo 5:9-10
Ufunuo 15:2-4
➡️Hapa duniani kazi ya uimbaji ilianza muda mrefu tangu enzi za agano la kale ni hii ni mara tu baada ya kuumbwa kwa Adamu na Hawa.
Mwanzo 4:21

KWA NINI HUDUMA YA UIMBAJI NDANI YA KANISA.
1petro 4:10-11
1Nyakati 6:31-32
1. Huduma ya uimbaji ikitumika vyema kwa kuongozwa na Roho mtakatifu, maombi na Neno la Mungu huleta mavuno mapya ndani ya kanisa.
2. Hufanya moyo wenye huzuni kupata furaha na Amani.
3. Hubadili moyo mgumu kuwa laini 
      1samweli 16:23
4. Mtu dhaifu hutiwa nguvu na uzima 
     1samweli 18:6-9
5. Hudhihilisha uwepo wa Mungu.
      2Nyakati 20:21-22
     2Falme 3:15-16
     Matendo 16:25-26
HUDUMA INAYOONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU, MAOMBI PAMOJA NA NENO LA MUNGU-
1.  Huonya na kufundisha kolosai 3:16
2.  Ni mahubiri kamili  Isaya 48:20
3.  Huleta faraja kwa waliokosa tumaini.
4. Humsifu na kumshukuru Mungu kwa matendo makuu 
Nb:
Zipo pia nyimbo za upuuzi kama ambavyo 
 Amosi 6:5 anaonyesha.
➡️Kama mtumishi wa Mungu unaetumika kwa njia ya uimbaji ni muhimu haya yafuatayo kuwa sehemu ya wimbo unaohudumia watu
1. Roho mtakatifu kuhusika
2. Neno la Mungu kujaa kwa wingi ndani ya mwimbaji.
3. Kufanya maandalizi kabla ya huduma kwa maana ya kuomba, kusoma neno na kuruhusu Roho mtakatifu kukuongoza ili kufanya huduma yenye connection ya mbingu na wewe kama mhdumu.
➡️Huduma ikiwa na uongozi wa Mungu lazima iwe ni ibada kamili ambayo itadhihilisha matendo makuu ya Mungu, mfano uponyaji, Faraja, nk.

➡️Tunaweza kujifunza kupitia wimbo alio imba Musa mtumishi wa Mungu na Israel baada ya kuwashinda wamisri.
 Ufunuo 15:3
➡️Ulikuwa wimbo wa matendo makuu ya Mungu
Aina nyingine ya nyimbo ni nyimbo ya mwanakondoo (Wimbo mpya) ambao unaelezea namna Yesu anavyostahili kuabudiwa, kupewa sifa kwa matendo makuu ambayo ametenda kupitia msalaba.
Zaburi 40:1-3
Ufunuo 14:1-3
Ufunuo 15:5-9
Wimbo ukitungwa kwa uongozi wa Mungu mwenyewe huwa ni wimbo wenye nguvu na huleta matokeo kusudiwa.
Ukiona waimbaji/mwimbaji anaimba na wala hakuna connection ya Kimungu, hiyo ni ibada ya sanamu ambayo imebeba kujiburudisha nafsi na ni makelele mbele za Mungu.
➡️Mwimbaji lazima ajawe na Roho mtakatifu kwa wingi ndani yake, Neno la Mungu na awe mtu ambae anaiombea huduma yake kwa kujitoa ili kuwa na huduma bora na yenye nguvu za Mungu.
➡️Ipo mifano ya huduma za uimbaji katika agano jipya na agano la kale ambavyo Mungu alohudumia watu kupitia waimbaji 
Luka 1:41&67
Efeso 5:18-20.
Kwa ufupi uimbaji ni kazi ya Roho mt. nje ya Roho mt.  uimbaji unabaki kuwa burudani tu, maana ni ngumu sana kuyaona matendo ya Mungu yakidhihilika.
➡️Uimbaji ukiwa na uongozi wa Mungu hiki tegemea kukiona kwa ukubwa katika huduma yalo ya uimbaji  2Nyakati 5:13-15
Neno la Mungu ni huduma kamili ya uimbaji hivyo kwa sababu neno ni chanzo cha ujumbe na mafunuo mengine ya kimungu lazima mwimbaji awe amejaa neno ndani yake, hii husaidia kuwa na huduma yenye matokeo.
Zaburi 45:1
Wakolosai 3:16
Mwisho.
Msingi wa huduma yeyote ya kimungu lazima iongozwe na 1. Neno la Mungu
                       2. Roho mtakatifu
                       3. Maombi na utii wa Mungu.
Ukiwa na hivi vyote lazima uwe na huduma ya nguvu za Mungu ndani yake
Mungu akubariki sana kwa kunisikiliza
0715366003 whatsup
0755632375 call and sms
mgemamoses@gmail.com




Thursday, September 23, 2021

UJASIRI NDANI YA YESU

Bwana Yesu asifiwe!

Waebrania 10:35 anasema,,"Basi msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kuu"

Ukisoma mstari huu ndani yake kuna kitu cha thamani na cha ajabu sana kinaitwa "UJASIRI" na huo ujasiri unaweza ukautunza au ukautupa ,"MSIUTUPE" maana yake unaweza kuwa nao na ukautupa.
Ndani ya "UJASIRI" kumebebwa kitu kinaitwa "THAWABU " 
Ukisoma katika kiingereza anasema hivi,,,,"Therefore do not throw away your confidence, which has a great reward."
Kiswahili anasema hivi,," Kwa hiyo, msipoteze ujasiri wenu, maana utawapatia thawabu kubwa" Sasa ukiunganisha na neno la 
Efeso 6:10 anasema "Hatimaye mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake" Utaona neno hili "HODARI" limetumika katika Waebrania 10:35 kama "UJASIRI" ambao ndani yake tunapewa "Thawabu KUBWA".

NINI MAANA YA UJASIRI/UHODARI.
UJASIRI-Maana yake ni uwezo alionao mtu wa kujiamini mbele za Mungu juu ya maisha yake yasiyo hukumiwa na dhambi moyoni mwake.

 1 Yohana 3:21 anasema hivi,,"Wapenzi, miiyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu"
Sasa jiulize swali hili pamoja na mimi, Ni nini kina hukumu moyoni? 
KUHUKUMIWA MOYONI"...kuna letwa na "DHAMBI" iliyo moyoni ambayo inapoteza UHODARI/UJASIRI wa mtu mbele za Mungu.

 Kama umepoteza "UJASIRI" ndani yako maana yake "UMETUPA UJASIRI" wako kwa kuruhusu dhambi iingie kwako, na madhara yake thawabu  unaipoteza ukiwa hapa hapa duniani.

Kama umepata "UJASIRI" wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu, maana yake umefutiwa dhambi, na moyoni mwako umepewa

 "UZIMA WA MILELE" Sasa unaporuhusu dhambi unapoteza "UZIMA WA MILELE" uliyo ndani, na maandiko yanasema MNA UZIMA WA MILELE NINYI MNAOLIAMINI JINA LA MWANA WA MUNGU" (1 Yohana 5:13)

SABABU ZA KUTUNZA UJASIRI.
Ni kutufikisha katika Tumaini ambalo Bwana ametuandalia watoto wake .
Waesfeso 3:12 "Katika yeye tuna ujasiri na uwezo wa kukaribia tumaini kwa njia ya kumwamini"
Huwezi kulikaribia "TUMAINI" uliloliweka ndani ya Kristo kama huna "UJASIRI NA UWEZO" unaokupa wewe kutarajia unachokitarajia katika Kristo.

Hakikisha haupotezi "UJASIRI" wako usije ukashindwa kukaribia tumaini lako uliloliweka kwa Yesu. Maana ujasiri na uwezo ndivyo vinakutengezea mazingira ya kukutana jibu lako/yetu. Ujasiri na uwezo unavipata ukiwa ndani ya Yesu.
UJASIRI UNARUHUSU KUPEWA NEEMA NA KIBALI MBELE ZA MUNGU 
.
Waebrania 4:16 "Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji"
Katika maneno hayo kuna..."KITI CHA NEEMA" na kuna....KUPEWA REHEMA..na pia kuna...KUPATA NEEMA. Kazi moja wapo ya kiti cha Neema ni sisi "TUPEWE REHEMA" kiingireza anasema,,, "GIVEN MERCY" Mercy inamaana ya "HURUMA"
Kwa maana hiyo kiti cha NEEMA kinatoa "HURUMA NA NEEMA" vinavyomsaidia mtu mwenye ujasiri ndani yake kutumia "NEEMA INAYOTOA MSAADA Msabato Neema hutoka kwa Mungu na Kwan njia y'all Neema tunapata kibali mbele Zach Mungu "
Kwa hiyo wakati wowote mahali popote anapohitaji msaada kutoka Kwa Mungu  night Neema yake Pelee ndio sababu yakupokea majawabu na mahitaji yako/yangu, maana kwa njia ya kristo tumepewa neema ya kupokea chochote tuombacho.

Maandiko yanasema hivi,,"Wapenzi, miiyo yetu isipotuhukumu tunaujasiri kwa Mungu, na lolote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa tumezishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake" (1 Yohana 3:21-22)

Ukiomba na hauna ujasiri ndani yako huwezi kupokea unachokiomba, kwa sababu "NEEMA" ya kukusaidia haipo
 kwa nini haipo?
Kwa sababu huna uwezo wa kusimama mbele za Bwana, maana dhambi hukosesha ujasiri na kibali cha kwenda mbele za Mungu, maana hukumu husimama mbele ya mwenye dhambi na kumwondolea ujasiri.

"TWAJUA YA KUWA MUNGU HAWASIKII WENYE DHAMBI; BALI MTU AKIWA MCHA MUNGU, NA KUYAFANYA MAPENZI YAKE HUMSIKIA HUYO" (Yohana 9:31)
Hili neno tumejifunza leo Kama msingi wa maombi yetu kwa sababu sisi tumepata Neema ya kristo ambayo imetuokoa na hatuko na dhambi inayohukumu mioyo yetu maana Bwana amekwisha kutusamehe na huo ndio ujasiri tulio nao unatufanya kwenda mbele zake kupeleka mahitaji yetu.
Kwa uhakika huo tunaamini kila tukipelekacho kwa Mungu naamini tutapokea sawasawa na mapenzi take. 
Amen
Prepared by Moses 
Moses z Mgema 
0715366003
24/09/2021

Sunday, April 18, 2021

Nimekuwa ni mtu mwenye ndoto na maono makubwa tangu nilipokuwa mtoto mwenye rika lakujitambua, shauku yangu nikuona kuwa nafikia mambo fulani kwenye maisha yangu duniani.
Pamoja na changamoto nyingi ambazo zinaweza kuwa zinajitokeza kwenye safari yakufikia maońo, uvivu wakati mwingine, kuchukulia kawaida, kuchoka, kutokufikia malengo kusudiwa ndani ya muda fulani bado naamini kwamba, hakuna njia nyepesi inayoweza kukupeleka kwenye mafanikio na malengo yenye kutimiza maono yako/yangu.
Maono ni picha kubwa na nzito sana, haibebwi na watu legevu, inahitaji watu shupavu, makini, wenye mtazamo mpana na uwezo wa kuona pasina kutumia upeo halisi wa macho yakawaida bali upeo wa macho ya ndani ya akili na fikra.

