Thursday, July 28, 2022

Definition ya unachokiona nje ya mtu yawezekana kisiwe kile ambacho mtu anacho ndani yake..
Hivyo uchakavu wa bodi la nje haimanishi hata kile cha ndani kimechakaa
Hivyo usimjaji mtu kwa mwonekano wake wa nje 
Goodmorning 

Sunday, July 24, 2022

MFUNGWA WA FIKRA


Moja ya sababu kubwa ambayo inalifanya bara la Afrika kuendelea kuwa kwenye kiwango kikubwa cha umasikini ni ufungwa wa fikra kwa viongozi wengi hali ambayo imekuwa ni donda ndugu kwa vizazi na vizazi.
Miaka zaidi ya hamsini Tangu Afrika ilipoanza kupata uhuru wa bendera hata sasa bado nchi nyingi zipo kwenye gereza la fikra, kuanzia watawala mpaka watawaliwa. Tumeshindwa kujitegemea kwa asilimia walau 75 hivi kila kitu tunategemea watu kutoka Amerika ya kaskazini, Ulaya na hata baadhi ya nchi za Asia kufanya maamzi ya namna ya kuendesha nchi zetu...
Miaka zaidi ya hamsini ya uhuru wa bendera kwa Mwafrika, hana uwezo wa kufanya maamzi yanayojitegemea, miaka zaidi ya hamsini nchi nyingi hazina hata kiwanda kimoja cha dawa muhimu za binadamu, pamoja na wingi wa madini ya aina mbalimbali katika ardhi ya Afrika lakini bado tunaagiza kuanzia vyeni mpaka magari kwenye mabara ambayo malighafi wanachukulia Afrika.

Hali hiyo imefanya hata mifumo ya uendeshaji wa mambo mengi muhimu kuwa katika hali ya utegemezi, elimu yetu ikiwa kwenye muundo ambao unamfanya mtu anapohitimu tageti ya kwanza ni kuajiriwa sio kuwa na fikra zenye lengo la kuongeza fursa za ajira, elimu yetu haitupi mwanga wakuliona bara letu kama fursa inayojitgemea na kila mmoja anaweza kuitumia na kumpatia uwanda mpana wa kulivua vazi la umasikini linalotesa familia nyingi hapa kwetu Afrika.

Ufungwa wa fikra ni mbaya kuliko ufungwa wa kuwa gerezani, akili inaposhindwa kufanya kazi sawasawa hulazimika kuwa tegemezi, maana akili tegemezi huwa haina uwezo wa kuziona fursa na hata ikiziona fursa huwa inalazimika kuhitaji msaada wa ziada ili kuweza kuzitumia.
Hili ndiyo koti ambalo limeshindwa kutuachia kwa muda mrefu kuanzia vizazi vya uhuru mpaka kizazi cha connection (dot.com generation) ambapo bado hatuamini katika kujitegemea na kusimama wenyewe...

Kila nikiwatazama vijana wenzangu tukiwa katika vijiwe mbalimbali, namna tunavyoishi kwa matumaini na matarajio ya kupokea muujiza Fulani, nashindwa kuwalaumu kwa sababu nikirudi nyuma kuanzia kwenye familia zetu, wazazi nao wanaishi kwa matumaini, kutwa wakipiga simu wakiulizia nafasi za kazi kwenye mashirika na serikalini, nina kijana wangu amemaliza chuo na amefaulu vyema sana hakuna nafasi hapo kwenu hata umshike mkono....
Nikikaa chini tena nahisi kuwalaumu wazazi kwa nini umemsomesha mtoto, amekuwa na elimu ya juu kuliko hata wewe bado unahangaika kumtafutia connection kwa nini usimwache ajitegemee, ndipo nakumbuka elimu ya kujitegemea ilikwenda na Julius Kambarage Nyerere katika kaburi lake pale Buatima, ahaa sasa tuna elimu ya faulu vizuri upate kazi nzuri, faulu vizuri maana mjomba wako yupo kwenye idara Fulani atakuvusha na wewe utakuwa na kazi nzuri...

Kijana tangu akiwa shule ya msingi anawaza kuajiriwa, anawaza kuna mjomba yupo kwenye nafasi Fulani atanisaidia kupata kazi, sio ajabu kusikia vijana vijiweni wakitambiana kuwa na ndugu kwenye nafasi za uongozi serikalini kwamba nikimaliza tu Anko, kaka, dada, shangazi, Baba mdogo watanivusha hata kama ufaulu ni mbovu as long as yupo ndugu nitakwenda...

Fikra tegemezi, ufungwa wa fikra, uliofungwa kwenye muujiza, ndiyo maana leo matapeli wa gospel wametapakaa nchi nzima kwa sababu asilimia kubwa tunaishi kwa kutaka kuwa watu fulani lakini uwezo wa kufikiri ukiwa mdogo tunawaza muujiza, bahati na sibu lakini na uchawa mwingi kwa wachache ambao wameamua kwa moyo wa dhati kujikomboa na kuishi ndoto zao...

Pingine tumeishi huko kwa muda mrefu sana, sio kwa sababu ya kizazi chetu bali ni mfumo na muundo ambao tumeukuta tangu zama zile. Mfumo wa zamani uliruhusu watu kuwa tegemezi kwa sababu ya kuwa na watu wachache waliokwenda shule, serikali na taasisi nyingi kuwahitaji watu kuliko leo tunavyohitajiwa na makampuni, maana tumekuwa wengi kuliko nafasi zenyewe....
Ni namna gani tunaweza kujikomboa kutoka kwenye hali ya kipato duni na kwend kwenye kiwango cha juu...

Kwanza kabisa nikuacha kuishi kwa kutegemea kuwa kuna siku nitakuja kupata ajira bali ishi kwa kusema ni namna gani nitayaishi maono yangu, iwe kwa ajira au kukosa ajira lazima niishi ndoto zangu. Ifungue akili na ufahamu wako, na kuanza kutazama na kufikiri upya, utaziona fursa nyingi ambazo tunazo katika taifa letu na bara zima la Afrika..

Ndoto za mwafrika zitatimizwa na mwafrika mwenyewe na ndoto zangu, ndoto zako zitatimilika kwa kuamua binafsi na si vinginevyo, maisha yetu leo ni maisha ambayo hayamhitaji mtu mwingine zaidi ya kujihitaji wewe mwenyewe kuamua kwa moyo wa dhati kwamba mimi ndiyo mwenye mamlaka yakujitoa hapa nilipo na kuwa mahali nataka kuwa..
Kila nikijitazama najiona mtu mkubwa lakini ili niwezd kufika mahali hapo juu, ni vyema kubadili mtazamo na fikra zangu juu ya uendeshaji wa maisha yangu, vivyo hivyo kijana mwenzangu unayo nafasi yakubadili hatima yako kwa nguvu na kwa maarifa yako...

