Sunday, May 24, 2020

BABA NI MZIZI NA NGUZO YA FAMILIA

BABA NI MZIZI NA NGUZO YA FAMILIA.
Sehemu ya 5
• Kazi za Baba.
• Kiwango ambacho tunapaswa kupima na Kufundisha akina baba kinaweza kupatikana ndani ya hizi Kazi kumi za msingi za baba wa kweli.
1.Baba ni Mzazi, Ni mlezi na mwelekezaji wa mwelekeo wa familia yake kwa maana ya mke & Watoto.

2. Chanzo, kama ambavyo alivyo umbwa alipewa majukumu na Mungu kwa hiyo yeye ni chanzo cha yote katika familia, kuanzia upatikanaji wa mke, watoto, mpaka kwenye maisha yote duniani.

3. Msimamiaji, pamoja na mama na watoto kuweza kufanya mambo mengine lakini msimamiaji mkuu na msemaji wa mwisho huwa ni Baba.

4. Mlinzi wa familia, mali, maadili na hii ni kuhakikisha kuwa kila kitu kinakuwa salama katika familia.

5. Mwalimu, anafundisha, kuelekeza, namna ya mambo kufanyika kwenye familia kwa hali ya mpangilio, na kwa ufasaha mkubwa.

6. Nidhamu, Baba ndiye mlinzi wa nidhamu namba moja, mambo yakiharibika wa kwanza kulaumiwa ni Baba kushindwa kutimiza wajibu na majukumu yake.

7. Kiongozi, Baba ni kiongozi wa familia, jamii na hata kwa ngazi ya kanisa na Taifa.

8. Kichwa, ni master planner, ni kichwa ndiye amebeba hatima na mwelekeo wa familia yake maana yake yeye ni mkuu wa familia.

9. Kujali, sifa nyingine ya mwanaume/Baba ni kujali, kutunza familia na kuhakikisha familia inapata mahitaji yake ya kila siku.

10. Mleta maendeleo, kwa kazi zake mipango yake na namna ya kuyatimiza majukumu yake basi mwisho wa siku huleta faida na maendeleo katika familia, pamoja na mama kufanya kazi, biashara lakin kiini namba moja ni baba, Baba akilala familia inaanguka na kupoteza mwelekeo hasa kama hakujenga misingi imara kwa watoto na mke wake.

Mwanaume, Baba Timiza wajibu, wajengee watoto, mke uwezo wa kuyaishi mazuri na maarifa ambayo yatawasaidia siku ukipumzishwa na Mungu.

Moses Zephania Mgema

No comments:

Post a Comment