Monday, October 25, 2021

ROHO YA KUCHELEWA ( THE SPIRIT OF DELAY) EP 1.

Bwana asifiwe mtu wa Mungu
Nipende kumshukuru Mungu kwa nafasi ya pekee ambayo ametupa tena kwa neema ambayo ni upendeleo wa Kimungu kwetu.
Leo tutajifunza neno la Mungu lenye kichwa cha somo ROHO YA KUCHELEWA ( SPIRIT OF DELAY).
Katika somo hili tutaona mambo kadhaa ambayo yamekuwa chanzo cha watu wengi kuchelewa kufikia hatima zao na bado wanachukulia kawaida bila kujali muda wa nyakati za kutimiza baadhi ya mambo katika wakati uliokusudiwa.
Note
Sio kila jambo linalochelewa ni mpango wa Mungu hapana ndivyo ilivyo hata kwa upande wa kuwahi kuwa sio kila jambo linalowahi ni mpango wa Mungu. 
➡️Mambo mengine yanachelewa kwa sababu za michezo anayoicheza shetani katika ulimwengu wa Roho bila watu wengi kujua na hivyo kuchukulia kawaida.
➡️ Mambo mengine pia yanawahi sio kwa mpango wa Mungu bali shetani anaweza kuwa amechungulia mbali na kuiona baraka yako iliyo kuu hivyo anapenyeza baraka feki kwa haraka ili kukupishanisha na Baraka ya Mungu.
Lakini hapa tutazungumzia somo lenye kichwa cha somo la Roho ya kuchelewa ( Spirit of delay).
Daniel 10:13-21
Habari ya Daniel aliyejulikana kama Belteshaza ambae majibu ya maombi yake yalishikiliwa na mkuu wa uajemi.
Hapa tunaona pamoja na Daniel kuomba na kufunga kwa majuma matatu lakini bado malaika aliyeagizwa na Mungu kuleta majibu ya Daniel alishikiliwa kwa kwa siku 21 sawa na majumaa matatu ya ambayo Daniel pia alitumia kumwomba Mungu wake.
Hapa nataka uone ni kwa kiasi gani shetani yupo kwa ajili ya kupambana kuhakikisha kwamba hupati kuwa sehemu unayopaswa kwa wakati sahihi uliokusudiwa na Mungu.
Tunayo mifano mingi ambayo imekuwa kama maisha ya kawaida kwa vijana wengi, mfano mtu anamaliza shule badala ya kutafuta kazi hata ndogo kutwa anatembea na vyeti kuomba kazi maofsini, anashindwa kutambua kwamba uzima, elimu na afya aliyo nayo ni mtaji namba moja kwenye maisha.
Mwaka 2016 wakati natoka chuo, nilikuwa na akili nyingi sana kwa sababu nilikubali kuanzia kwenye kiwango nilichokuwa nacho nikaanzisha biashara ndogo ndogo ya chakula mkoani kwangu singida na biashara ilikuwa inakwenda vyema sana na kipato changu ilifikia ikawa inaanzia laki tatu kwa mwezi na mtaji wa kwanza ilikuwa Tsh 30000 tu nilianza na miwa, miwa akaadimika nakaingia kwenye uji, chai na hatimae niliifikia hatua ya kuuza chakula cha mchana na ukuajia wake ulikuwa mkubwa sana.
Wakati naanza kufikiria kufungua mgahawa wakimataifa nikapata tangazo la kazi ambalo lilinifanya kuomba kazi kwa kweli kati ya makosa nimewahi kufanya nikuacha kazi zangu kwenda kwenye kazi ambayo nilifikiri ingenipa zaidi kumbe nilikuwa narudi hatua kadhaa nyuma.

Usiku wa juzi ndio Mungu alinipa mafunuo kwamba watu wengi wanachelewa kufikia malengo kwa sababu shetani amejiingiza katikati ya fikra za watu nakuanzisha mission ambayo imekuwa ni chanzo cha kuchelewesha baadhi ya mambo hasa kwa vijana.

Kijana unakuta anapambana kutafuta ajira na umri unakwenda mwisho wa siku alikuwa na maono makubwa anakuja kuishi kwenye robo ya maono yake kisa alishindwa kutambua kwamba mtaji wa kwanza sio fedha bali ile akili ambayo amepewa na Mungu inaweza kuwa mtaji mkubwa wa kumfanya kuishi kwenye maisha aliyokusudiwa kwenye wakati sahihi.