Ufungwa wa fikra ni mbaya kuliko kawaida, aina hii ya kifungo huwa imewekeza zaidi katika kulaumu, kutaka kuwa chawa, kutegemea miujiza, kutegemea watu fulani nk. Hali hii hujenga majeraha na huzuni moyoni ambayo matokeo yake huondoa ufanisi katika utendaji wa kazi...

Vijana tunahitaji kubadilika sana, tunahitaji kuondoa matajirajio kwa watu bali tunapaswa kuwafanya watu waone (value)Thamani kwa kuja na mawazo mbadala katika kuhakikisha kuwa tunaondoka kwenye ufungwa wa fikra na kuwa watu huru. Mtu akishakuwa huru kifikra ni rahisi zaidi kuwa huru katika kufanya maamzi, kuwa huru katika kuchakata mawazo chanya yenye kuleta matokeo chanya. 

Vijana wenzangu, wazazi na kaka zetu ni vyema kuwa mabalozi wema kwa watoto wetu walau kuanza kuwaonyesha kuwa, uhuru wa fikra hutengeneza hali ya kujiamini, hali ujasiri sio unyonge tena, hii huwa ni nguvu ambayo inamfanya mtu kujitegemea kwa sababu ndani yake ipo nguvu ya kujisimamia na kutimiza malengo yake kwa ukubwa na upana....
Mtu akiwa huru kifikra ni rahisi zaidi kujisimamia, 
Moses_mgema 
0755632375

Sunday, July 17, 2022

Mashujaa wengi wamevuja damu, jasho na maumivu makali, jua na baridi vilikuwa juu yao, miiba mikali ilichoma miguu yao, lengo ni kuupata utukufu wa mwisho.
Ndoto ni rahisi sana kuitamka, kuota ni rahisi sana na kusema ni rahisi sana pia lakini ukweli ni kwamba ndoto inahitaji vitu vingi sana ili kuweza kuikamilisha na kuwa kweli. Mtu akikusimulia waweza kuona ni rahisi sana lakini ukweli ni kwamba unahitaji mambo mengi sana binafsi ili kuweza kuifanya ndoto yako kuwa halisi....
Vijana wengi tuna tamani sana kumiliki, tunatamani sana kuwa watu wakubwa lakini, njia za kuelekea kumiliki hatutaki kuzipitia, katu kamwe tutabaki katika msongo wa mawazo na shauku ya kumili pasina kumiliki hizo ndoto...

Vijana wengi, tunapenda kuwa na magari mazuri, tunapenda kuwa nanyumba nzuri, familia nzuri lakini hatutaki kuitii michakato ambayo itatufanya kuwa wakubwa na wenye kumiliki mali na fedha tunazozitaka.....

Kumiliki hakuja kirahisi, kumiliki hakuji kama usiku na mchana, kumiliki kunahitaji sana kujitoa, kufanya kazi kwa jasho na damu, kuwa na nidhamu, kutumia muda na kuweza kusimamia kile unachokiamini, kuondoa aibu, kuondoa vijisababu vidogo vidogo, kuamini katika kile unachokiona na kukifuatilia kwa bidii na maarifa mengi...
Vijana wengi tunapenda kulala, vijana wengi tunapenda starehe, vijana wengi tunapenda fahari mbele za watu kuliko uhalisia wa maisha yenyewe, mwisho wa siku tunajikuta tunatengeneza lawama kwa watu wengine ambao tunahisi ndiyo chanzo cha maisha yetu kuharibika....
 Kama una ndoto kubwa ndugu na rafiki yangu ni vyema kuhakikisha kuwa unakuwa askari wa maisha yako mwenyewe, ndoto inafukuziwa na wewe/mimi.
Rafiki yangu muda bado tunao ni vyema kuhakikisha tunakwenda kwenye haki na njia 


Saturday, July 16, 2022

UMESHIKIRIA FUNGUO YA NDOTO ZAKO

Safari ya maisha huwa ni Safari ya mtu mmoja tu ukipata wa pili na watatu wakasapoti idea na kile unachokiona katika mchoro wako basi fahamu hao ni dhahabu na rubi ambayo hupaswi kuzipoteza kirahisi katika Safari yako ya kuzikimbiza ndoto zako.

Asilimia kubwa ya watu huwa hawaamini katika michoro ya awali ndiyo maana sio rahisi sana watu kukupongeza unapoianza Safari ya kuhakikisha unazifikia ndoto zako, wengi ukiwashirikisha watakukatisha tamaa, au kukupa wazo mbadala wakijaribu kukuonyesha udhaifu wa hoja yako mbele yao.

Hawa wanaweza kuwa ni watu wako wa karibu zaidi ya unavyozani, anaweza kuwa mzazi, rafiki, mke na hata kiongozi wako wa Imani, kati ya hao watakuambia unawaza vitu visivyowezekanika,unawaza vitu ambavyo ukiwa na njaa ndiyo vinakupelekea huko, ni vyema upatiwe chakula ule ushibe ili kuondoa stress yanayosababishwa na njaa, hivyo ukila na kushiba utakuwa sawa na kuwaza vyema.

Cha ajabu zaidi yule yule anaekukatisha tamaa unaweza kumkuta akimpongeza mtu mwingine ambae walau picha ya wazo lake imeanza kutengeneza mwonekano unaopaswa kuwa, na atamwona shujaa kisa ameona uhalisia na ndiyo maana imekuwa ni rahisi sana mtoto wa kitanzania ndoto yake kufa kuliko mtoto wa kizungu au watoto wa Afrika Magharibi na nchi za Amerika ya kusini.....

Ni rahisi zaidi kumkuta mtu akimwelezea vyema sana Dangote kutoka nchini Nigeria na kumpongeza tajiri huyu kwamba alianzia katika kazi ndogo za kuuza vitu vidogo mtaani kwake huku akimwona shujaa, mtu huyu akimsimulia vyema sana Mzee Bakhresa kwamba alianza kuuza bidhaa ndogo ndogo pale kariakoo jijini Dar es salaam mpaka alipofikia leo na moyo wake ukapata furaha na utulivu sana...

Kwa sababu wanakujua kwa sababu umekuwa wakikuona kwa sababu wanamjua Baba yako na familia yako wanaamini kwenu halijawahi kutoka wazo bora, ndiyo maana hawaoni kwamba unaweza kuifanya ndoto kubwa iliyoko mbele yako.

