Sunday, August 28, 2022

ROHO YA MATENGANO

Katika ulimwengu tulio nao leo, umekuwa ni ulimwengu wenye mkanganyiko na wenye taarifa nyingi zenye uhalisia na upotoshaji mwingi sana. Kuenea kwa maarifa kumeongeza uhalalishaji wa mambo mengi mabaya wenye lengo la kuhakikisha kuwa kila mtu anajitengenezea mazingira yakujinufaisha na kuishibisha nafsi yake....

Kutokana na kuongezeka kwa maarifa mengi duniani, mifumo mingi imeathiriwa na mabadiliko hayo kwa namna chanya na kwa namna hasi. Mfano kwenye upande chanya, watu wamerahisishiwa namna bora na nzuri ya kupata maarifa, ujuzi, na kuziona fursa, kujifunza maneno ya Mungu na kupata mafundisho kwa urahisi zaidi kutoka kwa watumishi wengi wa Mungu  kuliko kipindi cha nyuma kilichokuwa na ufinyu wa vyanzo vya maarifa....

Lakini pamoja na kuona manufaa mema ya kuongezeka kwa vyanzo vya maarifa, lakini kwenye upande wa mambo ya kiroho, kumekuwa na ongezeko kubwa sana la uasi, ujuaji, na watu kubeba maarifa machache yenye kujihalalishia baadhi ya mambo ambayo kiuhalisia ni chukizo na uasi mbele za Mungu...

Sio ajabu leo kumkuta mtumishi wa Mungu akiwa ameshikiria mstari toka kwenye Biblia ambao anautumia kama silaha ya kulinda maslahi yake binafsi. Ndiyo maana leo makanisani imekuwa ni jambo la kawaida kwa watu kufanya dhambi lakini hakuna mtu ambae anashughulika nao kama sehemu ya maonyo, kurejeshana, na kukumbushana kuwa baadhi ya mambo kama mkristo/wakristo hatupaswi kufanya kwa sababu ya kutunza moto katika madhabahu ya Mungu wetu...

Na kama ikitokea mtumishi wa Mungu akasimamia misingi ya kikristo basi anaonekana ni mtu mwenye ukengeufu, mtu mshamba, anajifanya yeye mtakatifu, anajiona, hajui kama ni kipindi cha neema, yeye ni adhabu tu, mtu asiye na huruma wala kuchukuliana na madhaifu ya watu. Na watu wamekuwa na baadhi yakujitetea na kujilinda kwa mlengo wa kuhalalisha yale wanayoyafanya mfano wa maandiko hayo ni......
Kutoka na ulimwengu kuzalisha watu wenye maarifa mengi, imechangaia kwa kiwango kikubwa sana, mioyo ya watu kuwa magumu, kiburi, hawapendi kuonywa, wanajiona wao ni bora wenye kujua na hawapaswi kuguswa wala kuelekezwa, ukiwagusa, wanajikunja, ukiwaonya hawaji kanisani au wanahama....

Nguvu hii yote inakuja kwa sababu ya kupngezeka kwa maarifa 

No comments:

Post a Comment