Monday, January 10, 2022

ONDOA WATU WASIO SAHIHI KATIKA CYCLE YAKO

Niliwahi kusoma article ya Bill Gates, moja kati ya matajiri wakubwa duniani, alisema alipopata wazo la kuanzia biashara yake ya windo aliwashirikisha watu 1200, watu 900 walimwambia hicho kitu hakiwezekani, 200 waliunga mkono wazo la Bill Gates, watu 89 hawakuwa na mchango au wazo lolote, na watu 11 waliunga mkono wazo la Bill Gates.

Wakati nasoma article  hii, ilikuwa kama stori hivi kwangu, sikuchukulia kiundani sana kwa sababu  niliona kama ni stori za kawaida za watu ambao  tayari wamekwisha piga hatua kwenye maisha yao, niliona ni stori za kawaida kwa mtu ambae amefanikiwa, maana hata akisema uongo anaamini watu watakubali tu kwa sababu  yeye ametimiza malengo na ndoto zake.

Nimekuwa nikifanya kazi nyingi na mara nyingi kazi ikiwa imekwisha kuanza hasa ikiwa imeanza kuonyesha matokeo, watu hunipongeza na kunitia moyo, lakini karibuni nimetaka kuanzisha kitu pamoja na rafiki yangu, kwa sababu ya usomi na akili Fulani  ya kuamini katika kuanza, tulifanya utafiti kidogo  kwa watu wa eneo hilo, pamoja na watu wanaofanya biashara  kama hiyo

Asilimia  kubwa ya washindani katika ile biashara walisema hapana, hii biashara kwa sasa ni ngumu, biashara hii inahitaji uzoefu maana changamoto  zake zinahitaji mtu mzoefu sana na biashara. Nikajikumbusha baadhi ya michakato ya kuomba kazi kwenye mashirika binafsi (Private sectors) kwamba ukitaka kuomba kazi au tangazo la kazi likitoka lazima uwe na uzoefu Fulani....

Swali  langu likaja kusema, hivi huyu asie na uzoefu afanye nini sasa maana kila sehemu uzoefu  unahitajika, kazini  uzoefuzi, biashara  ni changamoto  inahitaji  mtu mzoefu, sasa tufanye nini.....

Ili kutoka hapa ni vyema kuwa na watu sahihi au ambao wanaweza  kukwambia fanya hili linawezekana, usipofanya umasikini itakuwa halali yako, katu hautaweza kuijua potential  yako, katu hutoweza kupiga hatua hata moja.

Watu wengi  wanakatisha tamaa sana, watu wengi wanacheka na wewe ila katika mioyo yao hawakutakiii mema hata kidogo, wengine wanaogopa kukwambia ukweli wa biashara  wanayofanya kwa sababu wanajua unaenda kuongeza options  kwa wateja wa bidhaa yako.

Wakatu mwingine wamekutazama wamegundua kuwa unayo potential  kubwa katika kazi, Ubuntu, pengine wanaogopa Elimu yako, pengine wanaogopa IQ yako,  maana unauwezo wa kwenda kufanya zaidi ya wao.

Wapo dream  killers Waepuke, usiwape Wazo lolote, usiwape nafasi katika maisha yako, usiwape chansi  kwenye maisha  yako, wanakupotezea muda, wanashikilia hatua zako, put them aside move forward, have right  people  kwenye njia yako.

Hakuna asie weza, pamoja na changamoto  zote hizi lakini, hakuna mtu aliye wahi kujaribu kwa moyo akashindwa kufanya jambo, akiwa na bidii, maarifa kidogo lazima aone hatua kwenye jambo lolote hata kama shetani atasimama mbele yako

Nimejifunza mambo mengi sana unaposhare jambo lako na watu hata wale wa karibu yako wanaweza kuwa mwiba kwako, achana na watu wasio  na msaada  kwako, share nao kwa mambo unahisi ndio yaliwakutanisha.

Chagua watu wa msingi ambao watakupa mawazo mazuri, watakupush, watakushauri kwa lengo la kujenga, watakuencourage kufanya hatua katika kila jambo lako

Play fair, Be positive 
2022 ni mwaka wa kupiga hatua 

No comments:

Post a Comment