Asilimia kubwa ya watu wanao kukatisha tamaa wana lengo la kuendelea kukutumia, wamepima hiyo picha na kuona matokeo makubwa kama utaifikia hivyo ni rahisi sana kukuambia jambo hilo ni gumu, linahitaji fedha nyingi, muda mwingi hivyo watakupa wazo mbadala, wazo rahisi (cheap idea) kwa sababu wanajua kwenye wazo dogo hakuna thamani ile ambayo unataka kutengeneza hapo kesho...

Wanafanya hivyo kwa sababu pia wanajua uwezo wako, na wanatamani kuendelea kukutumia na kukupa either ujira mdogo huku wakitumia taaluma yako kwa manufaa yao binafsi, au wao ni furaha yao kukuona unaendelea kuwalamba miguu na Kuwaita boss hiyo ndiyo furaha yao, hawataki ufukie levo zao, wanatamani kukuona mnyonge...

Wengine ufahamu wao ni mdogo, unachokiona sicho wanachokiona wao, wakati wewe unaona mpenyo wao wanaona lile jiwe kubwa ambalo haliwezi kuvunjwa vunjwa na kutoa mpenyo wa kufika ng'ambo ya pili ya mlima. Always ndoto kubwa huwa hazina njia rahisi kuzifikia (has no cheap strategies to be reached).

Angalia sana watu unaofanya nao kazi, watu unaowashirikisha idea zako, aina ya watu wanaokuzunguka, nikuambie kitu kimoja hivi, kuna wengine ni very good friends for you kwa sababu bado wanakutawala na hujawashirikisha wazo lenye afya na misuli ya kukutoa hapo ulipo, wanakupenda na kukushauri,ukipata hela fanya hivi, au watakuuliza una wazo gani au njoo na wazo zuri tutakupiga tafu ili na wewe ujitegemee kiuchumi, au kwa nini usifanye biashara hii, huo ni muda ambao wewe bado huoni kama inawezekana, ukiamua kufanya watakaa nyuma na kukuonyesha ni kwa kiwango gani wazo hilo ni gumu, au kutokukupa ahadi ambayo waliitoa kabla hujalielewa wazo lako au wakati unajitafuta....

Rafiki yangu kipenzi akanishirikisha kusoma kitabu kimoja cha kijana Mzimbabwe ambae alikuwa akifanya kazi sehemu Fulani, na kila jioni alikutana na marafiki zake kwenye eneo Fulani la starehe wakinywa soda na vinywaji vikali huku wakifurahia maisha. Baada ya muda aliona mikusanyiko hiyo haikuwa na faida sana kwenye ustawi wa maisha yao, hivyo aliona fursa kwenye mkusanyiko huo na ungeweza kuwafanya kuishi maisha mengine tofauti kabisa kuliko kuwa na mkusanyiko wa kila siku kwa ajili ya kutumia hata kile kidogo walichokuwa wanapata na kukinywea vinywaji huku wakifurahia urafiki wao...

Alikuja na wazo jema kwa ajili ya manufaa yao wote, lakini kati ya kundi la watu wanaoweza kufika sita hadi nane ni mmoja tu ndiyo alioona ile idea kuwa ni njema na kumsapoti vyema mpaka mwisho ingawa hata yeye hakuwa amelivaa wazo hilo kama ambavyo mwenye wazo alikuwa akiliona na mkusanyiko wao ulifika mwisho kwa sababu namna ya kufikiri kulitofautiana...

Ndivyo ilivyo hata leo kuwa wapo watu watakupa offers, watakupa muda wao wa ziada kwa ajili ya starehe lakini ukitaka kujikwamua kwa kushare nao wazo zuri ambalo litakufanya na wewe kuwa na nguvu ya kifedha vizuizi vitakuwa vingi sana mbele yako kwa sababu either hawako pamoja na wewe katika uhalisia au wanafurahia wanavyokuona na utafikiri wanakuwazia mema kumbe wanakusema hata unapokuwa haupo mbele ya macho yao.....
My take: Ile picha unayoiona kwanza wewe ndiyo hali halisi ya kitu ambacho kiweza kutokea kama utafanya kwa vitendo na kuzuia kelele za watu wenye nia isiyo njema wanaokuja mbele yako na chambo mbele ya ndoano, usiwape nafasi wazo lako ni bora kuliko Lao, bora wakakaa kimya kuliko kukutengenezea wazo jipya ambalo kiuhalisia sio wazo lako  kama hawawezi kuliboresha ni vyema wakanyamaza, kama hawawezi kusiaidia ni vyema wakakaa kimya....

Muda uliotumia kuwaza, muda uliotumia kuomba, muda uliotumia kufanya utafiti ni vyema ukauheshimu na kuutendea haki vyema, rafiki wa kweli ni yule ambae unaweza kuona kile unachokiona, hata kama hawezi kuona vyema ila anaweza kusimama na wewe hata kwa kuafuata njia unayopita, hata kwa kukuombea tu....

Yesu alikuwa na watu wengi nyuma yake  marafiki zake na wengine hata tembea yake waliiga nankufanana nao, wengine sema yao ikawa kama yake lakini, msalaba na kifo kilikuwa chake, Jesus was chasing his purpose ndiyo maana hata kwenye ugumu na kuachwa na watu, wafuasi wake lakini alikwenda hakubadili msimamo wake bali aliamua kutimiza Safari yake....

Duniani hakuna wazo gumu, duniani hakuna project ngumu, ugumu wa kwanza utaanzia kwako mwenyewe, msimamo wako, watu wanaokuzunguka, watu unaoshare wazo lako, ndiyo inaweza kukupa kile unataka au kutokufikia kabisa 

My take two: Simaanishi ukatae ushauri, simaanishi usiwe challenged kwenye idea zako, wengine wapo kukamilisha kwa maana ya kukuboresha wewe, kwa hiyo wanapokupa wazo mbadala wanataka kufahamu hoja yako umeichukua kwa uelewa na upana kwa kiwango gani, je una maanisha, wengine hawatasema is wanakuunga mkono.

Usiache kwenda kwenye nyama choma kwa sababu unawazo lako, usiache kushirikisha watu idea zako kisa unaogopa kuwa opposed no, bali chagua watu sahihi kuwashirikisha, chagua muda sahihi kuwashirikisha pia, what I came to realise is that sio kila mtu anaesema ndiyo kwako ndiyo mtu sahihi au anasapoti idea yako, hivyo chagua 
1. Watu sahihi tena wachache kuwashirikisha mambo yako, wengine cheka nao lakini usiruhusu wakujue sana....
2. Sio kila kampani ni sahihi nyingine ni kuptezeana muda tu...
Mwisho kabisa kamapani bora ni wewe mwenyewe na Mungu wako, maana ndiyo anajua kusudi lako, pili ni wewe mwenyewe, tatu mkeo ndiyo maana tunashauriwa kuwa na right partners kwenye maisha ambae atakielewa kile unachokiona kwenye ile picha kabla ya kuja kwenye uhalisia ⏰ 

Tambua muda sahihi wa kuwashirikisha watu wako muhimu hata kama ni watu sahihi kwako.

