Saturday, February 19, 2022

Akili ya mtu mweusi ambayo imeshindwa kujitegemea kwa miaka yote, akili ya mtu mweusi ambae reference  yake ni kwa mtu mweupe. Mtu mweusi yuko tayari kuwa mbwa katika nchi ya mtu mweupe, yuko kuwa mfungwa katika Geneva moja katika nchi ya mtu mweupe, kuliko kuwa mtu huru katika ardhi mama katika bara la Afrika...

Akili ya mtu mweusi ambae anaweza kucheka katika uso na meno 32 yote nje huku katikati ya moyo na roho yake vikipingana na kicheko chake mwenyewe. Ni ajabu sana

Ni miaka zaidi ya hamsini mataifa ya Afrika tangu yalipo dai uhuru wake kutoka kwa mtu mweupe. Waasisi na viongozi wa awali ambao waliona mwanadamu hakuumbwa ili kutawaliwa na kuamliwa mambo yake, kwa jambo na damu bila elimu, bila silaha, bila kuwa na minutes kubwa za kivita waliweza kumwondoa mkoloni nakuweza kuicha Afrika huru yenye kujitegemea nakufanya maamzi juu ya mali zake yenyewe 

Nyerere akiwa na fimbo yake, Nkwame Nkurumah kutoka nchi ya Ghana πŸ‡¬πŸ‡­, Jommo kenyatta pale kenya πŸ‡°πŸ‡ͺ, Milliton Obote pale nchi ya πŸ‡ΊπŸ‡¬ mpaka miaka ya kuelekea mwisho mwa 1990s alipokuja mzee mwenye busara hekima na maarifa mengi Nelson Mandela alimaarufu Madiba....

Wakatengeneza bara jipya nje ya ukoloni walijua maumivu yakutawaliwa na watu wa nje, walijua maendeleo ya Afrika yataletwa na waafrika wenyewe, walijua jirani hawezi kujenga kwa jirani yake hata akijenga atajengq either kwa kiwango cha chini au kwa lengo Fulani, walijua jirani anaweza kuwahudumia watoto wa mwafrika lakini hawezi kufanya kama ambavyo mama au Baba halisi atakavyofanya....

Baada ya uhuru, nchi nyingi katika bara la Afrika zimerudi kwenye ukoloni mambo leo, asilimia kubwa tunaamini cha mzungu au mchina ni bora kuliko check ndio maana leo sio ajabu kumkuta kijana akitamani kuwa mbwa katika bara ulaya, kutamani kuwa mfungwa katika magereza ya watu weupe pale London, Washington Dc, Berlin, Paris pale Milan au hata pale Amsterdam nchini uholanzi kuliko kuwa mtu huru katika ardhi ya muasisi Nyerere mwana wa kambarage....

Fikra mfu, fikra finyu, fikra mgando usioweza  kuona thamani yakuishi katika ardhi ya nyumbani kwa uhuru na kwa amani. Nakwenda ulaya kwa sababu nyumbani hakuna fursa za ajira, nakwenda ulaya kwa viongozi wa Afrika ni watu wa made all sana watu wanasahau kuwa kwa njama ya mtu mweupe Muamar Gaddafi alipoteza uhai, kwa njama za mtu mweupe, Robert Mugabe alionekana kituko mbele ya Waafrika wenzake kisa alikataa kuishi kwenye fikra za mtu mweupe....

Naikumbuka hadithi ya kijana wa kisukuma kutoka wilayani chato, kando ya ziwa Victoria aliyeamini kuwa sisi ni nchi tajiri, aliamini bila fedha za Mzungu Tanzania inaweza kusimama yenyewe, aliamini kama taifa na bara zima la Afrika hatustahili kuwa hapa tulips kwa sababu  ya Mali zenye thamani  kubwa duniani zimelala Afrika, aliamini utajiri katika bara ulaya, America na kwingineko ni kwa sababu ya Afrika....

Naitazama Tanzania yangu ambayo watu wake wamechagua aina Fulani ya maisha, nchi ya Nyerere imebaki kuwa nchi ya made madeal kwa viongozi, wanachi wake kuwa chawa wa viongozi, aina ya maisha tumechagua ni kuwaumiza wengi ili mimi binafsi nite mbele kwenye hama iliyotokana na kuwa chawa wa mtu Fulani....

