Monday, January 4, 2021

BADILI MBINU ZA MAPAMBANO ILA SIO MALENGO, MAONO NA NDOTO YAKO.

Asilimia kubwa ya vijana Afrika husimama pekee yao.wazazi wengi wakishasomesha au ukishafikisha umri wa miaka 18 na hukufanya vizur kwenye masomo ndiyo muda wa mzazi kuachana na wewe, bila kujali una mtaji wakuanzia au la, kwa sababu tu umefikia hayo maeneo mawili, moja ulimalïza darasa la saba/kidato cha nne na haukufanikiwa kuendelea ngazi zinazofuata au baada ya chuo kwa waliofika hatua hiyo mzazi anakuwa amemaliza na wakati mwingine kuanza kudai marejesho ya kazi yake.

Hii inachangiwa na mtazamo wa watu wengi kuamini baada yakusomesha lazima asaidiwe na mtoto bila kujal ana nguvu au amezeeka, maisha duni ya familia zetu nk.Baadhi wanamaliza masomo yao wanakuta mazingira yako sawa, kazi ameandaliwa maana mzazi ana connection, ana kampuni yake, au ana mtaji wakumfungulia biashara nzuri mtoto wake. 

Haya ndiyo maisha yetu huwa tunatofautishwa na mazingira ya nyumbani wakati mwingine, wakati wengine ufaulu wa masomo sio kigezo chakupata kazi, wengine wanalazimika kupata alama zajuu ilikuwashawishi waajiri na serikali kuwapatia ajira kama mtaji wa kwanza wakuyaanza maisha.

Tuna ndoto na malengo, lakini wakati mwingine tunaanzia mbinu ya muda mrefu kwenye soka tunasema inabidi kuanzia lamansia, kuwa na mbinu ya Grass root kutengeneza wachezaji wa gharama ndogo ili miaka ijayo watufae katika kuyatimiza malengo na ndoto za team yetu.
Wengine wanamfumo wa Real Madrid, PSG, chelsea, man utd na man cïty, wana uwezo wakuchukua cream safi tayari kwa matumizi.

Unataka kuwa mfanyabiashara mkubwa lakini huna mtaji, ukienda benki wanadai hati ya kiwanja, serikalini mikopo haitoshelezi au mnahitakika watu wengi ili mpate milioni kumi, tańo au moja ili mgawane. Mazingira hayo yanakulazimisha kufanya kama umeisahau ndoto yako kwenda kumtumikia mwingine ïĺi kujenga misuli ya uchumi ndiyo uanze kuïfukuzia ndoto yako. 
Rafiki yangu kubali tu kuanzia huko ila isiwe sababu yakuyasaliti maońo, ndoto na malengo yako kwa msala upitao.Pambana jenga mtaji ila fahamu ulichepuka ili kwenda kujenga msingi imara wa kuyaweka maońo yako.
Kwa kila hali tupambane ila tusisahau kuwa tuna maono, ndoto na malengo ambayo hatupaswi kuyasaliti. Badili mbinu ila usibadili malengo na maono yako
Mgema Moses

No comments:

Post a Comment