Saturday, July 18, 2020

NGUVU YA MUNGU NDANI YA MKRISTO.

SOMO: NGUVU YA MUNGU NDANI YA KANISA.
 2 Wakorintho 2 :4…., Wakorintho 4:20
NGUVU ni uweza au mamlaka ya kufanya jambo Fulani,
 sisi kama wakristo tunahitaji nguvu ya kutuwezesha kutenda mapenzi ya Mungu na kazi za Mungu duniani, na Biblia inasema hatuwezi kutenda , kwa usahihi duniani kama hatutakuwa na nguvu za Mungu.

unapoongelea ukristo mahali jua unaongelea nguvu kwa maana ukristo ni nguvu.

Injili ya Yesu kristo imejengwa katika nguvu za MUNGU.
Kama tulivyoona ukristo sio maneno matupu tu au tunavyokili bali ukristo umejengwa kwenye nguvu ya Mungu.. nguvu ya kuponya, kufufua, kufungua na kuokoa..
na ndio maana mtume Paulo anasema Wathethalonike 1:8
1 Timotheo 1:7.. ´´Mungu hakutupa roho ya hofu bali roho ya nguvu ´´
na ndio maana biblia inasema kuwa ´´nanyi mtapokea nguvu akishawajilia juu yenu Roho Mtakatifu
Waefeso 3:20.. ´´ kulingana na NGUVU itendayo kazi ndani yetu´´ ndani ya kila mtu aliyeokoka kuna nguvu ya Mungu..
Waefeso 6:10 ´´katika uweza..¨ uweza unamaanisha nguvu.
1 Wakorintho 1:18 ¨ujumbe wa msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi lakini kwetu sisi tunaoamini ni nguvu ya Mungu¨ kumbe kwenye msalaba wa Yesu Kristo kuna uweza uletao wokovu. Msalaba wa Kristo una nguvu.

UKIWA NA NGUVU YA MUNGU NDANI YAKO UNAWEZA KUFANYA HAYA.
i.)Msamaha.
 Luka 23: 34 - alisamehe.. watu wa dunia wanaweza kukwambia nimekusamehe lakini sitasahau lakini Yesu akiwa msalabani na katikati ya maumivu makuu ya msalaba akasema ´´ baba wasamehe maana hawajui walitendalo
ii.)Nguvu ya Mungu ndani yetu inatupa nafasi ya kukumbukwa na Yesu.
 Luka 23:42-43 - ¨
na kwa andiko hili tunajifunza kuwa nguvu ya Mungu inatupa nafasi ya kukumbukwa kwenye Ufalme wa Yesu.Mungu anakumbuka maombi yako, kazi yako nk.
iii.)Hutakufa
Luka 23:46, Kwa mtu yeyote aliyeokoka ,amekabidhiwa kwenye mikono ya Yesu kristo.. na hutakufa mpaka siku ya Bwana , kwasababu roho yako imekabidhiwa kwenye mikono ya Yesu Kristo.. huu ni ulinzi ambao kila mtu aliyeokoka anakuwa nao.. tupo mikononi mwa Mungu na hakuna mtu awezaye kututoa kutoka katika mikono ya Yesu Kristo..
iv.) Ukiwa na nguvu ya Mungu unajenga mahusiano na Mungu.
Yohana 19:29 Yesu akiwa msalabani , alikuwa anajali mahusiano.. hii inaonyesha kuwa msalaba wa Yesu unatupa usalama ndani ya mahusiano na wazazi na watu wengine.. Msalaba wa Yesu unatupa mahusiano bora . ukimwomba Mungu akupe nguvu ya mahusiano.. Kumbe msalaba ulileta Nguvu ya upatanisho.. Nguvu ya Mungu inaleta watu pamoja , pamoja, familia pamoja.

v) Nguvu ya Mungu inatupa kiu ya kumtafuta Mungu. Yohana 19:28
vi) Ukiwa na Nguvu ya Mungu unakuwa na mamlaka Luka 10:19
vii) Unapata uwezo wa kuombea na watu kupokea uponyaji
Luka 5:17..... Luka 4:18

No comments:

Post a Comment