Tuesday, December 11, 2018

YOUR THE LIVING TESTIMONY/WEWE NI USHUHUDA UNAO ISHI.

Habari.
Mungu akubariki sana kwa kuendelea kuamini katika mfumo wa mabadiliko na mapinduzi ya fikra.

Mtu anae amini katika uwezo wake bila kujali mazingira, watu wanaomzunguka, hali ya kimaisha, Kielimu, kiimani na kadhalika mara nyingi mtu wa namna hii hufanikiwa sana kwenye maisha.

Mara nyingi huishi kwenye ndoto yake, malengo yake bila kujali amefikia ndoto na malengo hayo akiwa kwenye umri upi mwanzo kati au mwisho.

Mtu wa namna hii huwa hawaogopeshwi na hali yake, mazingira ila anachokiamini ni ule uwezo ulio ndani yake na kuamini kupitia uwezo huo ndiyo sababu ya yeye kuishi ndoto zake.

Sababu kubwa inayomfanya awe hivyo ni kuamini kuwa hakuna mtu aliumbiwa kuishi maisha ya hali fulani milele (uduni) na wengine kuwa na hali nzuri za kimaisha (utajiri).

Kupitia changamoto anazopitia humjengea shauku na imani kubwa ndani yake, kwamba kama wazazi wangu walishindwa kusapoti taaluma yangu kwa sababu ya Maisha duni,  umasikini wa kutisha basi, soluhisho la kuachana na hali hii duni, nikutumia uwezo mkumbwa ndani yangu kama daraja halisi la kunivusha hapa nilipo leo kwenda hatua bora zaidi ya kimaisha.

Hakuna kitu kizuri kama kuamini uwezo wako bila kujali wangapi wanakuona unajifurahisha, huwezi kufika popote  pale.

kuna watu wanavipaji katika maeneo tofauti tofauti ambao walipitia changamoto za kudharauliwa na kuonekana si chochote lakini kwa sababu waliamini walichonacho basi walipambana leo hii imebaki historia vijijini kwao na kuwaacha waandika historia za watu wakiendelea kujinasibu kuwa wanawajua sana huku wao wakila vyuku na bata mijini.

UMEWAHI KUJIULIZA UNA UWEZO GANI ?
Hili ni swali nyeti sana na muhimu kujiuliza hasa kwenye kipindi hiki cha ulimwengu kuamka na kutaka kila mtu kufanikiwa.
Mungu ameniumba mimi nikiwa na uwezo fulani, wewe pia...lakini je umeshatambua ?

Historia huandikwa na wengi lakini sababu ya historia kuandikwa na wengi kama hujua basi jua leo kuwa ni wewe.
Waandishi, marafiki ndugu  majirani na taifa kwa ujumla wanatamani kukusubilia wewe kwenye viwanja cha ndege vya  KIA au Julius k. Nyerere ukitoka nchi fulani ughaibuni kuiwakilisha nchi kwenye kwenye mashindano  fulani na hapo hapo una medani ya mashindano  hayo.

Ninachokijua na kukiamini ni kwamba kila jambo linawezekana kuandikwa kwa kusema wewe ni mshindi na mshindi ni yule ambae alitambua na kutumia uwezo wake ipasavyo.

Wewe ni ushuhuda unaoishi amini hivyo na jambo la msingi la kufanya ni wewe kujitafuta na kugundua uwezo wako uko kwenye eneo gani.

Kuandika, kucheza mpira, kuimba, kuigiza, kuongoza, kuongea, kucheza, kushauri, kushawishi, kuchora, kutawala eneo lolote, kufanya kazi na kufanya jambo la uwezo wako ni maeneo ambayo unaweza wekeza nakujitambulisha duniani kuwa wewe ni nani.

Wakati dunia ikimjua Bwana Samatta, Thomas ulimwengu, Diamond, Ally Kiba, Paul Clement, Joel Lwaga, Joel Nanauka, Eric Shigongo, Donie Moen, Mr Bin, Steven kanumba na jamii kutengeneza shauku ya kuwatazama basi hawa ndugu wanatengeneza fedha na utajiri wa kutisha sana.

Nini ulichonacho je unakijua je umepata njia ya kuiambia dunia kuwa wakati Mungu anaruhusu uje duniani alikupa uwezo fulani kwa ajili ya wanadamu kupata sababu ya kukupa fedha wakikutazama,  wakihangaika na mitandao kugugo ili wajue leo umefanya nini, nakinunua magazeti ili tu wajue una nini ?.....swali kubwa na muhimu sana kujiuliza.

Bado nina nafasi, bado una nafasi kaa chini jitathimini jiulize je umetumia kipaji chako kwa manufaa yako.
Nilipokuwa nikisoma historia ya Mwandishi Joel Nanauka na Eric Shigongo ndiyo mahali ambapo nilijua unaweza kuwa The living testimony kama ukijua thaman yako.

Nilikuwa nasoma tena na kusikiliza jitihada za Diamond, Mbwana Samatta, Watoto au wachezaji kutoka America ya kusini na wengine wengi ndipo nilipojua kuwa hakuna mtu ambae hana uwezo wa asili au (Natural ability) ambayo inaweza badilisha maisha yake.

Usikatishwe tamaa kuna wakati unapambana kwa bidii lakini mazingira sio rafiki,umasikini lakini mwisho wa siku Mungu hubariki sana mikono yenye bidii hasa kwenye eneo la kusudi lako.
Mbwana Samatta amelala sana kinesi, Uhuru stadium yote haya aliyafanya akiwa mbagala na alikuwa anawahi sana toka nyumbani ili program ya mazoez ya simba asikose hata point leo imebaki records kwenye vitabu ila yeye yuko ulaya.

Diamond, Harmonize na wengine wengi wamepambana sana kuwa mahali walipo leo jiulize wao waweze wana nini na wewe ushindwe una nini......Your the living Testimony jitambue.

Unaweza jiulize mimi nina nini.....ntakujibu mimi ni Ushuhuda unao ishi mwishoni mwa mwaka ujao utajua bila kusimuliwa kwa nini mimi ni The living testimony.

Hata wewe unaweza jipambanue, unaweza kuwa fulani kupitia kipaji chako, kazi unayofanya, biashara, kilimo na eneo lolote lile ulilopo ukishajitambua tu na kutambua thamani ya kile umekibeba ndani yako...
Mazingira, marafiki hukarii aina fulani fulani ya maisha, hapo ulipo unaweza nyanyuka vizuri kabisa acha visingizio pambana ongeza maarifa ujuzi na kupata wingi wa maarifa kwa kuendelea kusoma ili usiwe nje ya track.
Mgema Moses
P.o.box 166....
0755632375

Sunday, December 2, 2018

HONGERA SAMSON ERNEST KWA KUWA MFANO KWETU

Hongera katibu kwa uthubutu ambao hakika bado inatupa changamoto vijana wengine.
Chepeo ya Wokovu imeanza kama utani lakini leo ni moja ya website inayokuwa kwa kasi sana.
Kidogo kidogo leo umekuja na notebook, calendar kesho kitu kingine
Maisha yanahitaji sana, maamzi, bidii na juhudi, kujituma na kufanya kile ambacho unahisi ni sahihi kwa wakati sahihi, nidhamu, maarifa sahihi lakini ya kutosha, socialization. Juu yote haya Mungu lazima awe mbele kabisa maana ndo anahesabu kila hatua ya kila mtu.
Wakati najiunga na kundi la chepeo ya wokovu Facebook lilikuwa ni kundi dogo sana lakini leo ni kundi kubwa sana.

kila jambo lina vikwazo vyake kama vile  kukatishwa tamaa, watu kukuambia wewe huwezi, walikuwa kina fulani wakashindwa ije iwe wewe wapi..... vitu kama hivyo ni changamoto kwenye njia ya kila mtu lakini mwisho wa siku lazima uitambue focus na nia yako ni nini hapo ndipo unaweza thubutu na ukafanya kwa vitendo na vitendo vikaonekana kwenye matokeo.

Kalenda, Notebook vinaweza onekana ni vitu vidogo sana kwa Mtazamo wa watu wengi lakini kiufupi hili ni jambo kubwa sana ambalo kila mwenye akili anapaswa kulipongeza angawa kupongeza au kutokupongeza ni uamzi wa mtu Binafsi.
Vijana wezangu ni wakati wa kuamka na kutumia kila fursa inayopatikana Mbele yetu au kwenye mazingira yetu ili tuweze kuondoka kwenye maisha tuliyonayo kwa sasa.
Wakati wa kukaa tu, kulaumu, kuponda na kudharau na kujiona mwenye hadhi fulani huwezi kufanya mambo fulani umepotea na wakati ukiendelea kukaa kwenye mtazamo huo utajikuta unabaki mwandika historia za watu, kwamba huyu amekuwa tunamwona,tumesoma nae, amesoma hapahapa au amekuja akiwa hivi huku wenzako wameshasepa na maisha yao yako juu tayari.

Katibu ni somo kubwa sana kwangu, alinieleza alikoanzia mpaka alipo leo hakika ni mfano wa kuigwa sana ni mtu mpanaji asie kata tamaa, anafanya kazi sana, ana nidhamu sana kazini lakini ni mtu mwenye malengo makubwa, anaamini katika kile kidogo anapata ndicho kinaweza kumfanya akawa na kikubwa kesho.

Huwezi kuwa fulani kesho kama unakosa uthubutu, bidii, nidhamu katika kile kidogo unachopata, lakini bila malengo na nia ya dhati toka moyoni.
Kila mtu ana fursa kila mtu ana muda sawa na mwingine lakini namna ambavyo tunaweza kutumia huo muda.

Fedha watu tunapata lakini namna ya mgawanyo na matumizi ya hiyo fedha wapi unawekeza ni changamoto nyingine ambayo inatukumba vijana wengi, jitahidi kuheshimu kila kile kido unachopata ili kikufanye uwe na uwezo wa kusogea kesho huku ukijua kuwa hakuna siku utakuja kuwa na pesa nyingi kiasi kwamba utaanza kung'aa juu kwa juu ila katika vichache tunachopata ndicho chaweza kuleta kikubwa
Samson Ernest ni darasa kubwa sana kwa vijana wa Fpct Singida Mjini hakuna ubishi wala mashaka. Najua wapo wengi wamefanikiwa lakinikwangu mimi huyu ni mfano kwa vijana wengi
Tabua Thamani yako, tumia muda penda kujifunza ili kuongeza maarifa na ujuzi kwa ajili ya kuendelea kuwa bora

Sunday, November 18, 2018

MAISHA YA MAFANIKO HAYAHITAJI UDHURU.

Kuna wakati na nyakati unaweza ukawa unazipitia mpaka ukahisi hakika duniani kuna watu wamepangiwa kuwa na maisha mazuri na wengine maisha mabaya.

Maana kila jambo ambalo unakuwa unafanya ni kama haliendi kabisa daa....una kaa chini unawaza, unapanga mambo mengi lakini mwisho wa siku unaona ugumu kabla hata hujajaribu kufanya jambo lenyewe.

Ingawa kuna wakati unajitahidi  kufanya baadhi ya mambo lakini bado naamini hujajitoa kwa asilimia mia moja kabisa kufanya jambo hilo either kazini au kwenye biashara zako binafsi

Kitabu  kimoja niliwahi kukisoma kilichoandikwa na Brian aliandika mambo mengi sana ambayo kwa kweli binafsi yamenifikisha hapa nilipo leo japo bado sijafika ila kuna vitu tayari vimeanza kuthihirika kwangu baada ya kuanza kujitoa

Mwandishi Brian mwandishi wa Kitabu alielezea mambo mengi kwenye maeneo kama haya,  tabia za mtu ambazo zinamrudisha nyuma kufanya makubwa, ambazo kama tukikubali kuziacha leo na kuanza tabia mpya itaenda kutupelekea  Brian Amegusa umuhimu wa NIDHAMU BINAFSI na mambo ya kufanya ili uwe na hiyo nidhamu binafsi.

Kuna vitu au mambo kadha wa kadha ambayo ukiyafanya au ukiyabadilisha yawe katika mwelekeo chanya hakika kuna mwelekeo mwema utashika kwenye njia na mwelekeo wako wa mafanikio.

Unajua kuna vitu huanzia ndani namna unawaza, unafikiri na unavyotazama na kujigrede wewe kama wewe kule ndani. Yaani unajionaje, shauku ya moyo wako nini basi yote hayo yanaweza kuathiri matokeo ya nje either chanya au hasi.

Tutazame mambo haya kama yanaweza kuwa na manufaa kwako kama ambavyo yamefanikiwa kuwa na matokeo chanya kwa upande wangu.

Mafanikio yoyote yale ukiacha mitazamo, juhudi, maarifa na channel mbalimbali ambazo unazo basi ambatanisha na mambo yafuatayo kama ambavyo mwandishi amejaribu kuelezea kwa ufasaha.

