Saturday, October 12, 2019

ULIZALIWA KUTATUA CHANGAMOTO/YOU WERE BORN TO SOLVE CHALLENGES.

Your a problem solver.......
Wakati mwingine ni ngumu kuelewa mtu anapokupa scenario ya changamoto Fulani amabayo anapitia, au amewahi kupitia kwenye maisha yake.
Unaweza usimwelewe sana kwa sababu unahisi jambo hilo ni dogo au hakuna binadamu anaweza kuchomoka kwenye changamoto ambayo amejaribu kukusimulia, hii ni kwa sababu inaonekana kuwa kuubwa sana.
Kuna mambo mtu anapitia kwenye safari yake yake ya maisha akikusimulia unaweza kusisimkwa na mwili na hata mwili mzima.
Lakini kiukweli maisha bila changamoto maana ya maisha inakosekana kabisa, watu wanakwenda shambani, maofsini, shuleni, na kila mahali lengo ikiwa ni kutatua changamoto.
Unalowa na mvua, unachomwa na jua, miiba na kadhia mbalimbali lengo ni kutatua changamoto njaa.
Watu wanakwenda maofsini mapema, wanachelewa kulala wakiwa wanafanya mambo Fulani lengo ni kutatua changamoto.
Maisha hasa maana yake ni Changamoto, huyo ndiyo maana ya maisha kwenye dunia hii
...........................
> Huwezi kuwa bora bila kupitia changamoto.
> Ubora na uwezo wako huwezi julikana bila kutatua changamoto Fulani kwenye maisha.
> Waliofanikiwa walitatua changamoto na matatizo ya watu kwenye jamii ndiyo zikawafanya kuwa hapo walipo.
>Kuna watu wanafurahia maisha lakini nyuma ya furaha hizo kuna watu walitatua changamoto.
√••••••••••
Mwanadamu amejengwa na ameaminiwa na Mungu kuwa problems solver. Kwa hiyo kama kuna changamoto unapitia basi mshukuru Mungu kwa kuruhusu changamoto hizo.

Usiruhusu changamoto zikakurudisha nyuma, zikakukatisha tamaa, na kukuondoa kwenye mipango, malengo na maono yako.
Wapo watu makazini, mashuleni kwenye biashara wao ni kukatisha watu tamaa, hawakubali kazi zako, wapondaji, wanakudharau nk. Yote hayo yabaki kuwa mawe ya kukanyaga na kukuvusha kwenda ng'ambo ya pili.
Huwezi kuwa imara kama

YAWEZEKANA WEWE NI KATAPILLA, SOMA NA KUJIJUA WEWE NI NANI....

*-MFUMO WA MAISHA-*
•Dunia imeubwa kwa mgawanyo sawa wa muda, majira na nyakati, mpangilio wa kizazi kimoja kwenda kizazi kingine.
•Mzazi mmoja kwenda kwa mtoto na mtoto akileta mjukuu, vitukuu mpaka vilembwe, dizaina na mratibu wa mambo yote haya ni Mungu.
•Uwepo wa mtu kwenye kizazi Fulani, kwenye miaka Fulani lilikuwa kusudi, majira na wakati sahihi wa kila mtu kuwa tumboni mwa mama hatimae duniani kwa mwaka, sikunde, dakika saa, Siku, wiki mwezi,mwaka kwa muongo, karne na millennium pia.
• Waliozaliwa miaka ya mwanzoni mwa 1900, hao ndiyo Mungu aliwaamini kuwa hadi kufikia wakati wa Tanzania inataka kuwa nchi huru wataweza kupambana kwa hoja na watu kutoka bara Ulaya na nchi itakuwa huru.
• J.k. Nyerere na wenzake wakazaliwa na hatimae kukuwa, kwa ushirika wao walipambana na watu toka Ulaya, walionekana sokwe, wajinga, wapuuzi, waliumia, walibaguliwa na kuteseka lengo ikiwa ni kuhakikisha nchi yetu inapata uhuru na hatimae baada ya miinuko, miiba, jua, makorongo, milima na changamoto zote toka enzi za kina kinjikitile Ngwale, Mangi sina, na watawala wa kichifu ambao walikutana na ukatili wa kijerumani Leo Tanzania imekuwa nchi ya watu weusi na hata tunaona fursa za kusema na kufurahia kwa sababu ni wakati wetu na sisi.
• Tukiwa na matajiri na watu wa aina mbalimbali hapa nchini Leo kina Nyerere, chief mkwawa, Kijikitile Ngwale na wengine hawapo tena duniani na wakati mwingine uzuri wa Tanzania hawaujui kabisa wamelala na zama zao zimepita.

•√MFUMO WA MAISHA.......
•Mfumo wamaisha umegawanyika katika makundi tofauti tofauti, na mgawanyo huu umekuja ili kuifanya dunia kuwa mahali salama pakuishi na kufurahia zawadi ya Mungu ambayo ni pumzi ndani yetu.
• Kuna watu wamekuja kama waandaji wa mazingira ili wengine wafurahie ndiyo maana walizaliwa katika kipindi ambacho kila mtu WA kizazi hiki anajiuliza ni kwa namna gani watu waliweza kuishi enzi hizo ?....Je maisha bila simu, internet, lami, ndege nk yaliwezekanaje ?.
• Yaliwezekana kwa sababu kwa majira na nyakati Mungu aligawanya na kila mtu kwa kizazi chake aliaminiwa kuishi kwa miaka na karne yake na waliweza kwa sababu waliumbwa kwa muundo wa kuyaweza na kuyakabili maisha na mazingira ya kizazi chao.
• Wengine wameumbwa kama makatapilla na walishushwa duniani kwenye Yale mazingira magumu ampapo Hummer, Range, Harrier, Scuba, Subaru, Prado, Rav4, nk visingeweza kumudu mazingira hayo...
• katapillar likaja kuyakabili mazingira hayo na kusafisha, kushusha milima, mabonde, kung'oa visiki, kufukia mashimo, makorongo, kupasua miamba, na kuhakikisha kwa kiasi Fulani levo inakuwa sawa kwa ajili ya magari mengine.

• Baadhi ya watu ni makatapilla kwenye maisha, wapo kwa ajili ya kuwatengenezea wengine mazingira na barabara nzuri.
• Katapilla hukutana na visiki, miamba, makorongo, milima na miinuko mingi na kwa sababu hiyo hulazimika kung'oa, kupasua miamba, kukata miti, kufukia mashimo, makorongo na kusawazisha vyema na kisha kuweka jamvi zuri lami nk.
• Hivyo basi kama wewe uliishi maisha ya katapilla au unapitia maisha hayo kwa sasa usipende sana au kulazimisha na wengine kuishi maisha hayo wakati unyoofu na usawa wa barabara upo levo tayari.
• Acha wengine wafurahie ubora na uzuri wa barabara hiyo, wasimulie na kuwambia changamoto ulizopitia ili kuwapa changamoto ya kuilinda na kuitunza barabara hiyo vizuri, usilazimishe na wengine wapitie mapito uliyopitia wewe kwa kuwanyanyasa, kuwa mbabe, na kutumia nafasi ukiyonayo kuwaumiza wengine bila sababu za msingi.
• Kumuumiza, kumnyanyasa, na kutaka afanye matakwa yako hata kama anaona hatari mbele sio sahihi, wala humjengi Bali unajiumiza mwenyewe ukizani unamkoa kumbe unajiumiza wewe mwenyewe.

• Mtu hafundishwi kwa manyanyaso, masimango Bali hufundishwa kwa utaratibu mzuri na kupewa nafasi yakuonyesha ubora wake.......Ubabe, kutumia nafasi za utajiri, uongozi kuwanyanyasa na kuwadidimiza wengineo sio sawa na lazima ukumbuke kuwa maisha ni kama jua tu huanza kwa upole na kufurahiwa na watu lakini saa nane hakuna awezaye kukaa juani, na jioni jua huwa tamu na kila mtu aweza kulifurahia tena.
• Ndiyo maana Yesu alifanyika katapilla kwa niaba yetu, kilichobaki kwetu nikufuata misingi bora ya Imani ambayo aliyeileta aliumizwa nayo na leo tunafurahia.
• Katapilla Yesu alichonga barabara, alichomwa na miiba, walimpiga mijeredi, wakamtemea mate yetu, lakini kumvisha taji ya miiba kichwani ili Mimi na wewe tuwe tulivyo leo.
• Fikiria kama huyu Mungu angetaka kila mtu alipie pumzi yake ingekuwaje nafikiri hakuna angeweza kuishi.
• Kama wewe ni tajiri, kiongozi au mzazi usipende waliokuja na kukuta Mungu ameshakuinua kuwanyanyasa, kuwakandia na wakati kuumiza nafsi zao bila sababu ya msingi.
• Wambie kwamba haikuwa rahisi kuwa hapo ulipo, ulipitia changamoto nyingi, ambazo leo ndiyo zimekufanya ukawa hapo, hivyo kila mtu afanye kazi, asome kwa bidii na kutimiza jukumu lake sawasawa ili kulinda hatua ambayo mmenikuta nayo na ikiwezekana kwa sababu sasa haupo pekee yako, uunganishe nguvu na team yako kufikia malengo makubwa zaidi.
Note.....
Kama wewe ni boss, mzazi, kiongozi tumia changamoto ulizokutana nazo kuwakumbusha tu kwamba kuna milima mirefu, miamba, miiba nk. Mpaka kufikia hapo ulipo.
•Changamoto ni maisha ya mwanadamu ila  kwa majira na nyakati zina changamoto zake.
• Kama ulikuja mjini na madaso, usilazimishe na wengine wavae madaso wakati mitumba ya wachina imejaa k/koo.
Katika yote Mungu ndiyo msingi wa yote.
Kama umebarikiwa wewe basi wabariki na wenzako kwa wema na Mungu atakujazia
Prepared by
Moses Zephania Mgema
0755632375/0715366003
mgemamoses@gmail.com
mosesmgema.blogspot.com

Sunday, October 6, 2019

KILE CHA ZIADA NDO DUNIA INAKIHITAJI KUTOKA KWAKO, SIO ELIMU , KIPAJI NK KATIKA KARNE HII.......BALI KILE KINACHOKUFANYA UWE TOFAUTI NA WENGINE.

-Kila kijana anatamani kuwa mtu fulani kwenye maisha yake, leo, kesho hata kesho kutwa
- Ni furaha ya kila mtu kutimiza mambo yafuatayo....
1. Ndoto na malengo.
2. Kuwa na fedha na kazi nzuri.
3. Kufanya kila kitu unachokitaka.
> Pamoja na kutamani yote hayo lazima kama vijana tujikumbushe haya yafuatayo....
1. Dunia ya leo haitafuti mtu wa kusaidia katika eneo lolote la maisha Bali mtu mwenye kuleta na kuongeza ufanisi.
2. Dunia ya leo inahitaji ulicho nacho cha pekee (Your uniqueness) mfano kwa nini tukuajili wewe kati ya maafsa masoko 200 ambao wanataaluma kama yako, nini cha ziada kwako ambacho wengine hawana.
3. Wewe mwimbaji kwa nini uje wewe wakati kuna waimbaji wengi wanaoimba aina ya mziki wako.......nk.

åDunia ya leo ina kila aina ya watu inaowahitaji, wamejaa hawana kazi, wanafanana kwa minajiri ya taaluma, wanavipaji, kila eneo wapo, kitu ambacho kimepelekea kwamba Watu ndo watafute kuliko wao kutafutwa.

å Miaka ya nyuma, mtu angeajiliwa ikiwa hajamaliza darasa la 7, mtu angeenda form one akiwa na kazi lakini leo kila mahali pamejaa na maofsi hayahitaji watu tena Bali watu wanazihitaji nafasi ambazo hazitoshi tena.
√•. Shahada na Masters  sio sababu tena ya mtu kukupa kazi kwa sababu watu wa aina yako ni wengi sana wamejaa kila kona.
å Kumbe nini sasa kinaweza kukupa thamani na kukufanya uhitajike zaidi na hii dunia ni (Utofauti juu ya ubora, maarifa ya ziada, ujuzi na ubunifu wa pekee ambao wengine hawana.
å Leo kuna watu hawana hata elimu ila wapo kwenye nafasi nzuri sana na wanakula maisha kwa sababu tu wameweza kujitofautisha na wengine, wamejiongeza na kujitengenezea thamani na mazingira ya kuhitajika zaidi kuliko watu wengine.
√•  Cha kwako cha ziada ni kipi....tunatafuta MC, msemaji wa makongamano, mwalimu, mwimbaji, Daktar, mshauri wa ndoa na mambo ya kijamii nk. Kipi kinatufanya tumwache wa karibu na mwenye bei ndogo na kukufuta wewe wa mbali.
å kwa nini tukuajili, kwa nini tukupe milioni kumi kwa mwezi, kwa nini uwe mtu Fulani.
å Ni kwa sababu ya kitu kidogo tu kinachokufanya uhitajike *-UWE WEWE-* kile kidogo kinachokutofautisha na wenzako wenye kipaji, elimu, sawa na wewe.
åkwa nini wanunuzi wa mahitaji waje kwako sio kwangu wakati wote tunauza madafutali na kalamu za aina moja, kwa nini nije kushona kwako sio kwa James, kwa nini nije kula kwako sio kwa mama John........?
> Kile kitu cha ziada ulichonacho chenye ubora ndo kinachonifanya nije kwako, Lugha nzuri ya biashara, huduma nzuri ya chakula, usafi na nadhifu, kujali na kuthamani wateja ndiyo sababu inayonifanya kuja kwako.....
Je kama wote tunawahudumia vizuri wateja zetu nifanyaje....
>Mfanye kuwa rafiki wa karibu
> Tumia mapungufu ya mwenzako kuwin.
å Dunia ya leo imejaa changamoto na ushindani wa hali ya juu katika kila jambo so ni vyema kujitofautisha kwa mtazamo chanya kwenye kila kazi unayofanya.......
Dhahabu ni Dhahamu hata kama inaonekana kufifia kwa sasa, ila huwezi kuilinganisha na kioo hata kama kiooo kinang'aaa kiasi gani..
BE YOU
BE UNIQUE
BE DIFFERENT
WALK ON WHAT OTHERS ARE SHOWING WEAKNESSES.
USE EVERY OPPORTUNITY WHICH COMES AHEAD OF YOU EFFECTIVELY.........
MAKE PEOPLE TO NEED YOU TO SATISFY THEIR NEED......

