Wednesday, January 6, 2021

NYAKATI ZOTE NI BORA KWENYE MAISHA YETU.

wakati mwingine sio rahisi kueleweka na baadhi ya watu kutokana nakuwa na fikra na mitazamo tofauti juu ya mambo mbalimbali ya maisha. Ila ukweli ni kwamba NYAKATI ZOTE KWENYE MAISHA NI BORA bila kujali ni ngumu, chungu au nyepesi na tamu.
Kuna nyakati unapitia kwenye maisha mpaka unafikiri kuwa Mungu amegeukia ukutani au hayupo kabisa, unapitia mambo magumu kana kwamba uliwahi kumkufuru Mungu, au wewe ni mvivu, na hautimizi majukumu sawasawa, kila jambo unalojaribu kufanya halifanikiwi, mengine hayafanikiwi wakati una sifa na vigezo vyakuwa navyo au kuvifanya.
Una Elimu ila kila ukiomba kazi hufanikiwi sio kwa sababu umefanya vibaya kwenye usaili, unafanya kazi kwa bidii, biashara, unaongeza na ubunifu, kauli nzuri kwa wateja nk. lakini ndo kwanza unadidimia nakurudi nyuma, unafanya ibada na umwaminifu mbele za Mungu lakini kwanza ni kama vile uko jangwani.
Wengeni kila wakigusa jambo kwao ni vema na mafanikio, ana każi lakini akiomba kazi nyingine anapata madili yanamfuata, lakini wewe hata ukipata hela, utasikia mke ana umwa, mama anachangamoto fulani ni kama dunia iko kwako yote, kuna mahali umekata tamaa kabisa.
Nikukumbushe kuwa wewe ni bora sana,kuna kitu Mungu anakijenga kwako, kuna jambo Mungu analitaka kwako, Mungu anajua wewe ni zaidi ya vile ulivyo, anakujua vyema, anajua kama atayafanikisha mahitaji yako mapema kwa wakati unaotaka wewe kuna vitu ?hautavifanya kwa ubora na uwezo anaoutaka Mungu, maana utaridhika na kubweteka, labda utawadharau wengine, hautatambua kuwa ulipo ni kwa sababu ya Mungu ni kwa uwezo wako.
Kuna nyakati zakukufanya wewe kuwa ile dhahabu pure ambayo ikiingia sokoni kila mhitaji ataigombania, Mungu anakutaka wewe bora sio wewe unavyojitaka ....waoo kumbe bado hujawa tayari kuwa yule Mungu anamtaka
Turudi kwa Yusuph, habari hii huwa ina ujumbe mkubwa sana kwetu kujifunza kwa mfano, tazama pia mchakato na mapito ya Daudi kabla ya yeye kuwa Mfalme, alifanyiwa kila jambo gumu, lakini kumbe Mungu alikuwa anamwandalia hatima iliyo bora sana, kutukanwa na ndugu zake, kutokubalika, kutupwa shimoni, kuuzwa na kufungwa gerezani vyote hivyo vilikuwa vinamtafuta Yusuph pure/halisi...
Nyakati ngumu ni daraja la kukupeleka kwenye ubora wako, hivyo usijutie nyakati ngumu zifurahie ila usiridhike kuwa hapo, pambana huku ukijua malipo ya juhudi ni faida isiyo na mwisho
Mgema Moses

No comments:

Post a Comment