Thursday, August 31, 2023

incentives.

• Sixth, all employees must have a path to give feedback on the success of the process.

• Seventh, all employees must actively participate in the procedure.

• Eighth, the change may involve strategically-planned corporate “interventions” such as mergers.

Organizational Leaders

Many business experts believe that this type of leadership should come from the human resources department. An article in Forbes Magazine says the most important factor in organizational change is managing human capital. The article author says that human resource departments should focus more on being “strategic business partners” and less on implementing HR policies. The article goes on to say that the most important components of the development are identifying options for change that are available to the corporation and then to look at employees in terms of management talent and how to recruit, train and keep that talent.

HR also should be responsible for creating a motivational program that would permeate the entire organization. Obviously, the kind of assessment and change discussed here necessitates the leadership of people who understand human and organizational behavior and other components of the challenge of organizational change. Universities offer degree programs for professionals that include undergraduate and graduate degrees as well as doctoral degrees and certifications. Certificates can generally be earned in less than a year and can supplement other business degrees. Students take courses in areas like communications, conflict resolution, staff development, and human resource management.

ELIMU YA PADRE WA KANISA KATOLIKI

(Sehemu ya Tatu)

Na. John-Baptist Ngatunga
___________________________

Sifa za Kipee za Viongozi wa Kanisa Katoliki:

1. Baadhi ya Sifa hizo ni kwamba, Viongozi hawa kwa kawaida huwa hawahangaiki na Vioja; wanahangaika na Hoja. Ukija na Hoja watakujibu kwa Hoja; ukija na Vioja wala hawakuhoji. Wanajibu Hoja kwa Hoja sio Hoja kwa Vioja.

2. Mfumo wao wa kutatua changamoto daima huwa ni Majadiliano zaidi kuliko Mabishano. Hawawezi na hawapendi kubishana, ila wanapenda kujadiliana. Hii ni kwasababu wanajua kuwa kubishana ni kutaka kujua nani yuko sahihi ila kujadiliana ni kutaka kujua nini kipo sahihi. 

3. Wanapenda kucheza na Masuala (Issues) sio watu. Wanajadili Masuala hawajadili sana Matukio au watu. Ndio maana hata linapotokea jambo la Kitaifa kama hili suala la Mkataba wa Bandari kati Tanzania na DP World waliongelea suala lenyewe yaani MKATABA na wakajikita katika Hoja hiyo. Hawajamlenga Mtu au Watu. Wamezungumzia Mkataba (Issue) sio Watu na Dini zao au Makabila yao.

4. Hawana desturi ya kukurupuka katika Maamuzi yenye maslahi mapana kwa Jamii. Wanajipa muda wa kutosha kulitafakari jambo, kusali na kuliombea Taifa au Jamii, kufanya Tafiti juu ya jambo kabla ya kutoka hadharani na matakamko. Ndio maana wakitoa WARAKA au TAMKO unakuwa Mjadala wa Kitaifa. Na ndiyo desturi ya Wanafalsafa (They don't rush to conclusion without premisses).

Tofauti na baadhi ya Taasis ambazo hukurupuka tu kama chafya na kutoa matamko bila kufanya Tafiti. Wakati mwingine badala ya kujikita katika NINI, wao wanajikita katika NANI. Badala ya kujibu Hoja kwa Hoja wenyewe wanawashambulia watoa Hoja. But it's not to the Catholic Church.

5. Kwa kuzingatia historia ya Maisha yao ya Kitaaluma, usomi, akili, upeo na uelewa mkubwa walio nao;  itoshe tu kusema kuwa Kanisa Katoliki ni moja ya Taasisi zinazoongozwa na Viongozi wenye Matumizi mazuri sana Akili. Na kwamba 'Intelijensia' ya Kanisa Katoliki huwa haibabaishi, haibahatishi, haikisii, haikurupuki, haionei, haidanganyi. Ipo objective na inatenda haki.

6. Na kutokana na hilo sitakuwa nimekosea nikisema, "The Catholic Church is the Big Brain Institution; Full of Competent, Confident and Confidential Intellectuals led by the Power of the Holy Spirit to lead God's people bodily and Spiritually" (Kanisa Katoliki ni Taasisi yenye Akili kubwa; iliyojaa Wasomi Mahiri, wanaojiamini na wasiri wanaoongozwa na Nguvu ya Roho Mtakatifu kuwaongoza watu wa Mungu Kimwili na Kiroho).

7. Viongozi hawa ni Watu wenye Moyo wa kusaidia sana Jamii kwa kutoa Huduma mbalimbali za Kijamii ili kuiinua Jamii kutoka Lindi na Tupe la Umasikini. Angalia Huduma za Kijamii zitolewazo na Kanisa: Elimu, Afya, Maji, Nishati ya Umeme, Ajira, na nyingine nyingi.

