Monday, November 30, 2020

ELIMU NI MASTER KEY 4

Kila mmoja amezaliwa na uwezo wa asili (Natural ability) lakini wakati mwingine ni ngumu kujijua na kujua thamani ya kile ambacho tumkibeba ndani yetu...

Kipaji ni ni kifurushi kamili (complete package) ambacho tunapaswa kukitengenezea mazingira mazur ya ustawi wake. 

Katika nchi za magharibi kupitia elimu wamewekeza kwa kiwango kikubwa kwenye uwezo halisi wa mtu ndiyo maana kiwango cha ubora katika mambo mengi wanayofanya iwe katika mambo ambayo tunayaona ni kama kazi zinazoshusha hadhi kwa upande wa nchi za dunia ya tatu.

Wenzetu wanajal sana passion ya mtu kuliko matamanio yetu, ndiyo maana tunaweza kuona hata malezï na makuzi ya watoto hufuatiliwa kwa karibu sana lengo ikiwa ni kugundua ubora na uwezo wa mtoto kupitia michezo ambayo anaifanya kila siku.

Pamoja na kwamba dunia tuliyo nayo imekuwa ni dunia bize sana kwa maana ya wazazi na walezi kutingwa na kazi, lakini pia hata kwa muda mchache wamekuwa wakitoa muda wao kwa ajili ya kuwa karibu na watoto wao, lengo kubwa ni kufanya ugunduzi wa mtoto/watoto wao ni kina nani.

Utambuzi wa vipaji na passïon imesaidia kwa kiwango cha juu kuwapeleka watoto wao kwenye nafasi wanazo fiti kwa kiwango cha juu sana.

Ndiyo maana sasa unaweza kuona kuna watoto wanakwenda shule kupata elimu ya kawaida ambayo kila mtu ni haki yake, lakini bado wana muda wakufanyia mazoezi na kujifunza kwenye eneo la passion zao.

Mfano mzuri ni kwa mcheza mpira wa chini ya miaka 17 Kelvin John ambae alipata nafasi ya kwenda Ubelgiji kwa ajili ya kuendeleza kipaji cha mpira, lakini bado walimpeleka nchini England kwa ajili ya kuendelea na elimu ya kawaida lakini vilevile kupata muda mzuri wa kujifunza kwa ubora namna ya kuboresha na kukipa thamani kipaji chake.

Mtoto akiwekezwa kwenye eneo la uwezo wake na passion yake humfanya kutimiza majukumu yake kwa upendo, na kwa moyo wote kwa sababu anachokifanya sio kazi tu bali ni eneo linalompa furaha pia, hivyo hata kama kazi itakuwa ngumu kiasi gani bado ataendelea kufanya kwa sababu kwanza anapenda, anafanya kwa passion kwa hiyo kiwango cha ubora katika kazi hiyo kitakuwa cha kiwango cha juu sana.

Baadhi ya wazazi wanapenda na wanataka watoto wao kuwa madaktari, wahandisi, nk, lakini mtoto unakuta anataka kuwa mchoraji, mwalimu, au kuwa yeye kwa kile anakita tusiwanyime au kuwazuia kufanya wanachokipenda bali kama unaona mwelekeo au uchaguzi wa mtoto sio sahihi kwa maoni yako mshauri kwa upendo na kumweleza matokeo ya kile anachopenda kuwa haiwezi kumpa future nzuri.




ELIMU NI MASTER KEY 3

Elimu ni ufunguo ambao unatakiwa kutumiwa kwa ajili ya kufungua kila mageti na milango ya fursa kuanzia mtu binafsi mpaka kwenye mazingira ya nje...

Elimu ya kumfanya mtu kujielewa/kujitambua na kuelewa mazingira yake. Mungu ameumba kila mtu na kumpa uwezo na nguvu ya kujitawala, kujimiliki na kuyamudu mazingira yake.

Hivyo kitu ambacho tunapaswa kufanya kwenye mfumo wa elimu yetu, hata kama mitaala ya elimu rasmi bado haujabadilika ni vyema kutumia mifumo mingine ya elimu ambayo inatuwezesha kuwa na uelewa mpana zaidi wakujifahamu.

Elimu isiyo rasmi ipo kila mahali, kuanzia kwenye mazingira tunayoishi, kupitia mitandao ya kijamïï, websites, vitabu na vyanzo vingine vya maarifa ambavyo upatikanaji wake umekuwa rahisi sana.