1. Kiwango cha nidhamu kuanzia ndani inavyoweza kuathili hadi tabia yako ya maisha ya kila siku.

Nidhamu ni hali ya kuheshimu na kufuata ratiba, mipango na malengo yako ambayo umepanga kufanya kwa kipind fulani bila kujali changamoto yoyote ambayo unaweza kuwa inakukabili wakati unatekeleza mambo yaliyo ndani ya ratiba yako.

Katika mfumo wa maisha tulio nao kwenye karne hii, ili upate mafanikio lazima ujijengee nidhamu ya hali ya juu sana katika kutekeleza kila unalopanga, na lazima nidhamu uifanye kuwa msingi wako.

2. Tabia.
Nidhamu hujenga tabia, hivyo kama huna nidhamu utakuwa na tabia mbaya zisizo eleweka na ukiwa na nidhamu basi hakika utafikia malengo na ndoto zako.

Ukiona, huna ujasiri katika maisha yako, hujiamini katika kila unachokifanya basi jua wewe bado  ni mtu dhaifu sana, huwezi kuongea mbele za watu ukasikilizwa na kila unalofanya unaona unakosea, rudi nyuma ujitathimini upya. Jiulize je, ni mtu mwenye NIDHAMU katika mambo yangu ya kila siku ?

Tabia, ni kitu gani?
Ni mwenendo wa maisha yako, ni mjumuisho wa unachokisema na kukitenda kuanzia kwako binafsi hata mbele za watu tofauti tofauti bila kujali hadhi zao.

Mtu mwenye tabia bora, ni yule anae kiishi kile anacho kisema. Mfano kama unasema kesho nitaanza kutekeleza majukumu yangu saa moja asubui lazima kweli muda huo unapofika unapaswa kuwa kwenye eneo la kazi ili kwendana na muda ulio panga jana nje na hapo nidhamu yako itakuwa ya hovyo maana umeenda nje na mapatano yako mwenyewe.

Vile vile itamaanisha kuwa huwezi kuishi unachosema, na hiyo tabia ni mbaya na haitakufikisha kwenye mafanikio makubwa unayoyatamani

Njia pekee ya kujitengenezea sifa bora, ni kuwa na tabia bora lakini tabia bora msingi wake ni Nidhamu binafsi.

Nidhamu binafsi, Tabia bora, sifa njema, bidii, maarifa na ujuzi  hekima na busara maombi kwa Mungu wa kweli na Imani basi jawabu lake  ni mafanikio na matokeo makubwa.

Ukifanya yote hayo basi  hakuna wa kuzuia kufanikiwa kwako katika maisha. Lakini pia fahamu kuwa ukifanya bidii ofsini au kazini  kwako lazima upate promotion ya kupandishwa cheo. Kwenye  biashara yako lazima iwe na wateja wakutosha kabisa na utapata faida kubwa maana unatembea kwenye misingi ya nidhamu

3. Tabia njema inapelekea na  Uadilifu(Integrity). Ndugu yangu fahamu tunapozungumzia Nidhamu binafsi, siyo kitu kirahisi sana, ila ni kitu kinachowezekana hasa unapoamua kutoka ndani ya moyo wako kwa dhati.

Ukiweza kuwa na nidhamu binafsi lazima uwe mtu mwenye sifa njema kila unapokanyaga na itakujengea uadilifu wa hali ya juu kuanzia kwako wewe hata kwa watu wengine.

Nidhamu na Uadilifu ni kuwa mtu wa sura moja, yani ukisema hivi basi inakuwa hivi. Watu waone unafanya, ukimwahidi kitu aone unamfanyia kwa uwaminifu.

Mfano ulipoanza biashara, ulikuwaje ? Hebu jaribu kujitathimini, hivi wakati unaanza au kufungua biashara yako ulikuwa unawahi kufungua kauli njema kwa  wateja. Je leo bado uko hivyo?

Leo umebadilika sana umechoka huoni tena Thamani ya mteja umejawa na tamaa ya pesa unachoangalia ni pesa tu hakuna thamani ya mteja tena je utafika kwa mwenendo huo?

Nidhamu yako haipaswa kuwa ya muda wa uhitaji tu bali inapaswa kuwa mfumo wako wa maisha ya kila siku kwa kufanya hivyo basi hata misimgi ya biashara yako itaimarika sana. Lakini leo umekwisha sahau yote uliyokuwa unafanya mwanzo  unachelewa kufungua na wakwanza kufunga, unahifadhi bizaa zako ili mradi, hakuna mpangilio, umechoka umezoea kazi hakuna tena nidhamu.

4. Kipimo cha Tabia njema. 

Ili kujua kweli unachokisema ndiyo unachokiishi na ndiyo  tabia yako basi ni pale unapofanya kile unachokipanga kila siku kukufanya lakini pia muda nguvu, maarifa na ujuzi lazima kiendane na uzalishaji bora katika kila unachofanya.

Na kumbuka pia kuwa hata ukipita kwenye changamoto, tabia zako nzuri ziendelee au vilevile.
Swali ?

Je kwa mfano, ukipata hasara kwenye biashara, unaendelea kuwahi unawahudumia wateja vizuri, kuwahi kuamka , na kuiboresha biashara yako kama kipindi cha neema au kwa kuwa biashara imeyumba umeacha iwe hivyo hivyo ?

Mtu mwenye Tabia njema , hata apitie kwenye  changamoto zipi, bado mwenendo na mfumo wake wa maisha na tabia zake huwa hazibadiliki hata kidogo.

  Na mtu wa aina hii, kama leo akipata shida anarudi kwenye hali yake ya kawaida haraka sana na harakati za mafanikio zinaendelea, hivyo hata mafinikio yake ni makubwa sana.

5. Mambo matatu ya kutengeneza Tabia njema na imara.

a). Kujifunza kuishi tabia njema, kama uvumilivu, subira, upendo, kuchukuliana na kuwa mwaminifu. Na zaidi ya yote kuwa mkweli siku zote. Acha uongo, madhara yake ni makubwa na mabaya kuliko.

b).kuchagua watu bora ambao watakuwa kampani yako katika jamii na kuanza kuishi tabia zao.

c).Ishi tabia unazotaka kila siku.

Jambo la mwisho kwa siku ya leo.

Muundo wa utu na mifumo ya maisha ya kila siku.

Kama tulivyo ona mwanzo, Nidhamu binafsi ndio utu wako, sifa yako,na tabia yako pia.

Utu wako ni mjumuisho wa maeneo matatu,katika maeneo matatu.

1 Eneo la mfumo wa akili na mawazo yako.

Ni eneo la akili yako, ambalo limebeba mipango yako ya maisha, tabia bora unazotamani kuishi, thamani ya maisha yako na mambo ambayo unatamani kufanya ili kuwa mtu wa aina fulani unaye hitaji kuwa.

2.Mtazamo binafsi
Hili ni eneo la pili, namna unavyojiona wewe mwenyewe, mitazamo yako, je, unajiona ni mtu bora, mwenye faida kwa jamii, unaona uweza kufanya makubwa na kujiona una vitu vizuri kwajili ya wengine.

Ukisha jiona wewe bora, hakuna wa kukudharau, kila mtu atakuheshimu na utakuwa na ujasiri mkubwa sana mbele za watu, hata ukizungumza utaeleweka kwa urahisi kabisa.
Anza kutengeneza nguvu binafsi ya kuaminika na  wengine watakuona kufuatana na wewe unavyo jiona

3. kiwango cha kujipenda na kujikubali.
Ni kwa kiwango gani unajipenda mwenyewe, unajikubali, na kufanya mambo kwa ubora.

Jinsi gani unajielewa, unaijua mihemuko yako na kuweza kuidhibiti, unajua udhaifu wako, na kuweza kuutumia kwa faida na siyo hasara.

Hii itawafanya hata wengine wakupende na wakukubali sana.

Ila kama mwenyewe ni wa kwanza kujitukana, kujidharau, unajichukia, hakuna mwingine atakaye kupenda.

Maeneo hayo matatu yanatakiwa kutunzwa sana ndio utu wako, na ili kuweza kuyaishi vizuri, nidhamu haipingiki.

Leo, hii anza kujiuliza swali hili , Je je hivi kama kila mtu angekuwa kama mimi, hii dunia ingekuwa wapi ?

Kisha anza kubadilika,kwani kuna tabia unazo usingependa watu wengine wawe nazo, na kama watu wote wangekuwa kama wewe, basi dunia ingekuwa mahali pabaya zaidi mara nyingi  kuliko ilivyo leo.

Nikikukwaza nisamehe..ni hatua za kutaka tuwe bora zaidi.

Imeandikwa na
Moses z. Mgema
P.o.box.......
Dar es salaam Tanzania
mgemamoses@gmail.com
0755632375/0678355395
Kwa hisani ya kusoma vitabu vya kuongeza maarifa na utekelezaji

Friday, November 16, 2018

HAKUNA NAFASI YA UDHURU KAMA UNATAYATAKA MAFANIKIO

HAKUNA UDHURU KAMA UNATAKA KUFANIKIWA

Kuna mambo mengi sana kwenye Maisha yetu yanayoendelea kila mtu akipambana kuhakikisha maisha yake yanakuwa mazuri na yenye maana kubwa hasa kiuchumi, Kielimu, kiroho, eneo la Utawala na matumizi ya vipaji.

Sasa pamoja na mapambano yote hayo lipo daraja ambalo linatenganisha kati ya watu wanaofanikiwa na wasio fanikiwa japo watu wote tunaamka na tuna muda sawa wa kufanya kazi.

Pamoja nakuwa na muda sawa lakini ninachoamini kabisa kitu kinachotutofautisha hapa naamini ni mgawanyo wa muda na namna ambavyo tunaweza kupangilia namna ya utekelezaji wa majukumu yetu.

Mfano ukichukua kundi la watu ambao ndio wanaanza kiuchumi na wanafanana, na ukiwapa muda miaka miwili, utakuta kuna ambao wamepiga hatua zaidi na kubwa sana na wengine, wako palepale, je, unafikiri kuna uchawi hapo? Huwa tunaona kama wanabahati kwa kujitia moyo maisha ni foleni na sisi bahati yetu yaja.

Kila mtu anataka vitu vizuri ila kwa njia rahisi na za mkato, bila kujua maumivu yaliyopo nyuma yake.

Je, unataka kuongeza mauzo kwenye biashara mara dufu zaidi?, unataka kufanya ndoa yako kuwa bora zaidi?, unataka kujenga mahusiano bora zaidi? Unataka kuanza ukulima bora ?uwekezaji bora? , unampango wa kufikia uhuru wa kifedha na kustafu mapema?

Nini kina kuzuia kati ya unachojipanga kufanya na kuanza?

Huu, ndio mtego, anza kuutegua, kuvunja mara moja

Hapo ndipo kwenye shida, kwanza kabisa waafrika wengi tumejicholea mstari wa kutofanikiwa ila ni watu wenye kutamka kuwa  *siku moja, nitaanza* ? alafu pia *kesho nitaanzaa.....*

Utafiti unaonyesha 80% ya watu Duniani wapo kwenye *nitaa*  fanya, nitaanza, n.k.

Na 20% ni wale waliyofanikiwa, sana na wanachukua hatua kwa kila wanachopanga na kujifunza.

Kundi hili ni watu ambao wanapanga na kufanya.

Amua Leo,
  Kuendelea kusingizia, mambo ya nyuma, mazingira, ukosefu wa Elimu ,mara bosi simwelewi, ndoa inasumbua, sina kazi nzuri, sina shamba ila natamani kulima, natamani kufanya mauzo makubwa ila wateja hakuna, napenda kufikia uhuru wa kifedha ila, naona sina biashara kubwa* kama upo kwenye kundi la aina hiyo basi unajichelewesha, wewe ni moja kati ya watu wanaotakiwa kufanikiwa sana Duniani, kwani hata tunaofahamu wamefikia uhuru wa kifedha walikuwa na hizo sababu ila waliamua kuyakataa mazingira hayo na kutokuridhika nayo hata kidogo

   Amua leo  kutoka kwenye *Comfort zone* , kuachana na maisha ya watu wa kawaida, maisha ya mazoea, maisha ya kupanga kufanya, badala yake, *anza kuishi maisha ya kufanya.*  Jua hakuna mtu mbaya Duniani anaye jidanganya.

Amua.
  leo, kuwa chanzo cha mabadiliko kazini kwako, kwenye biashara yako,ndoa yako,familia yako,afya na elimu yako, kwa kuanza kufanya zaidi ya wengine, au kufanya vitu ambavyo wengine hawafanyi, kwa kuingia kwenye kundi la 20%.