Prepared by
MO_MGEMA........INSTA
Moses Zephania....FB
0715366003.......WHATSUP
Dar ea salaam

Sunday, September 22, 2019

WEWE NI WEWE.........

Usiruhusu mtu, au kitu chochote, mtu mwenye nguvu lakini hana hekima, busara na utu akuvunje moyo, au aiharibu njia yako kwa maneno ya dharau, kukatisha tamaa, kukwambia hujui wala huwezi.
åKama Mungu aliruhusu uzaliwe, maana yake Mungu alikuamini.
å Mungu amekupa talanta, uwezo wa pekee na sifa ya kwako tu.
åKuna jambo Mungu anatamani litimie kupitia wewe....
>Hivyo basi lazima ufahamu kwamba, njia ya mafanikio sio lelema, ina changamoto nyingi sana ambazo zinakuhitaji wewe kwanza ujijue kuwa wewe ni nani, kwa nini ulizaliwa, kwa nini upo hapo ulipo, unaenda wapi, na unaenda kufanya nini ? Hapo ndipo inaweza kukabiliana na changamoto yoyote njiani.

Kama hujijui basi ni rahisi kuyumbishwa, kukatishwa tamaa, kuhamishwa kwenye lengo na kusudi la kuzaliwa kwako..............

Tuna wazazi, viongozi, walezi, walimu, kaka & Dada, babu & Bibi, shangazi & mjomba hawa wanaweza kuwa wazuri kwako au wabaya kwako pia, hivyo tafuta kujijua kuwa wewe ni nani, hata wakija kwa lengo la kukuhamisha kwenye ndoto yako basi wakukute umekwisha jitambua.
Mafanikio ya mtu yako mikononi mwake yeye mwenyewe, wengine ni washauri wa pembeni lakini "constructor of your life is you".

Wapo watu duniani wanaamini kuwa wao ni sahihi daima, hawaruhusu wengine kuchipua mbele yao, any potential wakiona kwa kijana wanatumia nguvu kubwa kuizima, wanadharau, wajuzi wa kila kitu, wabinafsi, wakosoaji sio wajenzi, maboss sio viongozi, wamelewa madaraka na sifa, kwao miili yao sio chakula cha udogo, wanaishi milele.......hao ni hatari sana watambue na kuwaepuka.

Pamoja na kwamba dhahabu ili ing'ae inahitaji moto, vilevile mmea ukisongwa sana na miba pamoja na magugu hutoa matunda dhaifu na wakati mwingine kutokutoa kabisa jihadhari.

Sio kila jambo gumu ni changamoto bali ni vitu vya kuepuka, daima ukiona mto unaspeed ya maji kubali kusubili upungue au utafute namna nyingine ya kuvuka mto huo.

Njia nzuri ya kufanikiwa ni
1. Kumshukuru Mungu kwa kuwa ulivyo
2. Kujitambua, kujikubali na kujiamini
3. Kuwa na maarifa sahihi na ya wakati.
4. Kuwa wewe kwanza kabla ya kupokea ushauri
5. Epuka majungu,fitina na unafiki
6. Mwombe Mungu akujalie hekima, busara, na namna njema ya kuishi na watu.
> Wewe ni Wewe, Mimi ni Mimi, yule ni yule, pamoja na kwamba tunahitajiana lakini wewe ndiye C.E.O wa maisha yako.
Mfanye Mungu namba moja kwa kila kitu, atakubariki, atakupa maarifa, utulivu ambao utakufanya uamue vyema kwa kila jambo.
I love you brother & sister.
MO_Mgema
mgemamoses@gmail.com
0715366003/0755632375
Dar es salaam, Tanzania.
Facebook Moses Zephania
Twitter Mo Mgema
In stag Mo_Mgema
YouTube; Mo Mgema

Sunday, August 18, 2019

JE UNAISHI VILE ULITAKA KUWA HAPO KABLA..........?

..Vijana wengi tumekuwa na ndoto kubwa maishani, kila mtu ukimuuliza kuhusu maisha yake anakuambia nataka kuwa mtu Fulani hapo baadae.
Maisha haya yameanza tangu tukiwa watoto wadogo, ukiulizwa swali, jibu lake nataka kuwa daktari, Rubani, mwalimu, raisi nk. Haya ndiyo maisha na mfumo ambao mwanadamu ameumbwa nao, kuishi kwa kutamani kuwa mtu Fulani au kuwa sehemu fulani baada ya muda fulani kupita.
Pamoja na ndoto na malengo mengi tuliyonayo, changamoto kubwa imebaki katika kuyafikia yale tunayoyatamani au kuyaota, wengi tumefeli kuwa vile tulitaka kuwa na kuna sababu nyingi ambazo zinachangia kutokuishi maisha ya ndoto zetu  either kwa sababu za kimazingira, malezi, mifumo na mambo mengine kibao.

Pamoja na sababu nyingi ambazo zinaweza kuwa ndiyo sababu ya kutokufikia shauku na matanio ya mioyo yetu kuwa mahali fulani, lakini hizi ndizo sababu kubwa zinazowafanya watu wengi kutokutimiza malengo na ndoto zao.

1. Kutamka na kutenda kuna ombwe.
Wengi ni wazungumzaji ila sio watekelezaji wa kile wanachokizungumza na kukifikiri, unakuta mtu ana mipango mizuri lakini kufanyia kazi maono, ndoto, malengo, mipango na anachokizungumza ndiyo hapo changamoto inapoanzia.

2. Mipango mingi ambayo ni ngumu kutekelezeka.
Watu wengi wamekuwa wakiishi kwenye malengo mengi makubwa ambayo wakati mwingine ni makubwa na mengi ukilinganisha na uwezo wa mtu, mwisho wa siku anachopanga na anachotenda ni tofauti anakuwa confused na anaishindwa kujua aanze na lipi amalize na kipi au afanye jambo gani maana ana malengo mengi uwezo mdogo.

3. Watu wa sababu na lawama.
Watu wengi tunaishi kwenye kubebesha watu wengine mizigo ya lawama na kutengeneza sababu ambazo ni excuses zisizo na sababu za msingi sana mfano mtu unakuta ansema ningesoma, ningezaliwa sehemu fulani au nisingezaliwa kwenye umasikini, baba na mama wasingekufa mapema nk, lawama na malalamiko yasiyo na maana yamewafanya watu wengi kuishi maisha ambayo hawakuyatarajia kuyaishi hapo kabla.

4. Kupeperushwa na stori za vijiweni/kukosa msimamo wa kusimamia malengo na ndoto.
Watu wameshindwa kuishi maisha yenye mipango halisi ya maisha yao kwa sababu wamekuwa kama Bendera, akisikia stori Fulani ya kuvutia kuhusu mafanikio basi yuko tayari kuondoka kwenye malengo na mipango yake, mfano, mtu akisikia biashara Fulani inalipa, bila utafiti anaacha biashara yake na kuhamia huko, watu wengi wamekuwa ni watu wa kutanga tanga muda mwingi.

5.kutokutambua uwezo halisi/kutokujijua
Watu wengi hawajijui, hajui ana uwezo gani, hii inapelekea kufanya kila kitu kilichopo mbele yake. Kujitambua na kutambua uwezo wako ni moja ya nyenzo inayoweza kumfanya mtu akaishi kwenye ndoto na malengo yake.

6.Kutokutambua nyakati.
Kumbuka kwenye maisha kuna wakati wa kuandaa shamba, kulima, kupanda mbegu, kuota kwa mbegu, kumwagilia na kupalilia, kuweka  dawa, mazao kuanza kutoa matunda, hatimae matunda au mazao kukomaa. Wengi tunatamani kuanzia kwenye ukomavu wa matunda kwa sababu hatutaki kuchomwa na miba, jua, kunyeshewa mvua ila tunataka kula.

7.Hatukubali vile tulivyo.
Baadhi yetu huwa hatukubali kuwa tulivyo kwa wakati uliopo, hatupendi kuonekana uhalisia wetu kitu ambacho kimetufanya watu wengi kuishi kwa aibu na kuchagua kazi. Kumbuka kuna wakati unaenda mwanza ukitokea Dar unalazimika kupita  Kenya kwa sababu ya sababu za namna ulivyo, usilazimishe kula Serena hotel wakati uwezo wako ni kula kwa mama Ashura.

8.Elimu, Baba alikuwa Fulani.
Hadhi imewafanya watu wengi sana hasa vijana kuondoka kwenye malengo yao na ndoto hasa kwenye kipindi hiki ambacho ajira zimekuwa ngumu kupita Jana. Nikukumbushe kwamba ujenzi wa ndoto huanza na chochote ulichonacho. Mtu akitaka kuwa raisi, anaanza na levels za chini, diwani, au mbunge haya yote ni madaraja ya kutimiza malengo yake. Wakati mwingine sio straight Bali inamikunjo, milima na mambonde lakini haiondoi ukwel kwamba ndoto yako inatimia pale tu ubapokuwa na dhamira ya kweli toka moyoni.

9.Kutokufanya jambo ni kujipunguzia connections na firsa.
Fursa huja kwa namna ya ajabu sana, fursa sio kuwa na namba ya mtu fulani, sio kuwa karibu na viobgozi Bali wakati na mahali sahihi pakupata connection na fursa ni kile kidogo ulichoamua kukipa thamani, mfano kijana mwenye degree muuza genge la nyanya, matunda na mbogamboga anakutana na watu wangapi na wa aina gani kwa siku, je boda boda, huba driver nk. Je ni sawa na mkaaji ?.

Opportunities come where there is a beginning.
Hivyo basi hizi ni sababu na changamoto ambazo zimewafanya watu wengi na zinaendelea kuwatafuna watu wengi bila kujua, wengi wakiamini ipo siku watatoboa bila hata kuwa na chochote mkononi.

Moses Zephania Mgema
0715366003/0755632376
mgemamoses@gmail.com
Dar es salaam, Tanzania

Monday, May 20, 2019

USIKUBALI CHANGAMOTO NA SHIDA ZIKUONDOE KWENYE NJIA YA KUELEKEA MALENGO NA NDOTO ZAKO.

Tangu mwanzo wa muundo wa dunia, ukisoma historia ya dunia kwa mfumo wa maisha ya kawaida, kwa mitume na manabii walipitia changamoto, shida, vikwazo vingi mpaka kufikia malengo, ndoto hata mafanikio ya ambacho walilenga kukifanikisha hapa duniani.

Ndivyo ilivyo hata kwenye ulimwengu tulio nao leo, mafanikio ya kila mtu yamezungukwa na vikwazo, changamoto, mambo mengi ya kukatisha tamaa, kiasi kwamba sio rahisi kupasua na kufikia malengo na ndoto kama utaruhusu changamoto hizo zikuondoe kwenye njia.

Dhahabu haiwezi kuwa dhahabu kama haijapitia mchakato sahihi wa kupatikana. Ni nini maana yake: Ni kwamba kitu chochote kizuri kinahitaji mtu kujitoa, kufanya kazi kwa bidii na kwa ufanisi mkubwa ili kufikia kitu au jambo hilo zuri.

> Ili ufaulu masomo inakulazimisha kusoma kwa bidii na kwakutumia muda mwingi kusoma, kujadili na kujiepusha na mambo mengine ambayo yanaweza kuwa sababu ya wewe kufeli.

>Ukitaka kuwa mwimbaji mzuri unahitaji muda mwingi wa kufanya mazoezi, kusikiliza wengine wanafanya nini, kujifunza kila wakati.

>Ukitaka kuwa tajiri na huna misingi mizuri ya mitaji, huhitaji aibu katika kupambana ili kuweza kutoka mahali ulipo kwenda eneo lingine ambalo unataka kufika, utafanya kazi zisizofaa kwa macho ya kawaida lakini ndo unapaswa kufanya ili kesho yako iheshimike.

>Ukiwa na mtaji na unatokea mazingira mazuri kiuchumi and you're well supported lakini bila kuwa makini, kujinyima, kuongeza ubunifu kwenye biashara au kazi yako utajikuta unafeli.

√ Kwa hiyo unahitajika kufanya kazi kweli kweli katika eneo ulilopo, lakini pia kumbuka yako mengi magumu na yakukatisha tamaa kama hutojipanga kukabiliana nayo unaweza jikuta unaishia njiani,

Chakufanya...........