Friday, March 5, 2021

NIMEGUNDUA KUWA KILA MTU ANAUCHAGUZI WA MAISHA ANAYOYATAKA...NEVER GIVE UP MPANAJI

Nimejifunza kanuni moja ya maisha ambayo, kama mtu anaye kusimulia alishafanikiwa na anakueleza wewe mtu ambae bado hujafikia ndoto na malengo yako kwenye maisha,ni ngumu sana kuelewa au kumwelewa mtu huyo, kwa sababu wakati mwingine, unaweza kuhisi anasema hivyo kwa sababu ana mali tayari.
▶️Ukweli ni kwamba kuna kuamua ni aina gani ya maisha ungependa kuishi na ukayaishi, kupenda kuishi maisha fulani ni tofauti na kutamani kuishi aina fulani ya maisha. Watu wote duniani tunatamani kuishi mazuri, ila katikati ya kutamani kuishi mazuri wengi wetu hatupendi kuishi maisha  mazuri.
▶️Wengi wetu tunaongozwa na shauku na matamanio ila hatupendi maisha hayo, mwisho wa siku wengi wetu hatuyaishi matamanio yetu kwa sababu uvivu na kutokujituma ndiyo maisha ya watu wengi duniani tumeyachagua. Mtu yuko tayari kufanya kazi ya bei ya ajabu kïsa inampa pumziko la siku nzima, hatoki jasho, mtu yupo tayari kupokea dola tatu kwa siku hata kama anauwezo wakupiga hatua nakufanya kazi ambazo zinaonekana hazina hadhi lakini angalau zinakipato kizuri kuliko cha kivulini.
▶️Uvivu na kutokujituma kazini au katika kutimiza majukumu yetu sawasawa, inadhihirisha ni kwa kiwango gani tunapenda maisha duni na ya ufukara, ukipenda maisha mazuri utajituma na kufanya kazi kwa bïdii, kufanya kazi kwa bidii ni ishara ya kuyachukia maisha duni na umasikini ambayo ndiyo yamekithiri miongoni mwa vijana wengi hasa wakitanzania.
▶️Tumekaa kulalamika, kulaumu na kuwatwisha wengine lawama kama vyanzo vya maisha yetu kuwa yalivyo leo, umasikini wetu uko kwenye nguvu ya kuongea, na utajiri wetu uko kwenye nguvu yakufanya maamzi na kufanya utekelezaji wa vitendo. Kusema, kuongea na kuzungumza kwa wenye akili ni vyanzo vya fedha, ajira, biashara na utajiri, kwa mpumbavu ni dambo la lawama, majivuno, umbea, masengenyo na maneno bila utekelezaji wa vitendo, ni wazuri wa kunogesha mazungumzo na wavivu wakutekeleza yale wanayoyazungumza.
▶️Hatua za mwenye bidii huleta mavuno, hatua za mtu wa mipango ni utekelezaji na mipango humwonyesha utekelezaji na uwezekano wa kisichowezekana katika mitazamo ya wengi. Ukipenda kufanya kazi za kawaida jifunze kuwa mbunifu kwa sababu katika ule uzoelefu ukitiwa nakshi huja na matokeo chanya sana.
▶️Mtu tajiri akiandika ukweli mchungu, fukara na masikini huyachukulia maneno hayo kama matusi, dhihaka, majivuno, kiburi na dharau kwa wasio nacho, huu ni mtazamo wa watu masikini na fukara wa kuanzia ufahamu, kiroho na kimwili pia, bali maneno yenye kuchoma na kuumiza kwa sababu yanaweka wazi udhaifu na unalengo la kuponya, hujenga mtazamo chanya, na kuleta mapinduzi ya fikra ambayo pia huamsha hasira ya kupambana ili kuondokana na hali duni aliyo nayo mtu husika na huchukua hatua pia yakuanza.
▶️Nilichojifunza ni kwamba duniani hakuna fungu la kupata wala fungu la kukosa, bali aina ya maisha ninayoyataka yako ndani ya uwezo wangu wa kimtazamo, naona nini, natenda nini, nalenga wapi, nachukua hatua gani ni kwa kiwango gani nayachukia maisha duni kwa kiwango gani napenda maisha ya raha mstarehe.
▶️Aina ya maisha ninayotaka inaanzia kwenye fikra zangu, taarifa, maarifa ya aina gani napenda kuyatumia, aina ya watu nachangamana nao, marafiki pamoja na mazungumzo yao, uchaguzi wa mpenzi wa maisha, mumeo/mkeo, mpenzi/mchumba ni wa aina gani, Je ni mshikaji wako, rafiki yako, business/mfanyakazi mwenzako ambae una uhuru wakushikishana nae kwenye mipango na malengo ya familia yenu au mpo kutimiza majukumu ya ndoa yakiisha unarudi kwenye Ios au Adroid ya samsung na Tecno yako
▶️Kwa nini huyu ni rafiki yako au kwa nini cycle ya watu watu wako ni wainga fulani, unapata nini kupitia wao, mademu, umbea, utani kupindukia au mawazo gani, mazungumzo yenu hata kama hamjatoboa yakoje, umbea, starehe, mpira mchna kutwa,, kwenda kuchoma muda wote, ni aina gani ya watu umekubali wawe kampani yako.....
▶️Aina ya watu, marafiki, namna unavyowaza, mitazamo, aina ya mchumba au mke uliye nae ndiyo uhalisia wako wewe, na ndiyo picha yako wewe hasa ile ya ndani. Maisha ya mtu ni matokeo ya kile kilicho ndani ya mtu husika....
▶️Ni maneno mazito kiasi fulani, lakini ni elimu ambayo  inamgusa kila mtu, mama, Baba, kaka dada na mimi mwenyewe. Kiufupi maisha yako ndani ya uwezo wangu/wako, ukiamua kuishi high class, middle class au lower class au lowest class. chambua aina ya watu wakutembea nao, badili fikra zako, kubali kuanza upya katika fikra zak
▶️Sijaoa, sijawa na maisha ninayotaka, yawezekana pia kampanh imara sana, ila aina watu wangu wa muhimu wanajulikana, mke wangu ni sio tu atakuja kuwa mke bali hata yeye anajua kuwa mimi ndiyo rafiki yake namba moja, mshikaji wangu.
Vijana tupambane, tujitathimini, tuache uvivu tufanye kazi kwa bidii, tusichague kazi, matatizo yako yasiwe sababu ya kuyatumia kama mtaji hapana, ziugeuze changamoto na shida zako kuwa mtaji, badiliko la fikra na mawazo yako kuwa furaha yako, fanya kazi kwa bidii, panga kuwa tajiri, chukia umasikini, penda utajiri.

Pambana hata kama huoni, giza limetanda kila mahali, usikate tamaa, alfajiri iko karibu sana, mapambazuko yamekaribia na jogoo anawika jua ng'ambo imefika. Katika yote hayo Mungu ni wa kwanza.
Mgema moses 
Singida Tanzania

Thursday, February 11, 2021

NI KWA SABABU YA KILICHO KWENYE WALETI NA POCHI YAKO TU WALA SIO KINGINE

Wakati unafanya vizuri utakuwa mzuri na mwenye heshima kubwa sana mbele za watu. Ukiwa na fedha, kipaji ambacho kinakupa matokeo chanya na kuwagusa watu wengi kwenye jamii, ukiwa tajiri, kiongozi  kama mbunge na hadhi zingine kwenye jamii hasa jamii za kiafrika, utaitwa kila aina ya majina mazuri, tajiri, mweshiwa, kiongozi, doni, kaka, mkubwa, mzee hata kama una umri wa miaka chini ya kumi ila kwa sababu wanachokiita majina yote mazuri hata wewe unaheshimika.

Sio ajabu Tanzania mgonjwa kunyimwa hela ya matibabu na baadae watu kutoa mamilioni ya shilingi wakati umefumba kinywa na huzungumzi tena, jeza la kifahari, kaburi na chakula cha haja na sifa kedekede.

Ni rahisi mtoto kukosa ada ya shule baada ya kuvuja jasho na damu akitafuta ada ya shule tena ada ya shule za serikali kwa majirani, ndugu na jamaa akakosa kwa kunyimwa huku watu wakija na sababu kedekede za unajua mwanangu sina hata hela nimepeleka shamba, mama yangu ambae ni bibi yako alikuwa anaumwa na pole nyingi ningekuwa nayo ningekupa hela wakati huo asilimia kubwa wakijigeuza kuwa mamotivational na mainspirational speakers kukuita jiniazi na unatakiwa kupambana ili kufikia ndoto yako. Muda mfupi ukiondoka watu walewale ambao walikosa ada ya shule za serikali unakuta wanachangia malaki ya pesa kwenye harusi ya mshikaji wao au kwenda kuweka heshima bar na washikaji huku wakipeana stori, na stori zenyewe ni za yule yatima aliyepita mchana kuomba msaada kwa ajili ya ada na mahitaji ya shule ili kupigania ndoto zake.

Ni somo gumu sana lakini kuwa makini na watu wa nchi hii au ulimwengu huu, usipende kusifiwa na kuvimba kichwa kwa kuitwa majina yenye hadhi ukaona umefika, kumbuka kuna watu wanakuita majina mazuri huku wakiitazama waletï na pochi yako, uishimiwa wako ni kwa sababu ya dolla, misimbazi na pounds unazomiliki, heshima unayopewa si ya kwako ni kile ulicho nacho basï.

Hadhï yako ni kwa sababu ya kile ulichonacho kuanzia kwenye nyumba ya Baba yako maiti haitazikwa mpaka ufike hata kama uko ulaya na corona imefunga mipaka ya nchi unahitaji kuunga unga ili ufike kwenu mwandugembe ulipo msiba tena wa mtoto mdogo kabisa, ukoo utakutambua, kijiji mpaka tarafa watakuita majina ya heshima na hadhi na wewe utavimba kichwa, kwenye baadhi ya nyumba za ibada hata kama unatenda dhambi ambayo wengine wakifanya wanapigwa na fagio la chuma, wewe watachekacheka nakutengeneza mazingira ambayo kosa lako litaonekana la kawaida na vifungu vya Biblia vitatumika kukulinda na kukutetea USIHUKUMU USIJE ''UKAHUKUMIWA, YULE ANAE JIONA MWEMA AWE WA KWANZA KUMSIMAMISHA HUYU NK.''Sio wewe ni fedha, mali na utajiri wako.

Jitahidi kufanya mambo ya msingi, fanya ambayo unapaswa kufanya, usifanye jambo kwa sababu unafikiri una kundi kubwa la watu nyuma yako wanakupenda na kukuelewa hapana, wengi wao ni wasengenyaji na watoa taarifa zako pindi utakapojikwaa na utajiri ukaisha, pale kipaji chako hakitawagombanisha watu wanaojiita watu wa connection, mawakala na watu wa menejimenti muda huo watakuwa wametimua mbio.

Fanya kila unalolifanya huku ukikumbuka kuwa yule kijana mdogo aliyekosa ada kipindi kile nakazunguka mtaani, kwa ndugu kwa rafiki wa marehemu mama au Baba wakasema hawana hela na kuambulia kumpa pole, leo wanamwita mweshiwa baada ya yeye kuvuja jasho bila msaada leo wamegeuka nakuwa washuhudiaji na wenye kujigamba wakisema huyu amekuwa tunamwona, tumemsaidia sana Baba yake alipofariki sisi ndiyo tuĺisimamia masomo yake mpaka leo ni daktari.

Unapokuwa na mali wewe ni mtamu na unastahili kila jina zuri hakika, ila kumbuka wanaokusema vyema mchana katika giza wanakuita mpumbavu huna akili kazi kutumia mali na pesa vibaya, wengine hata hawajawahi kukushauri lakini wakiwa vijiweni kutwa kusema huyu jamaa hashauriki, tunamshauri sana lakini wapi kumbe masikini ya Mungu hata kukushauri hawajawahi kukuambia ukweli, kuwa makini ndugu yangu.....
Usirubunike na maneno matamu ya walimwengu, jenga msingi bora wa maisha yako, usikubali kurubuniwa kwa maneno mazuri ya watu kwa sababu ya utajiri wako, fanya jambo muhimu kwa wakati sahihi, usipende kuifurahisha kila nafsi ya mtu bali ishi wewe kwa utaratibu wako.
Mungu akupe kujua watu wakweli mbele yako na waongo ili kuyaweka maisha yako salama kesho.
Mgema Moses
0715366003/0755632375

Sunday, February 7, 2021

Tengeneza mahusiano mazuri na watu kwa kadri uwezavyo bila kujali hadhi yao, uwezo, kazi na mazingira yao. 
Kwenye maisha yatu kila mtu ana mchango wa moja kwa moja au si wa moja kwa moja sana ila pia anaweza kuwa sehemu ya wewe kutimiza malengo, kukuepusha na hatari fulani au kukupa dili fuĺani.
Nakumbuka siku moja ndugu mmoja ambae tulikuwa tukiishi mtaa mmoja yeye akifanya kazi ya bodaboda, hatukuwa tumezoeana ila nilikuwa namsalimia kila nikipita, kumbe yeye alikuwa anafahamu kuwa angalau nimepiga hatua katika masuala ya elimu, hakujua exactly nimefanya taaluma ipi ila alikuwa anajua nimesogea mbele 

Friday, February 5, 2021

AINA YA MAAMZI NA UTULIVU HUPIMA KIWANGO CHA HEKIMA NA UKOMAVU WAKO.