  Tuangalie mambo 5 yakujifunza ambayo watu wengi waliofanikiwa waliyagusa ama kuyapitia kutokana na vitabu ambavyo nimekuwa nikisoma ambayo pia ni muhimu ukayajua ili either yakuasaidie kupiga  hatua kwenye safari ya maisha uliyonayo*

Kitu ambacho kimekuwa ni changamoto kubwa kwenye kufikia mafanikio ni kukosa NIDHAMU BINAFSI.

Mafanikio kiuhalisia  yanaanzia kwenye nidhamu binafsi.

Aristotle aliwahi kusema, *nia kubwa ya maisha ni furaha*
Kama kila mtu ataweza kujiuliza nini afanye ili kuwa na hiyo furaha, hakuna mtu atashindwa kufanikiwa kiroho na kimwili.

1. *Pambanua maisha yako*

Unataka uwe mtu wa aina gani kazini, kwenye biashara, kwenye uongozi wako , ndoa au familia yako? , unataka kufanya kazi kampuni ya aina gani? Biashara yako unataka iweje, ? Je, unataka utengeneze kiasi gani cha pesa kwa sekunde, dakika, saa ,siku, wiki hata mwezi? Unataka kupunguza uzito? Kusafiri kwenda wapi?
  Jiulize maswali kujua nini unataka haswa.

Mfano, kama familia yako, ingekuwa na kila kitu, ungependa uishi wapi leo,? Upumzike hoteli gani? Usaidie watu wa aina gani, utembelee nchi zipi? Uwe na lifestyle ya aina gani?

Jiwazishe leo, kiuchumi,kiroho,kimahusiano,kiafya na kifikra ungependa uwe mtu wa aina gani?

2. Siyo kwamba watu hatujui nini,tufanye ili kuwa matajiri ila kukosa Nidhamu binafsi na kuwa na Excuses nyingi sana ndo sababu ya vile tunaishi leo.

Anza kuishi unachowaza kuanzia sasa, na kuzungukwa na watu unao wahitaji katika mazingira unayotaka.

3.Kanuni kubwa ya ulimwengu.

*Law of Cause and effects* inasema
Kwa kila matokeo kuna kisababishi, mfano kama unataka kufanikiwa katika eneo lolote la maisha yako, jua nini kinahitajika kufanikiwa na fanya hivyo kwa kurudia rudia kila siku.

Kama ni kuchelewa kula kwa sababu maalumu na kuwahi kuamka, basi fanya hivyo mpaka uyaone matokeo.

Jua, mafanikio yanatabilika, na wewe ndio  wa kuyatabili hayo mfanikio kwa tabia zako za kila siku, nini unafanya na nini hufanyi.

4. Siri ya mafanikio.

Lipa gharama, jifunze kwa waliyofanikiwa, anza kuwa yule unayemtaka, ishi tabia za kuwa bora kila siku

Acha maisha ya kawaida na historia, kila mtu anataka kufanikiwa ila siyo wengi wanajua tofauti ya waliyofanikiwa na waliyoshindwa, anza kujitofautisha leo.
Hutakufa kwa kuweka bidii ila utakufa kwa stress usipofikia malengo yako.

5.Jiulize maswali katika kila eneo la maisha yako, unayotaka mafanikio makubwa, *ni kipi ukikifanya kwa nidhamu maisha yako yataanza kubadilika mara moja?*

Ni mimi..
Moses zephania Mgema
0755632375
0678355394
mgemamoses@gmail.com
Dar es salaam,Tanzania

Sunday, November 4, 2018

MAMBO MUHIMU KUJIFUNZA

Key Skills To hold on
Kama mtu mwingine ambae ana kazi, vilevile mjasiriamali anahitaji ujuzi mkubwa ambao utamfanya aifanye kazi yake vema.
Unapozungumzia neno "UJUZI" ni kitu ambacho kimebeba vitu kama uwezo, utoshelevu,  na  uwezo wakufanya jambo fulani vizuri kabisa.
Ujuzi unafanya kazi na vitu kama, utalamu Fulani, maarifa, uwezo lakini lazima ujuzi usiutenganishe na kitu kinaitwa kipaji, kuna watu wanaujuzi wa jambo fulani kwa sababu ni kipaji chao
Kuna wakati lazima tukubali kwamba japo kwenye mafanikio ya ujasiriamali hakuna formula maalumu ya kutoboa kimaisha lakini kuna baadhi ya skills  (juzi) ambazo zina randana sana na mafanikio ya kijasiriamali na lazima mtu awe nazo au azijue.

Uwiano na mchanganyiko mzuri wa maarifa na juzi mbalimbali inamwezesha mjasiriamali kutegua au kupambanua mambo mbalimbali na kujenga lakini kuja na mawazo mapya ambayo yanamsaidia sana kuinua hali ya biashara na maisha kwa ujumla.

Tunapozungumzia ujuzi tofauti tofauti kwenye issue za ujasiriamali ni kwamba ujuzi una play role kubwa sana ya mjasiriamali kuwa mshindani wa kweli katika biashara, kuwa na akili wazi iliyofunguka na shapu ya kusoma hali ya soko kwa ujumla wake na kuweza kutembea kwenye hali yoyote ya soko
Tunapozungumzia suala la ujuzi maana yake tunazungumzia, ujuzi binafsi ambao ni kipaji, hard skills amabazo ndo ujuzi wa kibiashara. Ukiacha kipaji lakini ujuzi mwingine tunajifunza darasani na maeneo mengine, sasa Lazima Kama mjasiriamali ujue namna ya kutumia ujuzi wako to the maximum lengo ni wewe UNAFIKIA ndoto zako
Swali Je wewe unafikiri nini?

Ujuzi binafsi ni ule utaalamu tulionao ambao tunautumia kwa ajili kujiendesha kimaisha, ujuzi ni kile kitu kinakupa nguvu ya kufanya jambo fulanikwa sababu kiko ndani yako.
Ujuzi unapounganishwa na maarifa inatengeneza bond ambayo inapelekea kuboresha kabisa mfumo mzima wa ujasiriamali maana hapa itakupa nafasi yakuwa mbunifu, kuunda mbinu ndogo ndogo za kuwini washindani wako, kuwa na uwezo wa kutatua changamoto zinapokukabili, kukupa nguvu yakufanya maamzi mahali ambapo ni magumu na uthubutu wa kuanzisha mambo katikati ya woga wa wengine.
Ujuzi + maarifa inakupa nafasi ya kufanya kazi ya aina yoyote maana utakuwa na ujuzi wa kutengeneza mahusiano mazuri na aina za watu wote, hapa utakuwa na ujuzi wa kimawasiliano, nguvu yakufanya kazi kama team na kila mtu ambae analazimika kuwa mbia kwa namna yoyote ile.
Ujuzi unakupa nafasi ya kukufanya uyazoee maisha na hali yoyote kwenye maisha ya kibiashara ambayo unaweza kuyakabiri, uwezo wa mawasiliano mazuri na kila aina ya mteja au mbia.

Lakini pia ukiwa na ujuzi na maarifa itakupa nafasi kubwa mno pale kampuni au biashara yako inapokuwa kubwa namna ya kuunda uongozi na utawala wa usimamizi mzuri na biashara kusonga mbele zaidi kuliko ukiwa huna ujuzi ufahamu na maarifa juu ya ujasiriamali.

Vilevile ujuzi unakupa nafasi na uwezo mkubwa kutekeleza mipango na malengo amabayo ungependa kuyafikia ndani ya muda mfupi kati na mwisho ambao ni muda mrefu.

Ujasiriamali ni uwezo binafsi ambao unalifanya tatizo kuwa ni wazo linalotakiwa kutatuliwa kwa vitendo.

Kuwa mjasiriamali lazima uwe na uthubutu na uwezo  wa kuchukua na kutumia uwezo wa kufikiri, ubunifu na mtu mwenye kuchukua uamzi mgumu lengo kuu ni kutatua changamoto lakini pia kufikia lengo baada ya tatizo kuwa limepatiwa ufumbuzi.
Uwezo wa kujenga wazo, hoja uwezo wa kuwasiliana na namna ya kufanya kazi na watu sahihi ambao wanaweza kufanya nao kazi na kufikia malengo mfano unapokuwa na kampuni basi unapoajiri watu wawe na uwezo unaoutaka na wenye kuleta matokeo ya kile kilipelekea kuwaajiri.

Kumbuka ujasiriamali ni uchaguzi ambao mtu anafanya kwa manufaa yake na jamii, Kwa hiyo Lazima awe na mtazamo chanya endelevu, Thamani, uwezo binafsi, mwonekano na mapenzi binafsi na kazi husika.
Uchaguzi kwenye masuala ya ujasiriamali huzaliwa kwenye fursa amabazo unakuwa umeziona hapo ndipo unalazimika kufanya maamzi yanayowezekana katikati ya mambo ambayo yalionekana hayawezeakani kwa kutumia ujuzi sahihi.
Ujuzi pia unaotumika lazima uwe ujuzi sahihi ambao unaendana sana na hali ya utumiaji wa Teknolojia iliyopo ili kusapo ujuzi wako uwe sahihi zaidi hapa lazima pia utengeneza namnaya kuleta mabadiliko ya mifumo ya kimasoko ili kuleta matokeo unayoyataka. Hapa pia inaendana sana na uwezo wa kugundua uwezo na udhaifu wa washindani wako hapo utaweza kuwa mjasiriamali bora.

Ni ujuzi upi ambao unakutofautisha na wengine?. Kuwa na uwezo ambao utakupeleka kwenye uzoefu ambayo lazima tabia yako kabisa ambayo imekufanya kuwa hapo ulipo.
Ujuzi unao na uzoefu unao sasa yakupasa kuanza kufanya mambo mbalimbali yaliyo ndani ya uwezo wako lakini kuwafanya watu wakuhitaji zaidi wewe kwa kile unafanya.

Prepared by
Moses zephania Mgema
0755632375

Saturday, November 3, 2018

JUA HAYA MAMBO MANNE ILI UFANYE BIASHARA YAKO KWA UFANISI.

kuna sababu nyingi sana zimekuwa zikichangia kuanguka kwa biashara na watu wengi bado hawajafahamu  sababu critical za wao kuanguka kibiashara hasa kwenye dunia ya tatu ambayo watu wengi ni kama tunaingia kwenye biashara kwa sababu hakuna namna nyingine ya kufanya ili kujiingizia kipato
Pamoja na sababu nyingine nyingi kama ukosefu wa elimu juu ya biashara, ujuzi, maarifa, ukosefu wa mitaji au kuanza na mitaji midogo, ukosefu wa uzoefu nk. Lakini kuna mambo haya muhimu sana kama unataka kufanikiwa kibiashara na ni vema ukazingatia sana.
Kuna kitu kinaitwa 4ps kwenye biashara yoyote ile.
Kwa Lugha ya kigeni zimebebwa kwenye kitu kinaitwa  (Marketing Mix )
Marketing Mix-Ni muunganiko wa sababu au mambo ambayo huwaratibiwa na kampuni au Taasisi ili kuhakikisha inatoa huduma kulingana na mahitaji ya wateja iliyowakusudia 

Tutaangalia mambo makuu manne 4ps ambazo mfanya biashara yoyote lazima uyazingatie ili kuifanya biashara yako idumu kwa kiwango kilekile au ikuwe zaidi.

1. Bidhaa  (products)- hiki ni kitu cha kuzingatia sana unapotaka kuanza kufanya biashara, sio kila bidhaa yafaa kuwa mahali fulani kwa sababu tu ulikuja au ulienda mahali ukakuta watu wanauza sana 

Jiulize je hii bidhaa pamoja nakuwa inauza sana hapa Dar je ni kweli singida kwetu inawatumiaji au inahitajika, Je katikati ya waislam kibanda cha kitimoto kitalipa, je baibui na kanzu katikati ya jamii ya kikiristo kitalipa, senene, michembe na bidhaa fulani inahitajika 

Kwa hiyo unapotaka kufanya biashara lazima uzingatie aina ya biashara unayotaka kuifanya kwenye eneo ambalo umeliona lina manufaa 

Kumbuka si kila fursa yafaa kutekelezeka kila mahali fursa zingine hazilipi kwenye eneo fulani hapa tuanachoangalia ni uhitaji wa kitu sio kila biashara ya dar ifanyike Arusha. Arusha tunaweza uza masweta, blanket lakini dar maji feni kwa sababu ya hali ya hewa.