Kumbuka kuna nyakati ngumu na majira magumu ambayo ni kama Mungu haoni jitihada, nguvu, na maarifa mengi unayotumia ili kuyafanya maisha yako kuwa bora na mazuri

Kumbuka hata katika hayo Mungu amekuamini, hali yako uliyo nayo leo ni ya muda tu wala siyo ya kudumu, cha msingi endelea kupambana, kufanya kazi kwa bidii katika nafasi uliyopo, omba Mungu ipo siku utafanikiwa na kuwasimulia wengine.

> Changamoto ni silaha yako
> Mungu amekuamini na anajua unaweza. Kuna wakati tunapitia maisha yakuumiza kuondokewa na watu wakaribu, Baba, Mama, mke, kuachwa na mpenzi au mke/Mume lakini yote hayo yanakuja kwa sababu Mungu amekuamini sana.

> Don't be taken away from your focus, plans, kimbia kwa kadiri uwezavyo hiyo ndiyo silaha yakufikia unapotaka

Yesu aliumia na alipitia mateso kufikia lengo why not you ?. Zifanye changamoto kuwa sehemu za maisha na huwezi kuzimaliza na kila hatua unayopiga ndo zinavyozidi kuwa nyingi lakini pia katika hayo njia za kutatua zipo.

Mungu amekuamini, usimwangushe chini, pigana, pambania mafanikio yako huo ndo msingi sahihi wa maisha ya mtu mwenye lengo la kutimiza ndoto zake.
Musa/Moses Zephania Mgema
mgemamoses@gmail. com
0715366003/0755632375
Dar es salaam, Tanzania.

Sunday, May 19, 2019

THAMANI NA FAIDA YA UTULIVU WA AKILI KATIKA MAAMZI NA MAISHA KWA UJUMLA

Hello Friend.
Rafiki na ndugu yangu nikushirikishe jambo hili la thamani na lenye maana sana kwenye maisha yako.

Kwenye maisha ya kila siku kuna mambo mtu anakutana nayo, mazuri kwa mabaya, ambayo yanamfanya kuishi kwa amani na furaha au kama ni Magumu au mabaya yanamfanya kuishi kwa kukosa amani, furaha na utulivu kuanzia kwenye akili mpaka huku nje.

Nikuambie leo rafiki tangu, kukosa utulivu, amani na furaha ya akili, inaondoa uwezo wa kufikiri sawasawa na sahihi na hii inapelekea kuondoa afya na ubora wa akili yako.

Matokeo yake unajikuta unaamua vibaya kila jambo na kuleta athali kubwa kwenye mfumo mzima wa maisha yako.

Changamoto zipo, ugumu wa maisha upo, wakati mwingine unafanya kazi kwa bidii, maarifa, ujuzi na kwa kila namna lakini hatua unayopiga ni ndogo au wakati mwingine hakuna kabisa.

Nikuambie kitu................

Utulivu ni jambo moja la msingi na muhimu sana kwenye maisha ya mtu kwa sababu ukiwa na utulivu wa akili na nafsi pia itatulia, matokeo yake sasa ni......
1. Utaamua vyema
2.Utaona njia ya kutatua tatizo/ changamoto hiyo
3. Maamzi yako hayatakuwa na matokeo hasi.
4. Kiwango cha Maamzi sahihi kitakuwa juu
5. Afya ya akili na nafsi itachukua nafasi yake.
6. Utaona watu/Mtu sahihi wakumshirikisha changamoto yako na wakati mwingine kupata ufumbuzi wa changamoto hiyo.
7.Utajenga ujasiri zaidi na kujiamini hata wakati mwingine hutayumbishwa na aina yoyote ya changamoto hata itakuwa ngumu kiasi gani.
8. Utakuwa msaada kwa wengine
9. Utaishi kwa tumaini na kujiamini vyema
10.Hutoyumbishwa na mazingira hata yaweje.

Kwa ujumla utulivu unafaida na thamani kubwa mno kwenye maisha ya mtu ya kila siku.

Hivyo usikubali tatizo, au aina yoyote ya changamoto ikakuondoa kwenye utulivu, ingawa kuna matatizo ambayo ukiyapata hakika yanaumiza na kukatisha tamaa lakini bado utulivu na hekima ukiruhusu vitawale na kuzuia Maamzi ambayo yanaongozwa na mazingira, mihemuko, na maumivu basi kwako itakuwa kheri.
Be blessed so much for reading this beautiful message.
Musa Zephania Mgema
0715366003/0755632375
mgemamoses@gmail.com
mosesmgema12.blogspot.com
Dar es salaam, Tanzania

Saturday, May 18, 2019

NI WEWE MWENYE MAAMZI NA MAISHA YAKO.

Hello Friend.
Nia yakufikia ndoto na malengo yako unayo wewe mwenyewe, lakini changamoto na vizuizi vimekuwa vingi na wakati mwingine ni vikubwa kuliko nguvu na uwezo ulio nao wewe, na kuna wakati unafikia mahali unakata tamaa. Lakini ni............

Mambo machache unapaswa kujifunza na kuelewa kwamba, haya yote yanakuja kwa sababu kwanza, Mungu amekuamini na ana uhakika kabisa kwa nguvu na uwezo alioweka ndani yako unaweza kukabiliana na aina hizo za changamoto na wewe ndo mtu sahihi kupitia changamoto au milima hiyo ya maisha.

Lengo ni kwamba anakunoa ili uwe kisu kikali zaidi ambacho kitakuwa na uwezo wakulalua kila aina ya jambo liliko mbele yako.

Huwezi kuwa mwalimu mzuri wa nyimbo, ujasiriamali, mambo ya kijamii, huduma kwenye nyumba za ibada bila kupitishwa.

Huwezi kuwa mwandishi, public speaker, motivational speaker simply, huwezi kumiliki fedha kwa njia rahisi kesho utashindwa na utaanguka na kukata tamaa na kufa kabisa.

Dhahabu haiwezi kuwa dhahabu safi bila kupita kwenye moto, moto unaifanya ing'ae na thamani yake kupanda na kila mtu kuihitaji kwa gharama yoyote ile. Ndivyo ilivyo hata kwenye maisha yetu kama binadamu.

Tunakuwa vizuri zaidi kwenye maeneo ya kazi zetu, kwenye matumizi ya vipaji vyetu pale tu inapotokea umepambana sana kufikia mahali ambapo ulitamani kuwa hapo kabla.

Mapambano ya muda mrefu ambayo ulikutana nayo njiani, ndiyo sababu ya wewe kuthamini kazi uliyo nayo, kipaji ambacho wengine wanacho ila bado hawajafika pale ulipo wewe Leo na wanatamani siku moja wawe hapo lakini bado wako mbaaali sana.

Kwa hiyo usikatishwe tamaa na vikwazo vichache vilivyopo njiani, pambana hakikisha focus yako iko klia isiyoyumbishwa na pepo za kiangazi ambazo zina mwisho na masika yaja.

Usiyumbishwe na kelele za watu hasa ambao wamefanikiwa na kushindwa, maana kila mtu anamtazamo na mawazo yake, hivyo ukiwasikiliza utapotea maana miruzi mingi humpoteza mbwa asie na mmiliki bali mbwa anaemjua bwana wake huitambua sauti ya mruzi wa bwana wake, kwa hiyo usie mbwa mwitu asie na bwana wake.

Maamzi ya kufika mbali kihuduma, kibiashara na kwenye eneo lolote ulilopo iko mikononi mwako, hakuna mtu anaweza kuyaamua maisha yako yaweje kesho isipokuwa wewe mwenyewe, sio mazingira, sio Sera za nchi sio changamoto yoyote bali ni wewe.

>Maamzi yako ndiyo dira yako
>Malengo yako ndiyo dira yako
>Kichwa chako ndo dira yako
>uwazavyo ndivyo unavyoiamua kesho yako.
>Uwezo na kipaji ndani yako ni urithi wa Mungu.

Mwisho
Jitathimini na kujipambanua kama unaona kuwa unapita kwenye njia sahihi ya kuifuluzia ndoto yako

Moses Zephania Mgema
0755632375/0715366003
mgemamoses@gmail.com
www.mosesmgema12.blogspot.Com
Dar es salaam, Tanzania

Tuesday, April 30, 2019

NOTES OF LEADERSHIP.

What is Situational Leadership?

How Flexibility Leads to Success

Situational leadership is an adaptive leadership style.

This strategy encourages leaders to take stock of their team members, weigh the many variables in their workplace and choose the leadership style that best fits their goals and circumstances.

In the words of leadership theorist Ken Blanchard, “In the past a leader was a boss. Today’s leaders can no longer lead solely based on positional power.”

Situational leadership is the model of choice for organizations around the world that want to do the following:

1.Develop people and workgroups
Establish rapport and to bring out the best in their people
Use a common leadership style across all units in an organization, be it local, national, or international

Read more about situational leadership:
Situational leadership defined
History of situational leadership
Examples of situational leadership and quotations
Characteristics of situational leaders
Advantages and disadvantages of situational leadership
Benefits of situational leadership
Situational leadership defined
Situational leadership is flexible. It adapts to the existing work environment and the needs of the organization. Situational leadership is not based on a specific skill of the leader; instead, he or she modifies the style of management to suit the requirements of the organization.
One of the keys to situational leadership is adaptability. Leaders must be able to move from one leadership style to another to meet the changing needs of an organization and its employees. These leaders must have the insight to understand when to change their management style and what leadership strategy fits each new paradigm.
There are two mainstream models of situational leadership, one described by Daniel Goleman and another by Ken Blanchard and Paul Hershey.
The Goleman theory of situational leadership
Daniel Goleman, the author of “Emotional Intelligence,” defines six styles within situational leadership.
1. Coaching leaders , who work on an individual’s personal development as well as job-related skills. This style works best with people who know their limitations and are open to change.
2. Pacesetting leaders , who set very high expectations for their followers. This style works best with self-starters who are highly motivated. The leader leads by example. This style is used sparingly since it can lead to follower burnout.
3. Democratic leaders , who give followers a vote in almost all decisions. When used in optimal conditions, it can build flexibility and responsibility within the group. This style is, however, time consuming and is not the best style if deadlines are looming.
4. Affiliative leaders , who put employees first. This style is used when morale is very low. The leader uses praise and helpfulness to build up the team’s confidence. This style may risk poor performance when team building is happening.
5. Authoritative leaders , who are very good at analyzing problems and identifying challenges. This style is good in an organization that is drifting aimlessly. This leader will allow his or her followers to help figure out how to solve a problem.
6. Coercive leaders , who tell their subordinates what to do. They have a very clear vision of the endgame and how to reach it. This style is good in disasters or if an organization requires a total overhaul.
Situational leadership according to Blanchard and Hersey
The second model is based on the work done by Blanchard and Hersey. Their theory is based on two concepts: leadership itself, and the developmental level of the follower. Blanchard and Hersey developed a matrix consisting of four styles:
1. Telling leaders = S1 (specific guidance and close supervision): These leaders make decisions and communicate them to others. They create the roles and objectives and expect others to accept them. Communication is usually one way. This style is most effective in a disaster or when repetitive results are required.
2. Selling = S2 (explaining and persuading): These leaders may create the roles and objectives for others, but they are also open to suggestions and opinions. They “sell” their ideas to others in order to gain cooperation.
3. Participating = S3 (sharing and facilitating): These leaders leave decisions to their followers. Although they may participate in the decision-making process, the ultimate choice is left to employees.
4. Delegating = S4 (letting others do it): These leaders are responsible for their teams, but provide minimum guidance to workers or help to solve problems. They may be asked from time to time to help with decision-making.
Stages of employee development in situational leadership
Along with leadership qualities, Blanchard and Hersey defined four types of development for followers or employees:
1. Low Competence; High Commitment
2. Some Competence: Low Commitment
3. High Competence: Variable Commitment
4. High Competence: High Commitment
Blanchard and Hersey also suggest that each of the four approaches should be paired with different “maturity levels” among team members. For example, the lowest maturity level (M1) should work best with the “telling” style (S1), while the highest maturity level (M4) should be most responsive to the “delegating” approach (S4).
Differences between situational leadership and other leadership styles
The difference between situational leadership and other leadership styles is that situational leadership incorporates many different techniques. The style of choice depends upon the organization’s environment and the competence and commitment of its followers.
History of situational leadership
In 1969, Blanchard and Hersey developed situational leadership theory in their classic book “Management of Organizational Behavior.” This theory was first called the “Life Cycle Theory of Leadership.” During the mid-1970s, it was renamed the situational leadership theory.
In the late 1970s and early 1980s, the two developed their own styles. Blanchard’s first book, “The One-Minute Manager,” came out in 1982. Hersey further developed the situational leadership model in his 1985 book “The Situational Leader.” Both men have continued to refine and update their situational leadership theories.
Blanchard said situational leaders tend to choose between “directive behavior” (what and how) and “supportive behavior” (developing commitment, initiative, and positive attitudes). The maturity level concept for Situational Leadership II was revised to incorporate individual development levels.
Examples of situational leadership
Blanchard and his situational leadership collaborators have provided detailed case studies involving companies and public institutions. Prominent examples include Adobe, WD-40, Anthem Blue Cross Blue Shield, British Telecom, the city of Battle Creek, Michigan, Genentech, the San Diego Padres, and the Royal New Zealand Navy.
Any team environment that has frequent turnover provides an opportunity to apply situational leadership principles. Sports teams, for instance, represent clear examples of situational leadership because team rosters are constantly changing.
One president and two of the most successful coaches in college basketball history have attributed much of their success to how they adapted to changing players and circumstances.
Dwight Eisenhower
Dwight D. Eisenhower was the president of the United States after World War II. He was also the Allied Commander during the war. He was known for his diplomacy and his ability to get the allied leaders to work together to defeat the Nazi war machine. His background in the military taught him how to order and direct military exercises, and he needed to be a statesman not only to manage the strong personalities of the allied leaders, but to run for president and then win two terms of office.
Pat Summitt
Patricia Sue Summitt was the head coach of the Tennessee Lady Volunteers for over 38 years. Every few years, she was faced with building a whole new basketball team. Despite that, she ended her career with a 1,098-208 overall record as a basketball coach. She was named head coach for the U.S. women’s basketball team in the 1984 Olympics, where the team won a gold medal.
John Wooden
John Wooden was named the head coach of UCLA’s men’s basketball team. In his first eight years, he won three Pacific Coast championships. During that time he had team members graduate and new members start on the team. Beginning with the 1963-64 season, the team won seven straight championships.
UCLA’s record 88-game winning streak and string of championships ended in 1974. One of his quotes reflects his adaptive and situational leadership philosophy: “When you’re through learning, you’re through.”
Situational leadership quotations
How do professionals become better situational leaders? It might be helpful to consider these quotes from experienced leaders and apply them to your circumstances:
Margaret Wheatley : “Leadership is a series of behaviors rather than a role for heroes.”
Colin Powell : “Leadership is solving problems.”
Mahatma Gandhi: “I suppose leadership at one time meant muscles, but today it means getting along with people.”
John D. Rockefeller: “Good leadership consists of showing average people how to do the work of superior people.”
Margaret Thatcher: “You may have to fight a battle more than once to win it.”
John Wooden: “It’s what you learn after you know it all that counts.”
Situational leadership style requirements
Here are some of the characteristics of the situational leadership style:
Insight : The situational leader must be able to understand the needs of the followers, then adjust his or her management style to meet those needs
Flexibility : Situational leaders must be able to move seamlessly from one type of leadership style to another

