Tuesday, October 16, 2018

UKWELI NI UHURU

UKWELI NI UHURU

Misingi na nguvu ya Maono.

Mwandishi.
        Dr. Myles Munroe.

Kanuni ya sita ya kutusaidia kutimiza maono,..
........................................
Uwelewe mchakato wa maono /Understand the Process of Vision.
........................................
Mithali 16:9
Moyo wa mtu hufikiri(hupanga) njia yake, bali Bwana huziongoza hatua zake/In his heart a man plans his course but the Lord determine his steps. (emphasis added).

Maono ni mchakato wa siku nyingi, Mimi na wewe tunatakiwa kuwa na mipango lakini kazi ya Mungu ni Kuongoza hatua zetu.  Nini muhimu kujua ni kuwa utimilifu wa maono unaanza pale unapogundua maono yako na kupanga mipango ya kuishi maono.

Hii ni rahisi sana, unatakiwa kuishi maono yako, kwanzia sasa kwa kuwa umesha fahamu, huku ukijua kila siku kuna kitu Mungu atakuongoza kufanya.

Njia ya kufikia kutimiza ndoto zetu, inatuandaa kwa vitu viwili muhimu.
   Kwa sababu pamoja na kuona picha ya maono yako ambayo inaweza kukupelekea utamani kufika kesho lakini anakuwa amekuandalia njia ya kwake ya kufikia maono hayo. Kumbuka muda wa mfalme Daudi kupakwa mafuta na kuja kuwa mfalme ulikuwa mrefu sana,

Je, vipi kuhusu Joseph akiwa na miaka 17 aliota ndoto ya kuwa mkuu siku za usoni (Mwanzo 37:9-10), lakini mchakato wa wao haukuwa rahisi ilitakiwa wapite kwenye shule ya Mungu, ili Joseph kuja kuwa mtu mkuu sana Misri, kwanza njia alizopita kama Mungu angemwambia au muonyesha asingefika,angeishia njiani kwa sababu ya ugumu wake.

Ni kweli una ndoto kuwa sana za kugusa maisha ya wengine kwa maana hiyo unaenda kuwa mtu mkubwa na mwenye nguvu hata Kifedha lakini swali ni ulifikia hiyo hatua kubwa bado utaendelea kutenda mema kwa watu au utapotea?

Basi ukiwa katikati ya kufikia ukuu wako Mungu anafanya mambo mawili,

*Moja*
Mungu anatengeza sifa zetu /God develops our character.
Mungu anaanza kukupitisha kwenye mazingira mepesi na magumu ili kukuimarisha, na hapa mtu akipita kwenye changamoto nzito, ndio anakuwa mtu bora zaidi, Joseph alikataliwa na ndugu zake, akauzwa utumwani, hata alipofika utumwani akasingiziwa amembaka mke wa bosi, akitiwa jela na badae kutoka waziri Mkuu. Hapo tayari amejifunza uvumilivu, kusubiri, upole, kuchagua mambo mema, upendo na tabia ambazo hata akiwa kiongozi watu hawata juta, tofauti na leo kuna watu wamekuwa viongozi bila kuandaliwa na kupotelea kwenye nafasi na kusahau kilicho wapeleka.

  Unaweza kuwa na biashara kubwa, huduma, kazi n, nzuri, kampuni kubwa swali je, vipi ukipewa nafasi ya kumiliki leo, utaweza kugusa maisha ya watu au unajitazama wewe tu?

*Mbili*
Kuzalisha majukumu sahihi ndani yetu, Mungu anaruhusu changamoto ili tutambue majukumu yetu, hutakiwi kuogopa, kwani wakati tunazaliwa Mungu alitupa kusudi la kuishi duniani ila hatukujua majukumu yetu kutimoza hilo kusudi, hivyo ni muhimu ukae kwenye Darasa la Mungu ili uweze kujifunza namna bora ya kupifikia kule uwendako.

Mungu alihitaji kumtengeneza Joseph aweze kujizuia au kuwa na kiasi, /self control, ndio maana alimpitisha kwenye jaribu la kusingiziwa kumbaka mke wa bosi wake Potifa.

Ugumu wa maisha ni sehemu ya mpango wa  Mungu kukufikisha kule kwenye kusudi lako.

Mafanikio ni mchakato mrefu sana kuliko tunavyo danganywa na wahamsishaji tukichulia rahisi, ila ukweli tunatakiwa kuweka nguvu, bila kukata tamaa na kuwa na imani kubwa juu ya utimilifu wake.

No comments:

Post a Comment