Hivyo ni vyema kutumia uwepo wa teknolojia kubwa tuliyo nayo kwa sasa hapa duniani ambayo imetusogeża karibu zaidi na wenzetu waliotutangulia katika maendeleo na elimu ya kujitegemea.

Kuendelea kulaumu serikali ni kujichelewesha kufikia malengo hivyo kubaki kwenye maumivu, na lawama ambazo haziwezi kutatulika bila kuchukua hatua.

ufahamu ni jambo la msingi sana katika kufikia hatima na malengo ya kila mtu.
Tuna vipaji, vipawa na karama kubwa ndani yetu ambavyo ni uwekezaji wa Mungu kwetu.. 

Next epsode tutaangalia kwa mfano namna ambavyo tukiongeza maarifa kupitia namna nzuri ya kujifunza tunaweza kuona ni kwa kiwango gani vipawa vyetu vinaweza kutufanya kuishi kwenye ndoto, malengo na kusudi la uwepo wa vipaji hivyo ndani yetu... 
Tukutane next epsode....

Thursday, November 26, 2020

ELIMU NI MASTER KEY 2

Ugunduzi wa elimu duniani ulikuwa na maana kubwa sana kwenye maisha ya kila siku ya mwanadamu. Elimu ni zaidi ya fedha, ni zaidi ya siasa ni zaidi ya dini, elimu ni jumla ya maisha yetu ya kila siku
( Elimu ni jumla ya yote niliyoyataja hapo juu, ukitaka kujua kuwa elimu ni msingi wa mambo yote, mtu anaweza kupambana pekee yake kutafuta katika hatua za awali akifikia hatua ya kumiliki fedha nyingi na utajiri mwingi atahitaji watu wenye elimu ya fedha ili kuweza kuifanya fedha yake iendelee kuishi na kuongezeka zaidi, atahitaji wataaluma kwenye idara mbalimbali ili kumchorea na kumfungulia ramani na milango ya fursa ili kuifanya fedha iishi na kuzalisha zaidi.

Katika kitabu kitakatifu cha Biblia, Methali anasema mkamate sana elimu usimwache aende zake maana ni uzima wako, wahenga na watunzi wa Methali na misemo mingine wakasema Elimu ni mlango na ufunguo wa mafanikio ya mtu katika levels zote za maish yetu.

Tena wakasema wahenga mali bila daftari hutoweka bila habari, maana yake ni kuwa mali bila kuweka kumbukumbu hupotea bila kujua (elimu ya kutunza kumbukumbu hufundishwa kuanzia nyumbani, hapo ndipo unajua umuhimu wa elimu).
Watu wengi tumeishi nje ya ndoto na kusudi la Mungu kwa sababu ya kukosa ufahamu juu ya hazina kubwa ambayo Mungu amewekeza ndani yetu.

Elimu tumeiweka kwenye mfumo wa maisha ambayo jamii imeamua kuishi kwa kukariri, jamii inaamini kuwa elimu ipo kwa ajili ya kutumilikisha nafasi za juu katika ajira nasio kutengeneza ajira nyingi zaidi kwa ajiri ya wengine kupitia ugunduzi wa mambo au kuongeza ubora katika vile ambavyo vilishakuwepo tayari.

Wazazi wengi wameua ndoto za vijana wengi kwa sababu ya kukubali kuishi mfumo wa kukariri katika jamii zetu,
Kwa kukosa maarifa, na elimu yenye kuimarisha ufahamu tumeamua kuchagua maisha ya aina moja, sio ajabu mzazi kuua ndoto ya mtoto wake kwa sababu anataka matakwa yake yatimizwe na mtoto wake, utasikia mzazi/mlezi anamwambia mtoto, umemaliza kidato cha sita uende ukasomee Ualimu ili upate ajira uwasaidie ndugu zako, mtoto alitaka kuwa daktari, mwanasheria na taaluma hizo zinakuwa hazina nafasi kwa upande wa mzazi kwa sababu zinachukua muda mrefu nk.