Tumechagua kuwa chawa na watu wa vijiweni huku tukitoa lawama kwa watawala wa nchi, wabunge hawatimizi wajibu wao, viongozi wanakula nchi huku tukisahau kuwa hao hao tumewafanya kuwa miungu watu kwa kuwa machawa wao.....wakitupatia lak moja, mbili, tatu nk tunaona maisha tumeyawini na kuwa ni wajanja sana kuliko kawaida....

Sisi hao hao ndio wa kwanza kulaumu kuwa hospitality hakuna dawa, hakuna walimu katika mashule yetu na tunakuwa tuko seriously kama tuna pointi vile kumbe ugoro tupu.... tumechagua aina Fulani ya maisha ambayo hayana afya kwetu sisi na kwa kizazi kijacho....
Itaendelea...

Wednesday, February 9, 2022

AKILI SMART NI URITHI BORA

Urithi bora katika maisha ya mtu sio Mali, fedha, elimu. Nimejaribu kutafakari, kujifunza na kusoma watu wengi katika vipengere vingi kama kipengere cha kurithishwa au kupata mtaji wa fedha, wengine wamepata urithi bora wa elimu  na wana GPA kubwa, wengine wameachiwa biashara nzuri na kubwa, wengine wamepata kazi za kuajiriwa nzuri na zenye hadhi, wengine wameachiwa majumba na magari mengi nk..

Lakini watu wamezaliwa katika mazingira yenye giza nene na dim-witted kubwa la umasikini, walala njaa, nguo kwao ilikuwa ni urithi bora sana tena nguo zenye uchakavu wa kiwango cha kutisha, wengine hawakubahatika hata kupata malezi bora ya wazazi, elimu haikuwa sehemu yao sio kwa sababu waliamua kama wale vijana kutoka familia tajiri walioamua kwa matakwa yao kuchagua kutokwenda shule....

Aina na makundi yote haya mawili, nimegundua kuwa kutoka katika familia yenye uwezo, familia yenye kila kitu, sio sababu ya mtu kutoboa tundu la mafanikio. Ingekuwa hivyo wale manikins, kizazi chose katika mstari wa ukoo wao wangeusikia utajiri katika majirani zao, wangeona katika Television na kusikiliza kwa majirani zao....

Urithi bora hata kama umezaliwa nyikani, tamani kuwa na akili yenye akili sawa, akili yenye uwezo wa kuamua kwenda mabli, akili ambayo haisikitishwi na mahali ambapo umezaliwa, akili yenye kuona kuwa hata kama leo niko hapa kesho yangu yaweza kuwa bora sana kwa sababu nilizawaliwa kwa kusudi la Mungu....

Urithi bora wa mtoto sio elimu kwa sababu wapo watu wengi wenye elimu kwa viwango vya degree,  masters, PhD, wengine hata degree 100 lakini wayatendayo hayaendani na viwango vya elimu yao, wengi elimu imewafanya kuwa wa hovyo kuliko hata ya kabla yakuwa na elimu kubwa...

Wengi wameachiwa Mali nyingi za urithi lakini ziliwafanya kuwa watu wa hovyo. Baadhi yao walikuwa wacha Mungu kabla ya kupata urithi lakini Mali zemewabadilisha na kuwa watu wapumbavu na wasio faaa kwenye jamii hata kwenye familia zao....

Watu wengine wamepata fedha nyingi kwa mkupuo either kwa njia ya urithi, kwenye madini, kwenye ubashiri wa michezo ya kubashiri, wengine wana bidii ya kufanya kazi, wamepata fursa zenye hela nyingi katika biashara au katika kazi za kuajiliwa lakini zimewafanya kuwa watu wa hovyo na hofu ya Mungu sio sehemu yao tena....

Changamoto kubwa ambayo imekuwa ikitupata na watu wengi wamekuwa wakiamini kuwa elimu ndio urithi bora, ni kweli lakini elimu hata ingekuwa bora kiasi gani lakini kama inaenda mahali sio sahihi ni sawa na ile habari ya kwenye Biblia ambayo Yesu aliitoa wakati akiwafundisha wanafunzi wake.

Kwamba kulikuwa na mpanzi ambaye alikuwa na mbegu zake, kwa mfano huo Yesu anasema kuwa mbegu zingine zilianguka njiani mahali penye wapita njia wengi, nyingine katika miamba hakuna rutuba, zingine kwenye miba zilisongwa na miiba, zingine kwenye udongo mzuri zikastawi vyema kabisa.....