Ukomavu wa mtu haupimwi kwa wingi wa miaka, wingi wa nywele nyeupe kichwani, wingi wa vizazi kutoka kwenye viuno ama tumbo lako hapana.
Ukomavu wa mtu mara nyingi unapimwa kutokana na uwezo wa kukabiliana na nyakati ngumu, nyakati tata na milima mîgumu ambayo unakutana nayo na vile unakabiliana nayo katika hali ya utatuzi na kuweka sawa bila kulazimishwa na mazingira presha na mazingira ya uhitaji wa jamii inayokuzunguka.
Kuna nyakati tata na ngumu sana kwenye maisha yetu ambazo huwa tunapitia, wakati mwingine zinaumiza, zinatuchafua, zinakatisha tamaa, zinatukumbusha nyakati ngumu ambazo hazijawahi kuwa rafiki bali maumivu makali ambayo hata huwa hatupendi kuzikumbuka kabisa.
Wakati mwingine unapewa nafasi yakuwa mtoa maamzi ambayo haki inapaswa kutendeka bila kujali asie na haki ataumia kwa kiwango gani. Ukomavu wako pekee ndiyo inahitajika, hekima na busara yako ndio inahitajika sio kitu kingine.
Nayakumbuka mazingira ya Mfalme Sulemani ambae alipaswa kufanya maamzi ya haki dhidi ya wamama wawili ambao walikuwa wanagombea mtoto mmoja. Ni hekima, busara na ukomavu wa hali ya juu ulihitajika kufanya maamzi, maamzi sahihi yalihitajï kiwango kikubwa cha hekima ili kutambua nani alistahili nini kati ya wamama hao.
Pamoja na Daudi kuwa shujaa wa waesrael kwa kumpiga Goriath nakuahidiwa zawadi kemukemu na mfalme saul lakini mwisho wa siku Saul aligeuka kuwa adui mkubwa wa Daudi, hekima pekee toka kwa Daudi ndiyo iliyomfanya kuishi katika nchi yake kwa amani bila kupata madhara toka kwa sauli.
Nimefuatilia habari ya Elizabeth Michael na Mama Mzazi wa Stivie Kanumba ambae ameshindwa kumsamehe Elizabeth kutokana na tukio la mwaka 2012 nh kweli ni jambo gumu kusahau lakini bado haiondoi ukweli kwamba imekwishakutokea na haina budi kusamehe na kusahau na maisha kuendelea mbele bila shida
Pamoja na kusongwa songwa kwa maneno ya yule mama bado Elizabeth amekuwa ni mtulivu, mpole na mwenye heshim, hekima na busara akijitahidi kulinda hadhi na heshima ya mama kwa umri lakini pia utù. Nimemsikiliza akifanyiwa mahojiano na waandishi wa habari hakika ni mtu mkomavu pekee ndiyo anaweza kusimama na kujibu kwa hekima na utulivu wa kiwango cha juu.
Pamoja na kukiri kuwa maneno ya yule mama yamekuwa msalaba wake na yuko tayari kwenda nayo kalvari bado alimeendelea kuwa mkimya, akitambua kuwa yule ni mama yake kwa umri na akasema muungwana akivuliwa nguo huchutuma.
Sio rahisi kwa binti staa, binti mdogo kuwa na mtazamo chanya kwa kiwango kikubwa kiasi kile, alikuwa na nafasi kubwa yakuyatumia mazingira haya kama njia ya kujiongezea followers, kutengeneza attensheni kwa jamii kwa maslahi ya biashara zake za uigizaji lakini amekuwa tofauti.
Ukomavu ni vile ambavyo unauwezo wa kuipa hekima ikuongoze katika kufanya maamzi, busara ni ishara ya ukomavu wa mtu.
Halisia tumeumbwa tukapewa hisia, maumivu na kukerwa lakini kwa mtu mwenye ukomavu wa fikra, akili ni katika uwezo wa kukabiliana na mazingira ambayo ni magumu na yenye changamoto zilizo changanyika na maumivu makali yaliyoujeruhi moyo na nafsi.
Mungu ameumbia utashi, hekima na busara ni vyema kujifunza kuishi kwenye aina hizi tatu za maarifa maana ndiyo njia ya kwanza bora za kuishi kwenye mazingira yeyote na kuyamudu.
Maamzi ya mtu aliyekomaa huwa na matokeo makubwa sana ushindi katika chanya. Tumwombe Mungu kama ambavyo Sulemani alimwomba ampe hekima ambayo ilikuwa msingi wa mafanikio yake katika utawala wake.
Ukomavu ni kiwango cha juu cha hekima, mtu mwenye hekima ana maarifa sahihi, na ufahamu wake ameujenga katika mtazamo chanya, haendeshwi na gadhabu, uchungu, chuki na kisasi ndani yake bali hekima humfanya mtu kuyaweka pembeni matakwa yake binafsi kwa ajili ya wengi na haki kutendeka kama ambavyo sulemani alifanya bila kujali alitumia hekima bora kabisa.
Learn to be matured
Mgema Moses
0715366003/0755632375


Thursday, February 4, 2021

Ushindi ni ahadi ya Mungu kwa wanadamu, tuĺiumbwa tukiwa na nguvu ya ziada, tabia tofauti na viumbe wengine, tunautashi, tunasifa ya Mungu, hivyo basi kama tunasifa za Mungu maana yake kama alivyo yeye ni mshindi hata mimi na wewe ni washindi.
Ushindi wa mtu huanzia kwenye ufahamu, namna mtu anavyofikiri, anavyojitazama, anavyojiona na imani ya uwezo iliyo ndani yako/yangu. Jambo hili limekaa katika mfumo na mtazamo wa kiimani zaidi kama mtu hajafungua mtazamo wake vyema katika mukhutaza wa maisha yetu ya kila siku.
Kushinda na kushindwa ni mambo mawili ambayo yametenganishwa na uzi mwembamba sana, mentality na imani ya mtu juu ya vile ajionavyo kuanzia kwenye mfumo wa ufahamu wake...
Kuna stori moja inazungumzwa kwenye kitabu cha Joshua, kuna watu walitumwa mahali kwenda kuipeleleza nchi na walipofika huko walikuta watu wakubwa sana, katika kurudisha ripoti kwa aliyewatuma kundi la kwanza lilisema wamefika huko wameona majitu sasa sio watu ila majitu ambayo yaliwafanya wao kujiona kama mapanzi.
Kundi la pili likaja na ripoti yake ambayo ilikuwa imesheheni imani, ujasiri na nguvu ya ajabv kwamba wameona uwezekano wa kuivamia ile nchi na kuiteka nakuwa mali yao. Ndani ya kundi la watu kadhaa wamegawanyika mtazamo wapo wameona ushindi wengind wameshaona haiwezekani hata kidogo sisi ni mapanzi tu.

Wednesday, February 3, 2021

NGUVU YA MSAMAHA

Msamaha ni dawa, msamaha ni uzima jifunze kusamehe pale unapokosewa na aliyekukosea anapogundua kuwa amekosea na kuomba msamaha, wakati mwingine hata kama mtu hajakuomba msamaha samehe, msamaha ni kwa ajili yako sio kwa ajili ya alïyekukosea.

Kutokusamehe ni kubeba mzigo ambao hauna faida, na katika dunia tunayoishi leo huwezi kuishi bila kuudhiwa, kukosewa na kutendewa mambo ambayo ni kinyume na matarajio yako kwa sababu sisi ni binadamu na makosa yalianzia hapo zamani za edeni kwa Eva na Adamu....ni watu ambao walithubutu kumkosea Mungu huku wakijua uwezo na ukuu wake ije iwe wewe.....pamoja na makosa ya wengine Mungu aliamua kusamehe.

Unapokosewa fahamu na wewe pia huwa unakosea wengine na wanakusamehe, hivyo ukiwa katika ulimwengu huu, kukosea na kukosewa ni wajibu wa mwanadam, halafu kusamehe na kusamehewa ni tendo la lazima sio la hiyari,.... Kusamehe ni wajibu......ïli mradi unaishi duniani..

Msamaha ni suluhisho la uponyaji wa akili, afya ya mwili, msamaha ni ufunguo wa mahusiano mapya ambayo yalitiwa doa na kosa, msamaha ni uponyaji wa hisia zenye maumivu makali ndani yake, msamaha hurejesha furaha nakuondoa huzuni na hasira yenye uchungu ndani yake.

Yapo makosa ambayo sio rahisi hata ukiambiwa samehe ni ngumu lakini, Mungu anatutaka kusamehe 7x70 bila kujali ukubwa wa tatizo ila unachopaswa kufanya ni kusamehe tu.

Kuna namna inatokea kwenye maisha ni ngumu sana kusahau ila ndo unapaswa kusamehe bila kujali ukubwa wa kosa mfano, mume amekusaliti, umepigwa, mtu ameua ndugu yako, umeibiwa au kufanyiwa kitendo chochote ambacho kimeacha kovu moyoni na kwenye maïsha yako kwa ujumla, ni kweĺi tunarejea tu kwenye msingi wetu, Je usiposamehe ndio itarudi au kufuta kumbukumbu ya kilichotokea hapana kinabaki vilevile.

Umewahi kujiuliza gharama ambazo Mungu aliingia ili kutoa msamaha au kwa wakristo unaposoma neno lolote kwenye Biblia linalohusu ukombozi na msamaha wa Mungu kwetu huwa unachukuliaje, unaposoma Yohana 3:16 huo mstari huwa na maana ipi kwenye ufahamu wako.

MSAMAHA NI DARAJA JIPYA LA WASHINDI.
Kuna msemo mkubwa sana umekuwa ukisemwa na watu ingawa sijui kama watu wote wanaofanya kotesheni ya msemo huo huwa wana maanisha au huwa wanasema tu kwa sababu upo....
1.Weak people revenge. 
2.Strong people forgive. 
3.Intelligent people ignore.
Uliandikwa na Albert Einstein...
Maneno hayo ni mazito sana ukitafakari vyema, so maneno mepesi kama ambavyo mtu anaweza kulala nakuamka nakutamka tu kawaida.....

Ukiniuliza mimï leo mambo yapi ni msingi bora wa maisha yangu duniani nje ya wokovu na Imani yangu kwa Yesu kristo ambae ndiye alitufundisha kwa vitendo maana ya haya mambo matatu
1. Upendo
2.Msamaha
3. Utu 
Washindi wote husamehe bali failures hubaki na kinyongo, mzigo moyoni kwa kifupi ni watu dhaifu sana, watu wa kundi la kwanza.

Binafsi haya ni kati ya maeneo ambayo huwa najipima nayo kuona kiwango cha ukomavu wangu juu ya kufanya maamzi yenye kukulazimu hata kama yanakuumiza ila lazima uyafanye ili kuweza kuwa balozi mwema wa Mungu hapa duniani.

Najua sio jambo jepesi kufanya kwa vitendo, ila ndio tunapaswa kusamehe, kupenda na kuĺïnda utu kwa faida yetu wenyewe.
FAIDA YA KUSAMEHE 
1. Hurejesha mahusiano na kujenga kuheshimiana.

