Sunday, January 6, 2019

MAISHA YA YESU DUNIANI NI PAKITI KAMILI YA MAISHA HAPA DUNIANI.

Habari,
Natumaini kila mmoja watu amepata neema nyingine ya upendeleo kuifikia siku ya leo akiwa mzima wa afya.

Nitoe pole kwa yeyote ambae anapitia changamoto yoyote ambayo inamnyima furaha yake ya kila siku.

Niende moja kwa moja kwenye somo la kwanza la mwaka huu tangu kuanza, naamini utakuwa msingi mzuri wa kuunza mwaka huu baada ya mapumziko ya mwisho wa mwaka.

Somo letu kama linaposomeka katika kichwa cha habari, basi tuambane ili kuweza kufahamu nini hasa tunajifunza, lengo na nini matokeo yake baada ya kujifunza.

Yesu au Mesia sio jina geni kwa watu wote, ni mtu ambae alikuwepo duniani kwa hali ya mwili na aliishi kati ya maisha ya kwaida kabisa. Yesu alizaliwa kwa hali ya kawaida na akaishi kwa uhalisia wote wa dunia.

Na ndiyo sababu iliyonifanya kuja na somo hili kama msingi wa kila mtu ambae, ana shauku ya kuona ndoto, malengo, nia na matamanio yake yanatimia siku moja.

Yesu alikuwa na malengo ya yeye kuwepo duniani, na lengo kuu lilikuwa kuleta ukombozi wa maisha ya kiroho lakini hata katika mwili, lakini lengo kuu ilikuwa kukomboa watu waliokuwa wamepotea.
Hiyo ndiyo ilikuwa main purpose ya Yesu kuwepo duniani.
Pamoja na yote hayo, mimi nimejaribu kutafuta na kufikiri zaidi juu ya ujio wa Yesu duniani.

kusudi kuu la yeye kuja duniani linafahamika kwa kila mtu, lakini je ni hilo pekee ? hilo ni swali ambalo kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza zaidi.

Naufahamu uwezo wake, nguvu zake, mamlaka yake, uwezo wa kuona kesho kabla ya siku kufika lakini kwa nini alikubali kuja kufa huku duniani, je hapakuwa na njia nyingine ya ukombozi?.
Jibu hapana Yesu anajia nyingi ambazo zingemfanya kuikomboa dunia bila yeye kupata maumivu na mateso.
Kuna zaidi ya shughuli za kiroho zilizomfanya yesu kuja duniani. Na kama dunia ingemwelewa vizuri au ingeelewa vyema sababu zingine  zilizomlazimu yesu kuja duniani basi huyu pekee ndo angekuwa Role model wa wote.

Yesu ni pakiti kamili (Full package) ameenea kila kona ya maisha ya binadamu, anaemkubali na hata asiemkubali ila kiuhalisia Yesu anagusa kila kona na pembe ya maisha yetu.

Yesu ni mwalimu, na alikuja kufundisha uhalisia wa maisha ya duniani.

NAMNA GANI TUNAJIFUNZA KWAKE.
Lesson 1.
Yesu aliamini katika kufanya kazi kwa  bidii sana na kwa muda mrefu sana huku akiwa na focus na nia ya kufikia kile ambacho amedhamilia kukitimiza kwa siku. Ndiyo maana unaweza kuona kwenye mkusanyiko wa wanaume 500 na wanawake na watoto alilazimika kufanya muujiza watu wapate msosi palepale ili ratiba yake ya siku itimie hata kama ni usiku wa manane.
 
> Hapa tunajifunza kufanya kazi kwa bidii sana lakini kuhakikisha kila ratiba unapopanga mambo ya kufanya kwa siku, wiki, mwezi na hata mwaka lazima uhakikishe unapambana kutimiza ratiba ili kuepuka viporo, bora kuchelewa kurudi nyumbani lakini ukiwa umetimiza majukumu ya ratiba yako.
Lesson 2
Alipata habari ya kuumwa kwa lazaro rafiki yake, lakini tayari alikuwa kwenye ratiba ya mambo mengine aliyokuwa anayatimiza, kwa hiyo alilazimika kumaliza kwanza kazi zilizokuwa ndani ya ratiba yake ndo akaenda alikokuwa ameitwa.
Jiulize swali.
Je ni mara ngapi rafiki yako amekuondoa kwenye ratiba yako ?
    Majibu unayo wewe

>Hapa anatufundisha kuwa usikubali mtu awae yeyote kukuharibia au kuingilia ratiba yako pasipo sababu, hata kama kuna sababu ipime uzito wake kama unaona unaweza kuisolve hata kwa wakati mwingine basi timiza kwanza ratiba uliyonayo ili kuondoa uwezekano wa kuloose focus na concentration.
Ukikubali kila mtu aingilie ratiba yako na wewe umtimizie haja yake, basi wewe ni ngumu sana kufikia malengo kwa wakati ambao ulitazamia kutimiza. Maana mtu asiyekwenda na ratiba huyo ni kama bendera.
Kuna wakati unapokea taarifa ngumu ni vyema kutulia na kuonesha ukomavu, ukifanya hivyo basi utaipa akili kupumua vyema, hata unapoamua kufanya maamzi basi unatakuwa na asilimia kubwa ya kuamua vyema.
Lesson 3
Kutimiza malengo yako kwa wakati sio rahisi usipokuwa, mkomavu na mwenye nia ya dhati.
> pamoja na uwezo alokuwa nao lakini kuna wakati alikiri wazi kwamba yasingekuwa mapenzi ya Mungu basi yeye angeomba kikombe kimwepuke.

