Tuesday, October 16, 2018

NGUVU YA MAONO Na MAYLES

10. UKWELI NI UHURU.

Uchambuzi Wa Kitabu.
Misingi na Nguvu Ya Maono.

Mwandishi(Author).
        Dr. Myles Munroe.
        (1954- 2014)
Kanuni ya nne , ya kukuweza kuishi na kutimiza maono yako ni pamoja na :-
........................................
*Kuwa na shauku ya maono yako /Posses the Passion of Your Vision* .
........................................
Je, unahasira kiasi gani na maono yako? Unajisikiaje pale bado hujaanza kugusa maisha ya watu na uwezo umepewa?

Watu waliyotambua kuwa kuwepo hapa Duniani ni zaidi ya kuishi, ndio wanafanya mabadiliko makubwa katika ulimwengu huu toka mwanzo, watu ambao kwao maisha ni zaidi ya kula, kuvaa, kustarehe, yani watu ambao furaha yao haitokani na uwingi wa pesa wanazotengeza ila alama wanazo achilia ndani ya mioyo ya watu.

Watu wengi hawana shauku ya kufanya mambo makubwa katika maisha yao kwa sababu hawana shauku kutoka ndani ya Mioyo yao, na maono Pekee ndio chanzo cha shauku.

Shauku/Passion ina maanisha kile unacho kiamini ni kikubwa kuliko unacho kiona.

Ni shauku / Passion itakusaidia kushinda vikwazo kwa sababu kilichopo ndani ya moyo wako ndio kinakusukuma katika maisha yako ya kila siku, kuna wakati tunatafuta namna mbalimbali ili tuweze kufikia ndoto zetu lakini, bila kuwa na shauku ndani Mioyo yetu hatuwezi kustahimili vikwazo na changamoto zitakazo tokea njiani, zaidi ya yote ukiwa na shauku hata kama watu watakuangusha mara ngapi, utasimama Mpaka wao wachoke na kukuacha wenyewe.

Shauku ya moyo wako juu ya maono itakusaidia Kuzingatia ndoto yako bila kuishia njiani.

Hongera rafiki kwa mfululizo huu, endelea kupata Kilicho bora zaidi...

Kiu yangu ni kuona watu wanaoishi zaidi ya wanacho kiona leo, wenye uwezo wa kugusa maisha ya ulimwengu huu.

Mwisho.
Kwa mgeni karibu, kwenye kundi hili, tunajifunza na kuchukua hatua ili kufanya maisha yetu na wengine kuwa bora,zaidi.

Pia taarifa ya darasa la leo 14/10/018 juu ya uwekezaji, kwanzia saa 2:00-4:00usiku.

💥Maeneo tunayoenda kujifunza,
  1.maana ya uwekezaji na uhuru wa kifedha pamoja na umuhimu wake.

2.Maeneo matano ya kufanya uwekezaji katika maisha yako.

3.Mbinu za kufanya uwekezaji bora.

No comments:

Post a Comment