Mtoto anataka kutumia kipaji chake badala yakusaidiwa mzazi anakuwa mkali kama pilipili, usïponisikia ntakulaani, kama sijakuzaa mimi tutaona sasa mimi na wewe nani alitangulia kuliona jua, au nani amemzaa mwenzake si umekuwa, kijana wa watu anaanza safari nje ya ndoto zake bali  kutimiza matakwa ya mzazh

Kama wazazi, walezi tunamalaka juu ya watoto wetu, lakini sïo kuua kilicho uwezo na kusudi la maisha yao, tuna nafasi ya kushauri na kuwajeng ila sio kutaka kutimiziwa matakwa yetu, tuwasaidie tusiwazime, akiwa anauchaguzi sio sawa tafuta namna nzuri ya kusema nae akuelewe kuliko kutumia nafasi yako kama mzazi kuua

Jamii imeua vipaji na karama za asili nyingi kwa vivuli vya kwamba nataka usome ikiambatana na mifano mingi ya walïoshindwa, wazazi na walezi tumeua asili ya uwezo na uwekezaji wa vipaji wa Mungu kwenye maisha yetu  njia ya kivuli na kisingizio cha elimu...

Mwana wa Mungu Yesu anasema hakuja kutengua torati bali kuiendeleza, kuiboresha, kuifanya iondoe mamlaka ya kuchukua maamzi ya kuumiza wengi
Ndivyo ilivyo hata katika ugunduzi wa elimu, lengo la elimu ni kutupa uwezo na kujenga ufahamu wa kila mmoja kwanza kujijua zaidi, kuziona fursa, kuongeza ufanisi na ubora katika vile tulivyo navyo
Elimu nzuri ni ile ambayo imesemwa kwenye Methali kuwa ni uzima.

Elimu sio kiua ndoto, sio mficha na muua vipaji na vipawa vya asili ( dream killer, Is not a Talent hider and killer ).

Elimu ni ufunguo hazina kubwa iliyo kwa watu wengi, lakini namna gani tunaweza kuitumia elimu ili kutufanya kuishi kwenye kusudi la maisha ya ndoto zetu..
kwa kisingizio cha elimu tumelazimisha vipaji vya waimbaji, wacheza michezo mbalimbali kama mpira wa miguu, pete, wavu, kikapu, wachekeshaji, wafanyabiashara nk kwa sababu ya kukosa ufahamu wa elimu tunayoihitaji...

Mfugaji wa mifugo mingi alikufa akilalia ngozi, kula nyamafu, kulala kwenye tembe huku utajiri ukienda mbugani kuchunga na kurudi jioni zizini na aliona fahari, Je yule mama aliyefurahia kuona vikombe, masufuria, flask nzuri, masahani ya udongo nk. kwenye kabati lake zuri la vyombo akisubiri wageni asiojua watakuja lini ndô wavitumie, Je ile familia ya mama mfuga kuku ambae aliwafanya watoto na familia ishi kwenye kauri ya wageni njoo ili nasi tupone. Kwa kukosa elimu masikini mama, baba na familia zile walikwa katika hali ambayo hawakuistahili kabisa, sababu ya yote hapa ukosefu wa elimu ya ufahamu.

Ndivyo tunavyoishi tulio wengi leo, tuna hazina zimetuzunguka kwenye familia zetu, jamii kwa ujumla, tunalia kwa uchungu kwa kukosa vyanzo vya ajira wakati ajira tunaishi nazo makwetu....

Mwandishi nguli wa vitabu na journals toka Marekani hayati Dr. Myles Munroe aliwahi kuandika kweye kitabu chake cha Maximize your potential, alisema '' yadi chache kutoka kwenye milango yetu kuna nyimbo zimerudi nyumbani bila kuimbwa, vitabu vimerudi bila kusomwa, na vipawa vingi viko kweye makaburi ndani ya mashamba yetu

Dr. Myles alisema utajiri wa dunia hii hauko kwenye vitaru vya mafuta kule Qatar, Kuwait, vitaru vya mïgodi ya dhahabu kule kusini mwa bara la Afrika, Congo hata Katika migodi ya Tanzanite kule mererani, Almasi na dhahabu kwenye ardhi ya nyumbani kahama na shinyanga na maeneo mengi ya nchi yetu, bali utajiri either tumekubali watu kufa na talanta zao, au tumeamua kuvifungia kwenye kifungo kinaitwa elimu isiyo na matendo....
Tunahitaji kujua maana halisi ya elimu, elimu, kwa sababu Elimu ni master key wa mambo yote, ufunguo elimu hutumika kufungua mageti ya hazina zetu......
Next.......
Tukutane kesho...