Wengine wameondolewa shauku ya kuoa, fedha anayo, maisha ambayo yanaweza kuendesha familia vyema anayo lakini, hataki kuoa anaona kama wakati bado kumbe ndani yake shetani ameishaingia maana anajua kwamba kijana huyu akipata mke atakuwa amejipatia kibali kwa Bwana, na maana ya kibali ni upendeleo mkuu kutoka kwa Mungu na kuwa kwenye ndoa mtu anaweza kufanya vizuri zaidi kuliko akiwa pekee yake.
Wengine wamepandikizwa roho yakujiona bado ni watoto hasa vijana wa kiume, na mabinti nao Roho ya kuchaguachagua katika ule wakati sahihi ambao mtu alipaswa kuolewa hapa shetani anacheza na ufahamu wa binti mwisho wa siku umri unakwenda anaamua kuolewa na yeyote atakae kuja ili mradi amepata mume kumbe mtu sahihi alishakuja lakini kwa sababu ya kufungwa ufahamu binti alijiona bado au yule kijana alimwona sio hadhi yake.
Shetani pia amekamata kwenye eneo la elimu, kila jambo huwa linapaswa kuwa ndani ya muda fulani ndio maana kuna umri wa kuanza shule ya msingi na kuna umri mtu anapswa kuwa amemaliza chuo kikuu lakini unaweza anafeli masomo bila sababu za msingi na anakosa ufahamu hata wakuendelea na hatua ya cheti anarudia tena kidato cha nne anafeli tena, anarudia umri unakwenda na mtu anachukulia kawaida kumbe shetani amejiweka kwenye nafasi ambayo ni ngumu kuelewa isipokuwa uwepo wa Roho mtakatifu ndani yake ambayo itamfunulia vizingiti vilivyowekwa na shetani.
Magonjwa na changamoto zingine, ni kweli mtu amepata kazi lakini shida na matatizo ni chungu nzma kila wakati wa mshahara ukifika unasikia shangazi anaumwa, mama anaumwa, au misiba hivyo kumalizia fedha yote kwenye kutatua changamoto za kifamilia badala ya kupiga hatua ya maendeleo yako, hivyo unakuwa unazunguzunguka tua hapo.
Ndugu zangu inatupasa kumkatibia sana Mungu ili kuweza kutambua vita vya kiroho ambazo shetani amekuwa akizipigana dhidi ya ndoto na maono ya vijana wengi.
Biblia inasema katika kitabu cha Yak 4:7-10
Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. 
Ukiishi karibu na Mungu ni rahisi sana kujua makusudi na malengo mabaya ya shetani hivyo ni rahisi kupigana vita hivyo maana unajua njia anazotumia shetani kuharibu au kukuchelewesha 
usikubali kupiga makitaimu sehemu moja kwa muda mrefu yawezekana sio wewe bali yupo adui amejipenyeza katika safari yakuelekea maono yako.
Na ili uweze kutambua haya yote ni vyema kuishi maisha yakumpendeza Mungu na shetani hawezi kupata mwanya wa kupenyeza roho zisizokuwa na ubora ambazo ni chanzo cha kukufanya kuishi maisha yasikusudiwa na Mungu.
Usifurahie na kuridhika na maisha yako ya kawaida jaribu kuishi maisha yenye kujitathmini kila wakati na kuishi kwenye maisha ya kuomba na kusoma neno la Mungu hapo ndipo utangudua kama unatembea kwenye njia sahihi au umehamishwa na ibilisi unasafiri kwenye njia isiyo yako.
Usione kawaida kutokuwa kwenye ndoa au kwenye mchakato wa kufunga ndoa waakati umri umefika na Mungu ameshakubariki una kazi nzuri na uwezo mzuri tu wa kuendesha maisha pamoja na mwenza wako.
Ukiona changamoto ni uchumi.au kikwazo fulani, ikatar hiyo hali kwa vitendo chukua hatua na Mungu atakuonekania kwenye hatua yako lakini usipoanza hatua fulani kila mwaka utaisha uko pale pale mambo hayaendi kumbe njiani shetani amekaa na wewe unaona kawaida.
Kushinda yote haya mwombe sana Mungu, mkaribie Mungu, mruhusu Roho mtakatifu aweke makao ndani yako ili kuweza kukupa maarifa ya kujua kila mtego na kuutegua. 
Somo hili litapatikana Youtube kuanzia wiki ijayo kwa njia ya video
Kuanzia ijumaa subscribe channeli ya ngu Ms Tv kwa maarifa ya kimungu na maisha ya kila siku
Moses Mgema
0755632375
0715366003
mgemamoses@gmail.com
God bless you so much





Friday, October 22, 2021

HUDUMA YA UIMBAJI NDANI YA KANISA

Mwalimu: Musa (Moses) Zephania Mgema
Ijumaa tarehe 22/10/2021
FPCT -Singida town centre church.
Uimbaji ni nini ?
Ni sanaa ambayo inatumika kuwasilisha ujumbe kwa njia ya lahani (chord) na mpangilio wa sauti wenye kutengeneza ladha yenye mvuto kusikiliza.
➡️Uimbaji asili yake ni mbinguni. Huduma hii ilianzia mbinguni na kiongozi wa huduma hii huko mbinguni alikuwa anaitwa lusifa kabla ya kuasi.
Ezekieli 28:13-15
➡️Huduma ya uimbaji ni moja kati ya huduma muhimu ndani ya kanisa kwa sababu imefanyika chumvi nzuri kwa ustawi wa kanisa na hata huduma nje ya kanisa.
Uimbaji katika mfumo wa injili kwa maana ya nyimbo za kiroho sio burudani bali ni huduma nyeti na ya msingi wala sio burudani au huduma ya ziada ndani ya kanisa.
➡️Huduma ya uimbaji ni huduma ambayo haina mwisho maana hata baada ya unyakuo kazi pekee tutakayoifanya huko mbinguni ni kuimba tu.
Ufunuo 5:9-10
Ufunuo 15:2-4
➡️Hapa duniani kazi ya uimbaji ilianza muda mrefu tangu enzi za agano la kale ni hii ni mara tu baada ya kuumbwa kwa Adamu na Hawa.
Mwanzo 4:21

