Tuesday, April 30, 2019

NOTES OF LEADERSHIP.

What is Situational Leadership?

How Flexibility Leads to Success

Situational leadership is an adaptive leadership style.

This strategy encourages leaders to take stock of their team members, weigh the many variables in their workplace and choose the leadership style that best fits their goals and circumstances.

In the words of leadership theorist Ken Blanchard, “In the past a leader was a boss. Today’s leaders can no longer lead solely based on positional power.”

Situational leadership is the model of choice for organizations around the world that want to do the following:

1.Develop people and workgroups
Establish rapport and to bring out the best in their people
Use a common leadership style across all units in an organization, be it local, national, or international

Read more about situational leadership:
Situational leadership defined
History of situational leadership
Examples of situational leadership and quotations
Characteristics of situational leaders
Advantages and disadvantages of situational leadership
Benefits of situational leadership
Situational leadership defined
Situational leadership is flexible. It adapts to the existing work environment and the needs of the organization. Situational leadership is not based on a specific skill of the leader; instead, he or she modifies the style of management to suit the requirements of the organization.
One of the keys to situational leadership is adaptability. Leaders must be able to move from one leadership style to another to meet the changing needs of an organization and its employees. These leaders must have the insight to understand when to change their management style and what leadership strategy fits each new paradigm.
There are two mainstream models of situational leadership, one described by Daniel Goleman and another by Ken Blanchard and Paul Hershey.
The Goleman theory of situational leadership
Daniel Goleman, the author of “Emotional Intelligence,” defines six styles within situational leadership.
1. Coaching leaders , who work on an individual’s personal development as well as job-related skills. This style works best with people who know their limitations and are open to change.
2. Pacesetting leaders , who set very high expectations for their followers. This style works best with self-starters who are highly motivated. The leader leads by example. This style is used sparingly since it can lead to follower burnout.
3. Democratic leaders , who give followers a vote in almost all decisions. When used in optimal conditions, it can build flexibility and responsibility within the group. This style is, however, time consuming and is not the best style if deadlines are looming.
4. Affiliative leaders , who put employees first. This style is used when morale is very low. The leader uses praise and helpfulness to build up the team’s confidence. This style may risk poor performance when team building is happening.
5. Authoritative leaders , who are very good at analyzing problems and identifying challenges. This style is good in an organization that is drifting aimlessly. This leader will allow his or her followers to help figure out how to solve a problem.
6. Coercive leaders , who tell their subordinates what to do. They have a very clear vision of the endgame and how to reach it. This style is good in disasters or if an organization requires a total overhaul.
Situational leadership according to Blanchard and Hersey
The second model is based on the work done by Blanchard and Hersey. Their theory is based on two concepts: leadership itself, and the developmental level of the follower. Blanchard and Hersey developed a matrix consisting of four styles:
1. Telling leaders = S1 (specific guidance and close supervision): These leaders make decisions and communicate them to others. They create the roles and objectives and expect others to accept them. Communication is usually one way. This style is most effective in a disaster or when repetitive results are required.
2. Selling = S2 (explaining and persuading): These leaders may create the roles and objectives for others, but they are also open to suggestions and opinions. They “sell” their ideas to others in order to gain cooperation.
3. Participating = S3 (sharing and facilitating): These leaders leave decisions to their followers. Although they may participate in the decision-making process, the ultimate choice is left to employees.
4. Delegating = S4 (letting others do it): These leaders are responsible for their teams, but provide minimum guidance to workers or help to solve problems. They may be asked from time to time to help with decision-making.
Stages of employee development in situational leadership
Along with leadership qualities, Blanchard and Hersey defined four types of development for followers or employees:
1. Low Competence; High Commitment
2. Some Competence: Low Commitment
3. High Competence: Variable Commitment
4. High Competence: High Commitment
Blanchard and Hersey also suggest that each of the four approaches should be paired with different “maturity levels” among team members. For example, the lowest maturity level (M1) should work best with the “telling” style (S1), while the highest maturity level (M4) should be most responsive to the “delegating” approach (S4).
Differences between situational leadership and other leadership styles
The difference between situational leadership and other leadership styles is that situational leadership incorporates many different techniques. The style of choice depends upon the organization’s environment and the competence and commitment of its followers.
History of situational leadership
In 1969, Blanchard and Hersey developed situational leadership theory in their classic book “Management of Organizational Behavior.” This theory was first called the “Life Cycle Theory of Leadership.” During the mid-1970s, it was renamed the situational leadership theory.
In the late 1970s and early 1980s, the two developed their own styles. Blanchard’s first book, “The One-Minute Manager,” came out in 1982. Hersey further developed the situational leadership model in his 1985 book “The Situational Leader.” Both men have continued to refine and update their situational leadership theories.
Blanchard said situational leaders tend to choose between “directive behavior” (what and how) and “supportive behavior” (developing commitment, initiative, and positive attitudes). The maturity level concept for Situational Leadership II was revised to incorporate individual development levels.
Examples of situational leadership
Blanchard and his situational leadership collaborators have provided detailed case studies involving companies and public institutions. Prominent examples include Adobe, WD-40, Anthem Blue Cross Blue Shield, British Telecom, the city of Battle Creek, Michigan, Genentech, the San Diego Padres, and the Royal New Zealand Navy.
Any team environment that has frequent turnover provides an opportunity to apply situational leadership principles. Sports teams, for instance, represent clear examples of situational leadership because team rosters are constantly changing.
One president and two of the most successful coaches in college basketball history have attributed much of their success to how they adapted to changing players and circumstances.
Dwight Eisenhower
Dwight D. Eisenhower was the president of the United States after World War II. He was also the Allied Commander during the war. He was known for his diplomacy and his ability to get the allied leaders to work together to defeat the Nazi war machine. His background in the military taught him how to order and direct military exercises, and he needed to be a statesman not only to manage the strong personalities of the allied leaders, but to run for president and then win two terms of office.
Pat Summitt
Patricia Sue Summitt was the head coach of the Tennessee Lady Volunteers for over 38 years. Every few years, she was faced with building a whole new basketball team. Despite that, she ended her career with a 1,098-208 overall record as a basketball coach. She was named head coach for the U.S. women’s basketball team in the 1984 Olympics, where the team won a gold medal.
John Wooden
John Wooden was named the head coach of UCLA’s men’s basketball team. In his first eight years, he won three Pacific Coast championships. During that time he had team members graduate and new members start on the team. Beginning with the 1963-64 season, the team won seven straight championships.
UCLA’s record 88-game winning streak and string of championships ended in 1974. One of his quotes reflects his adaptive and situational leadership philosophy: “When you’re through learning, you’re through.”
Situational leadership quotations
How do professionals become better situational leaders? It might be helpful to consider these quotes from experienced leaders and apply them to your circumstances:
Margaret Wheatley : “Leadership is a series of behaviors rather than a role for heroes.”
Colin Powell : “Leadership is solving problems.”
Mahatma Gandhi: “I suppose leadership at one time meant muscles, but today it means getting along with people.”
John D. Rockefeller: “Good leadership consists of showing average people how to do the work of superior people.”
Margaret Thatcher: “You may have to fight a battle more than once to win it.”
John Wooden: “It’s what you learn after you know it all that counts.”
Situational leadership style requirements
Here are some of the characteristics of the situational leadership style:
Insight : The situational leader must be able to understand the needs of the followers, then adjust his or her management style to meet those needs
Flexibility : Situational leaders must be able to move seamlessly from one type of leadership style to another

