Friday, January 1, 2021

MWANZO MPYA BAADA YA COVID19, 2020

2020 Umekuwa ni mwaka ambao umeacha alama na historia kubwa kwa ulimwengu, kutokana na kulipuka kwa ugonjwa wa Covid19 ambao umekuwa na madhara na matokeo hasi kwenye maisha ya watu wengi Duniani.Nyanja zote za maisha ziliguswa, kuanzia maisha ya watu, tumepoteza ndugu, rafiki, jamaa zetu wakaribu,  mfumo wa ajira, watu wamepoteza ajira zao kutokana na kuyumba kwa mifumo ya uendeshaji wa makampuni hasa sekta binafsi, biashara nk.
Pamoja na hayo Mungu hata sasa anabaki kuwa Shujaa wetu maana ametupigania natuko salama 
Inawezekana hali hii ilibadili mwelekeo na malengo yako maana ilikuwa hali isiyotegemewa, imetokea hatuwezi kulaumu bali imetuachia funzo na darasa tumejifunza.
Kupitia changamoto hii naamini imekuimarisha na kukupa nguvu mpya tena, Na sasa uko tayari kwa mapambano ya mwaka huu wenye ishara ya mwanzo mpya kwa sababu unaanza na 1, kwa ufupi yakale yamepita na huu ni ukurasa mpya wenye matumaini mapya, Naamini umekaa chini umeweka mipango yako sawa na uko tayari kwa 2021.
Mungu ukupe nguvu mpya, maarifa na shauku yakufanya kazi kwa bidïï ili kufikia malengo yako
Mungu akubariki sana 
2021 Is the year of Greatness.
Mgema Moses.

No comments:

Post a Comment