Friday, October 5, 2018

NA MAONO YA MAYLES MUNROE

MISINGI NA NGUVU: Dr. Myles Munroe alikuwa raia wa Bahama, aliyezaliwa tar 20/04/1954 na kufariki 09/11/2014.(64) kwa ajali ya ndege Binafsi aliyokuwa akitumia akienda kwenye moja ya mikutano yake akiwa na mke wake na wengine nane walipoteza maisha katika ajali hiyo moja.

Shughuli zake
Alikuwa mhubiri wa kimataifa, mwandishi, mwanzilishi wa huduma ya BFMI (Bahamas Faith Ministry International). mwalimu wa masomo ya uongozi, uchumi, kiroho na maisha ya mafanikio.

Pamoja na kuwa Dr. Myles Munroe ni hayati lakini bado mpaka sasa anaishi kufuatana na kazi yake aliyofanya katika kugusa maisha ya vizazi vyake na kwa kauli yake *nitakufa mtupu* nafikiri ilitimia japo ukianza kufuatilia masomo yake mbalimbali unaweza kuona aliwahi kufa.

Kwa nini Nimekuletea hiki kitabu

Maono ni kitu muhimu sana na kama mtu yeyote anataka mafanikio makubwa sana ya kifedha, kiroho, kiafya, kielimu, kimahusiano na kiakili basi cha kwanza kabisa ni kuwa na maono, na hiki ni moja ya vitabu ambavyo vinaeleza vizuri sana kuhusu MAONO, yani kinaeleza kwa lugha rahisi sana, nini maana ya maono, misingi na nguvu yake katika maisha ya kila mtu

Binafsi nilikuwa nafuatilia namna watu wanavyofundisha kuhusu maono, ndoto na kusudi ila waliyo wengi wameshindwa kuelezea kiusahihi eneo hili, kwani kila mtu amekuwa na uwelewa tofauti lakini nilipo pata kitabu hiki niliona suluhisho kwa kila mtu endapo atapata nafasi ya ya kukisoma kitabu hiki cha Maisha bila maono

Maisha mazuri ni yale ambayo yanatokana na mtu kuwa na picha ya baadae yake, kujua unaenda kufanya nini miaka michache ijayo, kuishi maisha ya namna gani, kukaa na watu gani, na kugusa watu wa aina gani.

Mungu aliweka kusudi ndani ya kila mmoja ndani yake na hiyo ndio thamani yako katika Dunia hii, ndani yako kuna dhahabu ila haiwezi kuchimbwa na mtu yoyote ila wewe mwenyewe hivyo lazima uamue mwenyewe kuishi maono yako, kuwa na maana harisi ya maisha yako.

Pasipo maono huwezi kuona Mbali zaidi ya hapo ulipo leo, kuwa na maono ni sawa na kwenda kukaa kilele cha mlima na muono wako unaongezeka.

Hivyo kama umeishi muda mrefu bila maono ,Myles anatuonyesha kitu ambacho wachache wamekuwa wakiishi na kufanikiwa.

No comments:

Post a Comment