Trust : The leader must be able gain his or her followers’ trust and confidence

Problem solving : The situational leader must be able to solve problems, such as how to get a job done using the best leadership style available

Coach : The situational leader must be able to evaluate the maturity and competence of the followers and then apply the right strategy to enhance the follower and their personal character
Advantages and disadvantages of situational leadership

Situational leadership does not work well in all circumstances. Let’s look at the advantages and disadvantages of the leadership style:
Situational leadership pros:

Easy to use: When a leader has the right style, he or she knows it

Simple: All the leader needs to do is evaluate the situation and apply the correct leadership style
Intuitive appeal: With the right type of leader, this style is comfortable

Leaders have permission to change management styles as they see fit
Situational leadership cons:

This North American style of leadership does not take into consideration priorities and communication styles of other cultures
It ignores the differences between female and male managers

Situational leaders can divert attention away from long-term strategies and politics
Benefits of situational leadership

“What is the best leadership style?” Hersey and Blanchard found it fruitless to provide one answer to this question. Everything depends on the specific situation, which is why they collaborated to develop the situational leadership model.

Situational leadership means “choosing the right leadership style for the right people,” according to Blanchard and Hersey. It also depends on the competence and maturity of the followers. This is a time in history when leaders look less like bosses and more like partners.

Sunday, April 28, 2019

FAIDA YA KUWA MWAMINIFU

Mtu kumwamini mtu inaweza kuwa ngumu sana. Hii inatokana na baadhi ya watu kutendwa vibaya na watu ambao awali walijenga imani kwao lakini walioamini wakafanya kinyume na vile walitarajiwa kuwa hapo awali.

Kadri miaka inavyokwenda jambo kuaminika kwenye jamii limekuwa likipungua kila siku, kuanzia kwenye mahusiano ya ukoo, familia, ndugu jamaa na marafiki, mahusiano ya kimapenzi, na mambo mengine mengi ndani ya jamii yetu Tanzania hata duniani kwa ujumla.

Watu wengi wamepoteza uaminifu sana kwa sababu ya tabia yakutokuwa waaminifu, mtu anaweza akapewa pesa, au akatendewa jambo Fulani lakini mwisho wa siku matokeo yake yanakuwa hasi ambayo ni kinyume na matarajio

Jambo limetokea hata kwenye ngazi za kitaaluma, makazini, hata kwenye maeneo ya dini ambayo kwa kifupi yalikuwa ni maeneo yaliyoaminiwa na kuaminika zaidi ndani ya jamii.

Yapo mambo mengi yanachangia hali hii kutokea lakini mwisho wa siku hitimisho lake ni kwamba tabia ni hali ambayo mtu akiiendekeza inaweza kuwa sugu na kuathili moja kwa moja mfumo mzima wa maisha yake.

Ubinafsi, kutokufanya kazi, mazoea, kuuma kwa roho unapotaka kurejesha fedha ya uliyokopa, kujiendekeza na tabia Fulani, ulevi, udokozi, maisha ya kijamaa kutawala, kutokuthamini kitu au jambo la mwenzako, ubabe, utani uliovuka mipaka, kukosa hekima na busara, ugumu wa mioyo na kuishi maisha bandia ambayo hayana uhalisia na maisha halisi ya kwako hivyo watu vile wanakutazama na uhalisia wako ni tofauti kabisa, kutokuwa wakweli na kutumia njia za uongo ili kukidhi haja ya mahitaji yetu.

Hizi ni baadhi ya tabia ambazo zimechangia kwa kiasi kikubwa sana kupunguza uaminifu kwa watu wengi bila kujua madhara ya kukosa uaminifu kwa watu, jamii hata maeneo ya kitaaluma na maofsini ambapo tunafanya kazi kwa kuajiliwa au kujiajiri.

KATIKA SOMO HILI TUTAJIFUNZA MATOKEO CHANYA YAKUWA MWAMINIFU KATIKA JAMBO LOLOTE.

Hakuna jambo jema kwa mtu kama kuwa mwaminifu yeye mwenyewe binafsi, kwa wazazi wake, watoto, kazini, kanisani/msikitini na kwenye jamii kwa ujumla. Zifuatazo ni faida za kuwa mwaminifu.

