Thursday, February 11, 2021

NI KWA SABABU YA KILICHO KWENYE WALETI NA POCHI YAKO TU WALA SIO KINGINE

Wakati unafanya vizuri utakuwa mzuri na mwenye heshima kubwa sana mbele za watu. Ukiwa na fedha, kipaji ambacho kinakupa matokeo chanya na kuwagusa watu wengi kwenye jamii, ukiwa tajiri, kiongozi  kama mbunge na hadhi zingine kwenye jamii hasa jamii za kiafrika, utaitwa kila aina ya majina mazuri, tajiri, mweshiwa, kiongozi, doni, kaka, mkubwa, mzee hata kama una umri wa miaka chini ya kumi ila kwa sababu wanachokiita majina yote mazuri hata wewe unaheshimika.

Sio ajabu Tanzania mgonjwa kunyimwa hela ya matibabu na baadae watu kutoa mamilioni ya shilingi wakati umefumba kinywa na huzungumzi tena, jeza la kifahari, kaburi na chakula cha haja na sifa kedekede.

Ni rahisi mtoto kukosa ada ya shule baada ya kuvuja jasho na damu akitafuta ada ya shule tena ada ya shule za serikali kwa majirani, ndugu na jamaa akakosa kwa kunyimwa huku watu wakija na sababu kedekede za unajua mwanangu sina hata hela nimepeleka shamba, mama yangu ambae ni bibi yako alikuwa anaumwa na pole nyingi ningekuwa nayo ningekupa hela wakati huo asilimia kubwa wakijigeuza kuwa mamotivational na mainspirational speakers kukuita jiniazi na unatakiwa kupambana ili kufikia ndoto yako. Muda mfupi ukiondoka watu walewale ambao walikosa ada ya shule za serikali unakuta wanachangia malaki ya pesa kwenye harusi ya mshikaji wao au kwenda kuweka heshima bar na washikaji huku wakipeana stori, na stori zenyewe ni za yule yatima aliyepita mchana kuomba msaada kwa ajili ya ada na mahitaji ya shule ili kupigania ndoto zake.

Ni somo gumu sana lakini kuwa makini na watu wa nchi hii au ulimwengu huu, usipende kusifiwa na kuvimba kichwa kwa kuitwa majina yenye hadhi ukaona umefika, kumbuka kuna watu wanakuita majina mazuri huku wakiitazama waletï na pochi yako, uishimiwa wako ni kwa sababu ya dolla, misimbazi na pounds unazomiliki, heshima unayopewa si ya kwako ni kile ulicho nacho basï.

Hadhï yako ni kwa sababu ya kile ulichonacho kuanzia kwenye nyumba ya Baba yako maiti haitazikwa mpaka ufike hata kama uko ulaya na corona imefunga mipaka ya nchi unahitaji kuunga unga ili ufike kwenu mwandugembe ulipo msiba tena wa mtoto mdogo kabisa, ukoo utakutambua, kijiji mpaka tarafa watakuita majina ya heshima na hadhi na wewe utavimba kichwa, kwenye baadhi ya nyumba za ibada hata kama unatenda dhambi ambayo wengine wakifanya wanapigwa na fagio la chuma, wewe watachekacheka nakutengeneza mazingira ambayo kosa lako litaonekana la kawaida na vifungu vya Biblia vitatumika kukulinda na kukutetea USIHUKUMU USIJE ''UKAHUKUMIWA, YULE ANAE JIONA MWEMA AWE WA KWANZA KUMSIMAMISHA HUYU NK.''Sio wewe ni fedha, mali na utajiri wako.

Jitahidi kufanya mambo ya msingi, fanya ambayo unapaswa kufanya, usifanye jambo kwa sababu unafikiri una kundi kubwa la watu nyuma yako wanakupenda na kukuelewa hapana, wengi wao ni wasengenyaji na watoa taarifa zako pindi utakapojikwaa na utajiri ukaisha, pale kipaji chako hakitawagombanisha watu wanaojiita watu wa connection, mawakala na watu wa menejimenti muda huo watakuwa wametimua mbio.

Fanya kila unalolifanya huku ukikumbuka kuwa yule kijana mdogo aliyekosa ada kipindi kile nakazunguka mtaani, kwa ndugu kwa rafiki wa marehemu mama au Baba wakasema hawana hela na kuambulia kumpa pole, leo wanamwita mweshiwa baada ya yeye kuvuja jasho bila msaada leo wamegeuka nakuwa washuhudiaji na wenye kujigamba wakisema huyu amekuwa tunamwona, tumemsaidia sana Baba yake alipofariki sisi ndiyo tuĺisimamia masomo yake mpaka leo ni daktari.