2. Bei  (price) kitu kingine cha msingi sana kuzingatia unapotaka kufanya biashara. Hapa Lazima uangalie levels ya uchumi ya watu wa eneo husika je wanauwezo wa kumudu bei ya bidhaa yako, ukipeleka IPhone Singida, Manyara kigoma nk. Kwa asilimia ngapi wanamudu kununua IPhone yenye kuhitaji laki tano na kuendelea, ni kwel watu wanaipenda bidhaa lakini je wanaweza kumudu gharama za bidhaa hiyo

Lazima uzingatie kiwango cha uchumi cha eneo husika kabla hujapeleka bidhaa yako.usije anza kusema unalogwa kumbe ni wewe kushindwa kutambua level ya uchumi wa watu wa eneo la biashara yako

3. Eneo  (place)- Hii ni sababu ya msingi kuzingatia sana. mimi ntaanzia mbali kabisa kwamba Lazima eneo la biashara yako liwe karibu na wateja, Mazingira safi ambayo yatawavutia watu kuja, Mazingira Lazima yaweze kuwashawishi yaani eneo limtengenezee mtu sababu yakuja kununua kwako.kuna mambo sana ya kuzingatia kwenye uchaguzi wa eneo wataalamu wa masoko wametaja vitu vichache sana kwenye eneo hili ila Mimi naweza sema 

Eneo lako la biashara Lazima lijumuishe watu wa aina zote yaani wazima walemavu watoto eneo lako lazima liwazingatie sana maana wote ni wateja ukiacha mambo mengi ambayo yamezungumzwa na watu wa masoko 

Mazingira ya soko Lazima uyatengeze kwa namna yakumshawishi mtu kurudi tena na tena.

4. Promosheni (promotion) watu wengi huchanganya na wengi wanahisi ni gharama sana kufanya promotion hapana, promotion zipo za aina nyingi sana free promotion ambayo inaweza kuwa matumizi mazuri ya lugha kwa wateja kuwaja liwateja, kuchangamka kuwa na welcome face.

Kutumia zawadi ndogo ndogo kama pipi kwa watoto, kupitia mazingira safi yaweza kuwa means ya promotion. Achana na kutumia magari, media na vyombo vingine vya gharama ambavyo yawezekana huna mtaji wake.

Ivi sukari kwa sasa kilo unapata faida 1000 kwa mfano, na wengine wanauza bei hiyo hiyo kwa nini wewe usitoe hamsini au mia upate faida ya 900 shida iko wapi.

Lazima utumie akili na maarifa mengi ili kuifanya biashara yako kuwa stable na yenye kukuwa kila siku.

Kuna watu huona ugumu katika kila jambo ila mara nyingi sisi ndo tunatengeneza huo ugumu badilika nenda kisasa utafanikiwa 

Nimejaribu kutumia maelezo fulani ambayo sio kuntu sana ili uelewe vizuri 

MOSES MGEMA

0755632375

Saturday, October 27, 2018

I LIVE MY OWN LIFE....LEAVE MY LIFE ALONE

Nini.....niacheni naishi maisha yangu sitaki mtu anifuatilie kila mtu na maisha yake.
Nini......?
Nimemaliza ukiendelea kufuatilia Maisha yangu ntakuja pasua mtu sina swalia mtume........
Ok.........anyway

Socialization, civilization, Corporation,
Are are among of The fundamental which will take you to the place where you want to be.
Stori nyingi sana za vijiweni vinasikitisha na kukatisha tamaa kwa sababu vijana wengi tunapenda kuona

UPANDE WA PILI NA MTAZAMO WA WAJASIRIAMALI WENGI

-Kuna mwamko mkubwa sana wa watu kujiingiza kwenye ulimwengu wa biashara, ujasiriamali na utumiaji wa kila fursa ambayo inapatikana kwenye mazingira yanayowazunguka lakini pia watu kusafiri mahali mahali kuzifuata fursa zinakopatikana.
Lakini pia watu wameenda mbali zaidi kwa kuwa wabunifu, wenye kutumia maarifa, ujuzi na taarifa zinazopatikana lengo likiwa ni kutimiza malengo na ndoto zao.
Ugumu wa maisha na kuongezeka kwa mifumo ya Teknolojia mpya ambayo inawafanya watu wengi kujifunza kutoka kwa mataifa tofauti tofauti ambayo mfumo wa biashara na ujasiriamali umeendelea zaidi.

Thursday, October 18, 2018

GOODMONING TANZANIA

Good Morning Tanzania

Kila asubui ijapo ina maanisha kuwa tumefungua ukurasa mpya kuendelea na stori yetu tunayoisoma.
Na kila mtu amepewa kitabu na stori tofauti na mwingine, maudhui na wingi au achache wa pages.

Hii imefanyika hivyo kwa sababu kila mtu amepewa talanta, karama, vipaji na vipawa tofauti ili kutimiliza kusudi la Mungu hapa duniani.
Na hii ina maana kubwa sana kwenye maisha yetu ya kila siku
kwa nini? ........
Kwa sababu  kadri pages unapozifungua ndivyo zinavyoongezeka kule unatoka na kule uendako zinapungua.
Hapa ni kwamba miaka yako ya kuishi inazidi kupungua na kukaribia kurudi ulikotoka.
Lakini kwa maana ya maisha yetu ya kawaida yanayotufanya wakati mwingine tusahau kama kuna kifo basi kadiri unaposogea badala ya pages kupungua hapa pages zinaongezeka tena kwa kasi sana
Nini maana yake..............
Umri unaposogea mahitaji na majukumu yanaongezeka zaidi na jamii kuanzia ngazi ya wewe familia mpaka jamii kwa ujumla inakutazama. Haikutazami tu kwa sababu umekuwa, la hashaaa bali inategemea jambo kutoka kwako.
Ulisoma, wewe ujitegemee uitumie ile elimu yako kuboresha mwonekano style ya maisha mtazamo na kila kitu ili kuiweka hadhi ya taaluma yako salama
Baba mama na familia inakutegemea lakini jamii na Taifa na dunia unailetea nini....ndo maana nikasema inapokuja siku mpya kurasa za kuishi zinapungua lakini kwenye suala la Maisha kurasa huongezeka.
Kila siku dunia inakulazimisha kufikiria mbinu mbalimbali za kuendesha maisha yako huku ikikunong'oneza kuwa angalia kule yule rika lako ulisoma nae lakini anahiki na kile....hapa ndipo unachanganyikiwa ufanyaje ili kufanikiwa.

Ni changamoto moto katikati ya dunia inayohitaji ubunifu, ujuzi na maarifa mengi ili kuweza kuifanya dunia ikukabili wewe badala ya wewe kuikabili.
Ushauri........
Mungu ameniumba mimi vivyo hivyo wewe amekuumba na lengo na kusudi maalumu ambalo hakuna mwingine aweza kulitimiza isipokuwa mimi mwenyewe au wewe mwenyewe.

Mungu alifanya kila jema akakupa kipaji akili focus nguvu maarifa ujuzi na anakuumba kwa namna ulivyo lengo utimize kusudi lake ili Muda ukifika urudi mtupu na salama.

Itumie talanta/Karama na kipaji chako na nafasi uliyonayo sasa ya uhai kazi, biashara,elimu  na kila jambo unalofanya, Fanya kwa bidii kwa uaminifu kwa kujitolea na kwa kumaanisha sana.....hapo utafanikiwa utafurahia na kuiona dunia mujarabu sana......
Uvivu masengenyo zogo marafiki wabaya kulala,kulalamika,kulaumu, Kukosa uthubutu, kuchagua kazi nk. kuishi kwenye historia haikusaidii kabisa bali stay focused pekee...lazima utafanikiwa. Kumbuka Mungu huibariki kazi ya mtu mwenye bidii na kuilaani mikono milegevu.

Zaidi mkumbuke muumba wako kila sekunde ya pumzi yako ukisali kwa kushukuru na kutenda mema ili kuhesabiwa haki ya kuishi tena.
Matendo mema ni fahari ya Mungu kwetu sisi....Mungu wetu hutuwazia mema daima.

Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako kabla siku mbaya hazijaja kwako
Hii ikawe asubui na siku ya baraka na mafanikio.

Kila unalofanya likapate kibali mbele za Mungu na wanadamu
Moses z. Mgema
0755632375/0678355394
Moses Mgema Twitter and Instagram
2018/2019 Is THE YEAR OF ACHIEVEMENTS

Tuesday, October 16, 2018

NGUVU YA MAONO Na MAYLES

10. UKWELI NI UHURU.

Uchambuzi Wa Kitabu.
Misingi na Nguvu Ya Maono.

Mwandishi(Author).
        Dr. Myles Munroe.
        (1954- 2014)
Kanuni ya nne , ya kukuweza kuishi na kutimiza maono yako ni pamoja na :-
........................................
*Kuwa na shauku ya maono yako /Posses the Passion of Your Vision* .
........................................
Je, unahasira kiasi gani na maono yako? Unajisikiaje pale bado hujaanza kugusa maisha ya watu na uwezo umepewa?

Watu waliyotambua kuwa kuwepo hapa Duniani ni zaidi ya kuishi, ndio wanafanya mabadiliko makubwa katika ulimwengu huu toka mwanzo, watu ambao kwao maisha ni zaidi ya kula, kuvaa, kustarehe, yani watu ambao furaha yao haitokani na uwingi wa pesa wanazotengeza ila alama wanazo achilia ndani ya mioyo ya watu.

Watu wengi hawana shauku ya kufanya mambo makubwa katika maisha yao kwa sababu hawana shauku kutoka ndani ya Mioyo yao, na maono Pekee ndio chanzo cha shauku.

Shauku/Passion ina maanisha kile unacho kiamini ni kikubwa kuliko unacho kiona.

Ni shauku / Passion itakusaidia kushinda vikwazo kwa sababu kilichopo ndani ya moyo wako ndio kinakusukuma katika maisha yako ya kila siku, kuna wakati tunatafuta namna mbalimbali ili tuweze kufikia ndoto zetu lakini, bila kuwa na shauku ndani Mioyo yetu hatuwezi kustahimili vikwazo na changamoto zitakazo tokea njiani, zaidi ya yote ukiwa na shauku hata kama watu watakuangusha mara ngapi, utasimama Mpaka wao wachoke na kukuacha wenyewe.

Shauku ya moyo wako juu ya maono itakusaidia Kuzingatia ndoto yako bila kuishia njiani.

Hongera rafiki kwa mfululizo huu, endelea kupata Kilicho bora zaidi...

Kiu yangu ni kuona watu wanaoishi zaidi ya wanacho kiona leo, wenye uwezo wa kugusa maisha ya ulimwengu huu.

Mwisho.
Kwa mgeni karibu, kwenye kundi hili, tunajifunza na kuchukua hatua ili kufanya maisha yetu na wengine kuwa bora,zaidi.

Pia taarifa ya darasa la leo 14/10/018 juu ya uwekezaji, kwanzia saa 2:00-4:00usiku.

💥Maeneo tunayoenda kujifunza,
  1.maana ya uwekezaji na uhuru wa kifedha pamoja na umuhimu wake.

2.Maeneo matano ya kufanya uwekezaji katika maisha yako.

3.Mbinu za kufanya uwekezaji bora.

UKWELI NI UHURU 7

13.UKWELI NI UHURU.
UCHAMBUZI WA KITABU.

Kanuni na Nguvu ya Maono.

Mwandishi :
       Dr. Myles Munroe.

Kanuni ya 7.

...................   ...................
Tengeneza vipao mbele vya maono yako /Set the priorities of your Vision.
.................     ...................

Maisha yako ni mjumuisho wa maamuzi unayofanya kila siku,/ your life is the some total of the decision you make every day.

Kanuni hii inasema kama unataka kufanikiwa lazima utengeneze vipaombele kulingana na maono yako.

Kama kila siku tunafanya maamuzi basi, maamuzi sahihi ni zao la vipao mbele sahihi, utofauti wa kufanikiwa na kufeli unachangiwa na vipao mbele ulivyo navyo, kama huna vipaombele jua huwezi kufanya maamuzi sahihi katika maisha ya kila siku na hata kutimiza ndoto zako utashindwa.

Nguvu ya vipaombele katika kusema *YES* au *No*
   Kama unasema Yes kila linalokuja mbele yako ujue unatatizo la vipaombele. Myles anasema ukiwa na vipaombele utajua kipi useme Yes kulingana na vipaombele vya maono yako na nini useme No kama ni nje ya maono yako.

Ndio na hapana ni maneno ya muhimu sana katika safari ya mafanikio, huwezi kuwekeza kila mahali hata ushawishiwe kiasi gani, huwezi kufanya kila biashara au kudaga kila fursa, isipo kuwa ipo kwenye vipaombele vyako vya siku, wiki, mwezi na mwaka, hakika utafanikiwa sana.

1corintho 6:12.

*Vitu vyote ni halali kwangu lakini si vyote vifaavyo,......*

Ni kwamba Kuna vitu vingi ni halali lakini kwa kulingana na maono yako, si vyote vifaavyo lasivyo unauwa ndoto yako, hii ni kweli kitu kile kile mwingine akifanya anafanikiwa ila wewe ukijaribu una umia kwa nini,?  Hakipo kwenye maono yako rafiki, jifunze Kusema No.