Tuesday, November 24, 2020

ELIMU NI MASTER KEY YA HAZINA YAKO

Hazina ya Baba ambae hakujua kuwa duniani anaishi mara moja alifuga maelfu ya mifugo ya aina mbalimbali kondoo, ng'ombe, mbuzi nk, aliishi maisha ya shida akilala kwenye nyumba ya tembe, akilala kwenye ngozi ya mnyama, alikula michembe, makande, ugali na migagani(michicha pori) na aina nyingine ya mbogamboga kutoka kwenye ardhi...
Watoto walichomwa jua, miba na kunyeshewa mvua wakiwa kwenye nguo chafu zilizochakaa (madaso) wakichunga mifugo ya baba yao, shule kwao haikuwa fahari, nyumba nzuri kwao ilikuwa habari ngeni, macho yaliwaonyesha hazina ya Baba ilivyotengeneza fahari na majivuno kijijini, familia iliheshimika kijijini na watu ambao waliishi kwenye nyumba angalau za bati na kulala kwenye vitanda vya kamba.
Lakini pamoja na ufahari wa macho ya wale mifugo, lakini leo wanaishi ya kujiinamia na majuto mengi mioyoni mwao, baba akiwa amelala milele, shubiri ijuu yao kutwa mkono shavuni, ile fahari haipo tena...ndipo ambapo tunasema bora kufa huku fikra zako zinaishi kuliko kuishi mwili wakati fikra zimekufa.....

Mzee huyu tajiri wa ng'ombe namfananisha na mama mmoja aliyemiliki kabati zuri la vyombo na kununua vyombo vya Thamani nakuviacha kwenye kabati zuri vikipigwa vumbi akisubiri wageni asiojua watakuja linï ili wavitumie ajabu....

Hawa wawili nawaunganisha na msemo wa kale usemao kwamba MGENI NJOO MWENYEJI APONE, eti kama hakuna mgeni basi kuku wataendelea kuzaliana na kuliwa na mwewe huku familia wakila mlenda na mchicha pori...
Hawa wote wamekufa wakiwa na utajiri kweye hazina zao, walidhani kumiliki mifugo, kuhifadhi vyombo kabatini, kusubiri wageni ndo wachinje kuku ndo fahari na ndiyo maisha...
Baba huyu amekufa akiwa amezoea kula mboga za majani, amelala kwenye tembe, amewanyima watoto haki ya elimu, sasa amekufa, mama leo watu wanatumia vyombo vyako ukiwa umelala kwenye sanduku....
Yako mambo mengi ambayo yanaweza kutupa mifano hai ya maisha ya wazee wetu ambao waliishi maisha ambayo hawakuyastahili.   ...
Mungu amewekeza kwa kila mtu hazina (Treasure)kubwa sana ambayo ni full package ambayo kila mtu inaweza kumfanya kuishi kwenye lengo na kusudi la Mungu...
Upo uwezo wa ajabu kwenye uumbaji wa kila mtu, asili ya mwanadamu ni uwezo, kutawala na kutumia ile hazina iliyo ndani yeke, tumechagua maisha ya mfugaji, mama mwenye kabati zuri na vyombo vya gharama ndani yake au yule mama mfuga kuku aliyechagua kusubiri wageni waje ili na yeye apone...
Elimu ni master key ambayo inaweza kutufungua macho ya ndani na kufungua hazini iliyosheheni utajiri wa aina mbalimbali....
Tukutane kesho kwenye makala hii ambayo naamini itakupa kuijua hazina yako na ya watoto wako na itakusaidi kuepuka maisha ya mfugaji, mama mmiliki wa kabati zuri lenye vyombo vizuri au mama mfuga kuku anaesubiri mgeni aje ili nae apone....
0715366003/0755632375

