Thursday, July 26, 2018

NGUVU YA MTAZAMO CHANYA

Mtazamo ni moja ya vitu vyenye uwezo wa kuamua hatima ya maisha ya mtu binafsi na vikundi
Mfano mtu akiwa na mtazamo chanya Mara nyingi mambo haya huwa nayo:
1. Huwa jasiri
2. uthubutu
3. Ana uwezo wakujitia moyo na nguvu (self courageous)
4. Huona kuwezekana kwa kila jambo hata kama kwa wakati huo haoni mlango
5. Anajiamini
7. Huona nyuma ya vizingiti
8. Hutumaini kuwa ipo siku atatoboa mwamba
9. Anaishi kwa kutambua kuwa penye ugumu wa mwamba ndipo penye madini
10.Anaamini kama yule aliweza basi hata yeye ataweza
Imani yake huambatana na kuamini kuwa Mungu hubariki mikono yenye bidii

Mtu mwenye mtazamo hasi:
Ni kinyume ya yote aliyo nayo mtu mwenye mtazamo chanya
1. Huona vizuizi daima
2. Haamini katika uwezo alio nao
3. Mwepesi wa kukata tamaa
4. Anaamini kuwa kuna fungu LA kupata na fungu LA kukosa
5. Si mwenye bidii thabiti
6. Hana uthubutu
7.Ni mtu mwenye maneno mengi bila vitendo
8 Siku zote mifano yake Ni kwa walio shindwa
Note
Jitazame na jitathimini wewe uko upande upi kati ya pande hizi za mtazamo

No comments:

Post a Comment