Saturday, October 13, 2018

BADO WATU WANA NDOTO ZA KUWA MABILIONEA

BADO WATU WANANDOTO ZA KUWA MABILIONEA.

Kuna mabilionea 1,645 duniani.Lakini ni 400 hivi ambao wamekuwa hivyo wenyewe(wengine waliobaki wamerithi fedha zao.)

Katika hawa walioutengeneza wenyewe kwa idadi kubwa ni WAWEKEZAJI.

WAWEKEZAJI.

Haijalishi ni aina gani ya biashara unayotaka kuifanya,anza kuwa na mtazamo,siyo wa ujasiriamali au mfanyabiashara,bali wa mwekezaji.

Hata kama unataka kufungua kibanda cha kahawa,ubunifu wa mavazi,nk.-fikiri kama mwekezaji.

Na hii hapa ni misemo ambayo itakujenga zaidi.Minne niya wawekezaji wakubwa kwa sasa duniani na mmoja ni wa mtu mwenye hekima:

1."Kama hutofurahia kuwekeza katika kitu kwa miaka 10,basi acha kuwekeza hata kwa dakika 10."---Warren Buffett

2."Changamoto huja pale ambapo hujui cha kufanya."----Warren Buffett.

3."Bila ya hamasa,huwezi kuwa na nguvu.Bila ya nguvu,huna chochote".---Warren Buffett

4."Hatuhitaji kuwa na akili nyingi kuzidi wote.Tunahitaji kuwa na nidhamu zaidi ya wote."---Warren Buffett.

5."Uwekezaji wa fikra unalipa faida nzuri."---Benjamin Franklin

Katika biashara ishi na uvute pumzi ya kanuni hizo.Zikumbuke,zitakulinda hata usishindwe.

Chagua kitu kimoja,ambacho una hamasa na nguvu ya kukifanya na kifanye kwa muda mrefu.

Nidhamu itakuja yenyewe ukiwa na kitu kimoja ulicho lenga kukifanyia kazi.

Anza kwa kuwekeza muda mwingi kwenye kujifunza-ijenge akili yako.
Soma vitabu,hudhuria makongamano,tafuta mshauri,ukiwa kwenye gari sikiliza hotuba za wahamasishaji badala ya Singeli....

Mgema Jr

No comments:

Post a Comment