Tambua sio kila rafiki utamshirikisha wazo lako, warmup marafiki zako, wapo kwa ajili ya mambo ya kiroho, wengine kwa ajili ya mitoko na nyama choma, wengine kwa ajili ya mambo yako ya msingi zaidi nje ya mambo ya kiroho.

Hivyo kila mtu atakufaa kwa nafasi yake na atafanya vyema sana.

Let us enjoy and share this message 
Niachie kommenti na ushauri wako mzuri..

Mgema Moses Zephania 
mgemamoses@gmail.com 
0755632375


Friday, July 15, 2022

MY TEN COMMANDMENTS OF LIFE

Nataka kuishi maisha ambayo nitakuwa na ujasiri wa kuyasimulia kwa watoto wangu. Maisha ambayo hata kama wakitaka waishi kama Mimi sitakuwa na haja ya kutoa maelezo.

Ndiyo naweza kukosea wakati mwingine lakini  yawe ni makosa ambayo yana mlengo wa kuleta matokeo chanya ya juhudi zangu katika kutafuta ufanisi na ubora katika kuzifikia ndoto zangu kuliko kufanya ufuska usio kuwa na tija wala faida kwangu na vizazi vijavyo..

Lengo langu pia nikutamani waone namna ninavyo fanya bidii katika kusahihisha makosa ya nyuma ili wasije kudhani makosa kama yangu ndio njia sahihi ya kufikia kusudi na Mpango wa Mungu kwenye maisha yangu na yao pia.

KWA HIYO: NIKIWA NIKO HAI NA MWENYE AKILI ZANGU TIMAMU, NIMEAMUA KWAMBA HIZI NDIYO KANUNI ZANGU ZA MAISHA MPAKA KIFO....(room of amendment for the future)

Nimeamua kwamba;
1. Nitakuwa mwadilifu
2. Nitakuwa mkweli
3. Nitakuwa mchapa kazi.
4. Nitamcha Mungu.
5. Nitawaheshimu watu wengine na kuwasema vizuri.
6. Nitajihidi kwa gharama yoyote kuwa mnyenyekevu.
7. Nitahusiana kimapenzi na mwanamke mmoja nitakae mwoa kwa ndoa ya madhabahuni.
8. Nitakuwa mwaminifu kwa Mungu, mke wangu, wazazi wangu, familia yangu, kanisa na watu wengine.
9. Nitajitoa kwa ajili ya wengine na kwa taifa langu.
10. Nitaamka asubuhi na mapema kuianza siku yangu kwa kuzingatia muda kwa kila jambo langu.

This is my commitment and I will read them every morning...

NB:  Haya mambo ni binafsi yalipaswa kuwa kwenye notebook yangu ya ndani. Nimeshare na wewe ili yanikumbushe wajibu wangu lengo ikiwa na pace katika kufikia malengo na ndoto zangu. Kwa sababu nimeona itanisaidia kuhakikisha nayaishi.

God is Good all the time 
Mgemamoses@gmail.com 

Tuesday, July 12, 2022

IT'S YOUR OWN JOURNEY

Unapowaza kuwa mtu mkubwa, unapowaza kuifanya ile ndoto yako kuwa katika uhalisia, unapowaza kuwa lazima niwe na maisha mazuri, kuna maamzi unapaswa kuyafanya, kuna namna unapaswa kufanya ili kuwa yule Moses unayemtaka.
Kumbuka yule unayejitaka kuwa, haiwezi kuwa katika uhalisia kwa kutegemea msaada wa mtu, mtu Fulani kukupa chance, yupo kukutengenezea maisha hapana, utafurahia nao lakini mwisho wa siku kuna wakati wa kubaki wewe pekee yako.

Maisha yako yanakuhitaji wewe kuyafanyia maamzi, yanakuhitaji wewe kuyabadilisha na kuwa unavyotaka, sio Baba  sio mama wala sio hisani ya marafiki zako au marafiki wa Baba yako, ila ni wewe mwenyewe  ndiyo mwenye misuli yakuifanya ndoto yako kuwa katika uhalisia mkubwa na mpana.

Dunia ya leo iko wazi kwa kila mtu, dunia ya leo ni fursa sawa kwa kila mtu, hivyo ni uchaguzi wa kuwa wewe unavyotaka, ni uchaguzi wa kuchagua ni aina gani ya maisha unayataka sio watu wanataka nini kwenye maisha yako...

Ukitegemea kama kuna mtu atakuja kuwa sababu ya wewe kuishi ndoto yako sahau  hata kama huyo mtu atakuja kuwa daraja la maisha unayoyataka basi fahamu kuwa kuna kitu kimemfanya kuja ili kutengeneza WIN WIN situation, hakuna One side win, hivyo ni vyema kutambua nafasi yako wewe kama wewe...

Njia ya mafanikio ni pana sana ila pia ni nyembamba sana, ukiwa na fukra pana mlango wa kuyaendea mafanikio ni mpana sana bali ukiwa na chumba kidogo cha kuwaza na kufukiri basi mlango wa mafanikio ni mdogo kuliko lile tundu la sindano.

Ishi ndoto, ishi unavyotaka kwa kufanya maazi hata kama ni makali na yenye kuuma kiasi gani  just make it for your own benefit what I can say hata kama utakuwa na rafiki mzuri namna gani, ndugu wakati mwingine hata Baba yako, gawezi kukupa njia zote za mafanikil kwa sababu sio rahisi kufanya hivyo...

Kila mtu anapenda kuheshimiwa, kutawala na kuwaongoza wengine ndiyo maana ni ngumu sana kuigeuza nafsi iliyojaaa utajiri ikakupa mbinu bora ya kufanikiwa kwa uwazi na mapana kabisa bali mara nyingi watakupa samaki aliyevuliwa muda mrefu....

Fight your dream alone, let others come and witness the results 
Mgema Moses 
0719110760/0755632375
mgemamoses@gmail.com 
www.mosesmgema.blogspot.com
Instagram moses_mgema
amaris

Sunday, July 10, 2022

THE VALUE OF DREAM/THAMANI YA NDOTO YAKO

Safari ya maisha, ni safari ya kipekee sana katika ya Safari nyingi ambazo mwanadamu anazifanya akiwa kwenye sayari ya tatu. Safari hii ni Safari pekee ambayo mhusika huianza kwa kilio na wanaompokea duniani hufurahia na kutabasamu kumpokea mgeni duniani, mama hufurahi, Baba hufurahi, Bibi na Babu hufurahi na hata ndugu, jamaa, marafiki hufurahia ujio wa mwanadamu mpya duniani.