8. Hawa Viongozi wakiliamua jambo lao, ni lazima tu litafanikiwa kutokana na umakini, umahiri, uchapakazi, kujitoa, uadilifu, Imani. Angalia Jinsi Taasis za Elimu na Afya wanazozianzisha, kuzisimamia na kuziendeleza zinavyofanya vizuri: Angalia Vyuo Vikuu kama:
(i) St. Augustine University of Tanzania (SAUT) 
Pamoja na Vyuo vyake Vishiriki vyote

(ii) Ruaha Catholic University (RUCU)

(iii) Catholic University of Health and Aliened Sciences (CUHAS -BUGANDO)

(iv) Mwenge Catholic University (MWECAU) 

Sijavitaja Vyuo vya Kati, Seminari Ndogo na Shule za Sekondari ambazo zinafanya vizuri sana Kitaifa na Shule za  Msingi.

Angalia pia Hospitali mbalimbali:
(i) Hospitali ya Rufaa Bugando (Mwanza)
(ii) Hospitali ya Peramiho (Ruvuma)
(iii) Hospitali ya Ndanda (Mtwara)
(iv) Hospitali ya Ifakara (Morogoro)
(v) Hospitali ya Lugarawa (Njombe)

Zijavitaja Vituo vya Afya na Zahanati.

Na kwa hapa Tanzania ukiiondoa Serikali katika suala la utoaji wa Huduma za Jamii, Taasis inayofuata ni Taasis inayoongozwa na Viongozi hawa: Maaskofu, Mapadre, Watawa (Mabrother na Masista) yaani Kanisa Katoliki. Na usipolitaja Kanisa Katoliki kwa hilo utakuwa aidha haujui au unachuki binafsi.

9. Viongozi wa Kanisa Katoliki wanaupenda UKWELI. Na Mtumishi wa Mungu Father John Hardon, SJ aliwahi kusema, "Our Duty as Catholics is to know the Truth; to live the Truth; yo defend the Truth; to share the Truth with others; to suffer for the Truth" (Kazi yetu kama Wakatoliki ni kuujua Ukweli; kuuishi Ukweli; kuulinda Ukweli; kuutetea Ukweli; kuwashirikisha wengine Ukweli; kuteseka kwaajili ya Ukweli).

Na kimsingi huyo UKWELI ni YESU KRISTO. "Yesu akawaambia, 'Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba; ila kwa njia ya Mimi'" (Yohane 14:6)

10. Kutokana na ukweli huo, Viongozi hao wa Kanisa Katoliki huheshimiwa sana na Waamini wao. Na hapa nikuambie tu ukweli kwamba kwa Muamini Mkatoliki, anawaheshimu Viongozi hawa pengine kuliko Kiongozi wa aina yoyote ile unayoijua wewe.

Na linapotokea jambo lenye ukinzani kati ya Viongozi wao na Mtu au kundi fulani la watu, ni rahisi sana kwa Mkatoliki kuufuata upande wa Viongozi wao. Ukitaka kuamini hiki ninachokuambia, fuatilia suala zima la TAMKO LA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA (TEC)  KUHUSU MKATABA WA BANDARI.

Sio kwamba Waamini hawa Wakatoliki wanafuata tu mkumbo la hasha. Hii ni kwasababu wanawajua vizuri sana Viongozi wao kuwa wako serious (makini) sana na mambo yao. Ni Viongozi ambao wanaongea wanachokimaanisha na wanakimaanisha wanachokiongea.

Sio kama walivyo baadhi ya Viongozi wengi wanaoleta Propaganda za kishamba na Siasa za kitoto ambazo zina athari kwa Jamii wanayoiongoza halafu wenyewe hawajali, wabinafsi na wanaoyajali matumbo yao tu bila kuwa na jicho la huruma kwa raia wengi wanaotaabika kwenye wimbi la ufukara ulipitiliza.

Viongozi ambao wakati mwingine unaweza ukadhani labda Akili zao zina makengeza. Wanatamani kukiona hiki ila macho hayana ushirikiano na mshikamano na uso wao. Ni Viongozi ambao wanajua Ukweli lakini hawako tayari kukusema ukweli au wanaogopa kumshauri Boss wao kisa tu Boss ameshaonesha mwelekeo fulani wanaoujua kwahiyo wanaogopa kumshauri tofauti na ukweli kwa kuogopa kuvipoteza Vyeo vyao.
Very hopeless Leaders!!

11. Viongozi wa Kanisa Katoliki wana BUSARA. Na ninaposema Busara namaanisha, "Matumizi sahihi ya Maarifa". Ni wasomi walioelimika. Yaani ni wasomi wanaojua kuitumia Elimu yao kwa manufaa yao na manufaa ya Jamii inayowazunguka. 