Kwa kigezo kipi useme hapana?

Toka mwanzo tumejifunza kuwa mwanzilishi wa maono ndani yako ni Mungu mwenyewe, hivyo kama kuna jambo utakiwa ulifanye ila Mungu hawezi kulikubali, yani ukilifanya unakuwa unavunja uhusaino wako na Mungu acha, sema haoana, yani hapana rushwa, hapana kuwanyima watu haki na kuondoa furaha yao kwajili ya faida yako mwenyewe.

Vipaombele vinakupa nafasi ya kuzingatia jambo moja mpaka kuhakikisha limetimia kabisa, pia linakufanya uwe na uhakika kuwa baada ya miaka kadhaa ijayo utakuwa upo mahali gani kwani yapo mambo mengi ambayo utayakwepa kuyafanya na utashughulika na yale muhimu tu.

Kama vipaombele vyako vinatokana na maono yako, basi jua kabisa nidhamu itakuwa kitu rahisi kwako, kwani wengi wanakosa nidhamu sababu kubwa ni kukosa vipaombele.

Jiulize maswali haya kujua kama unaishi maisha yenye nidhamu kufuatana na ndoto zako?

.Nguvu zako nyingi unatumia kufanya nini? Wapi moyo wako upo?  Je, ni mambo yenye uhusiano na ndoto zako.

.Wapi unawekeza pesa zako? Je, unanunua vitu vya gharama kuliko hata uwezo wa Maisha yako binafsi? Unajikuta unamadeni mengi kiasi kwamba kila pesa unayopata haiendi kufanya mambo yanayohusu maono yako?

.Ni Movies gani unaangalia, unafuatilia nini kwenye mitandao ya kijamii, habari gani unafuatilia katika maisha yako kila siku, utajua maono yako?

.Vitabu gani unasoma, je, ni vitabu vya mapenzi na hadithi za umbea? Aina ya vitabu unavyotakiwa kusoma vitokane na maono yako.

.Ni mtazamo gani unao juu ya maisha?  Vitu gani hatari unafanya?(ngono, pombe, au madawa).

Amua kuchukua hatua ya kufanya mambo makubwa katika maisha yako, kama kuna jambo la kubadilisha maisha yako anza mara moja.

Mwisho.

Mambo ya kuchukua hatua.

1.Andika vipaombele vyako kila eneo la maisha yako,  (kiroho, kiuchumi, kiafya, kiakili na kimahusiano).

2.Vitu gani unataka kuviondoa kwenye maisha yako ili uweze kuishi maisha yako (Orodhesha na anza mara moja hatua za kuachana navyo)

3.Jibu maswali ya hapo juu vizuri kabisa Kwa kujichunguza Mwenyewe .

         

HATUA 10 ZA KUSAJILI KAMPUNI

Hatua 10 za kufuata ili kusajili kampuni imeelezwa hapa chini, tafadhali fuatilia.

HATUA 10 ZA USAJILI

1: Taarifa za msajili
Kitambulisho cha Taifa kwa wenyeji na Passport kwa wageni
Simu ya kiganjani
Barua pepe yaani email
Hatua

2: Taarifa za kampuni (Company Information)
Aina ya kampuni kama ni ya hisa au isiyo na hisa, ya binafsi au ya uma nk
Jina la kampuni
Kazi zitakazokuwa zikifanywa na hiyo kampuni tarajiwa (Activity description)
Hatua

3: Ofisi za kampuni (Office Location)
Aina ya eneo (Aidha limepimwa au la)
Kama halijapimwa tayarisha anuanii ya makazi yenye mfumo huu, jina la Mkoa, Wilaya, Kata, kijiji, kitongoji na ueleze kama eneo lipo karibu na alama zipi ambazo hazihamishiki kama shule ya msingi nk. Usiweke alama ambazo hazina uhakika wa kudumu hapo maana brela watazikataa.
Kama limepimwa tayarisha yafuatayo: Jina la Mkoa, Wilaya, Kata, kijiji/mtaa, barabara, namba ya kiwanja, namba ya kitalu na namba ya nyumba, sanduku la posta, simu ya ofisi/kiganjani na barua pepe (email)
Hatua

4: Shughuli za Kampuni (Company Activities)
Taja shughuli za kampuni kama ilivyoorodheshwa kwenye mfumo wa ISIC Classification
Hatua

5: Taarifa za Wakurugenzi (Directors Information)
Aina ya mkurugenzi kama ni mtu au taasisi
Asili yake kama ni mwenyeji au mgeni
Kitambulisho cha taifa kama ni mwenyeji au passport kama ni mgeni
TIN
Simu ya kiganjani
Barua pepe yaani email
Anuani ya makazi kwa kila mkurugenzi kwa kufuata mfumo wa anuani ya ofisi hapo juu
Hatua

6: Taarifa za katibu wa kampuni (Company Secretary)
Aina ya mtu kama ni mtu asili au taasisi
Asili yake kama ni mwenyeji au mgeni
Kitambulisho cha taifa kama ni mwenyeji au passport kama ni mgeni
Simu
Barua pepe - email
Anuani ya makazi kwa kila mkurugenzi kwa kufuata mfumo wa anuani ya ofisi hapo juu
Hatua

7: Taarifa za wanachama/wenye hisa (Subscribers Information)
Aina ya mtu kama ni mtu au taasisi
Asili yake kama ni mwenyeji au mgeni
Kitambulisho cha taifa kama ni mwenyeji au passport kama ni mgeni
Simu
Barua pepe - email
Anuani ya makazi kwa kila mkurugenzi kwa kufuata mfumo wa anuani ya ofisi hapo juu
Hatua

8: Viambatanisho (Attachments in PDF)
Viambatanisho vinavyotakiwa kuambatanisha kwenye maombi (zote katika pdf) ni:-
Memorandum and articles of association iliyosainiwa na wanachama/wenye hisa pamoja na mwanasheria wa uma (Notary Public)
Form 14b iliyosainiwa na mmoja wa wakurugenzi na mwanasheria wa uma (Notary Public)
Ethics and Integrity Forms iliyosainiwa na mmoja wa wakurugenzi
Company consolidated form iliyosainiwa wakurugenzi wote na katibu wa kampuni
Hatua

9: Ada za usajili na kufaili (Different Fees)
Aina za ada ni kama ilivyoonyeshwa hapa chini
Kusajili kampuni
Kuhifadhi nyaraka na
Stamp Duty
Hatua

10: Namna ya kulipa ada (Payment Methods)
Malipo ya ada yanafanyika kwa njia kuu mbili ambazo ni
Simu ya mkononi kwa kutumia akaunti za MPESA, Tigo Pesa, Airtel Money na HaloPesa
Kulipa moja kwa moja benki kwenye akaunti zilizopo CRDB au NMB
Kumbuka: Utaratibu wa malipo aidha kwa simu au benki utapewa ukishafikia hatua husika ya malipo.

USHAURI WA BURE

Brela sasa hivi hawataki usajili kwa njia ya zamani, yaani kupeleka makaratasi ngumu na kusubiri mlangoni kwa siku 6. Pia BRELA hawakubali mtu asiye na kitambulisho cha Taifa yaani #NIDA kusajili kampuni au jina la biashara.
Taarifa zilizotolewa hapo juu ni zile za lazima ambazo bila hizo huwezi kumalizia usajili na au usajili unaweza kukawia

Nashauri yafuatayo:
Nashauri kama unataka kufanya usajili wa Haraka na umeshaandikisha ili kupata kitambulisho cha Taifa, tembelea ofisi zozote za NIDA karibu na wewe ili wakupe angalau namba yako ya kitambulisho ili uweze kukitumia.

Nashauri pia kama bado hujajiandikisha ni vyema ukawahi, hata kupitia kwenye eneo ambalo zoezi linaendelea ili uwahi kwa maana serikali imeanza kuzuia kupata huduma za public kama huna kitambulisho.

Mwisho nashauri hizi taarifa zote uwe nazo mkononi kwa sababu huu mfumo wa usajili wa ORS unakupa siku sita (6 days) tu kukamilisha usajili kama baada ya hizo siku bado, taarifa zote zinafutika na itakubidi uanze upya from the scratch.

UKWELI NI UHURU

UKWELI NI UHURU

Misingi na nguvu ya Maono.

Mwandishi.
        Dr. Myles Munroe.

Kanuni ya sita ya kutusaidia kutimiza maono,..
........................................
Uwelewe mchakato wa maono /Understand the Process of Vision.
........................................
Mithali 16:9
Moyo wa mtu hufikiri(hupanga) njia yake, bali Bwana huziongoza hatua zake/In his heart a man plans his course but the Lord determine his steps. (emphasis added).

Maono ni mchakato wa siku nyingi, Mimi na wewe tunatakiwa kuwa na mipango lakini kazi ya Mungu ni Kuongoza hatua zetu.  Nini muhimu kujua ni kuwa utimilifu wa maono unaanza pale unapogundua maono yako na kupanga mipango ya kuishi maono.

Hii ni rahisi sana, unatakiwa kuishi maono yako, kwanzia sasa kwa kuwa umesha fahamu, huku ukijua kila siku kuna kitu Mungu atakuongoza kufanya.

Njia ya kufikia kutimiza ndoto zetu, inatuandaa kwa vitu viwili muhimu.
   Kwa sababu pamoja na kuona picha ya maono yako ambayo inaweza kukupelekea utamani kufika kesho lakini anakuwa amekuandalia njia ya kwake ya kufikia maono hayo. Kumbuka muda wa mfalme Daudi kupakwa mafuta na kuja kuwa mfalme ulikuwa mrefu sana,

Je, vipi kuhusu Joseph akiwa na miaka 17 aliota ndoto ya kuwa mkuu siku za usoni (Mwanzo 37:9-10), lakini mchakato wa wao haukuwa rahisi ilitakiwa wapite kwenye shule ya Mungu, ili Joseph kuja kuwa mtu mkuu sana Misri, kwanza njia alizopita kama Mungu angemwambia au muonyesha asingefika,angeishia njiani kwa sababu ya ugumu wake.

Ni kweli una ndoto kuwa sana za kugusa maisha ya wengine kwa maana hiyo unaenda kuwa mtu mkubwa na mwenye nguvu hata Kifedha lakini swali ni ulifikia hiyo hatua kubwa bado utaendelea kutenda mema kwa watu au utapotea?

Basi ukiwa katikati ya kufikia ukuu wako Mungu anafanya mambo mawili,

*Moja*
Mungu anatengeza sifa zetu /God develops our character.
Mungu anaanza kukupitisha kwenye mazingira mepesi na magumu ili kukuimarisha, na hapa mtu akipita kwenye changamoto nzito, ndio anakuwa mtu bora zaidi, Joseph alikataliwa na ndugu zake, akauzwa utumwani, hata alipofika utumwani akasingiziwa amembaka mke wa bosi, akitiwa jela na badae kutoka waziri Mkuu. Hapo tayari amejifunza uvumilivu, kusubiri, upole, kuchagua mambo mema, upendo na tabia ambazo hata akiwa kiongozi watu hawata juta, tofauti na leo kuna watu wamekuwa viongozi bila kuandaliwa na kupotelea kwenye nafasi na kusahau kilicho wapeleka.

  Unaweza kuwa na biashara kubwa, huduma, kazi n, nzuri, kampuni kubwa swali je, vipi ukipewa nafasi ya kumiliki leo, utaweza kugusa maisha ya watu au unajitazama wewe tu?

*Mbili*
Kuzalisha majukumu sahihi ndani yetu, Mungu anaruhusu changamoto ili tutambue majukumu yetu, hutakiwi kuogopa, kwani wakati tunazaliwa Mungu alitupa kusudi la kuishi duniani ila hatukujua majukumu yetu kutimoza hilo kusudi, hivyo ni muhimu ukae kwenye Darasa la Mungu ili uweze kujifunza namna bora ya kupifikia kule uwendako.

Mungu alihitaji kumtengeneza Joseph aweze kujizuia au kuwa na kiasi, /self control, ndio maana alimpitisha kwenye jaribu la kusingiziwa kumbaka mke wa bosi wake Potifa.

Ugumu wa maisha ni sehemu ya mpango wa  Mungu kukufikisha kule kwenye kusudi lako.

Mafanikio ni mchakato mrefu sana kuliko tunavyo danganywa na wahamsishaji tukichulia rahisi, ila ukweli tunatakiwa kuweka nguvu, bila kukata tamaa na kuwa na imani kubwa juu ya utimilifu wake.

Saturday, October 13, 2018

BADO WATU WANA NDOTO ZA KUWA MABILIONEA

BADO WATU WANANDOTO ZA KUWA MABILIONEA.