Unapokuwa na mali wewe ni mtamu na unastahili kila jina zuri hakika, ila kumbuka wanaokusema vyema mchana katika giza wanakuita mpumbavu huna akili kazi kutumia mali na pesa vibaya, wengine hata hawajawahi kukushauri lakini wakiwa vijiweni kutwa kusema huyu jamaa hashauriki, tunamshauri sana lakini wapi kumbe masikini ya Mungu hata kukushauri hawajawahi kukuambia ukweli, kuwa makini ndugu yangu.....
Usirubunike na maneno matamu ya walimwengu, jenga msingi bora wa maisha yako, usikubali kurubuniwa kwa maneno mazuri ya watu kwa sababu ya utajiri wako, fanya jambo muhimu kwa wakati sahihi, usipende kuifurahisha kila nafsi ya mtu bali ishi wewe kwa utaratibu wako.
Mungu akupe kujua watu wakweli mbele yako na waongo ili kuyaweka maisha yako salama kesho.
Mgema Moses
0715366003/0755632375

Sunday, February 7, 2021

Tengeneza mahusiano mazuri na watu kwa kadri uwezavyo bila kujali hadhi yao, uwezo, kazi na mazingira yao. 
Kwenye maisha yatu kila mtu ana mchango wa moja kwa moja au si wa moja kwa moja sana ila pia anaweza kuwa sehemu ya wewe kutimiza malengo, kukuepusha na hatari fulani au kukupa dili fuĺani.
Nakumbuka siku moja ndugu mmoja ambae tulikuwa tukiishi mtaa mmoja yeye akifanya kazi ya bodaboda, hatukuwa tumezoeana ila nilikuwa namsalimia kila nikipita, kumbe yeye alikuwa anafahamu kuwa angalau nimepiga hatua katika masuala ya elimu, hakujua exactly nimefanya taaluma ipi ila alikuwa anajua nimesogea mbele 

Friday, February 5, 2021

AINA YA MAAMZI NA UTULIVU HUPIMA KIWANGO CHA HEKIMA NA UKOMAVU WAKO.

