Monday, May 20, 2019

USIKUBALI CHANGAMOTO NA SHIDA ZIKUONDOE KWENYE NJIA YA KUELEKEA MALENGO NA NDOTO ZAKO.

Tangu mwanzo wa muundo wa dunia, ukisoma historia ya dunia kwa mfumo wa maisha ya kawaida, kwa mitume na manabii walipitia changamoto, shida, vikwazo vingi mpaka kufikia malengo, ndoto hata mafanikio ya ambacho walilenga kukifanikisha hapa duniani.

Ndivyo ilivyo hata kwenye ulimwengu tulio nao leo, mafanikio ya kila mtu yamezungukwa na vikwazo, changamoto, mambo mengi ya kukatisha tamaa, kiasi kwamba sio rahisi kupasua na kufikia malengo na ndoto kama utaruhusu changamoto hizo zikuondoe kwenye njia.

Dhahabu haiwezi kuwa dhahabu kama haijapitia mchakato sahihi wa kupatikana. Ni nini maana yake: Ni kwamba kitu chochote kizuri kinahitaji mtu kujitoa, kufanya kazi kwa bidii na kwa ufanisi mkubwa ili kufikia kitu au jambo hilo zuri.

> Ili ufaulu masomo inakulazimisha kusoma kwa bidii na kwakutumia muda mwingi kusoma, kujadili na kujiepusha na mambo mengine ambayo yanaweza kuwa sababu ya wewe kufeli.

>Ukitaka kuwa mwimbaji mzuri unahitaji muda mwingi wa kufanya mazoezi, kusikiliza wengine wanafanya nini, kujifunza kila wakati.

>Ukitaka kuwa tajiri na huna misingi mizuri ya mitaji, huhitaji aibu katika kupambana ili kuweza kutoka mahali ulipo kwenda eneo lingine ambalo unataka kufika, utafanya kazi zisizofaa kwa macho ya kawaida lakini ndo unapaswa kufanya ili kesho yako iheshimike.

>Ukiwa na mtaji na unatokea mazingira mazuri kiuchumi and you're well supported lakini bila kuwa makini, kujinyima, kuongeza ubunifu kwenye biashara au kazi yako utajikuta unafeli.

√ Kwa hiyo unahitajika kufanya kazi kweli kweli katika eneo ulilopo, lakini pia kumbuka yako mengi magumu na yakukatisha tamaa kama hutojipanga kukabiliana nayo unaweza jikuta unaishia njiani,

Chakufanya...........

Kumbuka kuna nyakati ngumu na majira magumu ambayo ni kama Mungu haoni jitihada, nguvu, na maarifa mengi unayotumia ili kuyafanya maisha yako kuwa bora na mazuri

Kumbuka hata katika hayo Mungu amekuamini, hali yako uliyo nayo leo ni ya muda tu wala siyo ya kudumu, cha msingi endelea kupambana, kufanya kazi kwa bidii katika nafasi uliyopo, omba Mungu ipo siku utafanikiwa na kuwasimulia wengine.

> Changamoto ni silaha yako
> Mungu amekuamini na anajua unaweza. Kuna wakati tunapitia maisha yakuumiza kuondokewa na watu wakaribu, Baba, Mama, mke, kuachwa na mpenzi au mke/Mume lakini yote hayo yanakuja kwa sababu Mungu amekuamini sana.

> Don't be taken away from your focus, plans, kimbia kwa kadiri uwezavyo hiyo ndiyo silaha yakufikia unapotaka

Yesu aliumia na alipitia mateso kufikia lengo why not you ?. Zifanye changamoto kuwa sehemu za maisha na huwezi kuzimaliza na kila hatua unayopiga ndo zinavyozidi kuwa nyingi lakini pia katika hayo njia za kutatua zipo.

Mungu amekuamini, usimwangushe chini, pigana, pambania mafanikio yako huo ndo msingi sahihi wa maisha ya mtu mwenye lengo la kutimiza ndoto zake.
Musa/Moses Zephania Mgema
mgemamoses@gmail. com
0715366003/0755632375
Dar es salaam, Tanzania.