Kuna mabilionea 1,645 duniani.Lakini ni 400 hivi ambao wamekuwa hivyo wenyewe(wengine waliobaki wamerithi fedha zao.)

Katika hawa walioutengeneza wenyewe kwa idadi kubwa ni WAWEKEZAJI.

WAWEKEZAJI.

Haijalishi ni aina gani ya biashara unayotaka kuifanya,anza kuwa na mtazamo,siyo wa ujasiriamali au mfanyabiashara,bali wa mwekezaji.

Hata kama unataka kufungua kibanda cha kahawa,ubunifu wa mavazi,nk.-fikiri kama mwekezaji.

Na hii hapa ni misemo ambayo itakujenga zaidi.Minne niya wawekezaji wakubwa kwa sasa duniani na mmoja ni wa mtu mwenye hekima:

1."Kama hutofurahia kuwekeza katika kitu kwa miaka 10,basi acha kuwekeza hata kwa dakika 10."---Warren Buffett

2."Changamoto huja pale ambapo hujui cha kufanya."----Warren Buffett.

3."Bila ya hamasa,huwezi kuwa na nguvu.Bila ya nguvu,huna chochote".---Warren Buffett

4."Hatuhitaji kuwa na akili nyingi kuzidi wote.Tunahitaji kuwa na nidhamu zaidi ya wote."---Warren Buffett.

5."Uwekezaji wa fikra unalipa faida nzuri."---Benjamin Franklin

Katika biashara ishi na uvute pumzi ya kanuni hizo.Zikumbuke,zitakulinda hata usishindwe.

Chagua kitu kimoja,ambacho una hamasa na nguvu ya kukifanya na kifanye kwa muda mrefu.

Nidhamu itakuja yenyewe ukiwa na kitu kimoja ulicho lenga kukifanyia kazi.

Anza kwa kuwekeza muda mwingi kwenye kujifunza-ijenge akili yako.
Soma vitabu,hudhuria makongamano,tafuta mshauri,ukiwa kwenye gari sikiliza hotuba za wahamasishaji badala ya Singeli....

Mgema Jr

KUACHANA NI FASHION MBOVU

DUNIA YA MAHUSIANO KIFO CHA MENDE-SEHEMU YA 2

DUNIA YA MAHUSIANO KIFO CHA MENDE

I
DUNIA YA MAHUSIANO KIFO CHA MENDE
SEHEMU 1.
Kwa miaka ya sasa yaani kizazi cha dot.com kama ambavyo kinaitwa suala la kuanza mahusiano rasmi na yasio rasmi sana limekuwa ni jambo la kawaida sana kwa Afrika ukilinganisha na miaka ya nyuma kidogo.
Ilikuwa ni nadra sana kwa vijana ambao nia ya dhati ya kuoa au kuolewa kuwakuta kwenye mahusiano ya kimapenzi lakini sasa limekuwa jambo la kawaida sana.
Miaka ya nyuma kidogo kukuta jamii ikizungumza mambo haya ilikuwa nadra sana lakini sasa ni kawaida sana na wakati mwingine ndiyo zimekuwa stori kubwa za siku kwa rika zote imani zote na kada zote kwa ujumla.
Stori bila kuwepo stori inazungumzia mapenzi hizo siyo stori tena.
Usasa na kuporomoka kwa maadili kwenda na kasi ya mabadiliko ya sayansi na Teknolojia lakini pia uhuru nje ya mipaka na kila japo kuwa chini ya sheria tetezi kwa vijana wa jinsia zote ni chanzo cha yote haya, imefikia mahali binti au kijana wa kiume kutokuwa kwenye mahusiano ni ushamba yawezekana ni kweli kabisa kwa sababu ushamba ni kutokuwa na taarifa kamili juu ya jambo fulani.
Kuwa kwenye mahusiano sio kesi sana kama nia ya dhati au mapatano ya wawili hawa yana nia moja kabisa na mwelekeo wao wanaufahamu vema.
Shida inakuja hapa wengi tunaingia kwenye mahusiano kama fasheni ili mimi nami nionekane nina boy au Girl friend bila hata kujua kwa nini uko kwenye hiyo chaini ya mahusiano inauma sana.
Wengi tumeingia hapa bila kuwa na elimu na kujua Thamani yake matokeo yake watu wameumiza mioyo ya watu wengi sana siyo wasichana wala vijana wa kiume
Watu wanaugulia maumivu makali kama mkuki wenye sumu kupenya kwenye moyo hakika ni majeraha na vidonda visivyopona.

Kwa kutokujua maana na malengo ya kuingia kwenye mahusiano wengi wamejikuta wakicheza mchezo na kujizawadia mimba ambazo hawakuzipanga mwisho ni kuchomoa na kuua.
Laana ya vizazi na vizazi inazitafuna familia nyingi Roho za watoto walionyofolewa damu zao zinalilia kwenye nyoyo na fahamu za waliotenda mambo hayo.
Laana juu ya laana tukijipa matumaini kuwa Mungu anasamehe siwezi bisha ila tunapishana na mafanikio mengi yenye baraka ndani yake.

Kwa nini umwache mwenzako bila sababu mabinti na vijana wakati mwingine watu wanakula viapo na machozi mengi lakini mwisho wa siku bila sababu ya msingi binti anasema kuanzia leo nasitisha mahusiano wewe...........kumbuka ukiumiza  moyo mtu alieyekuwa amemanisha ni madhara makubwa sana mbele yako.........kumbuka kila ufanyalo kwa wema ipo siku utapokea ijara njema lakini wewe mrubuni wa mapenzi utakufa kwa namna yoyote either kunyimwa watoto au kuachwa pia au kupewa jitu jeuri sana
Acha niishie hapa tutaendelea kesho kutwa
REMEMBER WHAT GOES AROUNDCOMES AROUND
2018 THE YEAR OF ACHIEVEMENTS

Monday, October 8, 2018

GUNDUA UWEZO NDANI YAKO

DISCOVER YOUR POTENTIAL IN YOU/ GUNDUA UWEZO NDANI YAKO ----1

Kila mtu ana uwezo wa kipekee.Kuna mtu ana uwezo mkubwa wa kuongoza lakini bado hajafahamu uwezo alio nao .Kuna mtu ana uwezo mkubwa wa kuzungumza lakini bado hajielewi .Kuna mtu ana uwezo mkubwa wa kuandika lakini hadi anavyosoma makala hii bado hajielewi maana hajawi kuanza kuonesha uwezo wake .Kwa kutambua uwepo wa watu wengi wasiojua uwezo walio nao nimekuandalia makala zitakazoamsha uwezo ulio ndani yako ili ukufikishe kule unakotaka kufika.

Mungu alivyokuumba aliweka ndani yako uwezo mkubwa sana kwa bahati mbaya watu tumeshindwa kutambua uwezo tulionao.Ni lazima kama unataka kufika kule unakotaka kufika kufahamu kabisa nini unaweza kufanya vizuri kwa uwezo uliopewa na Mungu .Acha kuwasikiliza watu wanaokukosoa na watu wanaokurudisha nyuma .Wewe amini katika uwezo wako ambao uko ndani yako .

Kama unaweza kuimba vizuri fahamu huo ndio uwezo Mungu alikupa .Tumia vizuri uwezo huo bila kugeuka nyuma na utafika mbali sana .Acha kuangalia madhaifu uliyonayo lakini angalia uwezo ulio nao .

Watu waliofahamu uwezo wao (maeneo yao ya kujidai ) na wakajua namna ya kuwajibika ,walifika mbali sana .Je ,watu hawa waliofika mbali hawakuwa na madhaifu ?  Jibu ni Hapana walichokiangalia ni uwezo ambao walikuwa nao kuliko madhaifu yao .

Uwezo ulionao hauzuiliwi na jambo lolote.Haijalishi umezaliwa wapi na unaishi wapi uwezo wako ukiamua kuutumia utaonekana tu.Kama unaweza kucheza mpira vizuri  hakikisha unacheza mpira kwa nguvu na akili yako yote maana hapa ndipo mafanikio yako yaliko .Kama unaweza kuchekesha watu fanya hivyo ukielewa kabisa wapo watu ambao wamefanikiwa kupitia uchekeshaji .

Watu hawa walivyoelewa uwezo walionao maisha yao leo yamebadilika.

Nick Vujic
Nick ni mlemavu asiyekuwa na miguu wala mikono ambaye mbali na kuwa alizaliwa mlemavu hivyo alielewa eneo lake ambalo alikuwa na uwezo nalo .Nick baada ya kuona hawezi kazi za kutumia mikono au miguu alianza kufikiri nini ana uwezo nacho na akagundua anaweza kuhamasisha watu na watu wakahamasika .Nick bila kuchelewa alianzisha taasisi yake ambaye yeye aliiita  taasisi ya maisha bila miguu (life without limbs) na akaanza kuzunguka dunia nzima kuhamasisha watu hasa walemavu .Leo Nick Dunia nzima inamfahamu.

Mwalimu Julius Nyerere
Mwalimu Nyerere ni ni mtu  ambaye alifahamu kuwa alikuwa na uwezo wa kuongoza watu na akatumia uwezo wake kwa viwango vikubwa sana leo Mwalimu Nyerere Dunia nzima inamkumbuka kwa kuwa alitumia uwezo wake aliokuwa nao.

Mbwana Sammatta
Mbwana Samatta baada ya kufahamu kuwa Mungu ameweka uwezo wa kucheza mpira vizuri ndani yake alianza mara moja kucheza mpira .Samatta hakuwa anacheza kama wachezaji wengine wanaofikiria kucheza mpira Simba na Yanga maisha yao yaishie hapo lakini yeye alicheza huku akijua siku moja dunia itakuwa ikimsikia na kufuatilia uwezo wake .Mtazamo wake ulikuwa mtazamo mpana wa kuhakisha uwezo wake unamtangaza Duniani .Leo Mbwana Sammatta Dunia inamjua na hakika mafanikio yake si haba.

MC PILIPILI
MC Pilipili alivyogundua kuwa ana uwezo wa kupangilia maneno na kuongea mbele za watu aliamua kuwa mshereheshaji (Master of Ceremony) .Leo Mc Pilipili amefika mbali sana kwa kuwa siku moja aliamua kutumia kile kilichoko ndani yake

Ni lazima ujue wewe ni mzuri na kufanya katika viwango vikubwa sana bila kuangalia mwenzako anafanya nini .Lazima ufike mahali uorodheshe vitu unavyofanya kwa uzuri na hivyo ndivyo vitakutoa katika maisha .Acha kuamini kuwa vyeti vyako ndivyo pekee vitakufanikisha utachelewa sana .Inuka anza kuangalia nini unaweza kufanya ili maisha yako yabadilike .

Unajua nini ? Unaweza kufanya nini ? unaweza kufanya nini kwa uzuri ? .Amsha uwezo wako leo

Itaendelea.

Friday, October 5, 2018

MANENO YA DIAMOND KATIKA SAFARI YA MAISHA YAKE

MAMBO MACHACHE AMBAYO NI MUHIMU KUJIFUNZA KUTOKA KWA KIJANA MWENZETU DIAMOND ALIYOYASEMA KWENYE SIKU YA KUZALIWA KWAKE

Tahere 2/10/2018 ilikuwa ni siku maalumu sana ya Nasibu Abdul alimaarufu diamond ilikuwa siku ya kuzaliwa kwake

Kuna mambo mengi sana alizungumza Diamond kuhusu maisha yake ya muziki hata maisha kabla ya mziki yani alikotoka hadi hapa alipo.
Yako mambo mazuri sana ya kujifunza kutoka  kwa Diamond  kwa kijana anayetaka kutoka kimaisha sio tu kwa njia ya muziki lakini katika kila jambo unalofanya.

Nimefurahia sana kusikia yeye mwenyewe akizungumza na kuelezea alikopita na mambo aliyofanya hapo kabla hajawa DIAMOND mpaka alipokuja kuwa DIAMOND offcourse amezungumzia mambo mengi mazuri kama ifuatavyo

Hakuchagua kazi diamond alifanya kila kazi iliyokuwa mbele yake ambayo haikuvunja sheria au kwa lugha nyepesi kazi haramu.......Diamonda
1.aliuza mchanga
2.Alifanya kazi petrol station
3.Aliuza nguo
4.Alipiga picha mfumo wa zamani
Then diamond alisema ili uweze kufanikiwa Pamoja na kufanya kazi kwa bidii mambo yafuatayo lazima yachukue nafasi kwenye harakati zako
a. Ubunifu katika kila kazi unafanya
B. Bidii na maarifa ujuzi pia ni lazima
C. Uaminifu katika kazi yako na kazi za watu hii itakusaidia kujenga brand yako ya kuaminika kwa watu na siku nyingine watu watatamani kufanya kazi na wewe.
d. Kutokukata tamaa...kuna wakati unahitaji mtu fulani awe daraja lako kufikia ndoto zako lakini ni ngumu kumpata lakini unachopaswa kufanya pambana hakikisha adhima yako inatimia
e. Mwombe Mungu sana kwa kila jambo
f. Weka nia ya dhati toka moyoni dhamiria kufikia matamanio yako.


