Tuesday, August 2, 2022

Cover book/ Kava la kitabu

Dunia ya leo, inaishi kwenye aina Fulani ya mitazamo na kuthaminishana kutokana na kile mtu ambacho anaweza kuwa anakisikia zaidi kuliko kukaa chini na kufikiri kabla ya kusambaza habari, au kukijaji kitu. Nje ya kava la kitabu watu wamejikuta wakijipa majibu ambayo sio sahihi..

Story ya kichaa mmoja kwenye stand ya zamani ya mabasi yaendayo mikoani, kando ya dambo la stand, mama mmoja aliyoenekana akiwa chakavu na mwenye kuishi maisha ya kuokota makopo na kula vyakula vya majalalani, kuvaa nguo chakavu na nywele ndefu zilizojaa uchafu mwingi...

Wengi kwa kumtazama walimwona ni kichaa, walimpita na kumsemea maneno mabovu, walimtazama kama mtu asie na thamani, mtu aliyepoteza dira ya maisha, value yake kama binadamu haikuwepo tena, lakini kumbe alikuwa ni mtu mwenye kazi yake kubwa na alikuwa kwenye kazi maalumu ambayo ilimlazimu kuishi katika hali hiyo, binadamu wasio jipa nafasi ya kufikiri walijipa majibu yao ambayo yalikuwa tofauti kabisa..

Ndivyo ilivyo kwetu, tumekuwa watu wepesi kuhukumu, kudharau watu, kuwaona watu hawana thamani, hawana tena mwelekeo wa maisha kwa sababu ya hali ya sasa kwa sababu mwonekano wao...

Wengine ni vijana wadogo tumeshindwa kuwaheshimu, tumeowaona ombaomba, watu wasio na maana dunia kwa sababu ya mwonekano wao, wengine wanatokeo familia duni, wengine wamekimbia familia zao kutokana na shida mbalimbali za kimaisha, wengine ni yatima hakuna aweza kuwashika mkono, wote hawa tunawaona watu wasio na malengo, watu wenye chembe chembe za wizi na udokozi...

Mitazamo yetu kwao ni mibaya, bahati mbaya hata tulio kulia mazingira kama hayo na leo Mungu ametupa nafasi, tumesahau kuwa hata sisi kuwa tulitokea huko, we don't value dhahabu chakavu kwa sababu haijapita kwenye moto bado.

Vijana wengi walio maliza vyuo, wapo wengi mitaani wakitafuta ajira, sio kwa sababu hawana mawazo mazuri ya biashara hapana ni kwa sababu mitaji ni changamoto kwao, ni sababu inawalazimisha kutafuta walau kazi ambayo itampa mshahara mzuri ambao utamwezesha yeye pamoja na familia yake, wadogo zake wanamwangalia kama kijana aliyetoka shule, kama kijana mwenye elimu, wazazi wametua mzigo kwake maana walimsomesha ili awasaidia, vijana hawa wanatafuta ajira ili kutatua changamoto za mapema sana...

Lakini kwa sababu ya kutembea mwonekano wa nje umechakaa sana, maisha ni magumu mno, maisha yamewapiga hawana tena mwonekano mzuri, yawezekana hata fedha ya kununulia walau mafuta mazuri hawana, kila kitu kwao ni kigumu ni matatizo juu ya matatizo.

Waungwana tunawaona hawafai tena kwa sababu ya mwonekano wao. Ukweli ni kwamba sio kila mtu anavyoonekana ndivyo alivyo, tusiwe wepesi kuwachukulia watu kwenye mitazamo yetu, we have to take time to study people so that we can know them in out by doing that ni rahisi zaidi kupata the best of a person....

Ni rahisi kumkuta mtu Ana mwongelewa mtu vibaya lakini ana ujasiri kana kwamba anamjua, wengine wanachukia watu bila sababu ya msingi, wengine wakisema huyu anatabia Fulani bila kuwa na uhakika na maneno hayo ila tu kwa sababu amesikia watu wakisema na yeye anabeba maneno hayo..

Watu wengi tumewavisha watu tabia ambazo sio zao, wapo wameitwa malaya, wengine wanaviburi wengine wachoyo, wabinafsi, wanajidai kwa sababu ya kutokupata nafasi ya kuwajua zaidi....

Sio rahisi kumfahamu mtu kwa kumwagilia, au kukutna nae kwa muda mchache, you need time, mtu hahitaji kuzungumzwa kwa kusikia story mtaani, hupaswa kumhukumu mtu kwa kusikia watu wanasema nini juu yake ni vyema kujiaminisha pia wewe kama wewe...

Ndiyo wengi wamejikuta wakipoteza watu wa muhimi zaidi kwa sababu ya mwonekano, na wamejikuta wakiingia kwenye mikono ya watu malaghai kwa sababu ya kutokujua na wengine kuvutiwa ba mwonekano wa nje...

Take time to know a person 
Usiishi kwa story za kusikia invest your time to know someone 

No comments:

Post a Comment