1. Kuaminika zaidi
Moja ya faida kubwa ya uaminifu ni jamii kukuamini, kazini, kwako au kwa wateja wako na kama wewe ni mfanyabiashara na ni mwaminifu kwa wateja wako, unafungua kwa wakati, unawahudumia vizuri kwa lugha mzuri na yakupendeza, bei sio za ubabaishaji, mtu akiacha pesa yake anaikuta, basi utajijengea idadi kubwa ya wateja kwa sababu ya uaminifu wako wao kwa wao watapeana taarifa zako,

2. Hujenga mahusiano imara na bora.
Ukiwa mwaminifu kwa jambo lolote lile lazima mahusiano yako na watu yatakuwa mazuri, iwe ni kazini, shuleni, kwenye nyumba za ibada, kwenye sehemu za mahitaji na sehemu nyingine nyingi hutasikia migongano na lawama kutoka kwa watu husika ambao labda unafanya nao kazi, bosi wako, walimu au wanafunzi, ndoa yako nk. Maeneo hayo yote yatakuwa bora na imara hivyo uaminifu ni jambo nyeti sana na ni vyema kulitilia mkazo na kulitimiza.

3. Huimarisha ushirikiano.
Mtu mwaminifu huwa na ushirika mzuri na watu wenzake, mfano wewe kama ni boss kuwalipa wafanyakazi wako kwa wakati, kutimiza ahadi zako au mzazi kutimiza ahadi unazoahidi kwa watoto au mke hii inatoa motisha na ushirika mzuri toka kwa wafanya kazi au kwa watoto kumfurahia baba au mama yao. Vile vile hata wafanyakazi wakitimiza kazi zao kwa uaminifu ushirika huwa ni mzuri kati yao na kiongozi wao. Na maeneo mengine ambayo sijayataja kama mifano hai kwenye maisha yetu.

4.Utapewa nafasi zaidi.
Hii hutokea kwenye jamii, makazini na hata nyumbani. Unapokuwa mwaminifu ndipo nafasi ya kupewa nafasi zaidi iwe ni kazini, nyumbani kwa wazazi basi nafasi hizo huwa ni kubwa na hata maeneo mengine mengi.

5.Utakula vya sirini.
Mtoto mtii na mwaminifu kwa wazazi wake hula vya uvunguni kwa sababu huyu mtoto hutekeleza majukumu yake kama mtoto vyema bila kusukumwa wala kubembelezwa na anajua wajibu wake. Ndivyo hivyo hata kwenye familia, jamii kwenye biashara, kazini  ni rahisi kushirikishwa mambo makubwa ya kiofsi kwa sababu wanajua wewe ni mwaminifu katika kutimiza, kutekeleza na kutunza siri za kampuni vyema hivyo ni rahisi kupata taarifa mapema.

6.Ni rahisi kusaidika.
Mtu mwaminifu huwa anatengeneza mazingira mazuri ya kupata msaada kwa haraka either wa kifedha, kimawazo au msaada wowote ule sababu kubwa ni ule uaminifu aliojijengea kwenye mazingira  yake ya maisha, iwe kwenye biashara, benki, nyumbani, kazini na maeneo mengine mengi ambayo yanamhusu.

7.Ni njia bora ya kuimarisha ndoa na mahusiano

Hakuna kitu kizuri kwenye mahusiano au ndoa kama uaminifu. Uaminifu ni ufunguo wa furaha ndani ya ndoa, ni ufunguo wa mafanikio na Uhuru wa nafsi, ufunguo wa kuyaona mahusiano  au ndoa yako ni ya maana kuliko zingine na kuongeza thamani ya penzi lenu ambalo litastawi na kuchanua vyema. Hivyo uaminifu kwenye mahusiano na ndoa ni msingi imara.

8. Utatetewa wakati wa Magumu au mapito.

Changamoto kubwa kwa watu ni kutokuimarisha mahusiano yao na watu wengine kwa njia ya amani, waonevu, wadhurumaji, kufanya mambo bila kujua kuna kesho ambayo inaweza kuwa na uhitaji wa wale watu unaowatendea ndivyo sivyo. Mtu mwaminifu hujiongezea nafasi ya kutimiza malengo yake kwa sababu ukifanya kwa uaminifu kwa watu basi watu hao hao kuna wakati watakuwa daraja lako la kufikia jambo Fulani maishani mwako, katika uonevu utapata watetezi wengi.

9. Mtu huishi kwa amani na furaha.
Mtu mwaminifu huishi kwa furaha, amani lakini pia huwa na upendo, hapendi kuiona nafsi yake ikisononeka, ikiumia kwa kuidhurumu kwa kukosa uaminifu, hupenda kutenda jambo kwa wakati na uaminifu kwa wengine. Kutokana na kufanya mambo hayo kwa uaminifu basi moyo na akili yake hubaki huru bila deni maana amefanya kila jambo kwa wakati na uaminifu.

10.Uaminifu ni dawa
Huondoa msongo wa mawazo, humfanya mtu kuwa huru asiye na hatia, kumbuka mtu asiye mwaminifu huishi kwa uongo, muda wote anatengeneza mazingira ya kuutetea uongo wake na kuuhalalisha bila kujua kuwa anajiumiza binafsi, anatumia nguvu nyingi kupanga namna ya kudanganya wakati kama angeamua tu kuwa mwaminifu nguvu ile ile  angetumia kwa ajili ya kufanya jambo lenye maana maishaini

Kwa hiyo ni vyema kutengeneza mazingira ya kuaminika na wazazi, watoto, mke, mume, jamii, na katika maeneo yote unayokuwa.
Kwa sababu uaminifu hutengeneza mahusiano mazuri na kuaminika na watu, na kama basi ikitokea kuna fursa inatokea watu watakufikiria na kukupa nafasi.
Prepared by..
Moses Zephania Mgema
0715366003/0755632375
Email mgemamoses@gmail.com
Dar es salaam, Tanzania

Saturday, April 20, 2019

Nianze kwa kukunukuu moja ya maneno ambayo yamewahi kusemwa na Raisi wa Marekani Bwana Abraham Lincoln kwamba " *-

Great mind discuss ideas, Average mind discuss events and Small mind discuss people "-*

Maana yake ni hii " Akili kubwa hujadili mawazo, akili ya wastani hujadili matukio na akili ndogo hujadili watu" mwisho wa kunukuu.