Ukomavu wa mtu haupimwi kwa wingi wa miaka, wingi wa nywele nyeupe kichwani, wingi wa vizazi kutoka kwenye viuno ama tumbo lako hapana.
Ukomavu wa mtu mara nyingi unapimwa kutokana na uwezo wa kukabiliana na nyakati ngumu, nyakati tata na milima mîgumu ambayo unakutana nayo na vile unakabiliana nayo katika hali ya utatuzi na kuweka sawa bila kulazimishwa na mazingira presha na mazingira ya uhitaji wa jamii inayokuzunguka.
Kuna nyakati tata na ngumu sana kwenye maisha yetu ambazo huwa tunapitia, wakati mwingine zinaumiza, zinatuchafua, zinakatisha tamaa, zinatukumbusha nyakati ngumu ambazo hazijawahi kuwa rafiki bali maumivu makali ambayo hata huwa hatupendi kuzikumbuka kabisa.
Wakati mwingine unapewa nafasi yakuwa mtoa maamzi ambayo haki inapaswa kutendeka bila kujali asie na haki ataumia kwa kiwango gani. Ukomavu wako pekee ndiyo inahitajika, hekima na busara yako ndio inahitajika sio kitu kingine.
Nayakumbuka mazingira ya Mfalme Sulemani ambae alipaswa kufanya maamzi ya haki dhidi ya wamama wawili ambao walikuwa wanagombea mtoto mmoja. Ni hekima, busara na ukomavu wa hali ya juu ulihitajika kufanya maamzi, maamzi sahihi yalihitajï kiwango kikubwa cha hekima ili kutambua nani alistahili nini kati ya wamama hao.
Pamoja na Daudi kuwa shujaa wa waesrael kwa kumpiga Goriath nakuahidiwa zawadi kemukemu na mfalme saul lakini mwisho wa siku Saul aligeuka kuwa adui mkubwa wa Daudi, hekima pekee toka kwa Daudi ndiyo iliyomfanya kuishi katika nchi yake kwa amani bila kupata madhara toka kwa sauli.
Nimefuatilia habari ya Elizabeth Michael na Mama Mzazi wa Stivie Kanumba ambae ameshindwa kumsamehe Elizabeth kutokana na tukio la mwaka 2012 nh kweli ni jambo gumu kusahau lakini bado haiondoi ukweli kwamba imekwishakutokea na haina budi kusamehe na kusahau na maisha kuendelea mbele bila shida
Pamoja na kusongwa songwa kwa maneno ya yule mama bado Elizabeth amekuwa ni mtulivu, mpole na mwenye heshim, hekima na busara akijitahidi kulinda hadhi na heshima ya mama kwa umri lakini pia utù. Nimemsikiliza akifanyiwa mahojiano na waandishi wa habari hakika ni mtu mkomavu pekee ndiyo anaweza kusimama na kujibu kwa hekima na utulivu wa kiwango cha juu.
Pamoja na kukiri kuwa maneno ya yule mama yamekuwa msalaba wake na yuko tayari kwenda nayo kalvari bado alimeendelea kuwa mkimya, akitambua kuwa yule ni mama yake kwa umri na akasema muungwana akivuliwa nguo huchutuma.
Sio rahisi kwa binti staa, binti mdogo kuwa na mtazamo chanya kwa kiwango kikubwa kiasi kile, alikuwa na nafasi kubwa yakuyatumia mazingira haya kama njia ya kujiongezea followers, kutengeneza attensheni kwa jamii kwa maslahi ya biashara zake za uigizaji lakini amekuwa tofauti.
Ukomavu ni vile ambavyo unauwezo wa kuipa hekima ikuongoze katika kufanya maamzi, busara ni ishara ya ukomavu wa mtu.
Halisia tumeumbwa tukapewa hisia, maumivu na kukerwa lakini kwa mtu mwenye ukomavu wa fikra, akili ni katika uwezo wa kukabiliana na mazingira ambayo ni magumu na yenye changamoto zilizo changanyika na maumivu makali yaliyoujeruhi moyo na nafsi.
Mungu ameumbia utashi, hekima na busara ni vyema kujifunza kuishi kwenye aina hizi tatu za maarifa maana ndiyo njia ya kwanza bora za kuishi kwenye mazingira yeyote na kuyamudu.
Maamzi ya mtu aliyekomaa huwa na matokeo makubwa sana ushindi katika chanya. Tumwombe Mungu kama ambavyo Sulemani alimwomba ampe hekima ambayo ilikuwa msingi wa mafanikio yake katika utawala wake.
Ukomavu ni kiwango cha juu cha hekima, mtu mwenye hekima ana maarifa sahihi, na ufahamu wake ameujenga katika mtazamo chanya, haendeshwi na gadhabu, uchungu, chuki na kisasi ndani yake bali hekima humfanya mtu kuyaweka pembeni matakwa yake binafsi kwa ajili ya wengi na haki kutendeka kama ambavyo sulemani alifanya bila kujali alitumia hekima bora kabisa.
Learn to be matured
Mgema Moses
0715366003/0755632375


Thursday, February 4, 2021

Ushindi ni ahadi ya Mungu kwa wanadamu, tuĺiumbwa tukiwa na nguvu ya ziada, tabia tofauti na viumbe wengine, tunautashi, tunasifa ya Mungu, hivyo basi kama tunasifa za Mungu maana yake kama alivyo yeye ni mshindi hata mimi na wewe ni washindi.
Ushindi wa mtu huanzia kwenye ufahamu, namna mtu anavyofikiri, anavyojitazama, anavyojiona na imani ya uwezo iliyo ndani yako/yangu. Jambo hili limekaa katika mfumo na mtazamo wa kiimani zaidi kama mtu hajafungua mtazamo wake vyema katika mukhutaza wa maisha yetu ya kila siku.
Kushinda na kushindwa ni mambo mawili ambayo yametenganishwa na uzi mwembamba sana, mentality na imani ya mtu juu ya vile ajionavyo kuanzia kwenye mfumo wa ufahamu wake...
Kuna stori moja inazungumzwa kwenye kitabu cha Joshua, kuna watu walitumwa mahali kwenda kuipeleleza nchi na walipofika huko walikuta watu wakubwa sana, katika kurudisha ripoti kwa aliyewatuma kundi la kwanza lilisema wamefika huko wameona majitu sasa sio watu ila majitu ambayo yaliwafanya wao kujiona kama mapanzi.
Kundi la pili likaja na ripoti yake ambayo ilikuwa imesheheni imani, ujasiri na nguvu ya ajabv kwamba wameona uwezekano wa kuivamia ile nchi na kuiteka nakuwa mali yao. Ndani ya kundi la watu kadhaa wamegawanyika mtazamo wapo wameona ushindi wengind wameshaona haiwezekani hata kidogo sisi ni mapanzi tu.

