Tuesday, August 23, 2022

MWANAUME V MWANAMKE

Tangu misingi ya ulimwengu kuumbwa na Mungu alipofanya maamzi ya kumfanya mtu kwa mfano wake, imani ya kwanza kabisa aliiweka kwa mwanaume. Imani hiyo ilijengewa msingi imara sana ambao huwa sio rahisi kuyumbishwa kwa namna yoyote ile kwa sababu ya ile nguvu ya kuaminiwa na Mungu na kushirikishwa hata katika uumbaji.

Wakati Mungu anafanya uumbaji wa vitu mbalimbali duniani, mwisho kabisa alimuumba mtu, (mwanaume) na baada ya kumuumba alimpa mamlaka na uwezo wa kuumba pia na kwa kulidhibitisha hilo, Mungu alimpa Adamu nafasi yakuwaita wanyama na vitu vyote majina kwa niaba yake....
Kwa maana hiyo basi, mamlaka na nafasi ya kwanza ya Mungu kwa mwanadamu aliweka kwa mwanaume, wakati huo mwanamke hayupo kabisa na wala wazo la yeye kuwepo duniani halikuwepo. Mwanamke amekuja duniani kwa sababu ya hitaji la Adamu ambae ni mwanaume, upweke katika ile bustani, Mungu akaona vyema ampe mtu ambae wanaweza kuishi pamoja na kushirikiana..

Kwa kifupi ni kwamba, Mwanamke asingeweza kuwepo kama either kungekuwa na njia mbili ambazo angepewa Adamu kama machaguo ya kuondoa Upweke wake pale bustanini, labda Angelina maamzi ya kuchagua kile kitu cha pili badala ya mwanamke.
Lakini kwa sababu Mungu alitoa chaguo moja na kulifanya chaguo hilo kuwa hitaji la mwanaume, basi mwanamke akawa ametoka na kuwa sehemu ya maisha ya mwanaume hata sasa...
Ndiyo maana leo ni rahisi zaidi mwanamke kuishi pekee yake baada ya mume wake wa kwanza kuondoka kuliko mwanaume na hata huyu mwanaume akiamua kuishi pekee yake baada ya mke kuondoka, jamiii na viongozi wa dini wanaweza kuwa sehemu ya kumshawishi ili kufanya maamzi ya kuoa tena kwa sababu si tu kuoa na kuzaa bali mwanaume kuishi na mwanamke ni hitaji maalumu sana...

Maaana yake ni kwamba mwanaume alitengenezewa uhitaji na uhitaji huo ukawa kwenye eneo la kutatuliwa na mwanamke. Na kwa sababu hiyo basi ili kuongeza thamani ya mwanamke kwa mwanaume, Mungu aliweka nguvu na mamlaka, utulivu na kiwango kikubwa cha kufikiri ndani ya mwanaume kuliko mwanamke....
Kwa point hiyo ni rahisi zaidi mwanaume kulaumiwa kwa sababu ya jambo fulani kuharibika wakati yeye yupo, kuliko mwanamke mwenye nafasi, uwezo na nguvu ya kutatua jambo hilo kwa sababu tu, mwanamke ni kwa ajili yake lakini mwanaume ni kwa ajili ya familia na jamii.
Mwimbaji mmoja akasema, ukiona jambo linayumba mahali fahamu mwanaume hajatimiza wajibu wake sawasawa. Uwezo wa mwanaume kufikiri ni mkubwa mno ukilinganisha na uwezo wa mwanamke katika kufikiri. 
Watu wengi husema kuwa mwanamke ana kiwango na uwezo mkubwa wa kufikiri kuliko mwanaume na akili nyingi sana lakini ukweli ni kwamba asilimia kubwa ya wanawake huwa hawafikiri bali huwa wanawaza. Na hapa ndipo kuna tofauti kati ya kuwaza na kufikiri na hapa hapa ndiyo njia panda ambayo inawatofautisha wanawake na wanaume...
Mfano, tatizo likitokea kwenye familia, mtoto ameungua maji ya moto wakati wazazi wako kazini, mfanyakazi wa ndani akapiga simu kwa Baba, Baba atasema mwandae umlete mjini utanikuta hapa hospital na fanya haraka, na kama huna hela ya nauli chukua bajaji au tax, utanikuta hapa nitalipa. Same scenario akifikishiwa mwanamke, jambo la kwanza atapaniki, hisia zitatangulia, atalia, atataka kujua ilikuwaje mpaka amwagikiwe maji, hapo hapo atakuwa anapanda bodaboda kwenda nyumbani umbali wa kilometa kadhaa, huku akigombeza mfanyakazi na kumlaumu, atapaniki, na akifika huko atafanya anachokijuq yeye, wakati huo akili yake ikiwa ina waza lile tatizo zaidi kuliko kufikiri namna ya kuondoa tatizo hilo...
Mwanamke anatawaliwa na hisia sana, anahamasika (Easy to be motivated) wakati mwanaume huwa anataka kulielewa jambo kwa undani na kufanya mchakato ndani ya akili yake, halafu baada ya kulipa hilo jambo kwa mapana na marefu huwa anakuwa Inspired kulifanya jambo hilo kwa ubora na kwa uhakika zaidi maana anakuwa amejipima na kujitathimini kuwa jambo hili liko ndani ya uwezo wangu au hapana...




No comments:

Post a Comment