Thursday, October 22, 2020

Dr. Paul book

Aliweza kununua kiwanja maeneo ya mtaa wa kindai Mkoani Singida na kuanza kazi ya kufyatua tofauli na kuanza ujenzi kwa mikono yake mwenyewe  kwa sababu alijigunza ujuzi wa kujenga nyumba, hivyo kwa kushirikiana na Mke pamoja na watoto wake waliweza kujenga nyumba ambayo ipo katika mtaa wa kindai mkoani Singida.
Maamzi ya Dr. Paul ya kuamua kujenga nyumba yake na kuondoka kwenye nyumba ya kanisa pamoja na kwamba haikupokelewa vyema na baadhi ya wachungaji na waumini wa kanisa kutokana na utamaduni ambao ulikuwa umezoeleka tangu awali kwamba makazi ya mchungaji yalipaswa kuwa kanisani, lakini Dr. Paul alisimamia malengo na sababu za kutoka kwenye nyumba ya kanisa sababu ili kuwa ni (.............)
Miaka michache baadae watumishi wa Mungu walimwelewa kwa nini alichukua uamzi huo, na kupitia maono yake ya kuhakikisha mchungaji anajitenga na kanisa kwa maana ya sehemu ya kuishi umeleta manufaa kwa watumishi wa Mungu na kujenga heshima kuanzia kwa mchungaji na familia kwa ujumla.
Pamoja na kwamba yeye alijenga nyumba yake, lakini pia amekuwa mstari wa mbele kuwahamasisha wachungaji wote kuwa na nyumba zao ili kujenga heshima ya utumishi wao kwa kanisa lakini pia kwa familia zao, baadhi ya juhudi zake kwa wachungaji kuwa na nyumba zao ni pamoja na hamasa aliyoitoa kwa Mchungaji Boniface Ntandu kujenga nyumba yake pamoja na Mchungaji Philipo Sospeter ambae aliweza kujenga nyumba yake pia katika mtaa wa jineri na wachungaji mbalimbali wamekuwa wakifanya hivyo na kuondokana na mtazamo wakuishi kwenye nyumba za kanisa.
 

Saturday, July 18, 2020

NGUVU YA MUNGU NDANI YA MKRISTO.

SOMO: NGUVU YA MUNGU NDANI YA KANISA.
 2 Wakorintho 2 :4…., Wakorintho 4:20
NGUVU ni uweza au mamlaka ya kufanya jambo Fulani,
 sisi kama wakristo tunahitaji nguvu ya kutuwezesha kutenda mapenzi ya Mungu na kazi za Mungu duniani, na Biblia inasema hatuwezi kutenda , kwa usahihi duniani kama hatutakuwa na nguvu za Mungu.

unapoongelea ukristo mahali jua unaongelea nguvu kwa maana ukristo ni nguvu.

Injili ya Yesu kristo imejengwa katika nguvu za MUNGU.
Kama tulivyoona ukristo sio maneno matupu tu au tunavyokili bali ukristo umejengwa kwenye nguvu ya Mungu.. nguvu ya kuponya, kufufua, kufungua na kuokoa..
na ndio maana mtume Paulo anasema Wathethalonike 1:8
1 Timotheo 1:7.. ´´Mungu hakutupa roho ya hofu bali roho ya nguvu ´´
na ndio maana biblia inasema kuwa ´´nanyi mtapokea nguvu akishawajilia juu yenu Roho Mtakatifu
Waefeso 3:20.. ´´ kulingana na NGUVU itendayo kazi ndani yetu´´ ndani ya kila mtu aliyeokoka kuna nguvu ya Mungu..
Waefeso 6:10 ´´katika uweza..¨ uweza unamaanisha nguvu.
1 Wakorintho 1:18 ¨ujumbe wa msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi lakini kwetu sisi tunaoamini ni nguvu ya Mungu¨ kumbe kwenye msalaba wa Yesu Kristo kuna uweza uletao wokovu. Msalaba wa Kristo una nguvu.

UKIWA NA NGUVU YA MUNGU NDANI YAKO UNAWEZA KUFANYA HAYA.
i.)Msamaha.
 Luka 23: 34 - alisamehe.. watu wa dunia wanaweza kukwambia nimekusamehe lakini sitasahau lakini Yesu akiwa msalabani na katikati ya maumivu makuu ya msalaba akasema ´´ baba wasamehe maana hawajui walitendalo
ii.)Nguvu ya Mungu ndani yetu inatupa nafasi ya kukumbukwa na Yesu.
 Luka 23:42-43 - ¨
na kwa andiko hili tunajifunza kuwa nguvu ya Mungu inatupa nafasi ya kukumbukwa kwenye Ufalme wa Yesu.Mungu anakumbuka maombi yako, kazi yako nk.
iii.)Hutakufa
Luka 23:46, Kwa mtu yeyote aliyeokoka ,amekabidhiwa kwenye mikono ya Yesu kristo.. na hutakufa mpaka siku ya Bwana , kwasababu roho yako imekabidhiwa kwenye mikono ya Yesu Kristo.. huu ni ulinzi ambao kila mtu aliyeokoka anakuwa nao.. tupo mikononi mwa Mungu na hakuna mtu awezaye kututoa kutoka katika mikono ya Yesu Kristo..
iv.) Ukiwa na nguvu ya Mungu unajenga mahusiano na Mungu.
Yohana 19:29 Yesu akiwa msalabani , alikuwa anajali mahusiano.. hii inaonyesha kuwa msalaba wa Yesu unatupa usalama ndani ya mahusiano na wazazi na watu wengine.. Msalaba wa Yesu unatupa mahusiano bora . ukimwomba Mungu akupe nguvu ya mahusiano.. Kumbe msalaba ulileta Nguvu ya upatanisho.. Nguvu ya Mungu inaleta watu pamoja , pamoja, familia pamoja.