Mtoto anapozaliwa huwa amefanya mawasiliano na muumba wake kwa kina, hivyo inapofika miezi tisa tumboni hupaswa kutoka ili kuja kuanza kuyaishi maelekezo na mapenzi ya Mungu hapa duniani. Mapenzi ya Mungu ni ule uwekezaji ambao Mungu ameuwekeza kwa mwanadamu, yale maono, kusudi na ile ndoto kubwa inayokunyima usingizi hiyo ndiyo mipango ambayo Mungu huiweka kwenye maisha ya kila mtu hapa duniani.

Ndoto ya mtu ni fumbo kubwa, maisha ya mtu ni Safari yenye kubeba tumaini na shauku ya kufanikiwa kufikia ile hatima ya Mungu kupitia mwanadamu. Ndiyo maana Safari hii huwa na vikwazo vingi, mabonde mengi, giza katikati ya mapori mengi yenye wadudu, wanyama wakali na hata jua lenye kuchoma utosi na kukatisha tamaa....
Hakuna Safari rahisi ya kuishi kile ambacho Mungu amekiweka ndani ya mtu, ila hakuna ugumu ulio ndani ya kusudi la Mungu ambao hauna mpenyo, wala njia ya kufikia ile hatima kubwa ya uwekezaji wa Mungu kwa Mwanadamu......

Haijalishi milima itakuwa na miinuko mikali kiasi gani, haijalishi jua litachoma kwa kiwango gani, haijalishi vizuizi vitakuwa vingi kwa kiasi gani as long as ni Purpose ya Mungu ndiyo inafanya kazi ndani yako, mlango wa kutokea na kufikia hatima lazima utaonekana tu hata kama bado giza ni nene na lenye kutisha sana...........

Hatima yenye matokeo makubwa haiwezi kupita kwenye kiwango kidogo cha vipimo, ndoto kubwa haiwezi kuwa na formula rahisi ya kufikia jawabu tarajiwa, hatima kubwa haiwezi kubebwa na akili yenye uwezo mdogo wa kuhimili mikimiki ya upanuzi wa barabara ya kupitishia matokeo makubwa ya kesho....

Mtu rahisi huwa haaminiki, mtu rahisi ni hubebwa na upepo wa kila namna, mtu rahisi hana misuli ya kusimama na kuitetea ile hatima anayoiona kesho, bali mwenye misuli, mwenye upeo , mwenye kuona kesho zaidi kuliko leo huyo ndiyo hubeba hatima kubwa maishani na huyo ndiyo huaminiwa na Mungu kwa makubwa 

Yesu kristo alikuwa na misuli, Musa na Joshua walikuwa na Misuli ndiyo maana walikabidhiwa majukumu makubwa kwa ajili ya kuwa njia kwa wengine, Yusuph ni miongoni mwao pia, Esther ni miongoni mwao na wengine wengi ambao walikuwa sababu ya hatima zao na hatima za wengine  kuwa kweli....Mungu amekuamini pia na wewe.

Asilimia kubwa ya sisi vijana leo, hatuamini kile ambacho Mungu ameweka ndani yetu, ugumu wa maisha umetuhamisha kutoka kwenye kufikiri na kuwekeza nguvu nyingi kwenye kuwaza. Kikawaida mtu anapokuwa ana waza hupunguza uwezo wa kufikiri sawasawa na matokeo yake huchukua maamzi yasiyofaa 

Miaka michache nyuma nilipitia changamoto kubwa sana ya ugumu wa maisha, sikuona njia ya kutoka mahali nilipokuwa, niliona giza na tope jingi mbele yangu, nilihitaji kutatua changamoto ngumu mbele yangu, lakini kila mlango ulionekana kufungwa, kila njia ilionekana kuwa na miba, hata nilipojaza baiskeli yangu upepo, mbigiri zilitoboa tairi yangu na upepo kuisha...

Niliwaza sana ni namna gani Baba yangu atatibiwa niliwaza ni namna gani familia yetu itakula, niliwaza sana hatima ya mdogo wangu Miriam na niliwaza sana kwa ajili ya ndoto zangu je kuna siku zitakuwa kweli, kila nilichokipata kilikuwa kinatosha kutatua changamoto tu na changamoto zenyewe nisingeweza kuzimaliza kwa sababu kipato changu kilikuwa chini sana......

Nilitamani walau nipate hela ya kubet, lakini pamoja na kubeti wala sikuweza kupata hela, kila nilichokifanya hakuna majawabu sahihi ambayo yatengenezwa kunitoa kwenye ile hali ya uhitaji. Changamoto hiyo ilinikondesha sana iliufanya mwili wangu kudhoofika sana na kupata hali ya weusi, akili yangu ilisinyaa badala ya kustawi, mwili wangu ulipungua kilo kutoka kilo sabini hadi kilo sitini, ilikuwa ni changamoto kubwa sana...

Siku moja nilikutana na mtu mmoja akaniambia Musa mdogo wangu utakufa, Musa mdogo wangu utafanikiwa ila kwa taabu sana, Musa mdogo utafanikiwa ila unaweza usinufaike na utajiri au mafanikio yako, kwa sababu kwa wakati utakapokuwa umeyapata either unaweza kuwa na maradhi ambayo yatakufanya kuishi kwa madawa au kupunguziwa vyakula vya kula kutokana na changamoto ya afya....

Mdogo wangu, ugumu wa maisha ni kipimo cha akili, ugumu wa maisha ni fursa ya mwenye akili, ila mwenye akili huwa pia haanzishi fursa kwa lengo la kutatua Changamoto iliyoko mbele yake, bali huivumilia hiyo changamoto akitafuta suluhisho la kudumu. Akaniambia ipe akili nafasi ipumue ili kesho uweze kufikiri vyema na sio kuwaza... ...

Akaniambia watu wengi wanawaza kuliko kufikiri, kama unataka kujua kama kweli huwa unawaza ni jawabu gani hata dogo ambalo limekupa hatua hata moja ya kupumua au kukupa way forward ya unachokiwaza kila siku na kupata majibu, ukweli hapana.

Hali hii inawapata vijana wengi sana, wamewekeza nguvu kubwa katika kuwaza tatizo kuliko kuwekeza nguvu ya kufikiri namna ya kuondoka kwenye eneo hilo zito. Akili ya mtu ni zaidi ya kompyuta, akili ya mtu ni kiwanda, karakakana ambayo mtu akiitumia vyema itampa matokeo super ya kazi.....

