Thursday, February 4, 2021

Ushindi ni ahadi ya Mungu kwa wanadamu, tuĺiumbwa tukiwa na nguvu ya ziada, tabia tofauti na viumbe wengine, tunautashi, tunasifa ya Mungu, hivyo basi kama tunasifa za Mungu maana yake kama alivyo yeye ni mshindi hata mimi na wewe ni washindi.
Ushindi wa mtu huanzia kwenye ufahamu, namna mtu anavyofikiri, anavyojitazama, anavyojiona na imani ya uwezo iliyo ndani yako/yangu. Jambo hili limekaa katika mfumo na mtazamo wa kiimani zaidi kama mtu hajafungua mtazamo wake vyema katika mukhutaza wa maisha yetu ya kila siku.
Kushinda na kushindwa ni mambo mawili ambayo yametenganishwa na uzi mwembamba sana, mentality na imani ya mtu juu ya vile ajionavyo kuanzia kwenye mfumo wa ufahamu wake...
Kuna stori moja inazungumzwa kwenye kitabu cha Joshua, kuna watu walitumwa mahali kwenda kuipeleleza nchi na walipofika huko walikuta watu wakubwa sana, katika kurudisha ripoti kwa aliyewatuma kundi la kwanza lilisema wamefika huko wameona majitu sasa sio watu ila majitu ambayo yaliwafanya wao kujiona kama mapanzi.
Kundi la pili likaja na ripoti yake ambayo ilikuwa imesheheni imani, ujasiri na nguvu ya ajabv kwamba wameona uwezekano wa kuivamia ile nchi na kuiteka nakuwa mali yao. Ndani ya kundi la watu kadhaa wamegawanyika mtazamo wapo wameona ushindi wengind wameshaona haiwezekani hata kidogo sisi ni mapanzi tu.

No comments:

Post a Comment