Nukuu hii nimeikumbuka leo baada ya kukutana na vijana Fulani ivi ambao kwa kweli ni vijana wenye nguvu, wadogo na wenye fursa za kuwafanya kuwa na maisha mazuri yanayotegemea utendaji wa kazi, ufanisi, maarifa, ujuzi na utayari wa kufanya kazi bila woga wala mashaka.

Tunapoizungumzia dunia hii leo, imekuwa ni dunia ya ajabu sana kwa sababu ukiangalia kuna baadhi ya watu wake kwa waume wanapambana kuhakikisha wanafikia malengo, ndoto na kuishi maisha mzuri ambayo yanwapa fursa ya wao kufanya jambo lolote kwa sababu ya uhuru wa kifedha ambao wanajua kuwa njia sahihi ya kuishi maisha hayo ninkipambana had I tone LA mwisho lengo kutimiza malengo yake.

Tunapozungumzia hali ya maisha lakini kuna wengine kila Saa na kila

Thursday, April 18, 2019

KUJIFUNZA NI SAFARI YA MAISHA YOTE YA MTU DUNIANI.

Tembea uone, usipotembea unaweza ukifiri kwamba maisha ya eneo unaloishi ni sawa na maisha ya watu wengine ambao wako maeneo mbalimbali ya dunia hii au wakati mwingine unaweza kufikiri kwamba sehemu unayoishi labda mna maisha duni kuliko maisha ya maeneo mengine ambayo huwa unasimuliwa na kupewa stori za huko au pia ukahisi maisha yako na jamii inayokuzunguka ndo mahali sahihi zaidi kuliko mahali pengine.

Ukitembea utajikuta unajifunza mambo mengi sana ambayo kwa ufupi yanakufanya ujue namna nyingine ya maisha ya watu, utamaduni, namna wanavyoadress matatizo, ushirikiano, mitazamo pamoja misingi halisi ya maisha yao.

Zipo stori nyingi sana duniani ambazo kwa ufupi ndizo zinazoyafanya maisha kuwa hasa ni completed circles ya maisha yetu ya kila siku bila kujal unaishi kwenye kusudi la maisha yako au kwa namna yoyote ambayo umeamua kuchagua kuishi.

Mchanganyiko wa maisha haya yanatufanya tujitenge sisi kwa sisi kutokana na levels za kielimu, kiuchumi, kisiasa, kiimani, kimitazamo na fikra. Hivyo kila mmoja wetu kufanya analoona jema analitenda ili kuifanya nafsi yake itulie na kujisikia Amani.

Wakati watu waliofanikiwa wakiwaza namna gani wataendelea kupaa na kuondoka mahali walipo, wanawaza, kuongezeka kwa fedha benki, majumba ya kibiashara, nk, Msomi mwenye kujua maana ya shule nae ataendelea kuhakikisha elimu yake inapaa juu sana ili kukidhi hitaji lake la kuwa na elimu kubwa.

Maisha yanaendelea, watu wa dini na imani nao huwa wanahakikisha kuwa wanafanya vizuri kwenye suala la kiroho huku wakitimiza matakwa kanuni na taratibu za ibada ambazo ndo fungu lao, muda wote watasoma neno, kuomba na kuwaza juu ya ufalme wa Mungu namna gani ataujenga na kuwa mwenye kufanya kusudi lake kwa kadri ya wito na utayari ndani.

Wapo wanasiasa, wanafalsafa, wanaharakati, na watu ambao wanapambania haki, maendeleo lakini pia kutengeneza mazingira ya wao kuonekana bora zaidi ya mwingine na mambo mengine mengi yahusuyo, itikadi, mila, taratibu na kanuni za vyama vyao.

Watu wengi wasio nacho either wanatokea kwenye makundi ya kijamii anabyo nimeyataja hapo juu lakini nimekuja gundua ni watu wenye upendo sana kwa wao kwa wao na hutiana moyo nyakati zote za furaha na nyakati za huzuni wakiamini kuwa hilo ni fungu lao.

Lakini inapokuja kwenye suala la usawa wa kiuchumi na maendeleo watu hawa wamekuwa ni watu wenye wivu, chuki na wenye kutamani siku moja kuona waliofanikiwa wakianguka chini ili kuwa sawa. Ndiyo maana mtu tajiri au aliyefanikiwa kwa kitu chochote kwenye maisha anapokwama maneno mengi huibuka mitaani hasa kutoka kwenye kundi la watu wa chini.

Ipo mifano mingi ambayo inaweza kukufanya ukaelewa nini nataka ujifunze hapa, mfano tulipokuwa shule watoto wengi sana tulipenda kuona yule mwenye uwezo darasani anashuka na kwel walikuwa wakiteleza stori inakuwa kubwa huku akinenewa mabaya, anajifanyaga sana huyu, anajipendekeza kwa walimu, mbinafsi, na hata akiongoza tulikuwa tunaamini anapendelewa na kubebwa na walimu ajabu sana .

Mtu mwenye Mali, uwezo akipatwa jambo baya asilimia kubwa watatengeneza scenario mbalimbali mbaya lengo ikiwa ni kuhakikisha nafsi zao zinafurahi kwa anguko lake hilo, utasikia kwanza alikuwa mwizi mzurumaji, muuji mtoa kafara na maneno mengi ambayo ukiyafuatilia kiundani hakuna maana hasa ndani yake.

Juzi hapa mahali nakaa tulipata changamoto ya nyumba ile kuuzwa na bank na utaratibu uliotumika haukuwa mzuri kwa sababu idhinisho la mahakama lilikuwa bado halijafika kwa aliyekuwa mmiliki halali wa nyumba, kwa tukio hilo kulikuwa na maoni mengi hasa toka kwa majirani, ukitazama watu walioumizwa na tukio hilo ni wale wenye nafuu ya maisha na baadhi yao walitoa machozi lakini wenzangu na mie ndo walishadadia kweli kweli kiasi unahisi kuna uadui kati ya hawa watu.

Sio kwamba matajiri wote wanaroho ya huruma na nzuri hapana ila tunatazama kwa asilimia kubwa.