Alisema tena kumbuka kutengeneza mazingira ya watu kukupa kazi ajira na mambo mingine
Hapa akasema kuwa smart kuanzia nje hadi namna ya kufikiri jiupushe na mihadarati haisaidii kabisa.


Katika safari ya mafaniko mambo ya kukatisha tamaa ni mengi lakini usikubali yakushinde bali pambana kuyashinda. Wapo watu wengi sana amabao wanakatisha vijana tamaa kuwa wewe huwezi jambo fulani labda jambo fulani ndo unaweza hapana hilo unaloamini unaliweza na linamanufaaa kwako fanya  pambana mpaka mwisho utafanikiwa.

Tumia kila nafasi unayopata ukijua nafasi nyeti huja mara moja tu kwenye maisha.
MWISHO
Kile Mungu anakupa baada ya kupambana kumbuka haya
Rudisha kwa jamii hata kama ni kidogo watu watakuombea na Mungu atakuinua zaidi ya mahali utakapokuwa
Aliyofanya diamond leo Tarehe 5/10/2018
Kawapa vijana wenzake wa tandale pikipiki 20
Watu 1000 kuwapa bima
Wakina mama 100 amewapa mtaji
Kuna mama mlemavu amempatia bajaji
Katoa Gari kwa mpiga picha wake
Mengi amefanya hakika sadaka humwinua zaidi mtu
Prepared by Moses Mgema
Source Diamond plutnum
Contacts: 0755632375/0678355394
Facebook Moses zephania
Instagram & Twitter moses mgema

NA MAONO YA MAYLES MUNROE

MISINGI NA NGUVU: Dr. Myles Munroe alikuwa raia wa Bahama, aliyezaliwa tar 20/04/1954 na kufariki 09/11/2014.(64) kwa ajali ya ndege Binafsi aliyokuwa akitumia akienda kwenye moja ya mikutano yake akiwa na mke wake na wengine nane walipoteza maisha katika ajali hiyo moja.

Shughuli zake
Alikuwa mhubiri wa kimataifa, mwandishi, mwanzilishi wa huduma ya BFMI (Bahamas Faith Ministry International). mwalimu wa masomo ya uongozi, uchumi, kiroho na maisha ya mafanikio.

Pamoja na kuwa Dr. Myles Munroe ni hayati lakini bado mpaka sasa anaishi kufuatana na kazi yake aliyofanya katika kugusa maisha ya vizazi vyake na kwa kauli yake *nitakufa mtupu* nafikiri ilitimia japo ukianza kufuatilia masomo yake mbalimbali unaweza kuona aliwahi kufa.

Kwa nini Nimekuletea hiki kitabu

Maono ni kitu muhimu sana na kama mtu yeyote anataka mafanikio makubwa sana ya kifedha, kiroho, kiafya, kielimu, kimahusiano na kiakili basi cha kwanza kabisa ni kuwa na maono, na hiki ni moja ya vitabu ambavyo vinaeleza vizuri sana kuhusu MAONO, yani kinaeleza kwa lugha rahisi sana, nini maana ya maono, misingi na nguvu yake katika maisha ya kila mtu

Binafsi nilikuwa nafuatilia namna watu wanavyofundisha kuhusu maono, ndoto na kusudi ila waliyo wengi wameshindwa kuelezea kiusahihi eneo hili, kwani kila mtu amekuwa na uwelewa tofauti lakini nilipo pata kitabu hiki niliona suluhisho kwa kila mtu endapo atapata nafasi ya ya kukisoma kitabu hiki cha Maisha bila maono

Maisha mazuri ni yale ambayo yanatokana na mtu kuwa na picha ya baadae yake, kujua unaenda kufanya nini miaka michache ijayo, kuishi maisha ya namna gani, kukaa na watu gani, na kugusa watu wa aina gani.

Mungu aliweka kusudi ndani ya kila mmoja ndani yake na hiyo ndio thamani yako katika Dunia hii, ndani yako kuna dhahabu ila haiwezi kuchimbwa na mtu yoyote ila wewe mwenyewe hivyo lazima uamue mwenyewe kuishi maono yako, kuwa na maana harisi ya maisha yako.

Pasipo maono huwezi kuona Mbali zaidi ya hapo ulipo leo, kuwa na maono ni sawa na kwenda kukaa kilele cha mlima na muono wako unaongezeka.

Hivyo kama umeishi muda mrefu bila maono ,Myles anatuonyesha kitu ambacho wachache wamekuwa wakiishi na kufanikiwa.

Wednesday, October 3, 2018

JIFUNZE USIIGE MAISHA YA MWINGINE

OHabari za muda huu
Napenda kushare nanyi jambo muhimu sana kwa muda huu inaweza kuwa faida kwako leo hata kesho

Duniani kuna watu ambao wamekuwa wakiishi maisha ya ku copy na ku paste.......Yaani mtu anamuiga mtu fulani kwa kila kitu anachofanya wakati mwingine bila hata kujiuliza kwa nini mtu huyu amefanya jambo hili mwisho wa siku wamejikuta wakiangamia na kupotea kabisa lakini pia kupoteza ndoto na uwezo wao kwa sababu tu waliamua kuishi Maisha fulani ya kukopi.
Kuiga sio jambo baya lakini pia kumbuka kuwa kila mtu ameumbwa kwa kusudi na kazi yake hapa duniani hivyo unapoondoka kwenye kusudi au kazi ambayo Mungu alikupa mwisho wa siku maisha yako yatakoma duniani hapa hakuna ulichokifanya maana uliamua kuishi nje ya kusudi la Mungu

Kumbuka kuwa maisha ni mtihani ambao kila mtu amepewa mtihani wenye maswali tofaut na mwingine.
Kumbuka Maisha ni moja ya mtihani mgumu sana na watu wengi wanafeli kwa sababu ya kukopi Maisha ya wengine pasipo kufahamu kwamba kila Mtu ana maswali yake katika katika chumba cha mtihani.

Hivyo Kijana jaribu sana kukaa chini jikague jitathimini ili kuweza kujipambanua kuwa wewe ulizaliwa na lengo gani
Fanya kazi kwa bidii kuwa mbunifu ongeza maarifa katika kila jambo unalofanya.
Note
Sijasema kuwa usiwe na watu unaopenda kuwa kama wao hapana jifunze kwao njia na kanuni walizopitia kufika mahali walipo then baada ya hapo kaa chini chukua jema tupa kule lisilo faa
Halafu anza kufanya kile moyo na akili yako inakuambia kuwa ukifanya hiki utafanya katika ubora kwa kiwango cha juu na kwa ubora mkubwa zaidi.
Life is too short try to utilize every single second effectively through the natural gift or talent that God created with
Be blessed and have a very good moment 
By Moses

Tuesday, September 25, 2018

WAZAZI NA WAZAZI MNAOKUJA AMKENI SIKU ZIMEBADILIKA

PARENTS AND UPCOMING PARENTS WAKE UP DAYS HAVE CHANGED:
Nimshukuru sana Mungu kwa kuniwezesha kuwa mzima na mwenye afya tele kufikia sasa.
Nitoe pole kwa ndugu jamaa marafiki na wanamwanza na Tanzania kwa ujumla kwa msiba mkubwa ambao umelikumba Taifa letu siku ya Alhamis Tarehe 20/09/2018 kwa Meri ya Mv nyerere kuzama katika ziwa victoria.
Yote kwa Yote mola anapo ruhusu haku na wa kupinga. Zaidi ya yote Tumshukuru Mungu.

Leo napenda sana tujifunze mambo machache ambayo kwa hakika ni muhimu sana kuyajua.
Dunia tunayoishi inakwenda kwa speed sana na hakika mambo yamebadilika sana katika karne hii tuliyo nayo
ongezeko la maendeleo ya Teknolojia na utandawazi umechukua hatamu kwa wingi.
Maendeleo haya ya sayansi na Teknolojia yameweza kurahisisha sana njia za mawasiliano na utendaji kazi pia ukilinganisha na huko tulikotoka.
mambo ambayo yangeweza faywa na watu kumi leo watu watatu wanaweza kuhatekeleza kwa ufanisi wa hali ya juu sana na wakati sahihi.

Mahali ambapo ilitupasa kusafiri kupeleka mizigo au kupeleka habari fulani leo hatufanyi tena.
umekaa kwenye kiti unaratibu kila kitu hapo hapo na kila kitu kinafanikiwa kwa ufanisi ule ule ulioutaka
Express=Digital Age period ni muda ambao tunaishi.
Maendeleo haya yamekuja na matokeo Yote yaani
matokeo chanya  (positive results)
Matokeo hasi  (Negative results)
Tumeona kwa uchache matokeo chanya hapo juu japo sio yote ila tunaweza ongeza zaidi na zaidi

MATOKEO HASI  (NEGATIVE RESULTS)
Baada ya maendeleo haya kuchukua nafasi watu wengi wamekosa ajira
Idadi ya watu ambao wangehitajika kuajiliwa mahali fulani kama ni 10 sasa wanahitajika wawili au watu wakati mwingine mmoja tu.
Jiulize swali hawa wengine tisa nane na saba wako wapi?
posta ilikuwa na madereva lundo na posta ilikuwa active. Jiulize baada ya simu na matumizi ya scanning, Email simu calling sms nk. kuchukua hatamu wako wapi waliokuwa waajiliwa posta na maeneo mengine.
Baada ya hapo dunia imejikita katika ujasiriamali  (Entrepreneurship) kila mmoja barabarani na maeneo mengi watu wanafanya business.
Lakini bado sijajua kama watu wanachukua tahadhali ya kuwa kama ajira zilikuwa nyingi enzi hizo na leo ni changamoto je mambo ya ujasiriamali hayatafika mahali yabane iwe ilimradi watu wanafanya business.
Kiufupi ni kwamba biashara hazitakoma hata kama watu watakuwa wanaigana lakini bado watu wataendelea kufanya biashara.
Faida Je hilo ni swala lingine la kusubiri.

Kuna jambo muhimu sana kizazi cha leo lazima tuyajue lakini pia kuyafanyia kazi kwa haraka na kuwekeza nguvu kwa nguvu zote kuanzia rasilimal nafasi tulizo nazo ushauri nk kwa watoto wetu.
Mungu atabaki kuwa Mungu kabla ya misingi ya dunia aliyajua yote haya ndiyo maana akamwezesha kila mtu kitu cha pekee sana ndani yake.
Kipaji ni zawadi na hii zawadi ni zawadi ambayo hakuna anaweza kuigawa mzazi anaweza mpa mtoto wake kila kitu elimu fedha na mahitaji yote lakini kipaji ni Mungu pekee.
Dunia ya kwanza yaani nchi zilizoendelea Nchi za ulaya Kama England, German France nk. zinafurahia faida kubwa kutokana na vipaji vya watoto wao kuanzia kwenye soka mziki, Kikapu wasemaji wa hadhara  (Public speakers) waandishi wasimuliaji washauri wa masuala ya biashara, saikolojia, kudansi kupiga mziki, kuchora, kuchekesha na kila aina ya vipaji.
wenzetu walishituka mapema wakawekeza sana kwenye kile mtoto anakipenda lakini pia alicho na uwezo nacho.
Wanachofanya wanatoa elimu ili kumwezesha mtoto kujua Thamani ya kile kitu alicho nacho na namna ya kukitumia na kumletea manufaa.

kupitia njia hizo hakika dunia imeweza kushuhudia burudani mbalimbali kutoka kwa watu mbalimbali ambao waliweza na wanaoendelea kutumia vipaji vyao.
Mfano dunia ya soka imeshuhudia watu wengi waliozaliwa kwenye familia masikini na fukara wakibadilisha sura na maisha ya familia zao.
Iko mifano mingi ya vijana kutoka Amerika ya kusini kwenye nchi kama
Argentina, Brazil chile Uruguay peru Ambao  ni kina Alexes Sanchez, Ronaldo, Leo Messi, Ronaldinho Gaucho, Angel Di maria na wengine wengi  na baadhi ya nchi za Afrika magharibi  amabao ni Nwango kanu Didie Drogba Samwel Eto'o na Afrika mashariki kidogo Mbwana Ally  Samatta, Donald mariga na ndugu yake Victor wanyama toka nchini kenya kwa hakika wengi na baadhi yao walizaliwa kwenye kaya fukara sana lakini leo ni mamilionea na mabilionea wa kutupwa sababu kubwa ni vipaji.