Trust : The leader must be able gain his or her followers’ trust and confidence

Problem solving : The situational leader must be able to solve problems, such as how to get a job done using the best leadership style available

Coach : The situational leader must be able to evaluate the maturity and competence of the followers and then apply the right strategy to enhance the follower and their personal character
Advantages and disadvantages of situational leadership

Situational leadership does not work well in all circumstances. Let’s look at the advantages and disadvantages of the leadership style:
Situational leadership pros:

Easy to use: When a leader has the right style, he or she knows it

Simple: All the leader needs to do is evaluate the situation and apply the correct leadership style
Intuitive appeal: With the right type of leader, this style is comfortable

Leaders have permission to change management styles as they see fit
Situational leadership cons:

This North American style of leadership does not take into consideration priorities and communication styles of other cultures
It ignores the differences between female and male managers

Situational leaders can divert attention away from long-term strategies and politics
Benefits of situational leadership

“What is the best leadership style?” Hersey and Blanchard found it fruitless to provide one answer to this question. Everything depends on the specific situation, which is why they collaborated to develop the situational leadership model.

Situational leadership means “choosing the right leadership style for the right people,” according to Blanchard and Hersey. It also depends on the competence and maturity of the followers. This is a time in history when leaders look less like bosses and more like partners.

Sunday, April 28, 2019

FAIDA YA KUWA MWAMINIFU

Mtu kumwamini mtu inaweza kuwa ngumu sana. Hii inatokana na baadhi ya watu kutendwa vibaya na watu ambao awali walijenga imani kwao lakini walioamini wakafanya kinyume na vile walitarajiwa kuwa hapo awali.

Kadri miaka inavyokwenda jambo kuaminika kwenye jamii limekuwa likipungua kila siku, kuanzia kwenye mahusiano ya ukoo, familia, ndugu jamaa na marafiki, mahusiano ya kimapenzi, na mambo mengine mengi ndani ya jamii yetu Tanzania hata duniani kwa ujumla.

Watu wengi wamepoteza uaminifu sana kwa sababu ya tabia yakutokuwa waaminifu, mtu anaweza akapewa pesa, au akatendewa jambo Fulani lakini mwisho wa siku matokeo yake yanakuwa hasi ambayo ni kinyume na matarajio

Jambo limetokea hata kwenye ngazi za kitaaluma, makazini, hata kwenye maeneo ya dini ambayo kwa kifupi yalikuwa ni maeneo yaliyoaminiwa na kuaminika zaidi ndani ya jamii.

Yapo mambo mengi yanachangia hali hii kutokea lakini mwisho wa siku hitimisho lake ni kwamba tabia ni hali ambayo mtu akiiendekeza inaweza kuwa sugu na kuathili moja kwa moja mfumo mzima wa maisha yake.

Ubinafsi, kutokufanya kazi, mazoea, kuuma kwa roho unapotaka kurejesha fedha ya uliyokopa, kujiendekeza na tabia Fulani, ulevi, udokozi, maisha ya kijamaa kutawala, kutokuthamini kitu au jambo la mwenzako, ubabe, utani uliovuka mipaka, kukosa hekima na busara, ugumu wa mioyo na kuishi maisha bandia ambayo hayana uhalisia na maisha halisi ya kwako hivyo watu vile wanakutazama na uhalisia wako ni tofauti kabisa, kutokuwa wakweli na kutumia njia za uongo ili kukidhi haja ya mahitaji yetu.

Hizi ni baadhi ya tabia ambazo zimechangia kwa kiasi kikubwa sana kupunguza uaminifu kwa watu wengi bila kujua madhara ya kukosa uaminifu kwa watu, jamii hata maeneo ya kitaaluma na maofsini ambapo tunafanya kazi kwa kuajiliwa au kujiajiri.

KATIKA SOMO HILI TUTAJIFUNZA MATOKEO CHANYA YAKUWA MWAMINIFU KATIKA JAMBO LOLOTE.

Hakuna jambo jema kwa mtu kama kuwa mwaminifu yeye mwenyewe binafsi, kwa wazazi wake, watoto, kazini, kanisani/msikitini na kwenye jamii kwa ujumla. Zifuatazo ni faida za kuwa mwaminifu.

1. Kuaminika zaidi
Moja ya faida kubwa ya uaminifu ni jamii kukuamini, kazini, kwako au kwa wateja wako na kama wewe ni mfanyabiashara na ni mwaminifu kwa wateja wako, unafungua kwa wakati, unawahudumia vizuri kwa lugha mzuri na yakupendeza, bei sio za ubabaishaji, mtu akiacha pesa yake anaikuta, basi utajijengea idadi kubwa ya wateja kwa sababu ya uaminifu wako wao kwa wao watapeana taarifa zako,

2. Hujenga mahusiano imara na bora.
Ukiwa mwaminifu kwa jambo lolote lile lazima mahusiano yako na watu yatakuwa mazuri, iwe ni kazini, shuleni, kwenye nyumba za ibada, kwenye sehemu za mahitaji na sehemu nyingine nyingi hutasikia migongano na lawama kutoka kwa watu husika ambao labda unafanya nao kazi, bosi wako, walimu au wanafunzi, ndoa yako nk. Maeneo hayo yote yatakuwa bora na imara hivyo uaminifu ni jambo nyeti sana na ni vyema kulitilia mkazo na kulitimiza.

3. Huimarisha ushirikiano.
Mtu mwaminifu huwa na ushirika mzuri na watu wenzake, mfano wewe kama ni boss kuwalipa wafanyakazi wako kwa wakati, kutimiza ahadi zako au mzazi kutimiza ahadi unazoahidi kwa watoto au mke hii inatoa motisha na ushirika mzuri toka kwa wafanya kazi au kwa watoto kumfurahia baba au mama yao. Vile vile hata wafanyakazi wakitimiza kazi zao kwa uaminifu ushirika huwa ni mzuri kati yao na kiongozi wao. Na maeneo mengine ambayo sijayataja kama mifano hai kwenye maisha yetu.

4.Utapewa nafasi zaidi.
Hii hutokea kwenye jamii, makazini na hata nyumbani. Unapokuwa mwaminifu ndipo nafasi ya kupewa nafasi zaidi iwe ni kazini, nyumbani kwa wazazi basi nafasi hizo huwa ni kubwa na hata maeneo mengine mengi.

5.Utakula vya sirini.
Mtoto mtii na mwaminifu kwa wazazi wake hula vya uvunguni kwa sababu huyu mtoto hutekeleza majukumu yake kama mtoto vyema bila kusukumwa wala kubembelezwa na anajua wajibu wake. Ndivyo hivyo hata kwenye familia, jamii kwenye biashara, kazini  ni rahisi kushirikishwa mambo makubwa ya kiofsi kwa sababu wanajua wewe ni mwaminifu katika kutimiza, kutekeleza na kutunza siri za kampuni vyema hivyo ni rahisi kupata taarifa mapema.

6.Ni rahisi kusaidika.
Mtu mwaminifu huwa anatengeneza mazingira mazuri ya kupata msaada kwa haraka either wa kifedha, kimawazo au msaada wowote ule sababu kubwa ni ule uaminifu aliojijengea kwenye mazingira  yake ya maisha, iwe kwenye biashara, benki, nyumbani, kazini na maeneo mengine mengi ambayo yanamhusu.

7.Ni njia bora ya kuimarisha ndoa na mahusiano

Hakuna kitu kizuri kwenye mahusiano au ndoa kama uaminifu. Uaminifu ni ufunguo wa furaha ndani ya ndoa, ni ufunguo wa mafanikio na Uhuru wa nafsi, ufunguo wa kuyaona mahusiano  au ndoa yako ni ya maana kuliko zingine na kuongeza thamani ya penzi lenu ambalo litastawi na kuchanua vyema. Hivyo uaminifu kwenye mahusiano na ndoa ni msingi imara.

8. Utatetewa wakati wa Magumu au mapito.

Changamoto kubwa kwa watu ni kutokuimarisha mahusiano yao na watu wengine kwa njia ya amani, waonevu, wadhurumaji, kufanya mambo bila kujua kuna kesho ambayo inaweza kuwa na uhitaji wa wale watu unaowatendea ndivyo sivyo. Mtu mwaminifu hujiongezea nafasi ya kutimiza malengo yake kwa sababu ukifanya kwa uaminifu kwa watu basi watu hao hao kuna wakati watakuwa daraja lako la kufikia jambo Fulani maishani mwako, katika uonevu utapata watetezi wengi.

9. Mtu huishi kwa amani na furaha.
Mtu mwaminifu huishi kwa furaha, amani lakini pia huwa na upendo, hapendi kuiona nafsi yake ikisononeka, ikiumia kwa kuidhurumu kwa kukosa uaminifu, hupenda kutenda jambo kwa wakati na uaminifu kwa wengine. Kutokana na kufanya mambo hayo kwa uaminifu basi moyo na akili yake hubaki huru bila deni maana amefanya kila jambo kwa wakati na uaminifu.

10.Uaminifu ni dawa
Huondoa msongo wa mawazo, humfanya mtu kuwa huru asiye na hatia, kumbuka mtu asiye mwaminifu huishi kwa uongo, muda wote anatengeneza mazingira ya kuutetea uongo wake na kuuhalalisha bila kujua kuwa anajiumiza binafsi, anatumia nguvu nyingi kupanga namna ya kudanganya wakati kama angeamua tu kuwa mwaminifu nguvu ile ile  angetumia kwa ajili ya kufanya jambo lenye maana maishaini

Kwa hiyo ni vyema kutengeneza mazingira ya kuaminika na wazazi, watoto, mke, mume, jamii, na katika maeneo yote unayokuwa.
Kwa sababu uaminifu hutengeneza mahusiano mazuri na kuaminika na watu, na kama basi ikitokea kuna fursa inatokea watu watakufikiria na kukupa nafasi.
Prepared by..
Moses Zephania Mgema
0715366003/0755632375
Email mgemamoses@gmail.com
Dar es salaam, Tanzania

Saturday, April 20, 2019

Nianze kwa kukunukuu moja ya maneno ambayo yamewahi kusemwa na Raisi wa Marekani Bwana Abraham Lincoln kwamba " *-

Great mind discuss ideas, Average mind discuss events and Small mind discuss people "-*

Maana yake ni hii " Akili kubwa hujadili mawazo, akili ya wastani hujadili matukio na akili ndogo hujadili watu" mwisho wa kunukuu.

Nukuu hii nimeikumbuka leo baada ya kukutana na vijana Fulani ivi ambao kwa kweli ni vijana wenye nguvu, wadogo na wenye fursa za kuwafanya kuwa na maisha mazuri yanayotegemea utendaji wa kazi, ufanisi, maarifa, ujuzi na utayari wa kufanya kazi bila woga wala mashaka.

Tunapoizungumzia dunia hii leo, imekuwa ni dunia ya ajabu sana kwa sababu ukiangalia kuna baadhi ya watu wake kwa waume wanapambana kuhakikisha wanafikia malengo, ndoto na kuishi maisha mzuri ambayo yanwapa fursa ya wao kufanya jambo lolote kwa sababu ya uhuru wa kifedha ambao wanajua kuwa njia sahihi ya kuishi maisha hayo ninkipambana had I tone LA mwisho lengo kutimiza malengo yake.