v) Nguvu ya Mungu inatupa kiu ya kumtafuta Mungu. Yohana 19:28
vi) Ukiwa na Nguvu ya Mungu unakuwa na mamlaka Luka 10:19
vii) Unapata uwezo wa kuombea na watu kupokea uponyaji
Luka 5:17..... Luka 4:18

Friday, July 3, 2020

Faida za kumtumikia Mungu

The benefits of serving God - Part 1
The apostle Paul made an intriguing statement in his letter to Timothy,
'This know also, that in the last days perilous times shall come. For men shall be lovers of their own selves...' (2 Timothy 3:1, 2) Pay attention to these words, 'Perilous time shall come because men shall be lovers of their own selves.' Our minds automatically go to the world when we hear and read these words especially when we see what is going on in the secular but the same can be applied to the church. Today a lot of believers in the church are happy to only show up for Sunday services and most are self serving and wallowing in self indulgence without ever giving a thought to serving the Lord who redeemed them from sin and eternal damnation.  That is not a criticism of the modern church but a matter of fact statement.
The Christians of yesteryear had a different concept of serving God. They would lay their lives down for the Gospel. It would not be unusual for a young soul to be converted years ago and be aflame to reach the world for Jesus. This was in spite of a lack of technological and communication advancement as well as the travel facilities that we enjoy today. Yet the Gospel reverberated around the world as wild fire. Millions upon millions of souls were added to the kingdom of God. Today we have everything at our disposal and we are not taking advantage of it because many in the church are simply not passionate about serving the Lord.
God has done much for us in the saving of our lives by sending his own Son as our redeemer and sin-bearer. To serve God is not a grievous or hard task because God is a great boss and a great rewarder. In fact the Bible reveals to us that there are great benefits in serving God.
And ye shall serve the Lord your God , and he shall bless thy bread, and thy water; and I will take sickness away from the midst of thee . There shall nothing cast their young, nor be barren, in thy land: the number of thy days I will fulfil . I will send my fear before thee, and will destroy all the people to whom thou shalt come, and I will make all thine enemies turn their backs unto thee. And I will send hornets before thee, which shall drive out the Hivite, the Canaanite, and the Hittite, from before thee.
Exodus 23:25-28
These verses could not be any more clearer to us that serving God is for our betterment and profit. Here are a few benefits of serving God. When you serve God,
He will bless your bread and water
He will take away sickness from your midst
There will be no miscarriage
There will be no barrenness
There will be no premature death
You will have long life and fulfill destiny
Your enemies will turn away from you
THERE IS NO MAN OR WOMAN WHO SERVES GOD THAT WILL WALK AWAY EMPTY HANDED. GOD WILL NEVER OWE YOU ANYTHING
Here is another great undeniable verse that shows the profitability of serving God,
 If they obey and serve him, they shall spend their days in prosperity, and their years in pleasures.
Job 36:11
I want to encourage YOU to get involved in serving God. You may ask,
'So how do I serve God?' Allow me to give you seven ways,
1. Serve God with your life
2. Serve God in your church
3. Serve God with your talents
4. Serve God with your time
5. Serve God with prayers and fastings
6. Serve God with your money - tithes and offerings
7. Serve God by serving others
You will never be at a loss when you serve God. He has done much for us and he will do much more for you. I want to challenge you with the words of President John Kennedy. In 1961 during his Inaugural Address, President Kennedy uttered these powerful words, 'My fellow Americans, ask not what your country can do for you, ask what you can do for your country.'
Today, I am asking you, 'My fellow believers, ask not what your God can do for you, ask what can you do for your God.'
A few words about Glenn