2. Hulinda amani na kuondoa chuki, maana kama unaweza kusamehe maana yake una upendo wa agape, upendo wa Kimungu.

3. Humfungua mtu aliyekosewa na aliyekosewa hivyo kuondoa uchungu, hisia zenye maumivu ambazo zinaweza kupelekea kuibuka kwa ugonjwa.

4. Huonyesha ukomavu wa akili, nafsi na roho na kumweleza mtu mhusika kama mtu anaeweza kubeba vitu na kuvimudu.

5. Hupima kiwango cha ukomavu wa kiroho maana utakuwa ukitenda sawasawa na agizo la Mungu 
Zipo faida nyingi kwa mtu ambae hupenda kusamehe na kuachilia. Naandika ujumbe huu nikiwa najua kuwa kuna mazingira ya kibinadamu ni jambo gumu kuĺiko ambavyo mtu anaweza kusema au kuandika wakati hali ya kukosewa au kutendewa jambo baya kwa kiwango cha kutisha.

Msamaha ni agizo msamaha ni kutenda, msamaha inaonyesha pia kiwango cha ustarabu, utii, utu, upendo, ukomavu na utofauti wako na watu wa kundi la kwanza la watu....

Ni ngumu ila tenda kwa manufaa yako binafsi
Mgema Moses
0755632375/0719110760


Tuesday, February 2, 2021

IMEKUWA TABIA YA WATU WENGI

Ni rahisi zaidi kumsema mtu aliyeshindwa kwenye jambo fulani, alifeli mtihani, biashara ilianguka, alipoteza kazi au amekuwa akifanya chini ya kiwango kwenye majukumu yake.
Ni rahisi zaidi kumtukana mcheza mpira anapokuwa uwanjani nakumsemea maneno mabaya huyu hajui, anakosaje goli jepesi vile, anapitwaje kirahisi, huyu kipa shati anafungwaje kizembe vile huo ni mdomo wa mtu mmoja akiwa amekaa jukwaani na wakati mwingine anaporomosha maneno yasio na staha kwa mchezaji, ni rahisi sana.
Utakuta mtu/watu wako busy huyu mwimbaji hajitambui kabisa ona mwenzake ameubadilisha muziki kuwa biashara anapiga pesa kila kukicha yeye yupo yupo tu hana mpango.
Watu wanasahau hata kukumbuka kuwa mpaka unamfahamu kuwa huyu ni mchezaji tena akiwa kwenye timu kubwa ni juhudi zake ndiyo maana umepata wasaha wa kutoa pesa yako kwenda kutazama mpira, ndiyo maana kutwa headphone masikioni na kukera watu kwa muziki mkubwa katika subwoofer hapo nyumbani kwako.
Kidole karibu na kidole gumba ni rahisi zaidi kumnyoshea yule mtoto aliyeanguka mtihani huku ukiwa umesahau kuwa vidole vitatu vinakuelekea wewe na kukumbusha kuwa mbona na wewe hukuwa ukifaulu masomo ?, mbona wewe hata kazi zako huzifanyi vizuri ndiyo maana kuĺa kuku hapa nyumbani ni mpaka bibi atuma kutoka kwetu singida, hata hawa wakizungu huwezi kununua walau kwa mwezi mara moja ?
Ni rahisi zaidi kumkosoa kiongozi kwamba hafanyi vizuri wakati wewe hata kuwa balozi wa nyumba kumi ulishindwa,
Yapo mengi yanatokea kwenye mzunguko wa maisha yetu, hisia na mawazo ya watu wengi yamejengwa kwenye hasi zaidi kuliko chanya. Mtu akianguka kwenye jambo fulani ni mzembe mjinga, hajielewi, mvivu, hajisomei, mbinafsi nk.
Ndiyo maana leo utakuta vijana wako kwenye mahusiano mmoja akikosea hata kidogo suluhisho tuvunje mahusiano, tuvunje uchumba kama ndio bado tuko kwenye uchumba mambo yenyewe ndïo haya mimi basi....sababu yenyewe ya kitoto wee, nani kakwambia utaolewa na malaika ambae ukiwa nae hatakosea, umewahi kujiuliza kwa nïni wazazi waliishi au wanaishi mpaka sasa na unawasifia sana kuwa ni wazazi bora na wamejenga familia imara.
Asilimia kubwa ya mambo hata kama yamekuja au kutokea kwa namna ya mtu kukosa kutimiza wajibu wake sawasawa ni vyema kujenga hisia na mtazamo chanya kwenye ufahamu wako kabla kinywa hakijasema, sio kila aliyeshindwa kufunga goli, kuzuia goli amependa iwe ivo, sio kila mtu aliyefeli mtihani, biashara, nk ni kwa sababu ya uzembe au kutokutimiza wajibu wake hapana.
Nimejifunza sana kwa baadhi ya watu ambao walifanya isivyosawa katika mtazamo wa watu wengi wakasemwa vibaya, ooh wazembe, wavivu hawajielewi nk walipotatuliwa vyanzo vya kufanya vibaya wamekuwa watu bora sana.
Vilevile kuna baadhi ya watu wanafanya vitu kwa viwango vyao waliojiwekea mfano kwenye kiwanda cha muziki na mpira, biashara na elimu, kuna baadhi wanaimba kama burudani, kipato anachoingiza amelizika nacho na ameamua kuseti kuishi kwa kiwango hicho, sïo kila mwanamziki, mcheza mpïra anataka kuwa Dïamodo, Mbwana Samatta, hashmu Thabiti mwingine ndoto yake iĺikuwa kufikia levo aliyepo ndio maana baada yakufika hapo ametulia na kuĺinda kiwango hicho na amedumu hapo.
Kuna watu wanatamani kufikia levo ya umilionea, ubiĺionea lakini kuna mwingine ameridhika na uwezo wa kusomesha watoto, kumïliki nyumba, kupata gari yake au kutokumiliki hata gari lakini ndio uchaguzi wake aliochagua.
Kuna mifano mingi hata shuleni kuna wanafunzi huwezi kuwakuta wamekuwa wa kwanza hata kumi bora lakini yupo kwenye viwango vya ufaulu, kama wastani ni 50 basi piga ua galagaza yupo, watafeli sana au kufaulu sana lakini yeye yupo kwenye wastani wakumvusha daraja jingine ndiyo viwango alivyoamua kuishi navyo.
Mwisho sio kila mtu anataka kuwa kama wewe unavyotaka, sio kila mtu ambae hafanyi au hakufanya vizuri imesababishwa na uzembe au kupenda hapana kuna mengine hutokea kwa sababu zilizo nje ya uwezo wa kujizuia.
Asilimia kubwa ya watu hutamani kuwa bora katika kila jambo lakini yapo mazingira yanalazimisha kuwa hapo alipo au kufeli kwake.
Badala yakuja na majumuïsho ya majibu yatokanayo na matokeo yaonekanayo kwa macho ni vyema pia kuwa na muda wakumtazama mtu huyo kwa jicho chanya, hii itarahisisha sana kukupa relief ya kujua chanzo cha tatizo hata unapokuja kutoa majibu yako yawe na uhakika kuwa ni kweli..
Ni rahisi zaidi kujidanganya kwa kusoma kichwa cha habari juu ya kitabu nakujipa majibu ya kusudi la mwamdishi juu ya kile kimefunikwa ndani ya kava la kitabu....
Ukiwa mkosoaji jaribu kuwa mtafiti zaidi utakuwa bora na mwelevu
Smartness.
Mgema Moses
0715366003/0755632375

Monday, February 1, 2021

Fimbo ya Musa iligeuka kuwa hatua yakuvuka kwa wanawaesrael kufika ng'ambo ya bahari ya shamu, Mungu alimuuliza Musa una nini mkono mwako, Musa alijibu kwa ujasiri nakusema nina fimbo katika mkono wangu, uwepo wa fimbo ile katika mkono wa Musa, Mungu aliona kuwa yafaa kuwa mtaji wa hawa watu kupiga hatua nyingind kubwa kuelekea hatima ya maisha yao.
Wakati Mungu anaona hahitaji nguvu nyingi na kutafuta vifaa vikubwa ili kukausha yale maji ya bahari aliamua kuzipandia nguvu na elimu mpya kwenye fahamu za waesrael. Haikuwa rahisi kueleweka kama fimbo ile inaweza kuwa sababu ya maji ya bahari kugawanyika nakutengeneza njia, lilikuwa jambo la kufikirika kiasi fulani.
Wakati Mungu anaona uwezekano kupitia fimbo ya Musa kuwa unaweza kuwa moja ya mtaji wa kusogelea hatua kadhaa katika mwelekeo sahihi kuyaelekea malengo na kusudi la hatima.
Kuna mkulima mmoja mwenye shamba 

Sunday, January 31, 2021

Kila hatua ya ukuaji huanza na mbegu kufa na kuoza, ndipo inaanza mchakato wakuchanua tena. Mfano mzuri uko kwenye upandaji wa miti, mbegu hufukiwa ardhini na kufuata hatua zote zinazotakiwa kufuatwa ili mmea tarajiwa ukue kwa kupitia njia sahihi ukiwa umepokea na kupitia mchakato sahihi wa ukuaji na hatimae matunda.
Mti ambao utakuwa na matunda bora yanaweza kuuzika kwenye soko la ndani lakini hata kwenye soko la kimataifa kutokana nakupitia mchakato sahihi ambao huleta ustawi wenye manufaa.
Niliwahi kuhudhuria semina moja ambayo 

Saturday, January 30, 2021

TAFUTA KUWA BORA NA SIO BINGWA

Unapotafuta kufika kwenye hatima ya ndoto au malengo yako kwenye kichwa chako huwa unawaza swali gani kati ya haya mawili.......
1. Kuwa bingwa ?
2.Kuwa bora.. ?
Kati ya haya maswali mawili kila mtu ana majibu yake katika ufahamu wake. Katika ulimwengu tunaoishi leo, watu wengi wamelazimisha kuwa mabingwa ili kupokea tuzo na sifa kedekede kwa sababu tu ya ile taji ya ubingwa juu ya jambo fulani ambalo alikuwa ana ndoto au shauku nalo.

Watu wengi wamekuwa wahanga wakutafuta tuzo, vyeti na heshima fulani ïlï kuongeza hadhi kwenye jamii zao. Jambo hïli limekuwa likiathili sana mifumo ya elimu kwa wanafunzi wa ngazi zote katika shule na taasisi zingine za elimu ya kati na juu, wafunzi na wanavyuo wengi wanakuwa na bidii ya kuhakikisha wanakuwa na matokeo bora ya mwisho wa kozi zao, mtoto hasomi wakati akiwa form one akifika form two atakazana sana ili asifeli kipimo cha kidato cha pïli atatafuta past papers, atakwenda kila chimbo kutafuta sio uelewa bali material yatakayomfanya kufaulu na kuingia ngazi inayofuata.

Mchakato huo upo kidato cha nne, cha sita hata ngazi ya vyuo vya kati na vikuu, watu wanahudhuria darasani ili kufanya Quiz, assigments na mitihani yakukamilisha kozi zao, akishakamilisha mchakato wa kozi tukutane UE hapo ndiyo zima moto inaanza, kichwani hakuna maarifa wala ujuzi wowote ila watu wanatazama joho la siku ya mwisho, watu wengi wanataka ubingwa hata kama ni wakununua kwa fedha bila jasho, wapo tayari kutoa fedha sio jasho kwa maana yakutafuta kuwa bora.
Watu wanataka kuwa matajiri kwa kubeti, watu wanakutana kimwili kabla ya ndoa na ndoa bora wanazitaka hapo kesho wakati hawataki kufuata misingi sahihi itakayowafanya kuwa na ndoa bora na zenye maadili ya Kimungu, changamoto sana.