Mbegu ni elimu na mtaji ni mzazi au mlezi na shamba ni mtoto anaepswa kupata elimu hiyo, lakini Changamoto kubwa inatokea pale shamba(mtoto)anakuwa ni ardhi ya Barabarani au akawa ni shamba lenye mwamba  mkubwa na mgumu....

Hapa hata kama mtaji mzazi/mlezi + mbolea ambayo ni mahitaji muhimu yakuwezesha elimu yawepo yote lakini kama hiyo mbolea na matunzo yanafanyika juu ya ardhi yenye mwamba au kando ya njia basi usitegemee matokeo bora kutoka kwenye ardhi ya namna hiyo....

Lakini kama elimu hiyo hiyo ikiienda kwa mtu sahihi yaani mtu mwenye ufahamu bora na mwenye kujua thamani ya kile mzazi anafanya basi huu ndio udongo mzuri ambao utaleta matokeo mazuri kuanzia kwa mtu husika, wazazi hata kwa taifa kutakuwa na manufaa na hatua nyingine kubwa ya maendeleo  kabisa....

Vivyo hivyo hata kwenye urithi wa Mali zingine, urithi ukienda kwa mtu smart mwenye ufahamu bora na mpana basi ni rahisi kuona hatua ya maendeleo katika zile Mali zinaongezeka. Ipo mifano hai ya kina Muhammed Dewji na wengine ambao walipata urithi na kuzitoa Mali zile kwenye kiwango walichopewa na kwenda hatua ya juu zaidi....

Smartness is the key of success 
Education is the factor to support and expose a personal to see opportunity in a third πŸ‘ 

Smartness can turned unproductive land to produce, take an example of John, who were taken to the desert 🏜  

Smartness is everything 

Moses_mgema 
0755632375
0719110760



Monday, February 7, 2022

Joel Nanauka, moja kati ya waandishi na wazungumzaji bora kabisa katika hadhara amewahi kusema kwamba " katika ulimwengu tulio nao, ulimwengu wa mitandao ya kijamii, watu wengi wanakuonyesha jambo/kitu wanachotka wao ukione sio kile unachotaka wewe kukiona 

Na mara nyingi tunachokiona katika social media ni matokeo ya michakato ya muda mrefu ambayo katu mtu huyo hawezi kushare na wewechakato mpaka kufikia level aliyofikia kwa wakati anaamua kushare matokeo ya alichokifanya.

Hali ya namna hii imekuwa chanzo kubwa sana kwa vijana wa leo ambao wamekuwa na shauku ya kumiliki vitu vyenye thamani kwa sababu tu wamemwona kijana mwenye rika Lao anamiliki baadhi ya vitu vyenye thamani kubwa...

Matokeo yake tumeishi kwa kupoteza focus na malengo ambayo tumekuwa tukijiwekea sisi, wenyewe kwa sababu tu kuna rafiki amekuwa akionyesha utajiri na thamani ya Mali zake ambazo wakati mwingine hatuna uhakika Mali hizo Americana kwa namna gani...

Changamoto hiyo imewafanya vijana wengi kupambania maisha kwa lengo la kuwa kama Fulani au kumiliki Mali Fulani ili aonekane ni.kijana mwelevu na mwenye akili ya maisha. Changamoto hii imegeuka kuwa sababu ya vijana wengi kupoteza maadili yao katika kazi walizoajiliwa, wamekuwa wakitumia nafasi zao vibaya kuiba Mali ya ofsi au ambayo ilipaswa kuwafikia watu.

Watu wamekuwa wakijiuza miili yao, kuuza madawa ya kulevya na kuiba lengo ikiwa ni kutengeneza hadhi (status) katika macho ya wengi wakodoleao mitandao  ya kijamii. Ndio maana leo ufasinisi wa kazi ni mdogo, heshimu ya nafasi zao ni ndogo.
Ni vyema vijana wenzangu tukasimama katika misingi ya uadilifu na kuacha kuishi ya kukopi katika mitandao ya kijamii, maisha ambayo sio halisi ni.maisha ya show off....

Ukitaka kuwa mkubwa ni vyema sana kuishi kwenye malengo yako.na kuhakikisha kuwa unayasimamia kwa asilimia kubwa, maana hapa.duniani we have an equal chance to make our life better