Unajua, hapa Tanzania tuna Wasomi wengi sana na tuna Viongozi wengi sana Wasomi ambao hawajafanikiwa kuelimika. Waliosoma ni wengi ila walioelimika wako wachache sana. Wengi wamesoma ila wachache wameelimika. 

Ndio maana tuna baadhi ya Viongozi ambao jinsi wanavyotumia Elimu na Akili zao katika baadhi ya Maamuzi huwezi kuamini kama kweli walifundishwa na Walimu wenye Vyeti halali au ni wale wa Vyeti Feki. Ukiwasikiliza jinsi wanavyotengeneza Logic zao katika maongezi unaweza ukadhani labda ni watoto wanaojifunza kuongea.

12. Viongozi wa Kanisa Katoliki ni mfano halisi wa MCHUNGAJI MWEMA ambaye Yesu Kristo Mwenyewe kwa kinywa chake alimsema, "Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema hutoa nafsi yake kwa ajili ya kondoo...... Mimi ndimi mchungaji mwema, nawajua walio wangu, nao walio wangu wanijua Mimi" (Yohane 10:11,14)

Mchungaji Mwema ana sifa kuu Tatu:
1. Mwema
2. Huitoa nafsi yake kwaajili ya kondoo wake
3. Huwajua kondoa wake nao walio wake wanamjua

Hawa Viongozi ni WEMA kwa kuwa wana NIA NJEMA na Wakatoliki na hata wale wasiokuwa Wakatoliki yaani ambao hawamo katika 'Zizi' la Ukatoliki (Yohane 10:16). Maana yake Mapadre na Maaskofu wetu ni WEMA kwa Watanzania wote. 

Viongozi hawa WANAZITOA NAFSI ZAO kwaajili ya Taifa la Mungu. Ndio maana wanapambana kuzitetea Rasilimali za Taifa hili kwa manufaa ya Watanzania wote japo wasiojua wanawatukana badala ya kuzijibu Hoja zao kwa Hoja.

Wanawajua Waamini wao wanataka nini na Waamini wao nao wanawajua Viongozi wao na wanawaheshimu. Ndio maana nilisema kwa Mkatoliki kindakindaki, huwezi kumwambia chochote kinyume na Wachungaji wao akakuelewa. Hii ni kwasababu Maaskofu na Mapadre wanajuana na Waamini wao.

Hapa nimejaribu kugusia tu kwa uchache kuhusu namna Padre wa Kanisa Katoliki anavyopitia Maisha ya Kimalezi ya Kiroho, Kielimu na Kijamii kwa wale wenye Wito wa Upadre. Lakini kama ulikuwa umenifuatilia toka mwanzo nimeelezea kuhusu upatikanaji wa Viongozi hawa na Elimu zao. Sasa kazi ni kwako kupima kati ya Elimu ya Viongozi wa Kanisa Katoliki na Elimu ya hao Viongozi wanaokuongoza Kidini au Kisiasa nani wanatumia vizuri Elimu  na Maarifa yao?

Niishie hapa!!

Sunday, August 20, 2023

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kurejeshewa 

Nina mfano wa rafiki yangu mmoja ambae alidhamiria kukamilisha ukarabati wa nyumba yake, sikiliza nikuambie, 
Rafiki alipokamilisha ukarabati wa kina kwenye nyumba yake
. Nilipokuwa nikifuatilia safari yake kwenye Facebook, nilishusha na kufurahia picha za bafu lake jipya kabisa. Nilifikiria ingekuwaje kuwa na hiyo nyumbani kwangu!

Pia niliona picha za kazi zao zinazoendelea, ambazo zilinisaidia kutambua ni muda gani, juhudi na kujitolea vilivyotumika kuunda mradi uliorejeshwa kwa uzuri. Bila kusahau vipaji vyao vya kujenga na kubuni.

Wednesday, August 16, 2023

Kwangu mimi, ni heshima kubwa. Ni bahati kubwa kuwa sehemu ya klabu hii kubwa, sehemu ya familia hii

Andre Onana ni nani?
 Andre Onana anatokea wapi, kwa nini amejizolea umaarufu kwa kasi hivi ukilinganisha na miaka miwili mitatu nyuma ?

Andre Onana kwa kifupi kabisa ni mmoja kati ya Magolikipa mahili sana katika soka la kisasa, Ni ajabu sana kumkuta GK wa Kiafrika akiwa kwenye lango la Team kubwa barani Ulaya lakini yeye amekuwa miongoni mwa hao wachache waliovunja record hiyo tena akiwa na man utd iliyokuwa na David De Gea kwa misimu 12 iliyopita

Monday, August 14, 2023

Mahusiano mazuri ya wazazi ni muhimu katika malezi ya watoto

Watoto hujifunza kutokana na matendo ya wazazi wao, kama watoto wakilelewa kwenye familia yenye mifarakano na kutokuelewana baina ya wazazi wao mara nyingi watarithi tabia hizo. Wakilelewa kwenye familia zenye mahusiano mazuri, majibizano yenye kuheshimiana nao watathamini umuhimu wa mahusiano. Tatizo kubwa linalopelekea mahusiano kuzorota ni mawasiliano dhaifu. Udhaifu wa mawasiliano tunaozungumzia ni pamoja na kukaripiana, kutukanana, kununiana na hata kusonyana mbele za watoto wenu.

