Sunday, November 4, 2018

MAMBO MUHIMU KUJIFUNZA

Key Skills To hold on
Kama mtu mwingine ambae ana kazi, vilevile mjasiriamali anahitaji ujuzi mkubwa ambao utamfanya aifanye kazi yake vema.
Unapozungumzia neno "UJUZI" ni kitu ambacho kimebeba vitu kama uwezo, utoshelevu,  na  uwezo wakufanya jambo fulani vizuri kabisa.
Ujuzi unafanya kazi na vitu kama, utalamu Fulani, maarifa, uwezo lakini lazima ujuzi usiutenganishe na kitu kinaitwa kipaji, kuna watu wanaujuzi wa jambo fulani kwa sababu ni kipaji chao
Kuna wakati lazima tukubali kwamba japo kwenye mafanikio ya ujasiriamali hakuna formula maalumu ya kutoboa kimaisha lakini kuna baadhi ya skills  (juzi) ambazo zina randana sana na mafanikio ya kijasiriamali na lazima mtu awe nazo au azijue.

Uwiano na mchanganyiko mzuri wa maarifa na juzi mbalimbali inamwezesha mjasiriamali kutegua au kupambanua mambo mbalimbali na kujenga lakini kuja na mawazo mapya ambayo yanamsaidia sana kuinua hali ya biashara na maisha kwa ujumla.

Tunapozungumzia ujuzi tofauti tofauti kwenye issue za ujasiriamali ni kwamba ujuzi una play role kubwa sana ya mjasiriamali kuwa mshindani wa kweli katika biashara, kuwa na akili wazi iliyofunguka na shapu ya kusoma hali ya soko kwa ujumla wake na kuweza kutembea kwenye hali yoyote ya soko
Tunapozungumzia suala la ujuzi maana yake tunazungumzia, ujuzi binafsi ambao ni kipaji, hard skills amabazo ndo ujuzi wa kibiashara. Ukiacha kipaji lakini ujuzi mwingine tunajifunza darasani na maeneo mengine, sasa Lazima Kama mjasiriamali ujue namna ya kutumia ujuzi wako to the maximum lengo ni wewe UNAFIKIA ndoto zako
Swali Je wewe unafikiri nini?

Ujuzi binafsi ni ule utaalamu tulionao ambao tunautumia kwa ajili kujiendesha kimaisha, ujuzi ni kile kitu kinakupa nguvu ya kufanya jambo fulanikwa sababu kiko ndani yako.
Ujuzi unapounganishwa na maarifa inatengeneza bond ambayo inapelekea kuboresha kabisa mfumo mzima wa ujasiriamali maana hapa itakupa nafasi yakuwa mbunifu, kuunda mbinu ndogo ndogo za kuwini washindani wako, kuwa na uwezo wa kutatua changamoto zinapokukabili, kukupa nguvu yakufanya maamzi mahali ambapo ni magumu na uthubutu wa kuanzisha mambo katikati ya woga wa wengine.
Ujuzi + maarifa inakupa nafasi ya kufanya kazi ya aina yoyote maana utakuwa na ujuzi wa kutengeneza mahusiano mazuri na aina za watu wote, hapa utakuwa na ujuzi wa kimawasiliano, nguvu yakufanya kazi kama team na kila mtu ambae analazimika kuwa mbia kwa namna yoyote ile.
Ujuzi unakupa nafasi ya kukufanya uyazoee maisha na hali yoyote kwenye maisha ya kibiashara ambayo unaweza kuyakabiri, uwezo wa mawasiliano mazuri na kila aina ya mteja au mbia.

Lakini pia ukiwa na ujuzi na maarifa itakupa nafasi kubwa mno pale kampuni au biashara yako inapokuwa kubwa namna ya kuunda uongozi na utawala wa usimamizi mzuri na biashara kusonga mbele zaidi kuliko ukiwa huna ujuzi ufahamu na maarifa juu ya ujasiriamali.

Vilevile ujuzi unakupa nafasi na uwezo mkubwa kutekeleza mipango na malengo amabayo ungependa kuyafikia ndani ya muda mfupi kati na mwisho ambao ni muda mrefu.

Ujasiriamali ni uwezo binafsi ambao unalifanya tatizo kuwa ni wazo linalotakiwa kutatuliwa kwa vitendo.

Kuwa mjasiriamali lazima uwe na uthubutu na uwezo  wa kuchukua na kutumia uwezo wa kufikiri, ubunifu na mtu mwenye kuchukua uamzi mgumu lengo kuu ni kutatua changamoto lakini pia kufikia lengo baada ya tatizo kuwa limepatiwa ufumbuzi.
Uwezo wa kujenga wazo, hoja uwezo wa kuwasiliana na namna ya kufanya kazi na watu sahihi ambao wanaweza kufanya nao kazi na kufikia malengo mfano unapokuwa na kampuni basi unapoajiri watu wawe na uwezo unaoutaka na wenye kuleta matokeo ya kile kilipelekea kuwaajiri.

Kumbuka ujasiriamali ni uchaguzi ambao mtu anafanya kwa manufaa yake na jamii, Kwa hiyo Lazima awe na mtazamo chanya endelevu, Thamani, uwezo binafsi, mwonekano na mapenzi binafsi na kazi husika.
Uchaguzi kwenye masuala ya ujasiriamali huzaliwa kwenye fursa amabazo unakuwa umeziona hapo ndipo unalazimika kufanya maamzi yanayowezekana katikati ya mambo ambayo yalionekana hayawezeakani kwa kutumia ujuzi sahihi.
Ujuzi pia unaotumika lazima uwe ujuzi sahihi ambao unaendana sana na hali ya utumiaji wa Teknolojia iliyopo ili kusapo ujuzi wako uwe sahihi zaidi hapa lazima pia utengeneza namnaya kuleta mabadiliko ya mifumo ya kimasoko ili kuleta matokeo unayoyataka. Hapa pia inaendana sana na uwezo wa kugundua uwezo na udhaifu wa washindani wako hapo utaweza kuwa mjasiriamali bora.

Ni ujuzi upi ambao unakutofautisha na wengine?. Kuwa na uwezo ambao utakupeleka kwenye uzoefu ambayo lazima tabia yako kabisa ambayo imekufanya kuwa hapo ulipo.
Ujuzi unao na uzoefu unao sasa yakupasa kuanza kufanya mambo mbalimbali yaliyo ndani ya uwezo wako lakini kuwafanya watu wakuhitaji zaidi wewe kwa kile unafanya.

Prepared by
Moses zephania Mgema
0755632375

No comments:

Post a Comment