Wednesday, February 3, 2021

NGUVU YA MSAMAHA

Msamaha ni dawa, msamaha ni uzima jifunze kusamehe pale unapokosewa na aliyekukosea anapogundua kuwa amekosea na kuomba msamaha, wakati mwingine hata kama mtu hajakuomba msamaha samehe, msamaha ni kwa ajili yako sio kwa ajili ya alïyekukosea.

Kutokusamehe ni kubeba mzigo ambao hauna faida, na katika dunia tunayoishi leo huwezi kuishi bila kuudhiwa, kukosewa na kutendewa mambo ambayo ni kinyume na matarajio yako kwa sababu sisi ni binadamu na makosa yalianzia hapo zamani za edeni kwa Eva na Adamu....ni watu ambao walithubutu kumkosea Mungu huku wakijua uwezo na ukuu wake ije iwe wewe.....pamoja na makosa ya wengine Mungu aliamua kusamehe.

Unapokosewa fahamu na wewe pia huwa unakosea wengine na wanakusamehe, hivyo ukiwa katika ulimwengu huu, kukosea na kukosewa ni wajibu wa mwanadam, halafu kusamehe na kusamehewa ni tendo la lazima sio la hiyari,.... Kusamehe ni wajibu......ïli mradi unaishi duniani..

Msamaha ni suluhisho la uponyaji wa akili, afya ya mwili, msamaha ni ufunguo wa mahusiano mapya ambayo yalitiwa doa na kosa, msamaha ni uponyaji wa hisia zenye maumivu makali ndani yake, msamaha hurejesha furaha nakuondoa huzuni na hasira yenye uchungu ndani yake.

Yapo makosa ambayo sio rahisi hata ukiambiwa samehe ni ngumu lakini, Mungu anatutaka kusamehe 7x70 bila kujali ukubwa wa tatizo ila unachopaswa kufanya ni kusamehe tu.

Kuna namna inatokea kwenye maisha ni ngumu sana kusahau ila ndo unapaswa kusamehe bila kujali ukubwa wa kosa mfano, mume amekusaliti, umepigwa, mtu ameua ndugu yako, umeibiwa au kufanyiwa kitendo chochote ambacho kimeacha kovu moyoni na kwenye maïsha yako kwa ujumla, ni kweĺi tunarejea tu kwenye msingi wetu, Je usiposamehe ndio itarudi au kufuta kumbukumbu ya kilichotokea hapana kinabaki vilevile.

Umewahi kujiuliza gharama ambazo Mungu aliingia ili kutoa msamaha au kwa wakristo unaposoma neno lolote kwenye Biblia linalohusu ukombozi na msamaha wa Mungu kwetu huwa unachukuliaje, unaposoma Yohana 3:16 huo mstari huwa na maana ipi kwenye ufahamu wako.

MSAMAHA NI DARAJA JIPYA LA WASHINDI.
Kuna msemo mkubwa sana umekuwa ukisemwa na watu ingawa sijui kama watu wote wanaofanya kotesheni ya msemo huo huwa wana maanisha au huwa wanasema tu kwa sababu upo....
1.Weak people revenge. 
2.Strong people forgive. 
3.Intelligent people ignore.
Uliandikwa na Albert Einstein...
Maneno hayo ni mazito sana ukitafakari vyema, so maneno mepesi kama ambavyo mtu anaweza kulala nakuamka nakutamka tu kawaida.....

Ukiniuliza mimï leo mambo yapi ni msingi bora wa maisha yangu duniani nje ya wokovu na Imani yangu kwa Yesu kristo ambae ndiye alitufundisha kwa vitendo maana ya haya mambo matatu
1. Upendo
2.Msamaha
3. Utu 
Washindi wote husamehe bali failures hubaki na kinyongo, mzigo moyoni kwa kifupi ni watu dhaifu sana, watu wa kundi la kwanza.

Binafsi haya ni kati ya maeneo ambayo huwa najipima nayo kuona kiwango cha ukomavu wangu juu ya kufanya maamzi yenye kukulazimu hata kama yanakuumiza ila lazima uyafanye ili kuweza kuwa balozi mwema wa Mungu hapa duniani.

Najua sio jambo jepesi kufanya kwa vitendo, ila ndio tunapaswa kusamehe, kupenda na kuĺïnda utu kwa faida yetu wenyewe.
FAIDA YA KUSAMEHE 
1. Hurejesha mahusiano na kujenga kuheshimiana.