Hili laweza kuwa tatizo la mahusiano yenu, lakini kwa nini muwahusishe watoto? Kwani ugomvi lazima ufanyike sebuleni? Hakuna faragha kama chumbani mkakaa na kuzozana?

Kupaziana sauti mbele ya watoto wako inawaletea watoto madhara mbalimbali ikiwemo nidhamu ya uoga na kutojiamini na hivyo kumyima fursa ya kuwa mdadisi na kudhoofisha uwezo wa akili yake kukua kadiri ya umri wake. Kwa maneno mengine, unamdumaza mwanao kwa wewe kutohsiana vyema na mzazi mwenzio. Wewe ni mama au baba kwa mtu na si vinginevyo. Hivyo majina mnayoitana mkiwa na mihasira yenu yanawaondolea uhalisia na heshima mbele za watoto wenu.

Inawezekana kabisa mzazi mwenzako ni mkorofi na hajali kama kuna mahitaji ya watoto na familia kwa ujumla. Ingawa tunatambua umuhimu wa kushirikiana katika kulea watoto, busara inahitajika katika kuhusiana na mwenza mkorofi wa namna hii katika ndoa. Haingii akilini kwa baba au mama kumcharaza mboko mwenza wake wa ndoa/mzazi mwenza kisa kakosea. Sasa unamcharaza viboko ili ajifunze ama unabomoa mahusiano yenu na maisha ya watoto wenu bila ya wewe kujua?

Suala lingine linaloathiri maadili ya watoto amabalo ni la kimahusiano katika familia ni ubinafsi uliokithiri kwa baadhi ya wazazi. Kuna wazazi ambao wanaishi kwa sheria ndani ya nyumba kwa kuwazuia wenzi wao ikiwemo watoto kutotumia baadhi ya miliki zilizomo ndani ya nyumba zao. Kwa mfano, kama baba hayupo TV, Radio, nk. haviwashwi ama akiwepo basi woote mnaangalia anachotaka yeye na hakuna mjadala juu ya hili. Bado yote haya ni kutowaheshimu wezi wao wa maisha. Dharau unazomfanyia mwenzio mbele ya watoto wenu unajenga maisha ya watovu wa nidhamu. Watoto namna hii hawatoweza kuwaheshimu watoto wenzao na hata watu wazima ikiwemo waalimu. Matokeo yake watoto hawa itawawia vigumu kusoma darasani na mara nyingi wataishia mitaani kuhangaikia matumbo kwa kugaagaa kuganga njaa ukubwani. 

Ikiwa huna mahusiano mema na mkubwa mwenzio vipi utakuwa na mahusiano wa watoto wenu? Watoto pia wanakumbana na changamoto kama ilivyo kwa watu wazima na wanahitaji mtu wa kuwasikiliza na kuwapa ushauri wa namna ya kuzitatua changamoto hizo. Kutokana na kukosekana kwa mahusiano na mawasilianao mazuri baina ya wazazi na watoto wao, watoto wanapata wakati mgumu kujenga ukaribu na wazazi. Pindi wanapopata changamoto, hasa katika kipindi cha balehe kwa kuogopa kuwahusisha wengi wao hutumbukia katika matatizo makubwa kama kutumia madawa ya kulevya na mimba za utotoni. Kuna wazazi ambao kwao ni mwiko kuongea na watoto wao ana kwa ana na badala yake husikiliza mahitaji ya watoto kupitia mzazi mwenza! Matokeo yake mtoto akipatwa na matatizo wazazi hawa mara nyingi huishia kuwalaumu wenza wao ambao eti wameshindwa kulea. Mmeshirikiana kuzaa. Shirikianeni kulea.

Familia nzuri na yenye amani hujengwa kutokana na uhusiano thabiti wa wanafamilia hasa baba na mama. Familia namna hii inayo mazingira muafaka kwa makuzi ya watoto. Ubora wa mawasiliano, uchaguzi wa maneno ya kusema hasa uwapo na hasira mbele za watoto ni muhimu kwa ukuaji na maendeleo ya watoto. Kutofautiana katika mahusiano kupo. Lakini ugomnvi wa maneno kati yenu ufanyeni faraghani, chumbani, n.k. Inawezekana

Prepared by Moses Z. Mgema