Maana yake nini kwenye maisha yetu ya kupambania ndoto zetu, kuna wakati unaona mlima mkubwa, huoni kama utaweza, kila unalofanya ni gumu lakini bado unapaswa kusimama kupambana ili kuvuka hapo

Hakuna mafanikio au kutimiza ndoto kirahisi lazima utoke jasho kweli kweli, no way ya kuepuka jambo hili.

4. Yesu anatufundisha kuvumilia sana kuna wakati mambo hayaendi, changamoto, unajisikia kuchoka, kukata tamaa lakini  bado hata kama hayo yanakuja bado unapaswa kupambana hata mwisho utakapoona umetoboa.

5.katika kila jambo unalofanya, watu watakudhihaki, kukusaliti, majungu, kukusengengenya, utaanguka au kutaitiwa mahali basi utasikia hata marafiki zako wakisema anajifanya eti mpambanaji basi ajitoe hapo alipokwama, wengine utasikia wanasema si alijifanya ana hela kwa sababu yeye ni mjasiriamali mbona siku hizi.....maneno mengi yote hayo yaache yapite ni upepo tu.

Mfano wa maisha ya Yesu
Wakati anachapwa mijeledi alithihakiwa, alitukanwa na kuambiwa kama yeye ni Mwana wa Mungu basi ajiokoe lakini hakutaka kuluzi focus kwa kuwajibu watu.

Lesson 6
Kupenda kile unachokifanya hata kama ni cha muda, maana yake nini hicho unachofanya ndiyo daraja la wewe kuifikia ile ndoto kubwa ya maisha yako.
Yesu alikubali kuja duniani lakini alikuwa anafahamu lengo ni nini. Alijua maisha ya duniani ni ya muda, pamoja na hayo aliithamini sana kazi yake hapa duniani, ndiyo maana leo tunamwita Mfalme wa wafalme.
Lesson 7.
Sio kila unachoombwa basi utoe, kuna wakati unapaswa kuwafundisha watu wanaokuomba namna yakufanya ili kuondoa jamu njiani wakati mwingine.

Yesu akawachia mwanafunzi wake kutoa pepo yeye akiwa hayupo, alitaka wajue na wawe na uwezo wa kujitegemea hata kama yeye hayupo. Hii ina jikita zaidi pale unapokuwa umefanikiwa, wengi hasa ndugu watakuja kukuomba fedha, wafundishe namna fedha inatafutwa.

Lesson 8.
Yesu ni mtoto wa tajiri ambae alikuja kuwafundisha masikini namna njema ya kuishi, hakuna lawama bali ni kufanya kazi bila kujali mazingira gani yanakukabili.

Alikuwa ni Mungu aliye uvaa utu ili kutufanya tujifunze kwa vitendo
Alifundisha pia yafuatayo
Kuwa na nia ya dhati.

General Lesson kwa mwaka huu 2019
Jitahidi sana kuwa wewe.
Fanya kazi zako bila kujali hali.
Focus kwenye malengo yako usipeperushwe na kelele za watu.
Fanya kwa bidii sana kila unapopata nafasi ya kufanya.
Simamia malengo yako.
Simamia ratiba zako.
Toa muda wa kujifunza na kuongeza maarifa ujuzi na taaluma mpya.
Fanya kazi kwa malengo na bidii
Baada ya yote.......
Kwa kila jambo Mungu ni wa kwanza.
Omba soma neno tafakari mtolee mungu kile kidogo anachokupa Mungu

Mwisho.
Yesu alikuja duniani kubadilisha fikra za watu kutoka mtazamo hasi mwenda Mtazamo chanya.
Mageuzi ya fikra yalianzia kwake.
Uaminifu na utii ndo yalikuwa maisha yake, hivyo yakupasa kuwa hivyo pia.
Kuthubutu hata kama huelewi, hata kama upo katika nchi ya ugeni mazingira   ni magumu
Yesu alikuja kukomboa
Roho
Fikra
Na ukombozi ulifanya katika aspects zote za maisha ya binadamu.
Mwaka huu ukawe mwaka wa mageuzi
Ya fikra, mitazamo na tuishi kwa malengo na targets huku tukimtumaini Mungu.

Mungu akubariki sana mwaka huu 2019 hasawewe uliemua kufanya kazi kwa bidii maarifa na ujuzi mwingi
Kwa utukufu wa Mungu utafanikiwa.

Prepared by:
Moses zephania Mgema
0755632375.
Mgemamoses@gmail.com
Dar es salaam Tanzania

No comments:

Post a Comment