Sunday, January 30, 2022

Siku nilikuwa namsikiliza Eric Shigongo moja kati ya wafanyabiashara wakubwa katika nchi yetu ambae amwekeza nguvu na akili yake katika kutengeneza mtazamo chanya kwa vijana juu ya ndoto zao.....
Shigongo Eric alisema kuna wakati unapaswa kutembea kwenye njia ambayo wewe mwenyewe unaiona sio ambayo wengine pia wanaiona ilimradi hiyo njia unaiona inakupeleka kwenye njia ya kufikia ndoto na malengo yako basi tembea hiyo njia bila kujali ni wangapi wataiunga mkono.

Kati ya sababu za watu wengi kushindwa kufikia malengo na ndoto katika ulimwengu nikuishi katika mawazo ya wengi, mawazo ambayo watu wengi wanasapoti na kuyakubali, mara nyingi mawazo kama hayo huwa hayana maajabu katika dunia iliyojaa ubunifu na uthubutu kila mahali....

Njia ngumu huwa na upkeep sana, njia ambayo wengi hawaiungi mkono, mara nyingi njia hiyo huwa na mafanikio au matokeo makubwa mbeleni kuliko easy way ambayo kila mtu anaweza kupita.

Yesu ni miongoni mifano hai ambao ulipita kwenye njia ambayo hakuna hata mmoja anae tamani kupita njia hiyo. Yesu mpaka anafikia lengo na kusudi la kuwepo duniani alipitia kukataliwa, kuwindwa kufa tangu akiwa katika umri mdogo, njia yake ilisongwa na changamoto nyingi kwa lengo la kumkatisha tamaa, lakini alifanikiwa kuishi kwenye kusudi lake kwa sababu tu kabla wengine hawajajua yeye alikuwa anajua nini anachofanya.....

Yusuph pia ni.miongoni mwa watu wa mfano katika ulimwengu, ni mtu aliyekoswa kuuwawa na ndugu zake, aliuzwa utumwani, pamoja na kuwa katika utumwani lakini hakuacha kufuatilia ndoto yake maana aliijua na alijua kusudi la Mungu ndani yake

No comments:

Post a Comment