Wala sio kila mtu masikini anashida hiyo hapana wengine wapo wenye upendo mzuri lakini asilimia kubwa anguko la mtu aliyefaniwa kiuchumi, kwa aina yoyote anapoanguka watu wengi sana wa chini hufurahi na kuzusha maneno mengi kama alikuwa anajidai, analinga ana majivuno nk.

Kwa njia hii
>Mtu mwenye chuki na wivu wa ubaya sio rahisi kufanikiwa sana.
>Masikini wataendelea kuwa masikini kama hawatabadili mitazamo yao na kuwa na imani potofu ya kuwa kila aliyefanikiwa anatumia vitu Fulani.
So is better to learn to appreciate for those who have already achieved and reached their dreams.

This will help poor people to have desire of working hard, learning from successful people and sometimes to pass on where successful people passed.

It gives an open space to the mind which brings easy way of cultivating ideas and coming with a clear solution, ways on how to move forward heading to the destination of our dreams.

Moses Zephania Mgema
0755632375/0715366003
mgemamoses@gmail.com
mosesmgema12.blogspot. com
Dar es salaam - Tanzania

AIBARIKI KAZI YA MWENYE BIDII.

Aibariki kazi ya mikono yako wewe mwenye bidii, hii ni ahadi ya Mungu kwa kila atendae kazi kwa nafasi yake.

Pamoja hayo yote kwa maana ya ahadi za Mungu ambae ndiyo muumba wetu bado iko haja ya kila mtu kujitathimini kama kweli nafasi aliyo nayo anaitendea haki sawa sawa na kusudi la kuumbwa na kuwekwa duniani.

Kwa kazi ya mikono yako yenye ufanisi wa hali ya juu kwa maana ya innovation, creativities, passion and love of it, daily learning kwa lengo la sustainability ndiyo misingi ya kufikia malengo na maono yako bila kujali muda ambao utafikia kwenye kilele cha matokeo yako.

Changamoto ni nyingi njiani kuliko wepesi kwa sababu inaamini kuwa kitu chochote kizuri kinahitaji maarifa mengi, ujuzi, uvumilivu, kwa maana ya njia tupitazo ni ngumu na zenye kusongwa na changamoto na vikwazo vingi.

Wengi waliofanikiwa kwenye mambo yao, kwa maana ya wafanyabiashara, wasomi, wachezaji wa michezo yote, waimbaji, na kwa kila kazi ambayo mtu amefikia kilele cha mafanikio basi hapo mwanzo alipambana sana huku akiweka uvumilivu na imani kubwa ya kwamba ipo siku atafikia malengo yake.

Huku njiani kuna mambo mengi sana mfano kuna watu wanakutia moyo sana na wanatoa semina bomba zenye kuinspire na kumotivate kwamba yeye kama ametoboa basi hata wewe unaweza, lakini ya wezekana mtu yule yule baada ya kumfuata na kuhitaji japo wazo jema alikujibu au kukutendea tofauti na ukivyotarajia, kuna ndugu yako ulimtegemea na alikuahidi jambo Fulani ukitimiza mambo Fulani yawezekana umetimiza yote lakini tena kwa kutumia gharama na akiba yako yote ukijua kuwa kuna support ndogo itafanyika mahali utakapopelea lakini mwisho wa siku yule MTU amekuangusha.

Kuanguka ukiwa unakimbia sio jambo la kushangaza kwa sababu unakuwa kwenye mwendo wa speed na mzunguko wa damu unakuwa juu sana ukilinganisha na ukiwa unatembea au umetulia mahali. Hivyo inuka jikung'ute endelea na mwendo.

Hata safari ya kuikimbilia ndoto na kusudi la Mungu kwako, kuna kuanguka, kuumia na kupoteza kabisa lakini usikate tamaa, no turning back utakuwa mke wa Luthu ambae aligeuka na kuwa nguzo ya chumvi.

Iko misemo na maneno matamu sana kwenye dunia ya Leo yenye kutia moyo, lakini yenye kuumiza ambayo ni machungu neno moja tu ulishike SITOKATA TAMAA.

Usikatishwe tamaa na maneno ya watu kwa sababu kusudi la kuumbwa kwako lazima litimie pambana iamini ndoto na uwezo mkuu ndani yako.

Fanya kwa nafasi yako kwa viwango vya ubora na uwekezaji wa nguvu, maarifa, ujuzi na kila kitu kinachohitajika kufanywa na wewe Fanya halafu Mungu anajua namna ya kufanya juu yako.

Jua kila kazi ufanyayo iwe kwa kutumia kipaji, kazini, unafanya biashara mlengwa mkuu ni mtu, hivyo Fanya huku ukiposition wewe kwenye nafasi ya mteja, msikilizaji wa nyimbo yako mtazamaji wa mpira unaocheza nk. then ujiulize je ingekuwa ndo Mimi natazama au nasikiliza ningeenjoy kazi hii ?

Usifanye kazi kama by the way Fanya hiyo kazi kama hutofanya tena hata kama una malengo ya kybadilisha hapo mbeleni.

Usiwaze matokeo ya kazi wakati hujaweka mikakati ya kuona hayo matokeo unataka uyapate, cha msingi waza matokeo hayo huku ukitimiza michakato ya kufikia huko kwa kufuata michakato sahihi na kwa uaminifu.

Kuwa na Imani na kazi yako lakini kumbuka imani bila matendo matokeo yake yanabaki kuwa ni zero.

Love, be patient, care, corporate with others, Think about the consumers before you serve or release your work hapo utajijuta una fly like Eagle kwa sababu utakuwa umetimiza majukumu yako.
Kila mtu Leo anapambana sana kuhakikisha afanikiwa na kuwa boss au mweshimiwa, hakuna mtu anataka kuwa mtumwa, wa mtu mwingine hivyo pambana kwa kadri ya nguvu zako.
Kazi rahisi itakupa matokeo rahisi, kazi iliyobebwa na umaanisha mkubwa ndani yake itakupa positive results.
Hakuna uchawi wala uganga kwenye mafanikio mchawi ni mimi au wewe hasa pale unaposhindwa kutimiza majukumu yako sawa sawa.