2. Hulinda amani na kuondoa chuki, maana kama unaweza kusamehe maana yake una upendo wa agape, upendo wa Kimungu.

3. Humfungua mtu aliyekosewa na aliyekosewa hivyo kuondoa uchungu, hisia zenye maumivu ambazo zinaweza kupelekea kuibuka kwa ugonjwa.

4. Huonyesha ukomavu wa akili, nafsi na roho na kumweleza mtu mhusika kama mtu anaeweza kubeba vitu na kuvimudu.

5. Hupima kiwango cha ukomavu wa kiroho maana utakuwa ukitenda sawasawa na agizo la Mungu 
Zipo faida nyingi kwa mtu ambae hupenda kusamehe na kuachilia. Naandika ujumbe huu nikiwa najua kuwa kuna mazingira ya kibinadamu ni jambo gumu kuĺiko ambavyo mtu anaweza kusema au kuandika wakati hali ya kukosewa au kutendewa jambo baya kwa kiwango cha kutisha.

Msamaha ni agizo msamaha ni kutenda, msamaha inaonyesha pia kiwango cha ustarabu, utii, utu, upendo, ukomavu na utofauti wako na watu wa kundi la kwanza la watu....

Ni ngumu ila tenda kwa manufaa yako binafsi
Mgema Moses
0755632375/0719110760


Tuesday, February 2, 2021

IMEKUWA TABIA YA WATU WENGI

Ni rahisi zaidi kumsema mtu aliyeshindwa kwenye jambo fulani, alifeli mtihani, biashara ilianguka, alipoteza kazi au amekuwa akifanya chini ya kiwango kwenye majukumu yake.
Ni rahisi zaidi kumtukana mcheza mpira anapokuwa uwanjani nakumsemea maneno mabaya huyu hajui, anakosaje goli jepesi vile, anapitwaje kirahisi, huyu kipa shati anafungwaje kizembe vile huo ni mdomo wa mtu mmoja akiwa amekaa jukwaani na wakati mwingine anaporomosha maneno yasio na staha kwa mchezaji, ni rahisi sana.
Utakuta mtu/watu wako busy huyu mwimbaji hajitambui kabisa ona mwenzake ameubadilisha muziki kuwa biashara anapiga pesa kila kukicha yeye yupo yupo tu hana mpango.
Watu wanasahau hata kukumbuka kuwa mpaka unamfahamu kuwa huyu ni mchezaji tena akiwa kwenye timu kubwa ni juhudi zake ndiyo maana umepata wasaha wa kutoa pesa yako kwenda kutazama mpira, ndiyo maana kutwa headphone masikioni na kukera watu kwa muziki mkubwa katika subwoofer hapo nyumbani kwako.
Kidole karibu na kidole gumba ni rahisi zaidi kumnyoshea yule mtoto aliyeanguka mtihani huku ukiwa umesahau kuwa vidole vitatu vinakuelekea wewe na kukumbusha kuwa mbona na wewe hukuwa ukifaulu masomo ?, mbona wewe hata kazi zako huzifanyi vizuri ndiyo maana kuĺa kuku hapa nyumbani ni mpaka bibi atuma kutoka kwetu singida, hata hawa wakizungu huwezi kununua walau kwa mwezi mara moja ?
Ni rahisi zaidi kumkosoa kiongozi kwamba hafanyi vizuri wakati wewe hata kuwa balozi wa nyumba kumi ulishindwa,
Yapo mengi yanatokea kwenye mzunguko wa maisha yetu, hisia na mawazo ya watu wengi yamejengwa kwenye hasi zaidi kuliko chanya. Mtu akianguka kwenye jambo fulani ni mzembe mjinga, hajielewi, mvivu, hajisomei, mbinafsi nk.
Ndiyo maana leo utakuta vijana wako kwenye mahusiano mmoja akikosea hata kidogo suluhisho tuvunje mahusiano, tuvunje uchumba kama ndio bado tuko kwenye uchumba mambo yenyewe ndïo haya mimi basi....sababu yenyewe ya kitoto wee, nani kakwambia utaolewa na malaika ambae ukiwa nae hatakosea, umewahi kujiuliza kwa nïni wazazi waliishi au wanaishi mpaka sasa na unawasifia sana kuwa ni wazazi bora na wamejenga familia imara.