KWA NINI HUDUMA YA UIMBAJI NDANI YA KANISA.
1petro 4:10-11
1Nyakati 6:31-32
1. Huduma ya uimbaji ikitumika vyema kwa kuongozwa na Roho mtakatifu, maombi na Neno la Mungu huleta mavuno mapya ndani ya kanisa.
2. Hufanya moyo wenye huzuni kupata furaha na Amani.
3. Hubadili moyo mgumu kuwa laini 
      1samweli 16:23
4. Mtu dhaifu hutiwa nguvu na uzima 
     1samweli 18:6-9
5. Hudhihilisha uwepo wa Mungu.
      2Nyakati 20:21-22
     2Falme 3:15-16
     Matendo 16:25-26
HUDUMA INAYOONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU, MAOMBI PAMOJA NA NENO LA MUNGU-
1.  Huonya na kufundisha kolosai 3:16
2.  Ni mahubiri kamili  Isaya 48:20
3.  Huleta faraja kwa waliokosa tumaini.
4. Humsifu na kumshukuru Mungu kwa matendo makuu 
Nb:
Zipo pia nyimbo za upuuzi kama ambavyo 
 Amosi 6:5 anaonyesha.
➡️Kama mtumishi wa Mungu unaetumika kwa njia ya uimbaji ni muhimu haya yafuatayo kuwa sehemu ya wimbo unaohudumia watu
1. Roho mtakatifu kuhusika
2. Neno la Mungu kujaa kwa wingi ndani ya mwimbaji.
3. Kufanya maandalizi kabla ya huduma kwa maana ya kuomba, kusoma neno na kuruhusu Roho mtakatifu kukuongoza ili kufanya huduma yenye connection ya mbingu na wewe kama mhdumu.
➡️Huduma ikiwa na uongozi wa Mungu lazima iwe ni ibada kamili ambayo itadhihilisha matendo makuu ya Mungu, mfano uponyaji, Faraja, nk.

➡️Tunaweza kujifunza kupitia wimbo alio imba Musa mtumishi wa Mungu na Israel baada ya kuwashinda wamisri.
 Ufunuo 15:3
➡️Ulikuwa wimbo wa matendo makuu ya Mungu
Aina nyingine ya nyimbo ni nyimbo ya mwanakondoo (Wimbo mpya) ambao unaelezea namna Yesu anavyostahili kuabudiwa, kupewa sifa kwa matendo makuu ambayo ametenda kupitia msalaba.
Zaburi 40:1-3
Ufunuo 14:1-3
Ufunuo 15:5-9
Wimbo ukitungwa kwa uongozi wa Mungu mwenyewe huwa ni wimbo wenye nguvu na huleta matokeo kusudiwa.
Ukiona waimbaji/mwimbaji anaimba na wala hakuna connection ya Kimungu, hiyo ni ibada ya sanamu ambayo imebeba kujiburudisha nafsi na ni makelele mbele za Mungu.
➡️Mwimbaji lazima ajawe na Roho mtakatifu kwa wingi ndani yake, Neno la Mungu na awe mtu ambae anaiombea huduma yake kwa kujitoa ili kuwa na huduma bora na yenye nguvu za Mungu.
➡️Ipo mifano ya huduma za uimbaji katika agano jipya na agano la kale ambavyo Mungu alohudumia watu kupitia waimbaji 
Luka 1:41&67
Efeso 5:18-20.
Kwa ufupi uimbaji ni kazi ya Roho mt. nje ya Roho mt.  uimbaji unabaki kuwa burudani tu, maana ni ngumu sana kuyaona matendo ya Mungu yakidhihilika.
➡️Uimbaji ukiwa na uongozi wa Mungu hiki tegemea kukiona kwa ukubwa katika huduma yalo ya uimbaji  2Nyakati 5:13-15
Neno la Mungu ni huduma kamili ya uimbaji hivyo kwa sababu neno ni chanzo cha ujumbe na mafunuo mengine ya kimungu lazima mwimbaji awe amejaa neno ndani yake, hii husaidia kuwa na huduma yenye matokeo.
Zaburi 45:1
Wakolosai 3:16
Mwisho.
Msingi wa huduma yeyote ya kimungu lazima iongozwe na 1. Neno la Mungu
                       2. Roho mtakatifu
                       3. Maombi na utii wa Mungu.
Ukiwa na hivi vyote lazima uwe na huduma ya nguvu za Mungu ndani yake
Mungu akubariki sana kwa kunisikiliza
0715366003 whatsup
0755632375 call and sms
mgemamoses@gmail.com