Vile vile kwenye music,waigizaji iko mifano hai ya watu wanaovuna pesa kwa sababu ya music na uigizaji na uchekeshaji mifano hai:Mr Bin waimbaji Boyce Michael Jackson na wengine wengi hata hapa nyumban kidogo kina diamond Ali kiba kwa uchache angalau mifano ipo.
Wazazi wengi tunajaribu kukariri maisha sana Kitabu cha Rich dad and poor dad kinagusia sana kwa habari ya kijana ambae aliona elimu ya darasani kwake haikuwa much paid kwa sababu ni kama aliona wazazi wake wanafanyia kazi maisha ya kulipa kodi na mafao ya uzeeni ndipo mama ake alipogundua kuwa wao kama wazazi walikuwa wamekariri mfumo wa maisha ambao wazazi wao waliutumia hapo awali na hakujua kuwa dunia tayar ilikuwa nje ya kile alikuwa akikisshi.
Ndiyo wazazi wengi tulivyo hata sio kwamba tunasema watoto wasiende shule hapana lazima watoto waende shule lakini lazima tuwe namna nzuri ya kufanya vipaji vya watoto vinakuwa na manufaa kwao sana
Ajira kwa sasa hakuna lakini pia mtu anaetumia kipaji chake vema hakika hakuna mfanya kazi anaweza mgusa kiuchumi na kifedha mifano angalia diamond Ali kiba  lady Jdee Harmonize  Mbwana Samatta kwa hapa nyumban na wengine wengi
Majuu
Cristiano Ronaldo Leo Messi David Beckham Ronaldo delima LeBron James nk  ni watu matajiri wa kupindukia kwa sababu ya vipaji vyao
Lazima wazazi tushituke tuache kuishi kwa mazoea tusitumie nafasi zetu za uzazi kudidimiza na kuua vipaji vya watoto
wewe kama mzazi onya elekeza shauri na tekeleza hitaji la mtoto ili afanye jambo anapenda kwa uhakika kwa moyo na kwa upendo na kwa manufaa yake na kwako pia.
kwa leo tuishie hapo itaendelea......next time
Moses zephania Mgema
mwandishi
mgemamoses@gmail.com
0755632375/ 0678355394

Friday, September 14, 2018

Brand yourself

*CHAGUA UNATAKA KUWA BORA KWENYE NINI?*

Kila jambo lina bingwa wake, kama unakumbuka Michael Jackson alikuwa Bingwa wa Muziki wa Pop Duniani, Michael Jordan alikuwa ni bingwa wa mchezo wa kikapu.

Vivyo hivyo Pelle, Mike Tyson, Diana King na wengine kibao. Ukija Bongo kwenye Muziki wa Taarab, Malkia wa Mipasho, Khadija Kopa anakaa, Mfalme Mzee Yusuph anachukua kwa wanaume, Kina  diamond Ali kiba  na wengine wengi na ndivyo ilivyo kwa wengine na wengine.

Nimetolea mfano vitu hivyo vichache lakini kuna vitu vingi sana vinahitaji bingwa au bora wa kuviongoza au kuvifanya. Je, leo hii wakiita bingwa wa jambo fulani mtaani kwako utatoka au na penyewe hautaweza kuonesha uwezo au ubora wako?
Kuna watu wao huwa nyuma kwa kila jambo yaani ile kujifanya nyuma nyuma kwa kila kitu na hii imechangia watu wengi sana kupoteza karama vipaji vyao kwa sababu ya kuwa nyuma nyuma kwa kila jambo.
Jiulize una uwezo gani wewe kama wewe au wakati Mungu anakuumba kitu gani aliweka ndani yako na ili iweje aweke kwako na sio kwangu au kwa yule kiufupi unagundua kuwa
Mungu alikuamini
alijua wewe pekee ndo unaweza kukitendea haki kitu hicho
hivyo basi jaribu kukitumia kwa ajili yako na kikutambulishe kuwa mtu akihitajika kwa jambo fulani basi iwe ni wewe
Leo dunia ina mfahamu Tyson Diamond,Eric Shigongo, c.Ronaldo, Leo Messi.
Jay z Beyonce, Bob Marley na wengine wengi ambao walijipambanua na kutumia vipawa vyao mpaka leo hata kama wengine wamekufa lakini bado kazi zao zinaishi
Jiulize Mimi nitakumbukwa na nini  ?

Jifunze au jitengeneze kuwa bigwa wa Jambo Fulani kama Mungu alikuamini na kukuumba na akakupa uwezo fulani tumia nafasi ya uwezo huo au kipaji hicho kujitanbulisha na kutambulika kwenye jamii kwa manufaa yako au manufaa ya kazazi chako ninacho
Muda wa kuwaandalia watoto wako maisha mazuri ni leo kwa kutumia kile ulicho nacho kama ni kipaji au kazi na biashara uliyo nayo
work hard

MUANDALIE  MAZINGIRA MWANAO  ULIYENAYE AUAJAYE.

0719110760
Email mgemamoses@gmail.com
Moses zephania Mgema.
Instagram: Mo_mgema

Thursday, August 2, 2018

Madhara ya kufikiri muda mrefu

Kiumbe binadamu ni kiumbe  aliyeumbwa  kipekee sana ukilinganisha na viumbe wengine kama mimea wadudu na wanyama wa aina zote.
Binadamu amepewa uwezo na utashi unaomfanya kuwa na uwezo wa kufanya mambo yake kwa weledi na kwa ufanisi na kujisimamia.
Amepewa utashi wa kutambua jema na baya kama vitabu vya dini vinavyotuambia.
Binadamu huyu tangu aumbwe amekuwa na maisha yenye mchanganyiko Fulani ambao unamfanya wakati mwingine atenge muda wake kwa ajiri ya kufikiri ili mambo yake yakae sawa.
Hebu tutazame mambo machache ambayo mtu anaefikiri sana yaweza kumpata ( matokeo hasi)
1. Kuchelewa kuchukua maamzi na wakati mwingine kusababisha madhara
2. Huwa ni ngumu sana kufikia malengo yao hasa kibiashara na kimahusiano kwa sababu muda wote anaofikiri
  . huona changamoto nyingi kuliko njia za kutatulia hizo changamoto hasa kwa suala zima la biashara na kazi
. wakati mwingine hupata msongo wa mawazo kwa sababu anaweza akachukua muda mwingi kufikiri jambo Fulani na akaona matokeo makubwa kabla hajaweka utekelezaji anapokuja kufanya kwa vitendo na isifikie mahali alitazamia basi kwake huwa anaumia sana
.Huzeeka kabla ya umri wao
. Hukosa fursa
. Huwa sio rahisi kukubali kama wanaweza kukosea.
Note
Hujashauriwa kuacha kufikiri ila jaribu kuwa na kiasi

Thursday, July 26, 2018

NGUVU YA MTAZAMO CHANYA

Mtazamo ni moja ya vitu vyenye uwezo wa kuamua hatima ya maisha ya mtu binafsi na vikundi
Mfano mtu akiwa na mtazamo chanya Mara nyingi mambo haya huwa nayo:
1. Huwa jasiri
2. uthubutu
3. Ana uwezo wakujitia moyo na nguvu (self courageous)
4. Huona kuwezekana kwa kila jambo hata kama kwa wakati huo haoni mlango
5. Anajiamini
7. Huona nyuma ya vizingiti
8. Hutumaini kuwa ipo siku atatoboa mwamba
9. Anaishi kwa kutambua kuwa penye ugumu wa mwamba ndipo penye madini
10.Anaamini kama yule aliweza basi hata yeye ataweza
Imani yake huambatana na kuamini kuwa Mungu hubariki mikono yenye bidii

Mtu mwenye mtazamo hasi:
Ni kinyume ya yote aliyo nayo mtu mwenye mtazamo chanya
1. Huona vizuizi daima
2. Haamini katika uwezo alio nao
3. Mwepesi wa kukata tamaa
4. Anaamini kuwa kuna fungu LA kupata na fungu LA kukosa
5. Si mwenye bidii thabiti
6. Hana uthubutu
7.Ni mtu mwenye maneno mengi bila vitendo
8 Siku zote mifano yake Ni kwa walio shindwa
Note
Jitazame na jitathimini wewe uko upande upi kati ya pande hizi za mtazamo

Sunday, July 22, 2018

DUNIA MPYA YA KUJIAJILI NA MAFUNDISHO HASI JUU YA MFUMO RASMI WA ELIMU

Habari, imeandikwa na.....
Moses z. Mgema
Ulimwengu unakwenda kasi sana, mabadiliko na mifumo ya maisha ya watu kila siku  unabadilika sana, ongezeko la maendeleo ya sayansi na teknolojia umekuwa kwa kasi sana kiasi kwamba dunia si tu imekuwa ni kama kijiji kimoja Bali imesogea kabisa kwenye viganja vya mikono yetu.
Taarifa mbalimbali umepatikanaji wake umerahisishwa sana kwenye nyanja zote za Habari ziwe in Habari rasmi, michezo, burudani, kijamii, kidini, taaluma na masuala ya siasa, biashara na uchumi.
Kutokana na ongezeko la upatikanaji huu wa taarifa na Habari watu wamefunguka na wamejua mambo mengi ambayo hapo awali haikuwa rahisi kuyapata hasa kwa watu ambao hawakupata nafasi ya kwenda shule.
Upatikanaji huu wa taarifa umejenga jamii kubwa iliyo elimika na kujitambua kwa kiasi kikubwa sana.
Watu wamepata taarifa wamejenga maisha yao.
Na mambo mengine mbalimbali ambayo kwa hakika pasipo ukuaji wa technologia na mafumo wa Habari na mawasiliano sijui tungekuwa wapi.....
Lakini katikati ya ukuaji wa mfumo wa habari lakini pia watu wengi wanajaribu kuipotosha jamii kwa Habari ya taaluma rasmi hasa ukizi gatia kuwa mtazamo wa zamani ulimwandaa mtu kuajiliwa kuliko kujiajiri.
Ilifahamika kuwa MTU aliyekwenda shule alikuwa na uhakika wa maisha yake ukilinganisha na MTU ambae hajaenda shule maana huyu angepata ajira ambayo ingeendesha maisha yake.
Lakini leo hii idadi ya wasomi imeongezeka sana ulimwenguni, kuanzia Nchi za dunia ya tatu mpaka kwa mataifa yaliyopiga hatua kiuchumi na mambo mengine ya kijamii.
Kutokana na idadi hiyo kuwa kubwa uwiano wa ajira zinazotengenezwa kwenye mataifa hairingani kabisa na idadi ya wasomi wanaohitimu kila mwaka kutoka vyuo mbalimbali duniani.
Hivyo ongezeko la watu kutokuwa na ajira inazidi kuwa kubwa kila kukicha na suluhisho lake ni kama halipati ufumbuzi zaidi yake linazidi kuongezeka sana
Lakini kwa wasomi wenye kuelewa maana ya Elimu toka zamani bado haiwapi shida wala changamoto
Maana kuwa na elimu ni kuelimika, kuwa mfano kwa wasio wasomi, kuleta mabadiliko ya fikra na mitazamo kwenye jamii na kutumia fursa zilizopo kwenye maeneo yetu.
Wasomi wengi wamefanya ivo, lakini shida inatokea kwa baadhi ya watu kupotosha uma kuwa elimu sasa haina maana sana maana watu wanamaliza vyuo lakini hakuna kazi.
Swali dogo.......?
Nani alikuambia msomi ni wa kuajiliwa tu au nani kakuambia kwenda shule lengo lake ni moja tu ? Hapo tunakosea
Maana ya elimu
Ni kuelimika
Kupata maarifa
Kufungua macho na kuziona fursa nje ya ajira
Kuwafanya wengine wasio na taarifa kuwa na taarifa
Kuwa chachu ya maendeleo
Kutengeneza ajira kwa wasio wasomi.
Kuhamasisha watu kuona thamani ya elimu
Mwisho kuajiliwa kama last option.

Note.
Kuna watu mitaani hata kwenye social media wanahamisha kuwaaminisha watu kuwa sasa elimu haina thamani tena, hapana
Mtazamo wa elimu ni kuleta mageuzi ya fikra kwa mtu mmoja mmoja mpaka jamii kwa ujumla, kazi ni ziada.
Kwa hiyo tusidanganyike watu wakaacha vyuo au kutokwenda shule kabisa kisa ajira hakuna ajira zipo vichwani mwetu tutumie vizuri
Tuachane na wapotoshaji wasio jua kuwa hata maarifa na madarasa wanayosoma online ni maarifa ya waliopita shule.
Elimu ni msingi imara wa mafanikio kwa kizazi mpaka vizazi
Kuajiliwa kuna mwisho Bali elimu ni hazina kwa vizazi na vizazi.
Tuwapuuze, tusome zaidi
Ili kuiendelea kuifanya dunia kuwa mahali salama na penye furaha ya kuishi
"This place is the better place for everyone