Leo tuna watu wenye degree, masters, PhD na hata maprofesa ambao tuzo zao haziendani na uwezo, maarifa na ujuzi ambao uko kwenye fahamu zao, lakini vyeti vina 1st, 2nd na 3rd classes za GPA toka vyuo vikubwa nchini.
Sikushangaa sana marehemu Ruge Mtahaba, Majizo na makampuni mengine yalipoamua kujiongeza nakuondoka kwenye usaili wa kawaida, kuajili vyeti vilivyobebwa na watu wenye uwezo mdogo hata wakutetea vyeti vyao...swali hili limefanya wasomi wengi kuangushwa na watu wa darasa la sababu na wenye elïmu ya kati hasa kwenye vyombo vya habari, wasomi hawezi basi hata kuwa na wazo jipya, basi kuboresha an existing Ideas.....swali kama hïli ni mwiba kwa wasomi wengi, unafikiri una nini cha ziada ukiacha ukubwa wa eĺimu na GPA yako, utatufanyia nini ambacho hata tukikulipa mshahara hatutaumia maana utakuwa umezalisha na sehemu ya ulichozalisha tukafanya malipo yako ya mwezi ?.... Huwezi laumu
Hadhi zakuwa mabingwa, kusifiwa mtaani umeondoka na div 1, div 2 na div 3 hata four umeïtafsiri vipi kwenye uhalisia wa maisha ya kawaida, ni kweli mifumo ya elimu ina changamoto yake lakini ndiyo iliyonipa hata huu uwezo wa kuandika maana yake bado ni bora na inaweza kututoa hapa tulipo.

Watanzania wengi tumekuwa ni watu wa zima moto, final touches hatutaki michakato yenye tija ambayo inaweza kutufanya kuwa mabingwa wenye ubora ndani yake, kifupi vyeti na tuzo zetu zisadifiwe na uwezo wa utendaji wa kazi kwa vitendo ili watu waipe thamani na umuhimu wa elimu nakuondoa kejeli za wasio na elimu.
Tujikite kwenye kutafuta ubora zaidi kuliko nishani za heshima ambazo hazina maana yeyote kama hazitafisiri uhalisia katika vitendo vyetu.

Niliwahi kusoma vitabu vya watu wawili walio wahi kufanya kazi na staa wa mpira duniani Cristiano Ronaldo mmoja wao ni Sir Alex Ferguson alïkuwa kocha wa Staa huyo, Carlos Tevez mchezaji mwenzake na Ronaldo pale Man utd, wanasema Ronaldo hakuwahi kutafuta kuwa bingwa bali alitafuta ubora ambao uliongeza ufanisi wake katika kucheza mpira, walisema pamoja na mafanikio na kiwango bora hata sasa lakini amekuwa akiamka mapema sana kukimbia na kufanya mazoezi, Tevez alijitahidi kuwahi mapema zaidi lakini alimkuta Ronaldo yuko uwanja wa mazoezi na baada ya mazoezi ya timu alibaki kucheza faulo lengo alikuwa akitafuta ubora.
Ronaldo amekuwa kwenye utawala wa mtoto mwenye kipaji sana Leo Messi na aliyekuwa akibebwa kwa kiasi kikubwa na sababu za kibiashara za makampuni ya Adidas na Nike, utawala wa Fifa kipindi hicho na kamati yake kuonyesha upendeleo wa wazi kwa Messi hata aliposhuka kiwango na kuzidiwa na Ronaldo.
Lakini Ronaldo alijikita kwenye kutafuta ubora ambao ndiyo umekuwa ukimpa ufanisi wa kazi yake ambayo mwisho wa siku walishindwa kuzuia ubingwa wa Ronaldo na Ronaldo ni  bingwa sio kwa mbeleko bali kwa kazi na ubora wake.
Historia ya Mbwana Samatta kati ya vijana wakitanzania ambao wameamua kuishi nje ya mfumo wa maisha ya vijana wengi wa kitanzania, kabla yakuwa bingwa aliamua kutafuta ubora ambo ulikuwa ni sababu ya yeye kuhitajika na vilabu vingine, alicheza Simba sehemu ambayo tayari alishafikia kiwango chakujivika ubingwa na heshima ila alikubali kwenda Tp Mazembe kuendelea kujitafuta zaidi ya vile alikuwa akiwa simba, muda ulipofika ubora ulimtambulisha, leo ukifika Lubumbashi jina la Samagoal sio geni kwa mashabiki wa mpira pale DRC nenda Genk pale ubelgiji Samatta anaimbwa na wazungu 
Chanzo cha yote Mbwana alikataa kuwa bingwa kwa kupewa sifa au kutafuta sifa toka nyumbani bali aĺijitahidi kutafuta ubora kwa matumizi ya kesho. 
Nimetumia mifano mingi ya wasomi na wacheza mpira lengo ikiwa nikueleweka vyema zaidi nakuipata poïnt na lengo la kuandika andiko hili.
Tuache Kukimbilha nishani, tuzo na vyeti bali tutafute ubora, bora uwe na wastani wa kati katika vyeti lakini katika utendaji uwe na GPA ya kwanza ndiyo maana halisi ya kuwa bingwa.
We are not supposed to be bĺinded with medals and rewards let us strive for Quality & better
Mgema Moses
0715366003

Friday, January 29, 2021

KIPAJI NI BORA, ELIMU NI MUHIMU JUU YA KIPAJI.

Nimekuwa napenda sana kusoma quotes ya Albert Einstein ambayo inasema ''Everybody is a genius. But if you judge a fish by it's ability to climb a tree, it will live it's whole life believing that it is stupid'' 
Naupenda sana msemo kwa sababu ni elimu na somo tosha kwa jamii ambayo imekuwa ikiishi maisha ya kukariri pasipokujua kuwa maisha ya mtu tangu mwanzo yalijengwa kwenye msingi wa kutembea kwenye channel ya kipaji chake.
Elimu imekuwa ni kificho cha watu wengi, huku pia asilimia kubwa tukiwa hatujui maana na lengo la elimu hasa kwa watoto, vijana na watu wote kwa ujumla. Elimu sio ajira, elimu haikutenganishi na talanta ambayo Mungu aliiweka ndani yako.
Elimu inakipa thamani ambacho tayari kinaishi ndani ya mtu, elimu tunayoipata shuleni, kwenye washa, semina na makongamano ya elimu rasmi na isiyo rasmi ina lengo kutujengea mtazamo mpana zaidi ya ule tunaokuwa nao kabla yakupata elimu hiyo.
Elimu ni mkusanyiko wa maarifa na ujuzi wa mambo mengi ambayo yanatugawanya na kila mtu kujigundua kuwa mimi ni wa sehemu au niko kundi gani. Changamoto kubwa imekuwa kwa wazazi na walezi kuwalazimisha watoto kufanya vitu ambavyo katu hata kama angekesha kusoma usiku kucha hawezi kuwa unavyotaka wewe mzazi au mlezi, mwisho wa siku atafeli nakuichukia shule .
Nimeandika makala hii baada ya ijumaa kumwona mtoto wa miaka nane, Juh Juh Ruge Mtahaba akifanyiwa mahojiano katika kituo cha redio clouds, namna anavyojielezea wakati anawasilisha kipindi cha watoto cha Smart Bees, unaona ambavyo mzazi alivyo karibu na mtoto na kufuatilia nini amebeba ndani yake ndiyo maana anaanza kumsogeza karibu na mahali ambapo anaweza kukifanya kipaji chake kuanza kuonekana vyema, mtoto yule sio kama hasomi ana soma lakini elimu yake imejikita zaidi katika kuboresha na kuinua kipaji chake vyema.
Tumekuwa na changamoto kama jamii ya watanzania na mgawanyiko mkubwa ndani yake, wakati vijana asilimia kubwa wakiamini kipaji pekee ndiyo suluhisho la wao kutoka kimaisha, wazazi wengi wanaamini njia pekee yakumfanya mtoto kutoka kimaisha nikusoma ili aajiriwe, vijana wamewekeza nguvu maana wanaona wasomi wengi hawana na ajira hivyo kudiriki kusema kuwa elimu imeshuka thamani.
Kipaji ni muhimu, ila elimu ni muhimu zaidi kwa sababu inakufanya kujitambua, kujua namna yakukipa thamani kipaji chako, namna yakufanya branding, kujiweka kwenye masoko, hata kama una watu wanakusimamia ni rahisi kujua mchakato wa mikataba maana elimu ipo.
Wazazi tubadilishe mtazamo juu ya elimu tunayopata kuwa sio kila unaempeleka shule lazima apate ajira serikalini bali elimu ifanyike kuwa mtaji wa kwanza kwenye kuelekea ndoto ya kijana au mtoto wako.
Tukiendelea kuwalazimisha watoto kufanya yaliyo matakwa yetu, tutakuwa tukiihalalisha kwa viteńdo kauli ya Albert Einstein ya samaki kushindwa kupanda mtini, nakubaki kuamini kwamba yeye ni mpumbavu, kumbe amevamia eneo ambalo sio eneo aliloumbiwa kuwa bora.
Elimu ni mhimu sana ila, kipaji ni chanzo kikubwa cha ajira na utajirh, vyote tutembee navyo, kipaji isibaki kama mbadala wa watu walioshindwa shule au watu masikini.
Open your mind
Mgema Moses
0715366003

Wednesday, January 20, 2021

MAARIFA NI DIRA YA MWELEKEO SAHIHI.