Asilimia kubwa ya mambo hata kama yamekuja au kutokea kwa namna ya mtu kukosa kutimiza wajibu wake sawasawa ni vyema kujenga hisia na mtazamo chanya kwenye ufahamu wako kabla kinywa hakijasema, sio kila aliyeshindwa kufunga goli, kuzuia goli amependa iwe ivo, sio kila mtu aliyefeli mtihani, biashara, nk ni kwa sababu ya uzembe au kutokutimiza wajibu wake hapana.
Nimejifunza sana kwa baadhi ya watu ambao walifanya isivyosawa katika mtazamo wa watu wengi wakasemwa vibaya, ooh wazembe, wavivu hawajielewi nk walipotatuliwa vyanzo vya kufanya vibaya wamekuwa watu bora sana.
Vilevile kuna baadhi ya watu wanafanya vitu kwa viwango vyao waliojiwekea mfano kwenye kiwanda cha muziki na mpira, biashara na elimu, kuna baadhi wanaimba kama burudani, kipato anachoingiza amelizika nacho na ameamua kuseti kuishi kwa kiwango hicho, sïo kila mwanamziki, mcheza mpïra anataka kuwa Dïamodo, Mbwana Samatta, hashmu Thabiti mwingine ndoto yake iĺikuwa kufikia levo aliyepo ndio maana baada yakufika hapo ametulia na kuĺinda kiwango hicho na amedumu hapo.
Kuna watu wanatamani kufikia levo ya umilionea, ubiĺionea lakini kuna mwingine ameridhika na uwezo wa kusomesha watoto, kumïliki nyumba, kupata gari yake au kutokumiliki hata gari lakini ndio uchaguzi wake aliochagua.
Kuna mifano mingi hata shuleni kuna wanafunzi huwezi kuwakuta wamekuwa wa kwanza hata kumi bora lakini yupo kwenye viwango vya ufaulu, kama wastani ni 50 basi piga ua galagaza yupo, watafeli sana au kufaulu sana lakini yeye yupo kwenye wastani wakumvusha daraja jingine ndiyo viwango alivyoamua kuishi navyo.
Mwisho sio kila mtu anataka kuwa kama wewe unavyotaka, sio kila mtu ambae hafanyi au hakufanya vizuri imesababishwa na uzembe au kupenda hapana kuna mengine hutokea kwa sababu zilizo nje ya uwezo wa kujizuia.
Asilimia kubwa ya watu hutamani kuwa bora katika kila jambo lakini yapo mazingira yanalazimisha kuwa hapo alipo au kufeli kwake.
Badala yakuja na majumuïsho ya majibu yatokanayo na matokeo yaonekanayo kwa macho ni vyema pia kuwa na muda wakumtazama mtu huyo kwa jicho chanya, hii itarahisisha sana kukupa relief ya kujua chanzo cha tatizo hata unapokuja kutoa majibu yako yawe na uhakika kuwa ni kweli..
Ni rahisi zaidi kujidanganya kwa kusoma kichwa cha habari juu ya kitabu nakujipa majibu ya kusudi la mwamdishi juu ya kile kimefunikwa ndani ya kava la kitabu....
Ukiwa mkosoaji jaribu kuwa mtafiti zaidi utakuwa bora na mwelevu
Smartness.
Mgema Moses
0715366003/0755632375

Monday, February 1, 2021

Fimbo ya Musa iligeuka kuwa hatua yakuvuka kwa wanawaesrael kufika ng'ambo ya bahari ya shamu, Mungu alimuuliza Musa una nini mkono mwako, Musa alijibu kwa ujasiri nakusema nina fimbo katika mkono wangu, uwepo wa fimbo ile katika mkono wa Musa, Mungu aliona kuwa yafaa kuwa mtaji wa hawa watu kupiga hatua nyingind kubwa kuelekea hatima ya maisha yao.
Wakati Mungu anaona hahitaji nguvu nyingi na kutafuta vifaa vikubwa ili kukausha yale maji ya bahari aliamua kuzipandia nguvu na elimu mpya kwenye fahamu za waesrael. Haikuwa rahisi kueleweka kama fimbo ile inaweza kuwa sababu ya maji ya bahari kugawanyika nakutengeneza njia, lilikuwa jambo la kufikirika kiasi fulani.
Wakati Mungu anaona uwezekano kupitia fimbo ya Musa kuwa unaweza kuwa moja ya mtaji wa kusogelea hatua kadhaa katika mwelekeo sahihi kuyaelekea malengo na kusudi la hatima.
Kuna mkulima mmoja mwenye shamba