Wednesday, October 3, 2018

JIFUNZE USIIGE MAISHA YA MWINGINE

OHabari za muda huu
Napenda kushare nanyi jambo muhimu sana kwa muda huu inaweza kuwa faida kwako leo hata kesho

Duniani kuna watu ambao wamekuwa wakiishi maisha ya ku copy na ku paste.......Yaani mtu anamuiga mtu fulani kwa kila kitu anachofanya wakati mwingine bila hata kujiuliza kwa nini mtu huyu amefanya jambo hili mwisho wa siku wamejikuta wakiangamia na kupotea kabisa lakini pia kupoteza ndoto na uwezo wao kwa sababu tu waliamua kuishi Maisha fulani ya kukopi.
Kuiga sio jambo baya lakini pia kumbuka kuwa kila mtu ameumbwa kwa kusudi na kazi yake hapa duniani hivyo unapoondoka kwenye kusudi au kazi ambayo Mungu alikupa mwisho wa siku maisha yako yatakoma duniani hapa hakuna ulichokifanya maana uliamua kuishi nje ya kusudi la Mungu

Kumbuka kuwa maisha ni mtihani ambao kila mtu amepewa mtihani wenye maswali tofaut na mwingine.
Kumbuka Maisha ni moja ya mtihani mgumu sana na watu wengi wanafeli kwa sababu ya kukopi Maisha ya wengine pasipo kufahamu kwamba kila Mtu ana maswali yake katika katika chumba cha mtihani.

Hivyo Kijana jaribu sana kukaa chini jikague jitathimini ili kuweza kujipambanua kuwa wewe ulizaliwa na lengo gani
Fanya kazi kwa bidii kuwa mbunifu ongeza maarifa katika kila jambo unalofanya.
Note
Sijasema kuwa usiwe na watu unaopenda kuwa kama wao hapana jifunze kwao njia na kanuni walizopitia kufika mahali walipo then baada ya hapo kaa chini chukua jema tupa kule lisilo faa
Halafu anza kufanya kile moyo na akili yako inakuambia kuwa ukifanya hiki utafanya katika ubora kwa kiwango cha juu na kwa ubora mkubwa zaidi.
Life is too short try to utilize every single second effectively through the natural gift or talent that God created with
Be blessed and have a very good moment 
By Moses

No comments:

Post a Comment