Maarifa ni ufunguo, maarifa ni daraja laini(soft bridge), Ni ufunguo kwa sababu kupitia maarifa tunafahamu mambo mengi ambayo yamefungiwa kwenye hazina mbalimbali katika dunia yetu na kwetu pia kama watu...
Maarifa ni daraja kwa sababu kabla ya kuwa na ufahamu wa jambo fulani mara nyingi tumeishi kwenye giza, lakini baada ya kupata maarifa kuna vitu vingi vimerahisishwa sana tofauti na hapo kabla yakupata maarifa yakutuvusha kwenda ng'ambo ya upande ambao tulikuwa hatuna namna yakuwaza kama inawezekana lakini baada ya maarifa imekuwa rahisi kufika huko.
 Kabla ya ukoloni wazee wangu pale mwadui walichukua almasi nakuchezea kama kete za bao, mzungu alikuja na golori nakuwarubuni wazee wangu hao, akawaaminisha kuwa golori ni bora zaidi ya almasi, wakavutiwa na mng'ao wa golori wakaona Almasi haifai, Mzungu akachukua mali wazee wakabaki na na golori kwa furaha najua moyoni walisemezana hawa wajinga tumewala, kumbe wao ndiyo waliliwa, hakika wajinga ndio waliwao. Ujinga sio tusi bali ni kukosa ufahamu juu ya jambo fulani, hata mimi ni mjinga wa mambo ambayo sina ufahamu nayo.
Huwezi kuwalaumu wale wazee kwa kuibiwa namna ile ilitokea hivyo kwa sababu hawakuwa na ufahamu juu ya hivyo vitu viwili kwa wakati huo, wakakutana na wajanja wenye uelewa, ufahamu ambao ulitokana na maarifa vichwani mwao, waliojua thamani ya almasi zaidi ya wazee wangu.
Biblia iko wazi inasema kuwa watu wangu wanaangamia kwakukosa maarifa, ni kweli bila maarifa ni ngumu kujigundua binafsi, kugundua fursa zinazotunguka, ni ngumu kupiga hatua, itakuwa ni kawaida kutumia nguvu nyingi kwenye jambo linalohitaji akili na uelewa mdogo tu...
Pasipo maarifa wazee wetu wamelala kwenye yadi za mashamba yetu wakiwa masikini, wameacha utajiri wa mifugo kwenye mazizi mengi, huku wengi wao walikuwa marafiki wa nyumba duni za majani, kulala kwenye ngozi nakula vyakula duni wakati utajiri umelala kwenye himaya zao.
Vipaji vingi vimekufa bila kutumika kwa sababu tulikosa maarifa yakuviendeleza nakuvigeuza kuwa mitaji ambayo ingetuletea utajiri na ajira zakutosha, .. Maarifa, Maarifa ni ufunguo
Bila maarifa tusingekuwa na ndege leo, meli, lami, madaktari bingwa, wahandisi wa majengo yanayopendeza kule Dar es salaam, bila maarifa tungewezaji kupita juu ya maji kama Petro, tungewezaje kupaa angani kama mwewe, bila maarifa tungewezaje kutunza kumbukumbu ya picha, video ya matukio tunayoyafanya katika kizazi hiki, tungejuaje historia ya kule tumetoka, kamera zemetusaidia kupata hifadhi ya matukio ya nyuma kwa manufaa ya kesho.
Matokeo ya haya yote ni zao la maarifa. Maarifa haya yanapatikana wapi ?
Mtu mmoja nilimsikia akisema elimu haina faida tena kwa sababu watu wanamaliza vyuo hata kazi hawapati wanarudi kuuza nyanya kwenye masoko na magenge ya mitaani huko mbagala, keko, kuuza supu ya mapupu huko vingunguti kati ya soko maarufu la mbuzi kutoka Dodoma huko Dar es salaam, nilitamani kushawishika kuwa ni kweli, lakini nikakumbuka tena kuwa Biblia inanikumbusha kwa habari ya Kumkamata sana Elimu nisimwache aende zake...nikashtuka kidogo, mshtuko wangu ukanikumbusha kuwa watu wangu wanaangamia kwakukosa maarifa, kwa stori za yule ndgu yangu, kama nisingekuwa nimepitia ule mstari wa watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa hakika ningeangamia maana ningemwamini bila kupinga ila kwa sababu nïĺïkuwa na maarifa nïliepuka muangamio mkubwa wa mawazo finyu na mgando toka kwa yule ndugu.
HAYA MAARIFA YANATOKA AU KUPATIKANA WAPI....
Elimu ni chanzo cha maarifa na ndio kiboreshaji cha juzi mbalimbali ambazo Mungu alituzawadia mfano vipaji mbalimbali katika michezo, kuimba, burudani, kwenye ufundi wa vitu mbalimbali ambavyo ni hard na soft skills.
Elimu itupayo maarifa na kuboresha ujuzi wa mtu haishii darasani tu kwenye elimu rasmi hapatana,...elimu ipo kwenye maeneo mengi, nyumbani, shuleni, kwenye jamii, kwenye majarida, vitabu, video, maandiko tofauti kwa maana ya makala, nyimbo, maïgizo nk.
Watu wengi tumekosa mambo mengi kwa sababu ni wavivu wakusoma, kuna msemo unasema ukitaka kumficha jambo Mtanzania jambo hilo weka kwenye maandishi ni hatari sana...
Maarifa hubadilisha fikra mgando, huibua talanta na kufungua hazina ya fursa zilizojificha. Hivyo tupende kuwa na kawaida yakujifunza kupitia kusoma vitabu nk, kwa lengo la kujiongezea maarifa ambayo yatatusaidia kwa matumizi ya sasa na baadae.
Mgema Moses
mgemamoses@gmail.com
0715366003,0755632375

Tuesday, January 19, 2021

MCHAKATO NDIYO MAFANIKIO SIO MATOKEO.

 watu wengi tumekuwa wahanga wa matokeo ya mwisho yanayoonekana kwa macho, tunazungumzia kwa kina na kupongeza kwa sababu tunamwona mtu akiwa na fedha nyingi, akimiliki nyumba, biashara na vitu vingine kama kazi nzuri.
Mara nyingi tumekuwa wagumu wakufuatilia chanzo cha mafanikio ya mtu alikoanzia, sio kila matokeo yanapaswa kupongezwa, jua chanzo kïlichomfanya kuwa hapo juu, ni kweli tunapaswa kupongezana pale mtu anapofanikiwa au kufanya vizuri lakini pongeza panapostahili kupongeza, mtu amepambana mpaka ametusua maisha,amekuwa na bidii yakusoma na mwisho wake amefanya vizuri, hivyo pongeza bidii na mchakato unaoambana na uvumilivu ambao umeleta matokeo yanayoonekana.
Usipende kumpongeza mtu kwa kuona matokeo ambayo hata hujui matokeo yale yametokana na nïni, kuna watu wana maisha mazuri kwa sababu yakuiba, kuna watu wamefaulu mitihani kwa kuigia na ukimwambia mtu yule ufaulu wa kwenye karatasi apeleke kwenye utendaji unakuwa ziro.
Mafanikio bora ni yale yanayopikwa kuanzia chini kwa kufuata misingi na mchakato sahihi ambayo siku ikionekana kwa macho inakuwa ni reflection ya mafanikio ambayo yameleta matokeo yanayoonekana kwa macho ya wengi.
Mafanikio ya ndoa sio kile kicheko kionekanacho kwenye nyuso za wanandoa no, mafanikio yao ni namna ambavyo kila mtu amempokea mwenzake nakuamua kustiliana na kubeba kwenye madhaifu na uimara nakuhesabiana kuwa bora kwa kila mtu
Ukiona timu ya mpira inapata matokeo bora kiwanjani, fahamu hayo ni matokeo ya mafanikio ya uwekezaji, na kupitia mchakato sahihi kwa kutengeneza mseto mzuri kuanzia utawala, team management, coaching stuff, wachezaji na timu nzima kwa ujumla, kionekanacho uwanjani ni matokeo ya mafanikio nyuma ya pazia.
ukiona matokeo bora kwenye biashara, fahamu akili ilifikiri vyema sana na kupeleka kwenye mawazo hayo kwenye karatasi na baadae kwenye utekelezaji.
Usipende kumpongeza mtu kwa matokeo yaonekanayo kwa sababu hujui matokeo hayo yametokana na mchakato sahihi au usio sahihi tujifunze Kupongeza mchakato ulisababisha matokeo yanayoonekana sio matokeo ambayo wakati mwingine huja bila kupitia njia na mchakato sahihi.
UKIONA  KOBE AMEINAMA FAHAMU TU KUWA ANATUNGA SHERIA,....
Mgema Moses

Monday, January 18, 2021

MTI WENYE MATUNDA UNAPIGWA MAWE

Watu wengi tumekuwa na kasumba ya kutokupongeza jitihada za wenzetu kwa maana ya vijana wenzetu na watu wazima ambao wamepiga hatua za maendeleo kwa kiasi fulani. Unakuta watu wanapiga stori kwenye vijiwe wakisema mtu yule anajisikia sana, amekuwa na roho mbaya, anatupita bila kutusalimia wakati jamaa wakati bado hajatoboa alikuwa mwana kinyama.
Wengine wanaanza kutengeneza scenario za kuwa hata mafanikio yake sio halali, haiwezekani atoboi kirahisi hivi itakuwa amejiunganisha na mambo ya freemason, atakuwa amewatoa ndugu zake sadaka na nk.
Yote yananenwa kwa sababu ya chuki, roho isiyokubali na kuamini kuwa mapambano ya maisha yanaweza kumpa hatua mtu kufikia malengo na ndoto zake. Bahati mbaya sana akifanikiwa Mtanzania ndio itakuwa habarï kubwa yakusemwa kwa mtazamo hasi, tumewaona wanamuziki wetu hapa nchini wamepambana wameutoa muziki kwenye vumbi lakini unakuta kuna mtu yuko swekeni huko anamponda anamsema vibaya, wakati huo huo anamsifia mwimbaji wa Nigeria, USA na nchi zingine kama vile wanawafahamu sana...
Hii inatokea kwenye maeneo yote kwenye maisha yetu, iwe kwenye biashara nje na muziki, madukani, kwenye soka, kwenye mafanikio ya dini zetu hasa watumishi wa Mungu, kwenye siasa, kwenye kazi za maofisini na maeneo mengine, utakuta watu wanasema huyu asingekuwa baba yake asingekuwa hapo, sasa tujiulize baba yako angekuwa kwenye nafasi ya kukunyanyua asingefanya ivo. Na asipofanya hivyo si ataonekana mpuuzi na asiye na akili.
Ukiona unaandamwa sana na maneno jua wewe una kitu cha ziada, watu wakawaida huwa hawazungumzwi maana hawana kitu chakuwafanya watu kuwazungumzia.
Huwezi kwenda kuchuma matunda kwenye mchongoma, na shida ya mchongoma kama mti una faida moja au mbili ambazo pia utazipata kwenye mchungwa, mwembe, mpera na mpeazi pia, unatoa kivuli labda na mbao ambazo pia sio mbao bora, kumbuka pia mwembe na miti mingine inatoa kivuli na mbao ambazo zinaweza zisiwe bora pia ila inatoa.
Sasa kama una sifa za mchongoma nani atakuzungumzia, maana sifa ulizo nazo kila mtu anazo, sifa za kawaida. lakini mti wa matunda unapigwa mawe kwa sababu una sifa ya ziada, wakati wa jua, wakati wa mvua na wakati wa hali zote watu wataufikia ule mti, watakula matunda, watajikinga mvua au jua nk.
Ndivyo ilivyo kwa watu wenye sifa za ziada, watasemwa vibaya vijiweni, wakipewa tuzo huko mataifani watapokelewa kwa nderemo na vifijo, kila mmoja atajifanya anampenda huyo shujaa.
Hivyo basi ni vyema kuilinda miti yenye matunda maana inatufaa sote, wapo watu wameajiliwa kupitia mafanikio ya mtu ambae ametutangulia, mfano mzuri ni Diamond ni zaidi ya familia hata hamsini wanakula kwa sababu ya matunda ya kazï yake. Hakika mti wenye matunda hupigwa mawe
Mgema Moses
mgemamoses@gmail.com

Thursday, January 14, 2021

VITO VYA THAMANI HAVIPATIKANI KIRAHISI.