Nimewekeza kwenye maarifa kwa miaka mitatu, na nilijitahidi sana kukataa kuishi maisha ya watu, maoni na mitamo ya watu, duniani kila mtu ana wazo zuri lakini ukweli ni kwamba sio kila wazo ni jema kwa matumizi yako bali mengi unapaswa kuyaandika na kuyaweka kama kumbukumbu kwa matumizi ya kesho.....

Leo naandika andiko hili kwa sababu, baada ya utulivu wa miaka almost mitano leo nainuka na kukung'uta mavumbi na safari yangu ya maisha inaanza rasmi kwa mwendo usio na kipimo cha kawaida. Nafanya hivi kwa sababu kila mtu alinidefine kwa namna alivyotaka, alinisema alivyotaka lakini, Mungu alinipa kuwa tahira ili kupisha kila aina ya upepo mzuri na mbaya.....

Rafiki yangu maisha ni fursa tosha, maisha ni upendeleo wa Mungu, fahamu kuwa watu wote brave kwa kutazamwa ndiyo waliofeli kwa asilimia kubwa bali watazamwao kwa jicho la kutokupewa thamani hao ndiyo wametengeneza thamani ya maisha yao. Nyakati ngumu kweli hazidumu bali watu imara hudumu....

Chagua kufikiri kuliko kuwaza kwa sababu penye kufikiri kuna jawabu sahihi zaidi bali kwenye kuwaza kuna kiwango kikubwa cha kupunguza uwezo wa kufikiri na kuja na majawabu sahihi.

Mungu amekuamini, Mungu ameniamini ndiyo maana amekupa fursa njema ambayo ni dhahabu, ni wewe tu kuona unafanya nini kwa kutumia utashi na akili yako aliyokupa Mungu, 

Opportunities are equally given but it depends on how you see them and utilise effectively for the purpose of gain what are supposed to be gained....
Enjoy your week...
Mgema Moses Zephania 
0719110760
Ni ngumu sana kuamini maneno ya kale, kwamba penye miti hapana wajenzi, ni ngumu sana kumwamini mtu tajiri anapo yakiri maisha yake ya ufukara miaka ya nyuma kabla yakuwa namna alivyo leo.
Ukimsikiliza Barack Obama, Oprah Wilfred, Mzee Yusuph Bakhresa, Eric Shigongo, mwanzo wa Joseph kusaga, kaka Yangu Francis Sizya (Majizo) Mmiliki wa Radio 📻 ya E-Fm na wengine wengi, wanasema maisha magumu wanayajua na waliyaishi kwa vitendo kutoka kwenye familia zao...

Majizo anasema kuwa katika kila hatua aliyopita kwenye maisha yake, katika ukoo wake yeye ndiye amekuwa wa kwanza kwa kila hatua ya mafanikio, alikuwa wa kwanza kununua gari na vitu vingine vya Thamani kutoka kwenye familia masikini isiyojiweza kufanya jambo lolote lile la maendeleo...

Historia ya Shigongo Eric, niliisikia kupitia kinywa chake akisimulia lakini kupitia maandiko ya vitabu vyake ambavyo vimeelezea historia ya maisha yake ya ufukara. Kama haitoshi nilikuwa sehemu ya familia yake ya Global publishers ambayo imebeba baadhi ya watu wakubwa kiumri ambao walishuhudia ukuaji wa Eric pale Jijini Mwanza, wanasema ametokea familia duni sana yenye kunuka umasikini, kikwetu ukiitwa madaso basi fahamu uko kwenye level mbaya sana ya umasikini....

Asilimia kubwa ya sisi vijana wa kitanzania, tunaamini katika watu fulani kutubeba, tunaamini tulivyo ni kwa sababu ya historia mbovu ya familia zetu, tunaamini kuwa ndoto zetu ziko gizani kwa sababu  ya watu fulani, au serikali na wazazi wetu. 

Tunaamini kuwa kufikia utajiri na fahari ya dunia sio rahisi, ila tunaamini kwenye bahati kuwa ndiyo inaweza kuwa njia nzuri ya kufikia malengo na ndoto zetu. 

PENYE MITI WAJENZI WAPO

Ni ngumu sana kuamini maneno ya kale, kwamba penye miti hapana wajenzi, ni ngumu sana kumwamini mtu tajiri anapo yakiri maisha yake ya ufukara miaka ya nyuma kabla yakuwa namna alivyo leo.
Ukimsikiliza Barack Obama, Oprah Wilfred, Mzee Yusuph Bakhresa, Eric Shigongo, mwanzo wa Joseph kusaga, kaka Yangu Francis Sizya (Majizo) Mmiliki wa Radio 📻 ya E-Fm na wengine wengi, wanasema maisha magumu wanayajua na waliyaishi kwa vitendo kutoka kwenye familia zao...

Majizo anasema kuwa katika kila hatua aliyopita kwenye maisha yake, katika ukoo wake yeye ndiye amekuwa wa kwanza kwa kila hatua ya mafanikio, alikuwa wa kwanza kununua gari na vitu vingine vya Thamani kutoka kwenye familia masikini isiyojiweza kufanya jambo lolote lile la maendeleo...

Historia ya Shigongo Eric, niliisikia kupitia kinywa chake akisimulia lakini kupitia maandiko ya vitabu vyake ambavyo vimeelezea historia ya maisha yake ya ufukara. Kama haitoshi nilikuwa sehemu ya familia yake ya Global publishers ambayo imebeba baadhi ya watu wakubwa kiumri ambao walishuhudia ukuaji wa Eric pale Jijini Mwanza, wanasema ametokea familia duni sana yenye kunuka umasikini, kikwetu ukiitwa madaso basi fahamu uko kwenye level mbaya sana ya umasikini....

Asilimia kubwa ya sisi vijana wa kitanzania, tunaamini katika watu fulani kutubeba, tunaamini tulivyo ni kwa sababu ya historia mbovu ya familia zetu, tunaamini kuwa ndoto zetu ziko gizani kwa sababu  ya watu fulani, au serikali na wazazi wetu. 

Tunaamini kuwa kufikia utajiri na fahari ya dunia sio rahisi, ila tunaamini kwenye bahati kuwa ndiyo inaweza kuwa njia nzuri ya kufikia malengo na ndoto zetu. 