Tunapozungumzia hali ya maisha lakini kuna wengine kila Saa na kila

Thursday, April 18, 2019

KUJIFUNZA NI SAFARI YA MAISHA YOTE YA MTU DUNIANI.

Tembea uone, usipotembea unaweza ukifiri kwamba maisha ya eneo unaloishi ni sawa na maisha ya watu wengine ambao wako maeneo mbalimbali ya dunia hii au wakati mwingine unaweza kufikiri kwamba sehemu unayoishi labda mna maisha duni kuliko maisha ya maeneo mengine ambayo huwa unasimuliwa na kupewa stori za huko au pia ukahisi maisha yako na jamii inayokuzunguka ndo mahali sahihi zaidi kuliko mahali pengine.

Ukitembea utajikuta unajifunza mambo mengi sana ambayo kwa ufupi yanakufanya ujue namna nyingine ya maisha ya watu, utamaduni, namna wanavyoadress matatizo, ushirikiano, mitazamo pamoja misingi halisi ya maisha yao.

Zipo stori nyingi sana duniani ambazo kwa ufupi ndizo zinazoyafanya maisha kuwa hasa ni completed circles ya maisha yetu ya kila siku bila kujal unaishi kwenye kusudi la maisha yako au kwa namna yoyote ambayo umeamua kuchagua kuishi.

Mchanganyiko wa maisha haya yanatufanya tujitenge sisi kwa sisi kutokana na levels za kielimu, kiuchumi, kisiasa, kiimani, kimitazamo na fikra. Hivyo kila mmoja wetu kufanya analoona jema analitenda ili kuifanya nafsi yake itulie na kujisikia Amani.

Wakati watu waliofanikiwa wakiwaza namna gani wataendelea kupaa na kuondoka mahali walipo, wanawaza, kuongezeka kwa fedha benki, majumba ya kibiashara, nk, Msomi mwenye kujua maana ya shule nae ataendelea kuhakikisha elimu yake inapaa juu sana ili kukidhi hitaji lake la kuwa na elimu kubwa.

Maisha yanaendelea, watu wa dini na imani nao huwa wanahakikisha kuwa wanafanya vizuri kwenye suala la kiroho huku wakitimiza matakwa kanuni na taratibu za ibada ambazo ndo fungu lao, muda wote watasoma neno, kuomba na kuwaza juu ya ufalme wa Mungu namna gani ataujenga na kuwa mwenye kufanya kusudi lake kwa kadri ya wito na utayari ndani.

Wapo wanasiasa, wanafalsafa, wanaharakati, na watu ambao wanapambania haki, maendeleo lakini pia kutengeneza mazingira ya wao kuonekana bora zaidi ya mwingine na mambo mengine mengi yahusuyo, itikadi, mila, taratibu na kanuni za vyama vyao.

Watu wengi wasio nacho either wanatokea kwenye makundi ya kijamii anabyo nimeyataja hapo juu lakini nimekuja gundua ni watu wenye upendo sana kwa wao kwa wao na hutiana moyo nyakati zote za furaha na nyakati za huzuni wakiamini kuwa hilo ni fungu lao.

Lakini inapokuja kwenye suala la usawa wa kiuchumi na maendeleo watu hawa wamekuwa ni watu wenye wivu, chuki na wenye kutamani siku moja kuona waliofanikiwa wakianguka chini ili kuwa sawa. Ndiyo maana mtu tajiri au aliyefanikiwa kwa kitu chochote kwenye maisha anapokwama maneno mengi huibuka mitaani hasa kutoka kwenye kundi la watu wa chini.

Ipo mifano mingi ambayo inaweza kukufanya ukaelewa nini nataka ujifunze hapa, mfano tulipokuwa shule watoto wengi sana tulipenda kuona yule mwenye uwezo darasani anashuka na kwel walikuwa wakiteleza stori inakuwa kubwa huku akinenewa mabaya, anajifanyaga sana huyu, anajipendekeza kwa walimu, mbinafsi, na hata akiongoza tulikuwa tunaamini anapendelewa na kubebwa na walimu ajabu sana .

Mtu mwenye Mali, uwezo akipatwa jambo baya asilimia kubwa watatengeneza scenario mbalimbali mbaya lengo ikiwa ni kuhakikisha nafsi zao zinafurahi kwa anguko lake hilo, utasikia kwanza alikuwa mwizi mzurumaji, muuji mtoa kafara na maneno mengi ambayo ukiyafuatilia kiundani hakuna maana hasa ndani yake.

Juzi hapa mahali nakaa tulipata changamoto ya nyumba ile kuuzwa na bank na utaratibu uliotumika haukuwa mzuri kwa sababu idhinisho la mahakama lilikuwa bado halijafika kwa aliyekuwa mmiliki halali wa nyumba, kwa tukio hilo kulikuwa na maoni mengi hasa toka kwa majirani, ukitazama watu walioumizwa na tukio hilo ni wale wenye nafuu ya maisha na baadhi yao walitoa machozi lakini wenzangu na mie ndo walishadadia kweli kweli kiasi unahisi kuna uadui kati ya hawa watu.

Sio kwamba matajiri wote wanaroho ya huruma na nzuri hapana ila tunatazama kwa asilimia kubwa.

Wala sio kila mtu masikini anashida hiyo hapana wengine wapo wenye upendo mzuri lakini asilimia kubwa anguko la mtu aliyefaniwa kiuchumi, kwa aina yoyote anapoanguka watu wengi sana wa chini hufurahi na kuzusha maneno mengi kama alikuwa anajidai, analinga ana majivuno nk.

Kwa njia hii
>Mtu mwenye chuki na wivu wa ubaya sio rahisi kufanikiwa sana.
>Masikini wataendelea kuwa masikini kama hawatabadili mitazamo yao na kuwa na imani potofu ya kuwa kila aliyefanikiwa anatumia vitu Fulani.
So is better to learn to appreciate for those who have already achieved and reached their dreams.

This will help poor people to have desire of working hard, learning from successful people and sometimes to pass on where successful people passed.

It gives an open space to the mind which brings easy way of cultivating ideas and coming with a clear solution, ways on how to move forward heading to the destination of our dreams.

Moses Zephania Mgema
0755632375/0715366003
mgemamoses@gmail.com
mosesmgema12.blogspot. com
Dar es salaam - Tanzania

AIBARIKI KAZI YA MWENYE BIDII.

Aibariki kazi ya mikono yako wewe mwenye bidii, hii ni ahadi ya Mungu kwa kila atendae kazi kwa nafasi yake.

Pamoja hayo yote kwa maana ya ahadi za Mungu ambae ndiyo muumba wetu bado iko haja ya kila mtu kujitathimini kama kweli nafasi aliyo nayo anaitendea haki sawa sawa na kusudi la kuumbwa na kuwekwa duniani.

Kwa kazi ya mikono yako yenye ufanisi wa hali ya juu kwa maana ya innovation, creativities, passion and love of it, daily learning kwa lengo la sustainability ndiyo misingi ya kufikia malengo na maono yako bila kujali muda ambao utafikia kwenye kilele cha matokeo yako.

Changamoto ni nyingi njiani kuliko wepesi kwa sababu inaamini kuwa kitu chochote kizuri kinahitaji maarifa mengi, ujuzi, uvumilivu, kwa maana ya njia tupitazo ni ngumu na zenye kusongwa na changamoto na vikwazo vingi.

Wengi waliofanikiwa kwenye mambo yao, kwa maana ya wafanyabiashara, wasomi, wachezaji wa michezo yote, waimbaji, na kwa kila kazi ambayo mtu amefikia kilele cha mafanikio basi hapo mwanzo alipambana sana huku akiweka uvumilivu na imani kubwa ya kwamba ipo siku atafikia malengo yake.

Huku njiani kuna mambo mengi sana mfano kuna watu wanakutia moyo sana na wanatoa semina bomba zenye kuinspire na kumotivate kwamba yeye kama ametoboa basi hata wewe unaweza, lakini ya wezekana mtu yule yule baada ya kumfuata na kuhitaji japo wazo jema alikujibu au kukutendea tofauti na ukivyotarajia, kuna ndugu yako ulimtegemea na alikuahidi jambo Fulani ukitimiza mambo Fulani yawezekana umetimiza yote lakini tena kwa kutumia gharama na akiba yako yote ukijua kuwa kuna support ndogo itafanyika mahali utakapopelea lakini mwisho wa siku yule MTU amekuangusha.

Kuanguka ukiwa unakimbia sio jambo la kushangaza kwa sababu unakuwa kwenye mwendo wa speed na mzunguko wa damu unakuwa juu sana ukilinganisha na ukiwa unatembea au umetulia mahali. Hivyo inuka jikung'ute endelea na mwendo.

Hata safari ya kuikimbilia ndoto na kusudi la Mungu kwako, kuna kuanguka, kuumia na kupoteza kabisa lakini usikate tamaa, no turning back utakuwa mke wa Luthu ambae aligeuka na kuwa nguzo ya chumvi.

Iko misemo na maneno matamu sana kwenye dunia ya Leo yenye kutia moyo, lakini yenye kuumiza ambayo ni machungu neno moja tu ulishike SITOKATA TAMAA.

Usikatishwe tamaa na maneno ya watu kwa sababu kusudi la kuumbwa kwako lazima litimie pambana iamini ndoto na uwezo mkuu ndani yako.

Fanya kwa nafasi yako kwa viwango vya ubora na uwekezaji wa nguvu, maarifa, ujuzi na kila kitu kinachohitajika kufanywa na wewe Fanya halafu Mungu anajua namna ya kufanya juu yako.

Jua kila kazi ufanyayo iwe kwa kutumia kipaji, kazini, unafanya biashara mlengwa mkuu ni mtu, hivyo Fanya huku ukiposition wewe kwenye nafasi ya mteja, msikilizaji wa nyimbo yako mtazamaji wa mpira unaocheza nk. then ujiulize je ingekuwa ndo Mimi natazama au nasikiliza ningeenjoy kazi hii ?

Usifanye kazi kama by the way Fanya hiyo kazi kama hutofanya tena hata kama una malengo ya kybadilisha hapo mbeleni.

Usiwaze matokeo ya kazi wakati hujaweka mikakati ya kuona hayo matokeo unataka uyapate, cha msingi waza matokeo hayo huku ukitimiza michakato ya kufikia huko kwa kufuata michakato sahihi na kwa uaminifu.

Kuwa na Imani na kazi yako lakini kumbuka imani bila matendo matokeo yake yanabaki kuwa ni zero.

Love, be patient, care, corporate with others, Think about the consumers before you serve or release your work hapo utajijuta una fly like Eagle kwa sababu utakuwa umetimiza majukumu yako.
Kila mtu Leo anapambana sana kuhakikisha afanikiwa na kuwa boss au mweshimiwa, hakuna mtu anataka kuwa mtumwa, wa mtu mwingine hivyo pambana kwa kadri ya nguvu zako.
Kazi rahisi itakupa matokeo rahisi, kazi iliyobebwa na umaanisha mkubwa ndani yake itakupa positive results.
Hakuna uchawi wala uganga kwenye mafanikio mchawi ni mimi au wewe hasa pale unaposhindwa kutimiza majukumu yako sawa sawa.

Moses Zephania Mgema
mgemamoses@gmail.com
mosesmgema12.blogspot. com
0755632375/0715366003

Monday, April 15, 2019

Acha matokeo ya kazi yako yakuelezee wewe ni nani. Dunia ya leo imejaa watu wengi wa aina mbalimbali, kuanzia namna wanavyoishi, wanavyofikiri, mitazamo mpaka utendaji wa mambo ndani ya mzunguko wa maisha wa kila siku.
Katika kupambania ndoto malengo na utendaji wa kazi, biashara na mambo mengine ambayo yanaikutanisha jamii kunekuwa na watu wenye fikra njema na wengine wenye fikra mbovu na mitazamo mibovu kitu ambacho kimeacha majibu ya changamoto ndani ya box ambalo kila mtu anaogopa kulifungua.

Sunday, April 14, 2019

INJINI YA MAFANIKIO NI INTERACTION/ KUCHANGAMANA

Kutokana na kuishi kwenye dunia huru kila mtu ana aina ya maisha ambayo amependelea kuyaishi kwa Uhuru na uchaguzi ambao yeye binafsi ameona kwa njia hiyo basi ni sahihi.
Hata mimi, wewe na yule kila mmoja ana aina yake ambayo anaitumia kuendesha maisha yake.
Pamoja na kuwa na Uhuru wa maisha na uchaguzi wa mfumo wa maisha ambao kila mtu amependelea lakini sio kila mfumo ni sahihi sana kuishi bali wakati mwingine ni mbaya sana
Kuna watu wanapenda sana kuishi maisha ya kuchangamana na watu, wako huru kushirikiana na kila mtu, watu wanaamini katika nguvu ya umma na ushirika na wenzao.
Lakini kuna watu ambao ni wakimya sana na ni watu ambao wao kuchangamana au kuwakuta wakipiga stori na kushare mawazo na wenzao ni ngumu sana
Na Mara nyingi husema wanaishi maisha yao hawataki mtu afuatilie maisha yao. Lakini kiuhalisia maisha ya kujitenga na watu kwa mtu mwenye malengo na nia ya dhati ya kufikia ndoto zake lazima achangamane na watu.
Hii inafaida nyingi sana kuliko kutengeneza mazingira ya kuwa mkimya na kuishi maisha yako binafsi.
Watu wengi wanatafsiri vibaya sana baadhi ya maneno kama ambavyo nitaelezea hapo chini
1. Hekima
Watu wengi sana wanaamini kukaa kimya ndiyo hekima na busara, lakini kumbe hiyo sio hekima wakati mwingine ni kwa sababu ya ujinga, kiburi, majivuno na kukosa uelewa wa mambo mengi yanayohusu jamii. Kwa hiyo si kila mtu mkimya ni mnyenyekevu na mwenye busara.
2. Imani
Kuna imani zimejengeka kwenye jamii nyingi kwamba, ukimya nao ni jibu ni kweli. Lakini je hilo ni jibu sahihi au ni tango pori kwa hiyo wakati mwingine ni vema kusema ili kujisaidia wewe binafsi ila pia kumsaidia mwingine.
3.Hakuna mtu anaweza kuishi pekee yake.
Tunategemeana sana kwa mambo mengi, sijui umewahi kujiuliza huwa unaenda kazini kumfanyia nani kazi, je ni boss, wanyama au kuna walengwa wa kazi unayoifanya wanatakiwa kupata huduma yako.