Kuna changamoto vijana au watu wengi tumekuwa tukiitengeneza mwisho wa siku imepunguza sana thamani ya watu wengi.
Mtu anaenda ametuma maombi ya kazi mahali, ana elimu na sifa zote zinazotakiwa na waajili, lakini cha ajabu mtu akiitwa kwenye usahili badala yakuwasilisha ubora wake kila anapoulizwa swali basi unakuta anapoteza hali ya kujiamini, anatetemeka, anajibu maswali kwa kuonyesha sura yakutaka kuhurumiwa, akiulizwa unataka tukupe mshahara wa kiwango gani basi anataja kiwango cha chini kabisa ili aonekani hapendi hela, weee watu hawakuchukui kwa sababu umetaja dau dogo, wanachukua ubora wako, ukitaja mshahara mkubwa na unasifa kwanza lazima huyu mtu hana njaa, anajielewa, na anajua thamani yake hivyo lazima wakuchukue mshahara mtajadiliana tu baadae.
Namna utakavyojirahisha ndivyo thamani yako itakavyokuwa chini, hata kama utapata kazi bado wanauwezo wa kukufanya chochote wanataka, sio kwa sababu huna uwezo au bora hapana, una uwezo na ubora ndiyo maana wamekuchukua changamoto namna ambavyö ulijiwasilisha kwa ile mara ya kwanza ndiyo maana wanakufanya wanavyotaka.
Ni kweli wakati wakutafuta maisha hasa kama umetokea maisha duni, umepigika kweli kweli unalazimika kusema ndiyo hata kwenye uonevu lengo nikuitumikia ile kauli isemayo mtumikie kafiri ili mradi mkono unaenda kinywani, hapana jaribu kuheshimu taratibu na kanuni za ofisi ila usijishushe thamani yako.
Kuna watu wana mawazo mazuri, na watu wengi wameyakubali baada yakuyapitia ni mawazo ya miradi mikubwa, bishara kubwa nk., lakini namna ya uwasilishaji wa mawazo hayo basi unajikuta uliopelekea idea hiyo wakuone wewe njaa na kupitia njaa yako basi unatoa mwanya kwao kuishusha thamani ya wazo lako, sababu ulitengeneza unyonge hata kabla. 
Ndiyo maana wahenga walisema, umaridadi huficha umasikini na matatizo yako, jaribu kwa kila hali kuiona thamani yako mbele ya watu unao amini wanaweza kuwa daraja la kwako kusogea mbele zaidi kuelekea ndoto zako.
Joel Nanauka mwandishi wa kitabu cha timiza malengo aliwahi kusema: kuna siku alitakiwa kwenda ofïsi moja kubwa jijini Dar es salaam, katika ile ofisi sio mkurugenzi wala wafanya kazi wengine ambao walimfahamu bwana Joel, siku ya mafunzo ilifika na viongozi wa kampuni walijipanga kumpokea cha ajabu walikutana na mtu ambae hawakumtegemea kabisa kutokana na mwonekano wake, umbo dogo, yuko simple sana, na waĺitegemea kuona V-8, mtu mkubwa sana katika mwili. Kwa kweli mwonekano wake ilikuwa dissapointment kubwa sana, mkurugezi alikataa kuwa sie mkufunzi na ilibidi yatengenezwe mazingira kule ndani ili kuwaanda kisaikolojia washiriki wa washa ile na hii ilikuja baada ya mazungumzo marefu kabla hawajakubali hata kwa shingo upande.
Bwana Joel alijeng Utulivu, kuitambua thamani yake, madini yake na maandalizi yalimpa ujasiri mkubwa na aliamini kitu pekee kinachoweza kumbeba ni uwezo wakuwasilisha mada na mafunzo kwa kiwango cha juu, misukosuko na dhoruba ya kugomewa kuwa si yeye mkufunzi haikumwondoa kwenye lengo la uwepo wake katika ile washa...
Muda ulipofika alipanda kwenye podium kwa ujasiri na nguvu na shauku yakufanya vizuri. Baada ya mafunzo kilichobaki ni historia na kila mtu anamfahamu joel Nanauka. Joel hakuwa yule waliyemwona katika umbo dogo, bali alikuwa ni Nanauka mwenye umbo kubwa sana ndani yake.
Una nafasi yakuwa prove wrong wale wanaokuona wewe ni mnyonge, sio kwa kuwalazimisha bali kwa thamani yako. Be you, create confidence, create your trust to the majority by making it to the maximum
Híi anaapply kwenye maisha yote mfano heshima ya mke ni namna ambavyo ulijiposition wakati umefuatwa na mwanaume,....Thamani yako ilipanda au ilishuka baada yakukutana na mtu kwa mara ya kwanza. Jenga heshima yako hata kama unahitaji jambo present yourself in a high value ili kesho mtu asiseme kuwa huyu mtu yuko hapa kwa kuwa alihurumiwa.
Tujifunze kwa mawe ya thamani, dhahabu, Almasi, Tanzanite, na madini mengine hayapatikani kirahisi wachimbaji hutoka jasho na damu ili kuyapata sio kirahisi. Ni mawe lakini thamani yake imekuwa juu kutokana na namna ya upatikanaji.
Fedha ina thamani kubwa kwa sababu sio kila mtu anaweza kuitengeneza, na ili uweze kuipata lazima upambane sana ndiyo uipate.
Hivyo ijenge thamani yako kutokana na kile unachomiliki, kama unakipaji basi kifanye kuwa na thamani.
Mgema Moses

Sunday, January 10, 2021

IFANYE JTATU YAKO IMARA KWA KUMALIZA WIKI NA FAMILIA YAKO.

Jumatatu ni siku ya kwanza ya wiki, ni siku ambayo huja baada ya mapumziko ya weekend. Siku hii huamliwa na namna ambavyo weekend uliimaliza. Kuna watu huitumia weekend kwa kukaa na familia, kucheza na watoto, ni siku ambayo hata kama atakuwa na kazi za hapa na pale lakini hujitahidi angalau kuwepo nyumbani mapema tofauti na siku za week, atakaa na watoto, atasikiliza kero na changamoto zao, atacheza na watoto, lakini ni muda mzuri wa tabasamu na mke au mume nk.
Jumapili inakuwa ni siku bora sana kwa ajili ya ibada, kumshukuru Mungu kwa kumvusha salama katika wiki inayoisha, kurudisha utukufu Mungu, na kutimiza wajibu wa ibada kama ambavyo ni utaratibu wa Mungu ulivyo, fanya kazi siku sita halafu siku ya saba, itakase maana ni sabato ya Bwana, ni siku muhimu sana.
Wengine siku hizi mbili huzitumia kwa kufanya mambo sio mazuri, kulewa na mambo ambayo yanageuka kuwa kero kwa familia na jamii kwa ujumla. Badala ya kutimiza angalau asilimia kadhaa zakukaa na watoto nyumbani au basi kutoka nao out, mtu anachagua kwenda kula maisha bar na kuwanyima watoto fursa yakuwa pamoja angalau kwa siku moja, ambayo ukiitazama vyema inaweza kuwa inajenga afya ya familia na furaha kwa watoto.
Tuko na mambo mengi kutokana na ulimwengu ulipofikia sasa, mambo mengi na yanamtaka kila mmoja kupambana, lakini bado tunawajibu kama wazazi kuwapa muda angalau wa wasaa kadhaa watoto wetu na familia kufurahia pamoja nasi.
Na hii huleta tabasamu na furaha kwa watoto kwa kuwa pamoja na baba pamoja na mama. Furaha ya watoto ni maombi tosha ya kufanikiwa kwako nakuwa na wiki yenye amani, furaha na shauku ya kutimïza kila jambo lilïlopo kwenye ratiba yako. Maombi ya watoto huwa na maana na nguvu sana kwa wazazi wao, hawawezi kuomba kama kuomba ila tabasamu na kicheko chao ndiyo maombi yao kwa wazazi wao.
Pata muda na familia yako ndiyo msingi wa furaha na mafanikio yako, mambo ni mengi lakini kumbuka kuwa familia ni muhimu sana pia kama ilivyo kazi na mambo mengine ya msingi. Ifanye jumatatu yako kuwa ya furaha kwa kuimalïza wiki na familia pamoja na ibada kwa Mungu wako.
Uwe na jtatu ya Baraka za Mungu.
Mgema  Moses
0755632375/0715366003

Friday, January 8, 2021

JENGA MAHUSIANO BORA NA WATU.

Duniani tunaishi kwa kutegemeana kwa 100% either moja kwa moja au kupitia mlango wa nyuma ila kwa kifupi tunategemeana ili kuweza kuishi na kuziishi ndoto na malengo yetu. 
Kila jambo ambalo mtu anabuni, anafanya liwe ni la burudani, kazi serikalini au sekta binafsi, biashara na shughuli nyingine mbalimbali mlengwa huwa ni mtu.
Hivyo basi jaribu kujenga mahusiano mazuri na bora na watu kwa sababu hujui kesho mtu huyo atakufaa kwa jambo gani. Kuna baadhi ya watu wanasema yeye anafuata mambo yake, yeye jambo la kuhusiana vyema na watu kwake anaona sio jambo la muhimu, ni kweli yawezekana kuna mtu unamwona hana faida wala umuhimu sana kwa sasa ila hujui kesho atakufaa kwa jambo gani.
Watu ndiyo wateja wetu katika biashara zetu, watu ndiyo watazamaji wa burudani na michezo tunayofanya kupitia vipawa na vipaji vyetu, tunaajïliwa maofsïni tageti kubwa ni watu, pasipo watu hakuna raisi, hakuna waziri, hakuna mwanachezo, muigizaji,wala mwanamuziki, kwa ufupi hakuna chochote pasipo watu.
Matajiri kwa masikini tunaamka mapema kwenda kwenye mahangaiko ya kila siku anaetafutwa ni mtu ahudumiwe kwa namna yoyote ile.
Hivyo ni vyema kujenga mahusiano bora na kila mtu, usipende kutengeneza uadui usiokuwa na lazima kwa kupitia lugha chafu za matusi, kupigana, fitina na mambo mengine yasio faa, tafuta amani na kama haiwezekani ni bora ukaondoka ili kulinda utu na hadhi yako kwa sababu hujui huyo mtu unaetengeneza nae uadui atakufaa kesho kwa jambo gani. Najua sio rahisi kuishi na watu wote vyema ila jaribu kuepuka kile ambacho kinaweza kuepukika kwa manufaa ya kesho, usitengeneze ugomvi na mteja wako wa kesho, daktari wako, mwalimu wako, mbunge wako, Raisi wako, mpiga kura wako mfanyabiashara wako nk. kwa sababu bado unaishi hujui nani atakufaa kesho.
Mahusiano bora na watu ndiyo msingi wa mafanikio yako kwa sababu bidii, ujuzi, maarifa bila watumiaji wa hayo yote ni kazi bure. 
Mgema  Moses
mgemamoses@gmail.com
0715366003/0755632375

Wednesday, January 6, 2021

CONNECTION...

Katika dunia ya leo kumekuwa na lawama nyingi kwa baadhi ya watu kwamba kuna sehemu walïstahili kuwepo kwa sababu ya sifa na uwezo ambao wanaamini wanao, wanataaluma, uwezo, maarifa na ujuzi katika mambo mbalimbali ambayo bila shaka yanawastahilisha kuwa sehemu fulani.
Changamoto ambayo wengi wanaamini ndiyo imekuwa sababu ya wao kutokuwepo wanapostahili ni ukosefu wa CONNECTION hawana mtu wa kuwavusha na kuwafikisha kwenye nafasi fulani. Changamoto hii imeanza tangu zamani utamsikia mzee anasema mimi nilikuwa na akili sana lakini kutokana na kukosekana kwa shule, kutokana na umasikini wa familia yangu sikwenda shule yawezekana ningekuwa waziri au mtu fulani mkubwa serikalini.
Hali hii imekuwa mwendelezo wa maisha yetu, wengi ambao hatujapata nafasi tunaamini kuwa hatupo kwenye position fulani, hatuna maisha fulani kwa sababu hatuna watu wakutupa connection/hatuna watu wakutushika mkono.
Ni kweli maisha yetu yanahitaji connection, maisha yetu yanahitaji watu ili kufikia hatua fulani. Pamoja na hayo yote huwezi kubweteka tu nakukaa unalalamika nakulaumu watu eti unakosa nafasi kwa sababu yakukosa nafasi.
Tunapaswa kuelewa kuwa hata hao ambao wanaconnection leo hawakuanza na connection za watu bali uwezo, uthubutu, kujionyesha nakuitangazia dunia kuwa mimi nina hiki kitu cha tofauti nastahili kuwa mahali fulani, hawatasema leo lakini kwenye mioyo yao watakuwa wamekubali, yawezekana wasikutafute leo, ila kesho watakutafuta tu.
Connection ya maana ni uwezo wako, sifa zako katika taaluma na unavyoweza kuifanya taaluma yako kuwa tofauti na wengine. Lawama, malalamiko sio suluhisho la kukufanya upate unachotaka.
Kumbuka kama huna mtu wakukutia birikani wewe unawajibu wakujitia birikani hata kama ni kwa kujivuta, dunia ya leo inahitaji utofauti wako ili wakupe connection, kama huna mtu pale mbele, ufanye uwezo wako, kipaji chako, taaluma yako kuwa connector, jionyeshe, iambie dunia kuwa mimi nina hiki chatofauti, sio kwa maneno bali kwa matendo na matokeo ya kazi yako hata kama ni ndogo, wenye akili wataona tu, hata kama hawatakuambia ila kumbukumbu zitabaki kichwani.
Jitambulishe hata kwa lazima, walazimishe watu wakujue wewe una uwezo gani, halafu kila kitu cha uwezo wako kifanye kwa uwezo wa kiwango ch juu sana, kama wewe ni mwimbaji, mtangazaji, mwandishi, photographer, videographer etc hata kama ni bure fanya kwa kiwango kama kuna dau nono mbele yako, ukienda kufanya Interview fanya, usionyeshe huruma ili watu wakuhurumie, umasikini wako sio sababu ya watu kukupa kazi au nafasi kweye jambo fulani, watu wanahitaji uwezo wako tu. Huruma peleka nyumbani kwa wazazi watakuhurumia, wala watu hawakuhitaji wewe wanauhitaji ujuzi, maarifa na uwezo wako period
Mgema Moses.
mgemamoses@gmail.com
0715366003/0755632375