Moses Zephania Mgema
mgemamoses@gmail.com
mosesmgema12.blogspot. com
0755632375/0715366003

Monday, April 15, 2019

Acha matokeo ya kazi yako yakuelezee wewe ni nani. Dunia ya leo imejaa watu wengi wa aina mbalimbali, kuanzia namna wanavyoishi, wanavyofikiri, mitazamo mpaka utendaji wa mambo ndani ya mzunguko wa maisha wa kila siku.
Katika kupambania ndoto malengo na utendaji wa kazi, biashara na mambo mengine ambayo yanaikutanisha jamii kunekuwa na watu wenye fikra njema na wengine wenye fikra mbovu na mitazamo mibovu kitu ambacho kimeacha majibu ya changamoto ndani ya box ambalo kila mtu anaogopa kulifungua.

Sunday, April 14, 2019

INJINI YA MAFANIKIO NI INTERACTION/ KUCHANGAMANA

Kutokana na kuishi kwenye dunia huru kila mtu ana aina ya maisha ambayo amependelea kuyaishi kwa Uhuru na uchaguzi ambao yeye binafsi ameona kwa njia hiyo basi ni sahihi.
Hata mimi, wewe na yule kila mmoja ana aina yake ambayo anaitumia kuendesha maisha yake.
Pamoja na kuwa na Uhuru wa maisha na uchaguzi wa mfumo wa maisha ambao kila mtu amependelea lakini sio kila mfumo ni sahihi sana kuishi bali wakati mwingine ni mbaya sana
Kuna watu wanapenda sana kuishi maisha ya kuchangamana na watu, wako huru kushirikiana na kila mtu, watu wanaamini katika nguvu ya umma na ushirika na wenzao.
Lakini kuna watu ambao ni wakimya sana na ni watu ambao wao kuchangamana au kuwakuta wakipiga stori na kushare mawazo na wenzao ni ngumu sana
Na Mara nyingi husema wanaishi maisha yao hawataki mtu afuatilie maisha yao. Lakini kiuhalisia maisha ya kujitenga na watu kwa mtu mwenye malengo na nia ya dhati ya kufikia ndoto zake lazima achangamane na watu.
Hii inafaida nyingi sana kuliko kutengeneza mazingira ya kuwa mkimya na kuishi maisha yako binafsi.
Watu wengi wanatafsiri vibaya sana baadhi ya maneno kama ambavyo nitaelezea hapo chini
1. Hekima
Watu wengi sana wanaamini kukaa kimya ndiyo hekima na busara, lakini kumbe hiyo sio hekima wakati mwingine ni kwa sababu ya ujinga, kiburi, majivuno na kukosa uelewa wa mambo mengi yanayohusu jamii. Kwa hiyo si kila mtu mkimya ni mnyenyekevu na mwenye busara.
2. Imani
Kuna imani zimejengeka kwenye jamii nyingi kwamba, ukimya nao ni jibu ni kweli. Lakini je hilo ni jibu sahihi au ni tango pori kwa hiyo wakati mwingine ni vema kusema ili kujisaidia wewe binafsi ila pia kumsaidia mwingine.
3.Hakuna mtu anaweza kuishi pekee yake.
Tunategemeana sana kwa mambo mengi, sijui umewahi kujiuliza huwa unaenda kazini kumfanyia nani kazi, je ni boss, wanyama au kuna walengwa wa kazi unayoifanya wanatakiwa kupata huduma yako.

Hapo jiulize sasa kwamba ni namna gani unaweza kuishi maisha yako bila kuwashirikisha wengine ?. Jibu rahisi kwamba hakuna mtu anaweza kuishi maisha yake pekee yake Bali tunategemeana.

Tunaendelea.............
Kuna aina ya maisha baadhi yetu tuliamua kuyaishi tangu tukiwa watoto kwa kulazimishwa na wazazi ndugu jamaa wa karibu, walimu na walezi wetu au hata baada ya mtu kukua anaamua kuishi maisha Fulani anayo yapendekeza yeye hata kama sio sahihi.

> kutokucheza na watu wa familia kadhaa kutokana na levo za maisha.
> Kuaminishwa imani Fulani hasa kwenye masuala ya imani, kwamba siwezi kucheza au kula kwa kina Jose kisa wao ni wakristo na Mimi ni mwislamu na kinyume chake.
>Wazazi kuwatenga watoto wao na kuwasimamia na kuwaondolea fursa ya kucheza wakiamini wanawapa malezi bora kumbe wanaua uwezo wa watoto wao na mengine mengi.

Social Interaction/Mchangamano ndani ya jamii ni muhimu sana.

Kama tulivyoumbwa toka mchakato wa kupatikana kwetu ulihusisha ushirikiano kati ya watu sio mtu na wewe au Mimi nikapatikana

Simpo kabisa kwamba binadamu aliumbwa kwa ushirika na ushirika una nguvu kubwa iletayo ushindi kwa mtu binafsi lakini pia kwa jamii.

Kuna faida nyingi na kubwa mno kwenye kushirikiana na wenzako mfano, kucheza pamoja, kupiga stori, kujiweka karibu na wenzao hii inakujengea uwezo wa
1. Kujifahamu zaidi
2. Kuwafahamu wengine
3. Na kufahamu zaidi mfumo wa maisha uko vipi kuanzia ngazi ya chini mpaka huko duniani.

Kupitia social groups interactions kuna elimu kubwa ambayo wakati mwingine huwezi kuipata ukiwa nje ya makundi haya ya kijamii. Mfano niliwahi kusoma historia ya moja ya matajiri hapa nchini kwamba pamoja na kwamba alianzisha biashara yake yeye kama yeye lakini amekuwa akipata mawazo mazuri sana kupitia kwenye makundi ya kijamii kama kwenye vijiwe vya kawaha na maeneo mengine alisema kwamba.
Alichogundua yeye watu wa chini huku mitaani wana mawazo mazuri sana ukilinganisha wakati mwingine na mawazo mengi yaliyopangiliwa kwenye vitabu wakati mwingine huwa na uhalisia wa maisha ya mbele zaidi ukilinganisha na stori za vujiweni vinavyogusa maisha halisi ya watu ambao wakati mwingine ndiyo wateja au walengwa wa huduma za kibisahara.