Hapo jiulize sasa kwamba ni namna gani unaweza kuishi maisha yako bila kuwashirikisha wengine ?. Jibu rahisi kwamba hakuna mtu anaweza kuishi maisha yake pekee yake Bali tunategemeana.

Tunaendelea.............
Kuna aina ya maisha baadhi yetu tuliamua kuyaishi tangu tukiwa watoto kwa kulazimishwa na wazazi ndugu jamaa wa karibu, walimu na walezi wetu au hata baada ya mtu kukua anaamua kuishi maisha Fulani anayo yapendekeza yeye hata kama sio sahihi.

> kutokucheza na watu wa familia kadhaa kutokana na levo za maisha.
> Kuaminishwa imani Fulani hasa kwenye masuala ya imani, kwamba siwezi kucheza au kula kwa kina Jose kisa wao ni wakristo na Mimi ni mwislamu na kinyume chake.
>Wazazi kuwatenga watoto wao na kuwasimamia na kuwaondolea fursa ya kucheza wakiamini wanawapa malezi bora kumbe wanaua uwezo wa watoto wao na mengine mengi.

Social Interaction/Mchangamano ndani ya jamii ni muhimu sana.

Kama tulivyoumbwa toka mchakato wa kupatikana kwetu ulihusisha ushirikiano kati ya watu sio mtu na wewe au Mimi nikapatikana

Simpo kabisa kwamba binadamu aliumbwa kwa ushirika na ushirika una nguvu kubwa iletayo ushindi kwa mtu binafsi lakini pia kwa jamii.

Kuna faida nyingi na kubwa mno kwenye kushirikiana na wenzako mfano, kucheza pamoja, kupiga stori, kujiweka karibu na wenzao hii inakujengea uwezo wa
1. Kujifahamu zaidi
2. Kuwafahamu wengine
3. Na kufahamu zaidi mfumo wa maisha uko vipi kuanzia ngazi ya chini mpaka huko duniani.

Kupitia social groups interactions kuna elimu kubwa ambayo wakati mwingine huwezi kuipata ukiwa nje ya makundi haya ya kijamii. Mfano niliwahi kusoma historia ya moja ya matajiri hapa nchini kwamba pamoja na kwamba alianzisha biashara yake yeye kama yeye lakini amekuwa akipata mawazo mazuri sana kupitia kwenye makundi ya kijamii kama kwenye vijiwe vya kawaha na maeneo mengine alisema kwamba.
Alichogundua yeye watu wa chini huku mitaani wana mawazo mazuri sana ukilinganisha wakati mwingine na mawazo mengi yaliyopangiliwa kwenye vitabu wakati mwingine huwa na uhalisia wa maisha ya mbele zaidi ukilinganisha na stori za vujiweni vinavyogusa maisha halisi ya watu ambao wakati mwingine ndiyo wateja au walengwa wa huduma za kibisahara.

Changamoto kubwa ambayo vijana wengi tunapitia ni ile hali ya kujifungia kwenye mitazamo na mifumo Fulani ambayo kwa namna moja ama nyingine inatuua tukidhani kwamba tupo sahihi.
Mfano mtu anafungua Instagram account anaweka private, kila jambo binafsi ukifuatilia undani wa hiyo private eti hataki mazoea inasikitisha sana.
Kila mmoja ana Uhuru wa kufanya anachoona ni sahihi kwake na maisha yake lakini kama hakuna sababu ya kujitenga na wenzako kwa nini ujitenge kisa tu ulimwona Fulani kaweka private na wewe ndiyo hivyo tena.

Watu kama hawa unakuta anafanya hivi akiwa chuo anapomaliza chuo basi ameanzisha biashara Fulani ndo anaanza kujipendekeza kwa watu na kuwalazimisha wakati mwingine wamfollow kisa tu ameanzisha online business.

Je watu wakivunga utasema unalongwa kumbe wewe ndo mchawi wa hiyo online business au hata huku kwenye jamii husalimii majirani kwa lugha rahisi unafunga vioo ukifungua duka basi unaanzisha ushositito wasiponunnua eti wana wivu yako huyakumbuki, unajitia msamalia mwema na kuwatangazia wakati ulikuwa unawaona  mawe tu hapo kabla.

Unakuta mtu yupo kwenye group la whatsup ambalo hata hakuungwa alijiunga mwenyewe kupitia Link lakini mtu huyo, ni kimya, hachangiaji chochote, hata kuitikia salaam, au kusalimia au mtu kapositi hata kupongeza au kukosoa hakuna kimya tu. Unajiuliza je huyu mtu yupo hapa kwa bahati mbaya au shida ni nini.
Ukimuuliza atakuambia niache na maisha yangu lakini wakati huo yuko ndani ya group huo ni ushamba na kutokujutambua.

Maisha yetu ni ushirika, kushare ideas, having funs na mambo mengine kitu ambacho kina leta faida na manufaa kwenye kazi hata afya kiujumla.

Kuna faida za kuchangamana na makundi ya kijamii japo si kila kundi au group ni sahihi.
1.Inatengeneza connection na watu wapya.
2. Kujua tabia za watu, hii inakupa fursa ya kujua ni watu gani sahihi wakuambatana nao.
3. Ni rahisi kugundua uwezo wako kwa maana ya kipaji ambacho kinaweza kukufanya kufikia ndoto na malengo yako.
4. Kupitia socializations una nafasi kubwa ya kugundua fursa mpya za kibiashara, maana kupitia mazungumzo utagundua mahitaji ya watu lakini pia changamoto ambazo unaweza kuzigeuza nakuwa fursa kwako.
5. Ni rahisi kupata social support unapokuwa na jambo lako au unapoanzisha kitu chako, maana wateja au watazamaji wa kipaji chako kama wewe ni mwimbaji au unakipaji chako.
6. Ni platform ya kujitangaza na kuimbia dunia kuwa wewe ndo unahitajika kwa jambo Fulani.
7.Nafasi ya kujifunza kila siku vitu vipya.
8. Nafasi ya wewe kujijua, maana wakati mwingine tunajijua kupitia watu. Hivyo inapelekea kujua nguvu na udhaifu wako.
Note.
Hizi ni baadhi ya faida ambazo mtu anaweza kuzipata pale anapokuwa ni mtu wakushirikiana na wenzake ndani ya jamii.
Lakini pia kuna faida za kiafya maana kupitia interaction unajifunza mengi, lakini vilevile unaweza kuwa unapitia changamoto Fulani kwenye maisha lakini unapokuwa mchangamanaji kwenye jamii unaweza kujikuta unakutana na watu ambao wamewahi kupitia changamoto kama yako na wakavuka.
Hivyo kupitia shuda hizo unaweza kupata nguvu na imani kwamba kumbe hata wewe unaweza kutoka hapo.
NB.
Pamoja na faida nyingi lakini fahamu kuwa si kila social groups lazima uitaract nao, tazama makundi yenye faida.
Sio kila page ya Instagram, group la whatsup ujiunge eti kisa umeambiwa na Moses uwe na social groups interactions, tafuta groups, na hudhuria semina zenye manufaa kwako.
Ipo nguvu kwenye ushirikiano, na hakuna mtu anaweza kuishi mwenyewe kama yupo jangwani.
Maisha yetu ni ecology kwa maana kwamba tunategemeana, ukianzisha biashara mlengwa ni binadamu, unapoamka kwenda kazini mlengwa ni binadamu nk.

Moses z. Mgema.
0715366003/0755632375
mgemamoses@gmail.com

MAARIFA KWENYE KARNE YA 21 NI MSINGI WA MAFANIKIO YAKO

Nimekuwa na muda mzuri sana wa kujifunza kila siku, na hayo yamekuwa ni maisha yangu sasa, na kupitia aina hii ya maisha nimejikuta binafsi nikipata nguvu na imani kwamba kwa kila jambo lina sababu ya kuwa mahali popote lilipo.
Kujifunza kama ambavyo waandishi wamekuwa wakiandika nami naungana nao kwa kusema: Kujifunza ni mchakato endelevu kwa yeyote ambae anaendelea kuishi.
Na tunajifunza kupitia mazingira yanayotuzunguka na Yale mapya tunayokutana nayo kila muda tunaopata tukitoka nje ya maeneo yetu tuliyoyazoea.

Kupitia kujifunza huku, tunawezesha akili zetu kushiba na kuwa na afya ya maarifa ambayo kwa namna moja ama nyingine maarifa hayo yakitumika vyema ndiyo yanayoweza kubadilisha mfumo mzima wa maisha ya mtu kutoka vile alivyo, namna anavyotazama, fikiria, kiwango cha kuamini kuwa alipo yawezekana si mahali pake lakini pia kupitia maarifa anaweza gundua kuwa ndani yake kuna uwezo wa ajabu kiasi kwamba akiamua kuutumia vyema unaweza kumpeleka mbali zaidi maishani.

Niliwahi kusikia msemo maarufu nchini Tanzania kuwa: " UKITAKA KUMFICHA JAMBO MTANZANIA BASI WEKA KWENYE MAANDISHI UTAKUWA UMEMALIZA KILA KITU" maneno haya sio mazuri sana kwa sababu yanajaribu kuelezea udhaifu wa watanzania wengi kuwa hatupendi kujifunza kwa Uhuru labda kwa shuruti kama inavyofanyika kwenye mfumo rasmi wa Taaluma ambao ni haki ya kila mtanzania kupata elimu hiyo.

Lakini kwa mtu ambae amekubali kuyafanya maisha yake kuwa ni yakujifunza kila muda, mtu wa namna hii huwa anakuwa na nguvu na uwezo mkubwa wa kufanya mambo yake kwa sababu

1. Maarifa hujenga uwezo wa kufanya mambo kwa ufasaha hasa kwenye eneo husika.
2. Maarifa hujenga imani na kujiamini.
3. Maarifa huvumbua fursa zilizojificha.
4. Hujenga uwezo wa kufikiri zaidi.
5 unaufanya ufahamu wa MTU kuwa updated muda wote na active
6. Kujua mahitaji ya wakati uliopo na kuweza kuitabili kesho.
Hizi ni baadhi ya faida ambazo mtu anaweza kuzipata kama tu amedhamiria toka ndani kuwa maisha ya kujifunza yawe ni maisha yake.

Niliwahi kusoma kitabu kimoja hivi kilichoandikwa na Brian Trace kinaitwa "NO EXCUSES" niligundua mambo mengi sana ambayo yamechangia watu wengi kuishi maisha ambayo hayawastahili Kati ya mambo makuu niliyojifunza kupitia kitabu hicho ambacho pia kilibadili kabisa mtazamo wangu ni
1. Kuishi kweye sababu.
2. Kuamini mtu alipo ni kwa sababu ya mtu Fulani.
3. Kutokuwa na nidhamu binafsi nk.

Pamoja na kusoma kwa undani niligundua kuwa maisha ya mtu yapo ndani ya mtu mwenyewe bila kujali umekulia mazingira yapi as long as umeshakuwa mtu mzima na unaafya njema basi wewe ndiye utabaki kuwa mwamzi sahihi wa maisha yako au mwamzi wa maisha yangu.

Kufeli, kutokwenda shule, wazazi kutokuona umuhimu wa jambo Fulani yaani elimu nk, bado haiondoi uhalisia kwamba maisha ya mtu yako ndani ya maamzi yake mwenyewe.

Watu wengi tumekuwa wavivu sana kwa mambo mengi, kuwaza, kujitoa kuanzisha shughuli ndogodongo kama kuuza matunda, kuuza bidhaa zilizo na uwezo wa kuwa na mtaji mdogo badala yake tunawalalamika au kuwalalamikia wengine

Wengine wamepata nafasi ya kufanya kazi, kujiajiri kwa kazi zao lakini wamekosa nidhamu ya kazi yao, wanachelewa kwenda kazini, wanafanya kazi kana kwamba wamelazimishwa kufanya hivyo, hawana upendo na kile wanachokifanya mwisho wa siku ubora au ufanisi wa kazi umekuwa mdogo kitu kilichopelekea kupoteza ajira zao au hata biashara zao kufa.
Nidhamu mbovu juu ya vipato vyao kitu kinachopelekea mtu kuonekana ana kazi au biashara lakini hatua ya maendeleo iko pale pale kila mwaka unapopinduka ajabu sana.