Kuna wakati wa kukubaliana na hali ya familia uliyotoka, hali uliyo nayo kwa sasa, kwa sababu kwa kufanya hivyo unatengeneza relief na chumba cheque hewa kwenye ufahamu wako. Unapokubaliana na hali hujenga nafasi nzuri ya kufikiri, kujifunza na kutafuta mbinu mpya ya kuhakikisha kwanza haurudii makosa ya wazazi, kuikataa hali uliyo nayo na hii inakupa courage na mwanzo mpya wa safari ya kuzifukuzia ndoto zako...
Tunajifunza kwa wazazi wetu waliofeli lakini baada ya kujifunza kwao tunageuka upande wa pili wa shilingi kwa kusema wazazi wangu walishindwa kwa sababu kadhaa lakini kuna familia ya moja kati ya vijana ambao tayari wameshaona mwanga wa maisha na vijana hawa ni wale wenye kutokea kwenye familia duni, wao walifanya nini mpaka wakaleta ukombozi wa kiuchumi katika familia zao.
Ndiyo maana ni vyema na ni nzuri sana kujifunza kwa aina vijana au watu waliofanikiwa ambao pia walipitia kwenye mikono ya wazazi wenye uchumi duni.
Inaweza isiwe rahisi kupitia njia ambazo wao walipita kufikia hapo walipo lakini kuwa kwenye kiwango cha maisha mazuri inaweza kukutia hamasa ya kuamini kuwa hata wewe unaweza kutoboa tundu la mafanikio kama wao...

Nimekuja gundua kuwa dunia iko na equal opportunity sasa ni mimi na wewe tunavyotazama hizo fursa na namna ya kuzitumia hizo fursa. Kama Mungu wetu yupo basi you can be a person you need to be and is very possible at any cost 

Wewe ni shujaa, make it to the maximum, trust the way you need to pass, and everything are possible under the beautiful world we have..
Glory be to God.
Mgemamoses@gmail.com 
Mgema Moses Zephania 

Friday, July 1, 2022

Nimezaliwa kwenye familia ya kitanzania, familia ya kawaida kabisa ambayo ni maisha ya familia nyingi za kiafrika hasa ambazo zilianza miaka ya 1660s kuja hadi Mwishoni mwa miaka ya 1990s. Maisha yetu hayakuwa mabaya na hayajawahi kuwa mabaya kiasi cha kusema tunatoka kwenye familia masikini isiyojiweza hata kwa chakula au kupata mahitaji muhimu ya binadamu...

Spendi kutangaza umasikini, umasikini sio sifa, umasikini sio fashion, maana ukimwona masikini unaweza kutoka machozi, masikini hawezi kudumu gharama za maisha hata yale ya kula na kuvaa, kujimudu kwenye matibabu ya magonjwa nyemelezi na changamoto ndogo ndogo za afya, masikini hawezi kuwahudumia watoto wake hata kwenye mambo muhimu kama elimu, masikini ni mtu fukara mwenye huzuni, aliyekosa tumaini la maisha  mwenye kujiona mwenye laana na asiye na bahati duniani....
Mimi sio masikini, mimi sio fukara, mimi sio ombaomba, mimi nina kila kitu, mimi nimezungukwa na fursa, mimi nina nguvu na maarifa yenye kuona fursa, jambo kubwa zaidi nina utajiri wa afya imara na uwezo wa kufanya kazi yoyote ile yenye kunipa matokeo bora ya kazi zangu zote.
Maisha ya mwafrika tako mikononi mwake mwenyewe, kusinyaa, kulaumu, na kumtegemea mtu akutoe mahali ni ngumu sana bali maamzi ya kuchoka na kuamka tako katika mikono na uwezo wetu wa kufanya jambo ili kubadili hatima na mwelekeo wa maisha yetu...
 Usiku wa leo, umekuwa ni usiku mkubwa sana kwangu, maana Mungu amezungumza nami kwa namna ya pekee sana juu ya maisha yangu pamoja na maisha ya kijana wa kitanzania. Amenichukua katika ndoto, akanionyesha Tanzania, akanionyesha Afrika na ulimwengu mzima ile fahari na utajiri mwingi katika bara hili tukufu la Afrika....
Kwa miak mingi moyo wangu alikuwa na simanzi, akili yangu ilipoteza nuru, moyo wangu ulisinyaa na kuna wakati ulikata tamaa ya maisha, sikuona kuishi tena, niliamini mwanadamu ndiyo anaweza kuyafanya maisha yangu kuwa bora tena, niliyatamaza matatizo kama sehemu ya mgandamizo mkubwa uliyoifanya akili yangu kusinyaa na kuamini kuwa maisha yangu yalikuwa yamepoteza mwelekeo....
Ilikuwa ni muda mchache sana baada ya Baba yangu mzazi kufariki dunia, nikaiona nuru na tabasamu using mwangu likififia siku kwa siku, ghadhabu ya moyo, na hasira nyingi moyoni mwangu ilikuwa ni suluhisho sahihi kwangu katika kufanya maamzi, nilimuwaza sana Baba yangu, nilifikiri sana mama yangu, niliona giza zito mbele yangu, akili yangu ilifungwa na uwezo wa kufikiri ulikwisha in short  I lost everything.......
My education was not something could help to solve my problems, afya yangu haikuwa mtaji wa kunitoa mahali nilipokuwa, maombi yangu mbele za Mungu haikuwa kitu chochote, imani yangu kwa Mungu iliyumba sana, pamoja na kwamba nilikwenda magotini kila wakati lakini imani yangu ilikuwa chini sana na wala maombi hayakuwa suluhisho ya hali yangu kwa wakati huo.....

Usiku wa leo nimeiona Tanzania, usiku wa leo nimeiona Afrika na usiku wa leo nimeiona dunia yote katika ndoto zangu, kuna jambo Mungu alikuwa ananisemesha, kuna jambo Mungu alikuwa ananikumbusha ndani yangu, kuna jambo Mungu alikuwa ananikumbusha kwa msisitizo mkubwa na kunilazimisha kufanya halafu niseme na kijana mwingine ambae kwake haoni mlango tena......

Mungu amenipa kalama na kipaji kikubwa cha kuandika, sihitaji kufanya nukuu au kusoma mahali ili kutengeneza mada ya kuzungumza, ninachohitaji, ni mikono na utayari wangu kufanya andiko lolote lile kwa lugha yangu ya kiswahili au kwa lugha ya kiingereza, hiyo ni talanta aliyonipa Mungu kufanya....

Mungu akanikumbusha jambo la msingi Sana kupitia stori ya Yesu kristo pamoja na Yusuph, hawa ni watu ambao Mungu alinisemesha kwa upana na kunitaka nawe nikushirikishe kwa mapana na marefu sana. Naandika haya kwa sababu Mungu amenipa ufunguo wa hazina yangu, God has already gave me the key 🔑 to unlock the treasure ahead of me.

Akaniambia kuwa Yusuph alikuwa na ndoto na hiyo ndoto aliiona akiwa katika hali ya umasikini, hali ambayo hakuna mtu angeweza kumwelewa wakati anawasimulia ndugu zake, ndiyo maana baada ya kusimulia habari ya ndoto zake, waliona kitu ambacho kiliwachukiza wao, na ikawq sababu ya Yusuph kwenda shimoni na hatimaye kufika Misri nchi ya Ugenini....