Changamoto kubwa ambayo vijana wengi tunapitia ni ile hali ya kujifungia kwenye mitazamo na mifumo Fulani ambayo kwa namna moja ama nyingine inatuua tukidhani kwamba tupo sahihi.
Mfano mtu anafungua Instagram account anaweka private, kila jambo binafsi ukifuatilia undani wa hiyo private eti hataki mazoea inasikitisha sana.
Kila mmoja ana Uhuru wa kufanya anachoona ni sahihi kwake na maisha yake lakini kama hakuna sababu ya kujitenga na wenzako kwa nini ujitenge kisa tu ulimwona Fulani kaweka private na wewe ndiyo hivyo tena.

Watu kama hawa unakuta anafanya hivi akiwa chuo anapomaliza chuo basi ameanzisha biashara Fulani ndo anaanza kujipendekeza kwa watu na kuwalazimisha wakati mwingine wamfollow kisa tu ameanzisha online business.

Je watu wakivunga utasema unalongwa kumbe wewe ndo mchawi wa hiyo online business au hata huku kwenye jamii husalimii majirani kwa lugha rahisi unafunga vioo ukifungua duka basi unaanzisha ushositito wasiponunnua eti wana wivu yako huyakumbuki, unajitia msamalia mwema na kuwatangazia wakati ulikuwa unawaona  mawe tu hapo kabla.

Unakuta mtu yupo kwenye group la whatsup ambalo hata hakuungwa alijiunga mwenyewe kupitia Link lakini mtu huyo, ni kimya, hachangiaji chochote, hata kuitikia salaam, au kusalimia au mtu kapositi hata kupongeza au kukosoa hakuna kimya tu. Unajiuliza je huyu mtu yupo hapa kwa bahati mbaya au shida ni nini.
Ukimuuliza atakuambia niache na maisha yangu lakini wakati huo yuko ndani ya group huo ni ushamba na kutokujutambua.

Maisha yetu ni ushirika, kushare ideas, having funs na mambo mengine kitu ambacho kina leta faida na manufaa kwenye kazi hata afya kiujumla.

Kuna faida za kuchangamana na makundi ya kijamii japo si kila kundi au group ni sahihi.
1.Inatengeneza connection na watu wapya.
2. Kujua tabia za watu, hii inakupa fursa ya kujua ni watu gani sahihi wakuambatana nao.
3. Ni rahisi kugundua uwezo wako kwa maana ya kipaji ambacho kinaweza kukufanya kufikia ndoto na malengo yako.
4. Kupitia socializations una nafasi kubwa ya kugundua fursa mpya za kibiashara, maana kupitia mazungumzo utagundua mahitaji ya watu lakini pia changamoto ambazo unaweza kuzigeuza nakuwa fursa kwako.
5. Ni rahisi kupata social support unapokuwa na jambo lako au unapoanzisha kitu chako, maana wateja au watazamaji wa kipaji chako kama wewe ni mwimbaji au unakipaji chako.
6. Ni platform ya kujitangaza na kuimbia dunia kuwa wewe ndo unahitajika kwa jambo Fulani.
7.Nafasi ya kujifunza kila siku vitu vipya.
8. Nafasi ya wewe kujijua, maana wakati mwingine tunajijua kupitia watu. Hivyo inapelekea kujua nguvu na udhaifu wako.
Note.
Hizi ni baadhi ya faida ambazo mtu anaweza kuzipata pale anapokuwa ni mtu wakushirikiana na wenzake ndani ya jamii.
Lakini pia kuna faida za kiafya maana kupitia interaction unajifunza mengi, lakini vilevile unaweza kuwa unapitia changamoto Fulani kwenye maisha lakini unapokuwa mchangamanaji kwenye jamii unaweza kujikuta unakutana na watu ambao wamewahi kupitia changamoto kama yako na wakavuka.
Hivyo kupitia shuda hizo unaweza kupata nguvu na imani kwamba kumbe hata wewe unaweza kutoka hapo.
NB.
Pamoja na faida nyingi lakini fahamu kuwa si kila social groups lazima uitaract nao, tazama makundi yenye faida.
Sio kila page ya Instagram, group la whatsup ujiunge eti kisa umeambiwa na Moses uwe na social groups interactions, tafuta groups, na hudhuria semina zenye manufaa kwako.
Ipo nguvu kwenye ushirikiano, na hakuna mtu anaweza kuishi mwenyewe kama yupo jangwani.
Maisha yetu ni ecology kwa maana kwamba tunategemeana, ukianzisha biashara mlengwa ni binadamu, unapoamka kwenda kazini mlengwa ni binadamu nk.

Moses z. Mgema.
0715366003/0755632375
mgemamoses@gmail.com

MAARIFA KWENYE KARNE YA 21 NI MSINGI WA MAFANIKIO YAKO

Nimekuwa na muda mzuri sana wa kujifunza kila siku, na hayo yamekuwa ni maisha yangu sasa, na kupitia aina hii ya maisha nimejikuta binafsi nikipata nguvu na imani kwamba kwa kila jambo lina sababu ya kuwa mahali popote lilipo.
Kujifunza kama ambavyo waandishi wamekuwa wakiandika nami naungana nao kwa kusema: Kujifunza ni mchakato endelevu kwa yeyote ambae anaendelea kuishi.
Na tunajifunza kupitia mazingira yanayotuzunguka na Yale mapya tunayokutana nayo kila muda tunaopata tukitoka nje ya maeneo yetu tuliyoyazoea.

Kupitia kujifunza huku, tunawezesha akili zetu kushiba na kuwa na afya ya maarifa ambayo kwa namna moja ama nyingine maarifa hayo yakitumika vyema ndiyo yanayoweza kubadilisha mfumo mzima wa maisha ya mtu kutoka vile alivyo, namna anavyotazama, fikiria, kiwango cha kuamini kuwa alipo yawezekana si mahali pake lakini pia kupitia maarifa anaweza gundua kuwa ndani yake kuna uwezo wa ajabu kiasi kwamba akiamua kuutumia vyema unaweza kumpeleka mbali zaidi maishani.