NYAKATI ZOTE NI BORA KWENYE MAISHA YETU.

wakati mwingine sio rahisi kueleweka na baadhi ya watu kutokana nakuwa na fikra na mitazamo tofauti juu ya mambo mbalimbali ya maisha. Ila ukweli ni kwamba NYAKATI ZOTE KWENYE MAISHA NI BORA bila kujali ni ngumu, chungu au nyepesi na tamu.
Kuna nyakati unapitia kwenye maisha mpaka unafikiri kuwa Mungu amegeukia ukutani au hayupo kabisa, unapitia mambo magumu kana kwamba uliwahi kumkufuru Mungu, au wewe ni mvivu, na hautimizi majukumu sawasawa, kila jambo unalojaribu kufanya halifanikiwi, mengine hayafanikiwi wakati una sifa na vigezo vyakuwa navyo au kuvifanya.
Una Elimu ila kila ukiomba kazi hufanikiwi sio kwa sababu umefanya vibaya kwenye usaili, unafanya kazi kwa bidii, biashara, unaongeza na ubunifu, kauli nzuri kwa wateja nk. lakini ndo kwanza unadidimia nakurudi nyuma, unafanya ibada na umwaminifu mbele za Mungu lakini kwanza ni kama vile uko jangwani.
Wengeni kila wakigusa jambo kwao ni vema na mafanikio, ana każi lakini akiomba kazi nyingine anapata madili yanamfuata, lakini wewe hata ukipata hela, utasikia mke ana umwa, mama anachangamoto fulani ni kama dunia iko kwako yote, kuna mahali umekata tamaa kabisa.
Nikukumbushe kuwa wewe ni bora sana,kuna kitu Mungu anakijenga kwako, kuna jambo Mungu analitaka kwako, Mungu anajua wewe ni zaidi ya vile ulivyo, anakujua vyema, anajua kama atayafanikisha mahitaji yako mapema kwa wakati unaotaka wewe kuna vitu ?hautavifanya kwa ubora na uwezo anaoutaka Mungu, maana utaridhika na kubweteka, labda utawadharau wengine, hautatambua kuwa ulipo ni kwa sababu ya Mungu ni kwa uwezo wako.
Kuna nyakati zakukufanya wewe kuwa ile dhahabu pure ambayo ikiingia sokoni kila mhitaji ataigombania, Mungu anakutaka wewe bora sio wewe unavyojitaka ....waoo kumbe bado hujawa tayari kuwa yule Mungu anamtaka
Turudi kwa Yusuph, habari hii huwa ina ujumbe mkubwa sana kwetu kujifunza kwa mfano, tazama pia mchakato na mapito ya Daudi kabla ya yeye kuwa Mfalme, alifanyiwa kila jambo gumu, lakini kumbe Mungu alikuwa anamwandalia hatima iliyo bora sana, kutukanwa na ndugu zake, kutokubalika, kutupwa shimoni, kuuzwa na kufungwa gerezani vyote hivyo vilikuwa vinamtafuta Yusuph pure/halisi...
Nyakati ngumu ni daraja la kukupeleka kwenye ubora wako, hivyo usijutie nyakati ngumu zifurahie ila usiridhike kuwa hapo, pambana huku ukijua malipo ya juhudi ni faida isiyo na mwisho
Mgema Moses

Monday, January 4, 2021

BADILI MBINU ZA MAPAMBANO ILA SIO MALENGO, MAONO NA NDOTO YAKO.

Asilimia kubwa ya vijana Afrika husimama pekee yao.wazazi wengi wakishasomesha au ukishafikisha umri wa miaka 18 na hukufanya vizur kwenye masomo ndiyo muda wa mzazi kuachana na wewe, bila kujali una mtaji wakuanzia au la, kwa sababu tu umefikia hayo maeneo mawili, moja ulimalïza darasa la saba/kidato cha nne na haukufanikiwa kuendelea ngazi zinazofuata au baada ya chuo kwa waliofika hatua hiyo mzazi anakuwa amemaliza na wakati mwingine kuanza kudai marejesho ya kazi yake.

Hii inachangiwa na mtazamo wa watu wengi kuamini baada yakusomesha lazima asaidiwe na mtoto bila kujal ana nguvu au amezeeka, maisha duni ya familia zetu nk.Baadhi wanamaliza masomo yao wanakuta mazingira yako sawa, kazi ameandaliwa maana mzazi ana connection, ana kampuni yake, au ana mtaji wakumfungulia biashara nzuri mtoto wake. 

Haya ndiyo maisha yetu huwa tunatofautishwa na mazingira ya nyumbani wakati mwingine, wakati wengine ufaulu wa masomo sio kigezo chakupata kazi, wengine wanalazimika kupata alama zajuu ilikuwashawishi waajiri na serikali kuwapatia ajira kama mtaji wa kwanza wakuyaanza maisha.

Tuna ndoto na malengo, lakini wakati mwingine tunaanzia mbinu ya muda mrefu kwenye soka tunasema inabidi kuanzia lamansia, kuwa na mbinu ya Grass root kutengeneza wachezaji wa gharama ndogo ili miaka ijayo watufae katika kuyatimiza malengo na ndoto za team yetu.
Wengine wanamfumo wa Real Madrid, PSG, chelsea, man utd na man cïty, wana uwezo wakuchukua cream safi tayari kwa matumizi.

Unataka kuwa mfanyabiashara mkubwa lakini huna mtaji, ukienda benki wanadai hati ya kiwanja, serikalini mikopo haitoshelezi au mnahitakika watu wengi ili mpate milioni kumi, tańo au moja ili mgawane. Mazingira hayo yanakulazimisha kufanya kama umeisahau ndoto yako kwenda kumtumikia mwingine ïĺi kujenga misuli ya uchumi ndiyo uanze kuïfukuzia ndoto yako. 
Rafiki yangu kubali tu kuanzia huko ila isiwe sababu yakuyasaliti maońo, ndoto na malengo yako kwa msala upitao.Pambana jenga mtaji ila fahamu ulichepuka ili kwenda kujenga msingi imara wa kuyaweka maońo yako.
Kwa kila hali tupambane ila tusisahau kuwa tuna maono, ndoto na malengo ambayo hatupaswi kuyasaliti. Badili mbinu ila usibadili malengo na maono yako
Mgema Moses
Mwaka 2011 nilifika St. Augustine University Jijini kwa mara ya kwanza kumsalimia kaka yangu George aliyekuwa akisoma hapo chuoni. Baada yakufika chuoni, nilivutiwa sana na mazingira ya chuo, pamoja na namna ambavyo kilikuwa kinapendeza, lakini hata baada yakufuatilia taarifa za ndani kabisa nikavutiwa sana na nilifanya maamzi kwamba baada ya masomo ya Advance ilikuwa lazima katika chuo hicho.
Mwaka 2013 ndiyo ulikuwa mwaka ambao nilipaswa kuanza masomo yangu ya chuo, lengo na mpango wangu haikuwa chuo kingine hapa nchini isipokuwa St. Augustine. Mchakato ulipofanyika nikama niliingiwa na roho yakutokujiunga na chuo, lakini rafiki yangu Jose Mdamanyi alinishauri nijiunge na chuo, lakinï muda wakutuma maombi ulikuwa uko ukingoni, lakini alijitahidi mpaka akafanikiwa kutuma maombi ya chuo. Baada ya wiki mbili baadhi ya majina yalirudi 

Sunday, January 3, 2021

WEWE SI UNAISHI LEO, WEWE UTAISHI KESHO.

Kuna mawazo yanakujia kwenye ufahamu wako na wakati mwingine yanakutia unyonge kwa sababu ni kama unaona umeshatumia kila njia ili kufikia malengo yako lakini inaonekana ni ngumu kufikia kusudi la juhudi zako, umefika mahali picha kubwa inakujia kichwani mwako kuwa wewe uko kwenye fungu la kukosa..........
Hapana wewe ni shujaa, wewe ni uwekezaji wa Mungu, kuna kitu cha tofauti umebeba ndani yako, wewe ni ardhi ambayo ndani yake imebeba utajiri mwingi wa madini, nani mgunduzi na mchimbaji, bado hajapatikana, nani atakuja kugundua kuwa katika ardhi wewe umehifadhi madini ambayo bado hayajagundulika...
Baba na mama walishindwa kugundua mapema, bahati mbaya kuanzia mwalimu wako wa chekechea hadi chuo kikuu hajafanikiwa kugundua madini yaliyo katika ardhi wewe, Jirani na mtaa kwa ujumla nao umeshindwa kugundua nakutambua kwenye ardhi wewe kuna madini yanayosubiri kugunduliwa na kuanza kuchimbwa.
>Kuna majiolojia wachache wamefahamu kuwa ardhi wewe umehifadhi madini lakin bahati mbaya wamepatwa na woga kuwekeza mitaji yao kwa kuhofia kula hasara kwa sababu serikali haina swalia mtume, muda wa janja janja umekwisha, TRA na serikal wako macho kudai chao mapema ingawa kwa sasa ni kama hawaoni....
Nani mwekezaji mwenye uthubutu, mwekezaji mwenye kufuata kanuni na taratibu za serikali ïli akipata kibali cha kazi kesho asiletewe taabu, nani yuko tayari kuwekeza fedha muda, kwa manufaa ya kesho, nani ambae haionei serikali wivu kwamba mimi niweke mtaji wangu halafu tuje tuvune wote faida...
Uwezo ulio nao, hujaugusa, wazazi, ndugu, marafiki, walimu na jamii kwa ujumla hawakutambua uwezo huo. Ni wakati wako kukaa chini na kujitathimini ili kujigundua uwezo wako, ukifanikiwa kujigundua basi wewe si wewe unaishi sasa, wewe ni yule ambae alikusudiwa na Mungu ambae aĺiweka uwezo wa kipekee ndani yako. Kwa sababu hujaishi leo umebaki kuzurura, Wewe wa Mungu anakutegemea uishi kesho.
Rudi kwenye kiti, jisome, jitathimini ndiyo njia sahihi yakujifahamu na ukishajifahamu ndiyo utakuwa umefika muda wa kuishi ndoto na maono yako, kubali kurudi kwenye kiti na meza ya tathimini kule mahali pautulivu.
Mgema Moses

Friday, January 1, 2021

MIPANGO, MALENGO NA MIKAKATI

MWANZO MPYA BAADA YA COVID19, 2020

2020 Umekuwa ni mwaka ambao umeacha alama na historia kubwa kwa ulimwengu, kutokana na kulipuka kwa ugonjwa wa Covid19 ambao umekuwa na madhara na matokeo hasi kwenye maisha ya watu wengi Duniani.Nyanja zote za maisha ziliguswa, kuanzia maisha ya watu, tumepoteza ndugu, rafiki, jamaa zetu wakaribu,  mfumo wa ajira, watu wamepoteza ajira zao kutokana na kuyumba kwa mifumo ya uendeshaji wa makampuni hasa sekta binafsi, biashara nk.
Pamoja na hayo Mungu hata sasa anabaki kuwa Shujaa wetu maana ametupigania natuko salama 
Inawezekana hali hii ilibadili mwelekeo na malengo yako maana ilikuwa hali isiyotegemewa, imetokea hatuwezi kulaumu bali imetuachia funzo na darasa tumejifunza.
Kupitia changamoto hii naamini imekuimarisha na kukupa nguvu mpya tena, Na sasa uko tayari kwa mapambano ya mwaka huu wenye ishara ya mwanzo mpya kwa sababu unaanza na 1, kwa ufupi yakale yamepita na huu ni ukurasa mpya wenye matumaini mapya, Naamini umekaa chini umeweka mipango yako sawa na uko tayari kwa 2021.
Mungu ukupe nguvu mpya, maarifa na shauku yakufanya kazi kwa bidïï ili kufikia malengo yako
Mungu akubariki sana 
2021 Is the year of Greatness.
Mgema Moses.