Lakini kumbe chanzo cha haya yote ni ukosefu wa elimu na maarifa ya namna gani yakufanya ili kwa kila jambo ambalo mtu anafanya liweze kuwa endelevu na lenye kumfanya apige hatua ya maendeleo yake binafsi lakini pia familia.

Pamoja na kwamba ukisoma vitabu vingi sana hasa hizi inspirational books unaweza jikuta unaona ni kama umechelewa, au uone kumbe kufanikiwa ni rahisi, lakini kuna umuhimu wa kujifunza maana mazuri ni mengi kuliko mabaya kupitia elimu.

Tuwe ni watu wakujifunza, kupitia kujifunza utapata shuhuda za watu waliofanikiwa, utaongeza ujuzi na maarifa mapya juu ya kazi au biashara unayofanya na unaweza kuiboresha zaidi.

Utapata mbinu mpya za namna ya kufanya kazi zako lakini pia kama ni biashara unaweza gundua vitu vipya ambavyo kwenye mazingira yako havipo na wewe kuwa mwanzilishi wake.

Kwa hiyo kujifunza jambo nyeti na muhimu sana kwenye maisha yetu hasa kama unataka kufikia ndoto na malengo yako, tunafanikiwa kwa kuangailia wengine walifanya nini.
Elimu ina transform namna yakuwaza, kufikiri na namna ya kutenda.
Note.
Kusoma sana vitabu au kupata muda mwingi wa kujifunza na kuhudhuria semina za wajasirimali haimanishi kwamba ndiyo tiketi ya mafanikio hapana.
Kujifunza na kupata maarifa ni jambo moja lakini utekelezaji wa maarifa hayo ni jambo LA muhimu zaidi na hilo ndilo linaweza kuwa ndo msingi na ngao ya ushindi wa maarifa hayo.

Maarifa na ujuzi bila utekelezaji wake ni sawa na kukubaliana na msemo wa wahenga usemao, "PENYE MITI HAPANA WAJENZI"
JIFUNZE+ WEKA KWENYE UTEKELEZAJI = MAFANIKIO
Mungu ayape nguvu maono yako kwa nguvu unayoitumia kuhakikisha unafikia malengo yako.

Elimu ni mtaji wa kila jambo

Moses z. Mgema
0715366003/0755632376
mgemamoses@gmail.com
Dar es salaam, Tanzania

Tuesday, January 8, 2019

KWA KILA JAMBO ANZA, TEMBEA NA MALIZA NA MUNGU.

Pamoja na maarifa, ujuzi, elimu, shauku, uwezo mkubwa wa kufanya kazi, bidii ya kufanya kazi bila kuchoka.

Haitoshi kwenda pekee yako na kujitegemea mwenyewe au watu wanaokuzunguka.

Fedha na kila aina ya rasimali ulizonazo haziwezi kukubeba katika kila jambo.

Ufanyaje sasa ?
Kwa kila jambo tembea na Mungu, mshirikishe Mungu, mwache Mungu awe kiongozi kwa kila kazi yako.

Ukitembea na Mungu hakika huwezi kuona unaanguka kibiashara au katika kazi zako kwa sababu yeye atasimama na kupigana  na maadui wa kazi zako.

Ukiwa Mwaminifu kwa Mungu kwa kutoa fungu la kumi, hakika Mungu ataibariki kazi ya mikono yako.

Ukiwa mwaminifu kwa Mungu, Mungu atakutetea wakati wa ukame wako.

Kumbuka Biblia inasema yeye alikujua kabla ya misingi ya dunia kuumbwa, kwa hiyo hatima ya maisha yako iko mikononi mwake.

Kwa hiyo hata alipokuumba aliweka kusudi na maono yake ndani yako ili uyatimize kwa utukufu wake.

Kwa hiyo unapaswa kufahamu kuwa mafanikio yote, maarifa yote, ujuzi wote na utajiri ulio nao ni kwa sababu Mungu alipanga maono yake kupitia wewe, na amekupa uwezo wa kujua na kutambua uwezo wako na wewe kufanyia kazi, fahamu huyo ni Mungu.

Usikubali kutembea pekee yako mwaka huu tembea na Mungu hakika utaona matunda mazuri kwa sababu Mungu atakuwa na wewe.
Wakati mwingine biashara, kazi zetu hazisimami kisawasawa kwa sababu tujiona kuwa tunaweza bila Mungu.

Tumejitegemea sana sisi pasipokujua kuwa wakutegemewa pekee ni Mungu

Jiepushe na watu ambao wanaushauri mbaya kuhusu Mungu, acha kutegemea mwadamu, mfano kwenda kwa waganga, maana Biblia inasema kwamba amtegemeae mwanadam amelaaniwa kabisa.
Kwa hiyo kila mmoja lazima amtegemee Mungu kwa akili yake yote.
Pamoja na kufanya kazi kwa bidii na kufuata kanuni zote zinazotakiwa kwenye kanuni za kazi bado kanuni kubwa na yenye nguvu basi ni kumtegemea Mungu
Yeye ndiye anajua hatima ya maisha yako.
Msingi wa mambo yote mema ni Mungu tu.

Barikiwa kwa kusoma ujumbe huu mwanzoni kabisa kwa mwaka huu
Mwaka huu tembea Na Mungu
Acha kutembea pekee yako.

Moses zephania Mgema
0755632375.
mgemamoses@gmail.com
Dar es salaam Tanzania

*-2019 Is the year of achievements-*

Sunday, January 6, 2019

MAISHA YA YESU DUNIANI NI PAKITI KAMILI YA MAISHA HAPA DUNIANI.

Habari,
Natumaini kila mmoja watu amepata neema nyingine ya upendeleo kuifikia siku ya leo akiwa mzima wa afya.

Nitoe pole kwa yeyote ambae anapitia changamoto yoyote ambayo inamnyima furaha yake ya kila siku.

Niende moja kwa moja kwenye somo la kwanza la mwaka huu tangu kuanza, naamini utakuwa msingi mzuri wa kuunza mwaka huu baada ya mapumziko ya mwisho wa mwaka.

Somo letu kama linaposomeka katika kichwa cha habari, basi tuambane ili kuweza kufahamu nini hasa tunajifunza, lengo na nini matokeo yake baada ya kujifunza.

Yesu au Mesia sio jina geni kwa watu wote, ni mtu ambae alikuwepo duniani kwa hali ya mwili na aliishi kati ya maisha ya kwaida kabisa. Yesu alizaliwa kwa hali ya kawaida na akaishi kwa uhalisia wote wa dunia.

Na ndiyo sababu iliyonifanya kuja na somo hili kama msingi wa kila mtu ambae, ana shauku ya kuona ndoto, malengo, nia na matamanio yake yanatimia siku moja.

Yesu alikuwa na malengo ya yeye kuwepo duniani, na lengo kuu lilikuwa kuleta ukombozi wa maisha ya kiroho lakini hata katika mwili, lakini lengo kuu ilikuwa kukomboa watu waliokuwa wamepotea.
Hiyo ndiyo ilikuwa main purpose ya Yesu kuwepo duniani.
Pamoja na yote hayo, mimi nimejaribu kutafuta na kufikiri zaidi juu ya ujio wa Yesu duniani.

kusudi kuu la yeye kuja duniani linafahamika kwa kila mtu, lakini je ni hilo pekee ? hilo ni swali ambalo kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza zaidi.

Naufahamu uwezo wake, nguvu zake, mamlaka yake, uwezo wa kuona kesho kabla ya siku kufika lakini kwa nini alikubali kuja kufa huku duniani, je hapakuwa na njia nyingine ya ukombozi?.
Jibu hapana Yesu anajia nyingi ambazo zingemfanya kuikomboa dunia bila yeye kupata maumivu na mateso.
Kuna zaidi ya shughuli za kiroho zilizomfanya yesu kuja duniani. Na kama dunia ingemwelewa vizuri au ingeelewa vyema sababu zingine  zilizomlazimu yesu kuja duniani basi huyu pekee ndo angekuwa Role model wa wote.

Yesu ni pakiti kamili (Full package) ameenea kila kona ya maisha ya binadamu, anaemkubali na hata asiemkubali ila kiuhalisia Yesu anagusa kila kona na pembe ya maisha yetu.

Yesu ni mwalimu, na alikuja kufundisha uhalisia wa maisha ya duniani.

NAMNA GANI TUNAJIFUNZA KWAKE.
Lesson 1.
Yesu aliamini katika kufanya kazi kwa  bidii sana na kwa muda mrefu sana huku akiwa na focus na nia ya kufikia kile ambacho amedhamilia kukitimiza kwa siku. Ndiyo maana unaweza kuona kwenye mkusanyiko wa wanaume 500 na wanawake na watoto alilazimika kufanya muujiza watu wapate msosi palepale ili ratiba yake ya siku itimie hata kama ni usiku wa manane.
 
> Hapa tunajifunza kufanya kazi kwa bidii sana lakini kuhakikisha kila ratiba unapopanga mambo ya kufanya kwa siku, wiki, mwezi na hata mwaka lazima uhakikishe unapambana kutimiza ratiba ili kuepuka viporo, bora kuchelewa kurudi nyumbani lakini ukiwa umetimiza majukumu ya ratiba yako.
Lesson 2
Alipata habari ya kuumwa kwa lazaro rafiki yake, lakini tayari alikuwa kwenye ratiba ya mambo mengine aliyokuwa anayatimiza, kwa hiyo alilazimika kumaliza kwanza kazi zilizokuwa ndani ya ratiba yake ndo akaenda alikokuwa ameitwa.
Jiulize swali.
Je ni mara ngapi rafiki yako amekuondoa kwenye ratiba yako ?
    Majibu unayo wewe

>Hapa anatufundisha kuwa usikubali mtu awae yeyote kukuharibia au kuingilia ratiba yako pasipo sababu, hata kama kuna sababu ipime uzito wake kama unaona unaweza kuisolve hata kwa wakati mwingine basi timiza kwanza ratiba uliyonayo ili kuondoa uwezekano wa kuloose focus na concentration.
Ukikubali kila mtu aingilie ratiba yako na wewe umtimizie haja yake, basi wewe ni ngumu sana kufikia malengo kwa wakati ambao ulitazamia kutimiza. Maana mtu asiyekwenda na ratiba huyo ni kama bendera.
Kuna wakati unapokea taarifa ngumu ni vyema kutulia na kuonesha ukomavu, ukifanya hivyo basi utaipa akili kupumua vyema, hata unapoamua kufanya maamzi basi unatakuwa na asilimia kubwa ya kuamua vyema.
Lesson 3
Kutimiza malengo yako kwa wakati sio rahisi usipokuwa, mkomavu na mwenye nia ya dhati.
> pamoja na uwezo alokuwa nao lakini kuna wakati alikiri wazi kwamba yasingekuwa mapenzi ya Mungu basi yeye angeomba kikombe kimwepuke.

Maana yake nini kwenye maisha yetu ya kupambania ndoto zetu, kuna wakati unaona mlima mkubwa, huoni kama utaweza, kila unalofanya ni gumu lakini bado unapaswa kusimama kupambana ili kuvuka hapo

Hakuna mafanikio au kutimiza ndoto kirahisi lazima utoke jasho kweli kweli, no way ya kuepuka jambo hili.

4. Yesu anatufundisha kuvumilia sana kuna wakati mambo hayaendi, changamoto, unajisikia kuchoka, kukata tamaa lakini  bado hata kama hayo yanakuja bado unapaswa kupambana hata mwisho utakapoona umetoboa.

5.katika kila jambo unalofanya, watu watakudhihaki, kukusaliti, majungu, kukusengengenya, utaanguka au kutaitiwa mahali basi utasikia hata marafiki zako wakisema anajifanya eti mpambanaji basi ajitoe hapo alipokwama, wengine utasikia wanasema si alijifanya ana hela kwa sababu yeye ni mjasiriamali mbona siku hizi.....maneno mengi yote hayo yaache yapite ni upepo tu.

Mfano wa maisha ya Yesu
Wakati anachapwa mijeledi alithihakiwa, alitukanwa na kuambiwa kama yeye ni Mwana wa Mungu basi ajiokoe lakini hakutaka kuluzi focus kwa kuwajibu watu.

Lesson 6
Kupenda kile unachokifanya hata kama ni cha muda, maana yake nini hicho unachofanya ndiyo daraja la wewe kuifikia ile ndoto kubwa ya maisha yako.
Yesu alikubali kuja duniani lakini alikuwa anafahamu lengo ni nini. Alijua maisha ya duniani ni ya muda, pamoja na hayo aliithamini sana kazi yake hapa duniani, ndiyo maana leo tunamwita Mfalme wa wafalme.
Lesson 7.
Sio kila unachoombwa basi utoe, kuna wakati unapaswa kuwafundisha watu wanaokuomba namna yakufanya ili kuondoa jamu njiani wakati mwingine.

Yesu akawachia mwanafunzi wake kutoa pepo yeye akiwa hayupo, alitaka wajue na wawe na uwezo wa kujitegemea hata kama yeye hayupo. Hii ina jikita zaidi pale unapokuwa umefanikiwa, wengi hasa ndugu watakuja kukuomba fedha, wafundishe namna fedha inatafutwa.

Lesson 8.
Yesu ni mtoto wa tajiri ambae alikuja kuwafundisha masikini namna njema ya kuishi, hakuna lawama bali ni kufanya kazi bila kujali mazingira gani yanakukabili.