Niliwahi kusikia msemo maarufu nchini Tanzania kuwa: " UKITAKA KUMFICHA JAMBO MTANZANIA BASI WEKA KWENYE MAANDISHI UTAKUWA UMEMALIZA KILA KITU" maneno haya sio mazuri sana kwa sababu yanajaribu kuelezea udhaifu wa watanzania wengi kuwa hatupendi kujifunza kwa Uhuru labda kwa shuruti kama inavyofanyika kwenye mfumo rasmi wa Taaluma ambao ni haki ya kila mtanzania kupata elimu hiyo.

Lakini kwa mtu ambae amekubali kuyafanya maisha yake kuwa ni yakujifunza kila muda, mtu wa namna hii huwa anakuwa na nguvu na uwezo mkubwa wa kufanya mambo yake kwa sababu

1. Maarifa hujenga uwezo wa kufanya mambo kwa ufasaha hasa kwenye eneo husika.
2. Maarifa hujenga imani na kujiamini.
3. Maarifa huvumbua fursa zilizojificha.
4. Hujenga uwezo wa kufikiri zaidi.
5 unaufanya ufahamu wa MTU kuwa updated muda wote na active
6. Kujua mahitaji ya wakati uliopo na kuweza kuitabili kesho.
Hizi ni baadhi ya faida ambazo mtu anaweza kuzipata kama tu amedhamiria toka ndani kuwa maisha ya kujifunza yawe ni maisha yake.

Niliwahi kusoma kitabu kimoja hivi kilichoandikwa na Brian Trace kinaitwa "NO EXCUSES" niligundua mambo mengi sana ambayo yamechangia watu wengi kuishi maisha ambayo hayawastahili Kati ya mambo makuu niliyojifunza kupitia kitabu hicho ambacho pia kilibadili kabisa mtazamo wangu ni
1. Kuishi kweye sababu.
2. Kuamini mtu alipo ni kwa sababu ya mtu Fulani.
3. Kutokuwa na nidhamu binafsi nk.

Pamoja na kusoma kwa undani niligundua kuwa maisha ya mtu yapo ndani ya mtu mwenyewe bila kujali umekulia mazingira yapi as long as umeshakuwa mtu mzima na unaafya njema basi wewe ndiye utabaki kuwa mwamzi sahihi wa maisha yako au mwamzi wa maisha yangu.

Kufeli, kutokwenda shule, wazazi kutokuona umuhimu wa jambo Fulani yaani elimu nk, bado haiondoi uhalisia kwamba maisha ya mtu yako ndani ya maamzi yake mwenyewe.

Watu wengi tumekuwa wavivu sana kwa mambo mengi, kuwaza, kujitoa kuanzisha shughuli ndogodongo kama kuuza matunda, kuuza bidhaa zilizo na uwezo wa kuwa na mtaji mdogo badala yake tunawalalamika au kuwalalamikia wengine

Wengine wamepata nafasi ya kufanya kazi, kujiajiri kwa kazi zao lakini wamekosa nidhamu ya kazi yao, wanachelewa kwenda kazini, wanafanya kazi kana kwamba wamelazimishwa kufanya hivyo, hawana upendo na kile wanachokifanya mwisho wa siku ubora au ufanisi wa kazi umekuwa mdogo kitu kilichopelekea kupoteza ajira zao au hata biashara zao kufa.
Nidhamu mbovu juu ya vipato vyao kitu kinachopelekea mtu kuonekana ana kazi au biashara lakini hatua ya maendeleo iko pale pale kila mwaka unapopinduka ajabu sana.

Lakini kumbe chanzo cha haya yote ni ukosefu wa elimu na maarifa ya namna gani yakufanya ili kwa kila jambo ambalo mtu anafanya liweze kuwa endelevu na lenye kumfanya apige hatua ya maendeleo yake binafsi lakini pia familia.

Pamoja na kwamba ukisoma vitabu vingi sana hasa hizi inspirational books unaweza jikuta unaona ni kama umechelewa, au uone kumbe kufanikiwa ni rahisi, lakini kuna umuhimu wa kujifunza maana mazuri ni mengi kuliko mabaya kupitia elimu.

Tuwe ni watu wakujifunza, kupitia kujifunza utapata shuhuda za watu waliofanikiwa, utaongeza ujuzi na maarifa mapya juu ya kazi au biashara unayofanya na unaweza kuiboresha zaidi.

Utapata mbinu mpya za namna ya kufanya kazi zako lakini pia kama ni biashara unaweza gundua vitu vipya ambavyo kwenye mazingira yako havipo na wewe kuwa mwanzilishi wake.

Kwa hiyo kujifunza jambo nyeti na muhimu sana kwenye maisha yetu hasa kama unataka kufikia ndoto na malengo yako, tunafanikiwa kwa kuangailia wengine walifanya nini.
Elimu ina transform namna yakuwaza, kufikiri na namna ya kutenda.
Note.
Kusoma sana vitabu au kupata muda mwingi wa kujifunza na kuhudhuria semina za wajasirimali haimanishi kwamba ndiyo tiketi ya mafanikio hapana.
Kujifunza na kupata maarifa ni jambo moja lakini utekelezaji wa maarifa hayo ni jambo LA muhimu zaidi na hilo ndilo linaweza kuwa ndo msingi na ngao ya ushindi wa maarifa hayo.

Maarifa na ujuzi bila utekelezaji wake ni sawa na kukubaliana na msemo wa wahenga usemao, "PENYE MITI HAPANA WAJENZI"
JIFUNZE+ WEKA KWENYE UTEKELEZAJI = MAFANIKIO
Mungu ayape nguvu maono yako kwa nguvu unayoitumia kuhakikisha unafikia malengo yako.

Elimu ni mtaji wa kila jambo

Moses z. Mgema
0715366003/0755632376
mgemamoses@gmail.com
Dar es salaam, Tanzania