In short alipitia changamoto nyingi za kukatisha tamaa sana, mambo magumu, mambo ambayo hakupaswa kuyapitia katika umri wake, lakini Yusuph aliyapitia kwa maumivu makali kwa jasho na damu. Pamoja na nyakati hizo ngumu, Mungu alikuwa kimya sana, sio wakati akiwapa simulizi wale ndugu zake pamoja na wazazi wake, wala kipindi cha kutupwa shimoni, kuuzwa kwa wafanyabiashara, kwenda kuwa sehemu ya watumwa katika nyumba ya potifa hatimaye kuwa mmoja wa wafungwa Gerezani huko Misri, katika kipindi chote hicho Mungu alikuwa kimya sana tena kimya kisicho na mshindo wowote.  Tupumzike hapo.

Mungu akanipitisha kwenye stori ya Yesu Kristo na baada ya kupitia maandiko matakatifu ya Biblia nikagundua kuwa, Mungu hakuwa na Yesu kwa zaidi ya miaka Thelathini, alikuwa kimya, Yesu alikuwa akifanya kazi zake bila mawasiliano yoyote yale ya ana kwa ana mpaka kipindi cha mateso yalipoanza, ndipo Yesu akahitaji msaada wa Mungu lakimi pamoja na Yote, Mungu alimkataa na kukaa pembeni. Ilikuwa ni wakati Mungu, majira ya damu na jasho jingi kwenye mwili wa Yesu lakini Baba yake alikuwa kimya kama haoni....

Habari hizi mbili zimekuwa sehemu ya usiku wangu wa leo, Mungu akinipitisha na kunifundisha jambo kubwa sana kwenye maisha yangu na maisha yako pia. Mungu anapokaa kimya sio kwamba haoni wala sio kwamba hayupo pamoja na wewe, anakuwepo, anakuona na yupo karibu na wewe kuliko unavyofikiri wewe.

Mungu akaruhusu mateso kwa Ayubu si kwamba alikuwa haoni, ndiyo maana shetani alipokuwa anajaribu kumshawishi Mungu amruhusu akaiguse Roho ya Ayubu, Mungu alimkatalia kwa sababu kama shetani angegusa roho ya Ayubu kulikuwa na kifo moja kwa moja lakini Mungu hakuwepo lakini alikuwa pamoja na Ayubu...

Mungu hakuwepo kwa Yusuph na Yesu lakini alikuwa pamoja nao katika yote waliyokuwa wakiyapitia kwa ugumu, jasho na damu. Ni matukio mazito ya UKIMYA WA MUNGU, ni Nyakati ambazo Mungu huwa hayupo kabisa lakini yuko pamoja na wewe katika kila hatua ya mapito yako au mapito yangu......

Baada ya kunipitisha kwa watu hawa wawili Yesu na Yusuph halafu kwa Uchache sana kwa Ayubu, kisha akanikumbusha kwa mapana na marefu jitihada zangu, nguvu zangu, shauku yangu, na nia yangu ya kufanikiwa kwa haraka sana, lakini Mungu akanipitisha kwenye baadhi ya historia ya maisha yangu.

Nikiwa darasa la tatu katika shule ya Nyahanga Wilayani Kahama, Mkoani Shinyanga, I was very young, siku moja katika kanisa la Assemblies, nikiwa na mdogo wangu Japhet siku ile nililia sana, and I tried to wipe the tears 😢 buy wasn't wiped, and my heart was full of sorrow and sudnes, wishing to stay with our beloved father ambae kwa kipindi hicho alikuwa Nzega Tabora, machozi hayo yalihitishwa kwa neno moja kuwa Mungu fanya njia ili tuhamie kwa Baba Nzega, is where the tears ended baada ya wiki moja Baba alipiga simu akasema tunahamia Nzega familia Nzega and that one was time of more than four years since he left us in  kahama.
Akanipitisha kwenye nyakati ngumu ambazo niliwahi kupitia baada yakumaliza Elimu ya sekondari, kipindi hicho sikuwa na tumaini la kuendelea na shule, lakini tukiwa katika maombi na kaka na rafiki yangu Cornelio, Mungu alifanya mpenyo ambao mpaka leo sina namna ya kuelezea matendo makuu ya Mungu katika mpenyo huo wa wajabu sana....

Akanikumbusha tena muujiza na mpenyo nilipokuwa nimekaribia kwenda chuo kikuu, kuna jambo kubwa pia alifanya na Eliya John Tikilu aweza kuwa shahidi wa maneno yangu niliyomwambia wakati na msindikiza baada ya kupitia nyumbani pale mwenge mwaka 2013 mwezi wa saba, neno langu lilikuwa nitakwenda kusoma St. Augustine Mwanza I had no any option badala ya SAUT, it was hard but God opened the door after fasting prayer...

Cha mwisho alichonikumbusha Mungu usiku wa leo ni jambo nyeti na muhimu sana kwenye maisha yangu, kwa sababu bado sio officially to the public sitosema hili kwa sababu ya kimaadili ya kipentekoste na kwa sababu pia sijawiwa kuliweka wazi, ila ni jambo kubwa na la muhimu ambalo Mungu alisema na mimi katika kipindi ambacho sikuwa na shauku wala wazo tena la kuwa kama ilivyo sasa kwa sababu jambo lenyewe lilikuwa ni miaka zaidi ya tisa ilikuwa imepita tangu nilipopata shauku na nia yakulifanya jambo hilo, na nilijaribu mara kadhaa lakini was difficult lakini miaka miwili kasoro miaka mitatu iliyopita nikiwa Dar es salaam Mungu akasema na Mimi nikiwa kwenye namna ya sintofahamu na hata niliporudi nilipotaka kupita kushoto bado Mungu alinifanya kuwa kwenye njia sahihi aliyoikusudia.....

Baada ya kunipitisha katika historia ya maisha ya Yesu, Yusuph na kunikumbusha mambo makubwa ambayo amewahi kunifanyia mimi binafsi miaka ya nyuma. Ndipo akasema kwenye ukimya wangu sio kwamba sioni, bali nakuandaa kuwa yule ninaye mtaka mimi, sio unaejitaka wewe. 

Naruhusu baadhi ya nyakati ngumu maishani ili kukufanya kuwa bora mara dufu, ili unitukuze mimi, kuna jambo la ziada ambalo nalitaka mimi wewe hulioni. Nyakati ngumu huwa na maana kubwa sana kwangu, kama ilivyotokea kwa Yusuph pamoja na Yesu...

Mnung'uniko, kukataa tamaa, kulaumu, na mutumia akili zetu wenyewe ndiyo sababu ya Mungu kukaa kimya wakati mwingine