Alikuwa ni Mungu aliye uvaa utu ili kutufanya tujifunze kwa vitendo
Alifundisha pia yafuatayo
Kuwa na nia ya dhati.

General Lesson kwa mwaka huu 2019
Jitahidi sana kuwa wewe.
Fanya kazi zako bila kujali hali.
Focus kwenye malengo yako usipeperushwe na kelele za watu.
Fanya kwa bidii sana kila unapopata nafasi ya kufanya.
Simamia malengo yako.
Simamia ratiba zako.
Toa muda wa kujifunza na kuongeza maarifa ujuzi na taaluma mpya.
Fanya kazi kwa malengo na bidii
Baada ya yote.......
Kwa kila jambo Mungu ni wa kwanza.
Omba soma neno tafakari mtolee mungu kile kidogo anachokupa Mungu

Mwisho.
Yesu alikuja duniani kubadilisha fikra za watu kutoka mtazamo hasi mwenda Mtazamo chanya.
Mageuzi ya fikra yalianzia kwake.
Uaminifu na utii ndo yalikuwa maisha yake, hivyo yakupasa kuwa hivyo pia.
Kuthubutu hata kama huelewi, hata kama upo katika nchi ya ugeni mazingira   ni magumu
Yesu alikuja kukomboa
Roho
Fikra
Na ukombozi ulifanya katika aspects zote za maisha ya binadamu.
Mwaka huu ukawe mwaka wa mageuzi
Ya fikra, mitazamo na tuishi kwa malengo na targets huku tukimtumaini Mungu.

Mungu akubariki sana mwaka huu 2019 hasawewe uliemua kufanya kazi kwa bidii maarifa na ujuzi mwingi
Kwa utukufu wa Mungu utafanikiwa.

Prepared by:
Moses zephania Mgema
0755632375.
Mgemamoses@gmail.com
Dar es salaam Tanzania

Wednesday, January 2, 2019

THAMANI YA WAZO LAKO.

Mungu amenissaidia, nmeamka salama kabisa. Nitoe pole kwa ndugu jamaa na marafiki ambao wanapitia changamoto mbalimbali, kwamba Mungu yupo atarejesha neema ya uzima au kuiondoa changamoto yoyote unayopitia sasa.
Mungu ni yule yule aliyemtendea Ayubu, lazaro na wengine, hata sisi pia lakini jambo jema ni kuendelea kumtumaini Mungu siku zote.

Leo ningependa tujifunze tena kitu muhimu na cha msingi sana hasa tunapoendelea na mchaka mchaka wa maisha ya kila siku.

Leo tutajifunza kitu kinaitwa        

*-THAMINI YA WAZO LAKO-*

Mungu wetu ni Mungu wa maarifa na maajabu mengi ambayo kiufupi tu hakuna mtu anaweza kuyaelewa zaidi ya kukiri tu kwamba Mungu ni kila kitu kwenye maisha yetu.

Mungu alituumba akatupa uwezo na akili yakuweza kutumia ili kuzitambua fursa na kuzitumia vyema kwa manufaa binafsi, familia, jamii lakini kwa ajili ya utukufu wake yeye Mungu.

Wazo  (Idea) ni moja ya silaha kubwa ambayo Mungu alimpatia mtu, na akampa uwezo wa kulinyumbua wazo hilo na kuwa faida kwake. Hapa ndipo tunaona watu wanagundua fursa mbalimbali zinazoendesha maisha yao.

Wazo (idea) ilimwijia Biligate, Wallace Wattle, mmiliki wa Facebook Mark Zuckerberg, wamiliki wa Twitter, whatsup, na mitaondao mingine ya kijamii hatimae leo tunatumia vitu hiv, Microsoft, Fb nk.  ni kati ya viungo vya mawasiliano ambavyo vimerahisisha sana njia za mawasiliano ukilinganisha na zama za kale.

Wazo la wagunduzi wa baiskel, pikipiki, gari, treni, meli na ndege, liligeuka kuwa fursa ambayo imeleta mageuzi makubwa sana kwenye nyanja za usafiri na usafirishaji.
Wazo ni kitu cha Thamani sana kama kikiheshimiwa na kupewa heshima yake, wazo hugeuza umasiki kuwa utajiri, wazo hugeuza woga kuwa ujasili, hapo ndipo tunapata watu waliojitoa muhanga bila kujal hadhi zao na leo ni watu wa mfano na matajiri duniani kote.

Kila jambo huanza kama wazo, liwe jambo baya au zuri lakini asili yake ni wazo moyoni na kwenye ufahamu wa mtu kabla halijaja katika ubayana wake.
Mpira wa miguu ulianzia nchini England kama wazo la wafanyakazi kujiburudisha baada ya kazi, lakini leo ni kati ya sekta inayozalisha ajira na utajiri mwingi kwa vijana na jamii kwa ujumla hapa (IDEA WAS IMPLEMENTED)

Mifano ni mingi mno ambayo tunaweza kuitumia, *-WALLACE WATTLE-* moja ya matajiri waliotokea kwenye familia masikini huko nchini marekani mwishoni mwa miaka ya 1880s hadi alipofariki dunia miaka ya 1900s aliwahi kusema, kila mtu ana wazo jema lakini namna ya kulitekeleza hilo wazo.

Watu duniani wana Mawazo mazuri sana na baadhi ya Mawazo ya watu masiki leo, yaliwahi kuwa ngazi ya watu matajiri duniani.
Kupitia vijiwe vya kawaha na vijiwe vya stori mawazo mengi huzalishwa na ni mawazo kuntu sana, shida iliyopo wale wanao zalisha mawazo hayo wengi wao hufanya ivo ili kunogesha vijiwe na kufanya siku iende wakalale.

Wachache sana wanaokuwa ndani ya vijiwe hivyo hung'amua mawazo hayo na kuyakusanya na kuyafanyia kazi na leo hawa matajiri tulio nao duniani na hapa Tanzania.
Hujawahi kupita mitaa ya jiji la Dar es salaam ukawasikia wazee wakisema huyu Bakhresa tulikuwaga tuko hapa anatuuzia kashata na kawa na wana feel proud kabisa kusema ivo, yawezekana ndani ya stori hizo kuna Mawazo bora kabisa Bakhresa aliyapata na kuyaboresha na leo yamemfanya kuwa  moja ya matajiri Tanzania na Afrika kwa ujumla.

Nimekutana na mawakala na watu wengi wanaosema tulimpokea Shigongo alipotoka kwao Mwanza, na baadhi yao wanamwelezea kama mtu aliyekuwa duni sana lakini mwenye focus na malengo kwenye Idea yake.

Wengine wanasema waliuza naye magazeti,hata alipokuwa anaanzisha gazeti la uwazi akiwa hana kitu wengi wao walikuwa wanamtazama wanasema, wakati mwingine aliwaomba pesa ili kuzalishia gazeti la siku inayofuata na mengine mengi, lakini  leo Ndugu Shigongo ameajili zaidi ya watu mia kuanzia kwenye hotel zake, Global publishers, Global online Tv na vitega uchumi vyake vingine kama, Dar live mbagala ukumbi maarufu kabisa wa burudani.

Wazo ni kito cha Thamani sana, Je ni namna gani unaitumia, hakuna masikini duniani maana kila mtu ana wazo, wakati mwingine mawazo yetu ni bora kuliko waliofanikiwa, lakini hayaonekani bora kwa sababu hatujayaweka katika utekelezaji kwa kumaanisha toka ndani.

Wazo bila kuamua kulitekeleza ni sawa na midori ya wauza nguo sokoni kariakoo.
Amua leo bila kujali mazingira ya kiuchumi, kimaisha, nk. Amua kutoka moyoni.
Kufeli na kufaulu huwa ni maamzi ya mtu binafsi, ukiamua kufeli ni rahisi, ila ukiamua kufaulu au kufanikiwa ni maamzi magumu ya kutamani kutoka hapo ulipo kwenda eneo lingine.
Wazo ni jema pale tu unapolifanyia kazi kwa uaminifu, na kumaanisha, maisha yamekuwa na changamoto nyingi sana lakini hatuwez kuacha kupambana.
Kila mtu huwa na wazo, hivyo hakikisha unapopata wazo hilo lifanyie kazi immediately, bila kuchelewa, unapochelewa wengine wataliona na kulifanyia kazi.
Epuka kushirikisha ideas zako kama unaona kwamba bado huna uwezo wa kutekeleza kwa wakati huo, maana ukishare tu na watu, watu wenye nafasi zao watalitumia na wewe kubaki kwenye kushangaa.
Tumia wazo lako vyema, kuna wakati kama utakuwa na mawazo mazuri na huyatendei kazi basi kuna hatariya wewe kuumia kila siku kwa kuona watu wengine wakiyatumia mawazo yako
Heri ya mwaka mpya.
Moses zephania Mgema
0755632375
mgemamoses@gmail.com

ASANTE 2018, KARIBU SANA 2019

Mwaka 2018 umepita, tuna sababu ya kumshukuru Mungu sana kwa mengi mazuri aliyotutendea, mengi magumu aliyotuvusha, haikuwa rahisi hata kidogo maana ndugu jamaa, marafiki, majirani wameshindwa kuambatana nasi kwa kuunza mwaka huu.

Wengi wamefariki na wengine wameingia wakiwa wagonjwa na wengine wanapitia changamoto mbalimbali, lakini yote juu ya yote ni vyema kumshukuru Mungu tu.

Ni kwa neema wala sio kwa welevu, ujanja, ubora na utakatifu mwingi uliotufanya kuwa hai, is by Grace tu ndiyo maana tuko ndani ya mwaka huu tena, hakika ni kwa neema tu.

2019 tumeuanza kwa amani na furaha kubwa, wengi tukiwa na matumaini makubwa kwa kuset, mipango, malengo, shauku na hamasa ya kwamba mwaka huu basi ni mwaka ambao ni mwaka wa taofauti kabisa.

Kiuhalisia imekaaje, kiuhalisia kabisa kugeuza mwaka ni kama kulala na kuamka siku mpya, au kutoka mwezi mmoja kwenda mwezi mwingine in short ni mwendelezo wa maisha yaleyale tu.

Kwa kweli ndugu yangu tufanye kazi zaidi kuliko kuongea, mipango bila utekelezaji wa majukumu au wa mipango hiyo, kikawaida imekuwa ni mazoea ya kila unapoanza mwaka watu kupanga mipango na malengo, lakini kadri siku zikiwa zinasonga basi watu wanafunika diary zao na kusahau zile hamasa za mwanzo wa mwaka kabisa.

Kuanza mwaka sio kigezo cha wewe kubadilika kitabia na kimtazamo bali, maamzi ya dhati ya kuacha tabia za mazoea ndiyo kitu kinaweza kukufanya kufikia malengo ya kile ulichokifanya.

Pasipo Kuacha kufanya kazi kwa mazoea, kuongea bila kutekeleza unachozungumza tutakuwa tunaanza na kumaliza miaka na miaka tukiwa kwenye tabia zilezile.

Lazima mabadiliko yaanzie kwenye fikra na maamzi ya dhati toka moyoni hapo ndipo unaweza kuona kweli mwaka umebadilika na uko tofauti na mwaka uliopita.

Katika kila jambo unalofanya mshirikishe Mungu, maana Mungu ndiyo  mwamzi na maratibu wa kila jambo tunalofanya, ni signatory wa kila jambo kwenye maisha yetu hakuna sababu ya kuishi bila kumtegemea Mungu.

Kufanya mambo ambayo yanamsikitisha mzazi wako basi jua Mungu anasikitika zaidi na hapo unajichumia laana utakuwa ukifanya mambo lakini hufanikiwi kumbe umeishi maisha yenye kumchukiza muumba wako.

God ni kila kitu fanya kila jambo kwa kumshirikisha Mungu, toa sadaka, fanya ibada, achana na waganga, na kuwategemea viumbe ambao pia kesho na kesho kutwa watakufa, na Biblia inasema amtegemeae mwanadam amelaaniwa achana na kuwategemea viumbe kama wewe.

Jifunze mara kwa mara ili kuujengea ubongo wako maarifa mengi kwa ajili ya matumizi yako binafsi na jamii.

Epuka mogogoro isiyo ya Lazima, hata kama ni ya lazima basi jitahidi kuepukana nayo kwa kila hali.

Samehe kwa kadili uwezavyo, ni afya ya akili nafsi na moyo, ukiombwa msamaha samehe, ukijua kuwa kila mtu anakosea, waweza kukosewa kama binadamu samehe maana hujui kesho yako wewe

Usiwe mtu wa kubeba mambo yasiyokuwa na faidia hata kidogo, kumbuka jambo likitokea limetokea huwezi kulifuta zaidi ya kusamehe tu.

Ushirika na wenzako liwe ni jambo la lazima kwa mwaka huu, baraka zingine za mafaniko zimefungwa kwenye ushirikiano na watu, kupitia ushirika mzuri na watu hapo ndipo unajenga connection na channels zingine ambazo huwezi zipata ukiwa pekee yako kama mkiwa jangwani.

Hekima, Busara  ni jambo jema kwa mwelekeo mzuri wa maisha yetu.

Nikutakie baraka za Bwana kwa mwaka huu, ukawe mwaka wa ushindi na utajiri kwa kila nyanja ya Maisha yako.

Kumbuka mkono mlegevu huleta umasikini bali mkono wenye bidii hutajilisha.
2019 Is the year of achievements
By
Moses zephania Mgema
0755632375