Sunday, May 19, 2019

THAMANI NA FAIDA YA UTULIVU WA AKILI KATIKA MAAMZI NA MAISHA KWA UJUMLA

Hello Friend.
Rafiki na ndugu yangu nikushirikishe jambo hili la thamani na lenye maana sana kwenye maisha yako.

Kwenye maisha ya kila siku kuna mambo mtu anakutana nayo, mazuri kwa mabaya, ambayo yanamfanya kuishi kwa amani na furaha au kama ni Magumu au mabaya yanamfanya kuishi kwa kukosa amani, furaha na utulivu kuanzia kwenye akili mpaka huku nje.

Nikuambie leo rafiki tangu, kukosa utulivu, amani na furaha ya akili, inaondoa uwezo wa kufikiri sawasawa na sahihi na hii inapelekea kuondoa afya na ubora wa akili yako.

Matokeo yake unajikuta unaamua vibaya kila jambo na kuleta athali kubwa kwenye mfumo mzima wa maisha yako.

Changamoto zipo, ugumu wa maisha upo, wakati mwingine unafanya kazi kwa bidii, maarifa, ujuzi na kwa kila namna lakini hatua unayopiga ni ndogo au wakati mwingine hakuna kabisa.

Nikuambie kitu................

Utulivu ni jambo moja la msingi na muhimu sana kwenye maisha ya mtu kwa sababu ukiwa na utulivu wa akili na nafsi pia itatulia, matokeo yake sasa ni......
1. Utaamua vyema
2.Utaona njia ya kutatua tatizo/ changamoto hiyo
3. Maamzi yako hayatakuwa na matokeo hasi.
4. Kiwango cha Maamzi sahihi kitakuwa juu
5. Afya ya akili na nafsi itachukua nafasi yake.
6. Utaona watu/Mtu sahihi wakumshirikisha changamoto yako na wakati mwingine kupata ufumbuzi wa changamoto hiyo.
7.Utajenga ujasiri zaidi na kujiamini hata wakati mwingine hutayumbishwa na aina yoyote ya changamoto hata itakuwa ngumu kiasi gani.
8. Utakuwa msaada kwa wengine
9. Utaishi kwa tumaini na kujiamini vyema
10.Hutoyumbishwa na mazingira hata yaweje.

Kwa ujumla utulivu unafaida na thamani kubwa mno kwenye maisha ya mtu ya kila siku.

Hivyo usikubali tatizo, au aina yoyote ya changamoto ikakuondoa kwenye utulivu, ingawa kuna matatizo ambayo ukiyapata hakika yanaumiza na kukatisha tamaa lakini bado utulivu na hekima ukiruhusu vitawale na kuzuia Maamzi ambayo yanaongozwa na mazingira, mihemuko, na maumivu basi kwako itakuwa kheri.
Be blessed so much for reading this beautiful message.
Musa Zephania Mgema
0715366003/0755632375
mgemamoses@gmail.com
mosesmgema12.blogspot.com
Dar es salaam, Tanzania

Saturday, May 18, 2019

NI WEWE MWENYE MAAMZI NA MAISHA YAKO.

Hello Friend.
Nia yakufikia ndoto na malengo yako unayo wewe mwenyewe, lakini changamoto na vizuizi vimekuwa vingi na wakati mwingine ni vikubwa kuliko nguvu na uwezo ulio nao wewe, na kuna wakati unafikia mahali unakata tamaa. Lakini ni............

Mambo machache unapaswa kujifunza na kuelewa kwamba, haya yote yanakuja kwa sababu kwanza, Mungu amekuamini na ana uhakika kabisa kwa nguvu na uwezo alioweka ndani yako unaweza kukabiliana na aina hizo za changamoto na wewe ndo mtu sahihi kupitia changamoto au milima hiyo ya maisha.

Lengo ni kwamba anakunoa ili uwe kisu kikali zaidi ambacho kitakuwa na uwezo wakulalua kila aina ya jambo liliko mbele yako.

Huwezi kuwa mwalimu mzuri wa nyimbo, ujasiriamali, mambo ya kijamii, huduma kwenye nyumba za ibada bila kupitishwa.

Huwezi kuwa mwandishi, public speaker, motivational speaker simply, huwezi kumiliki fedha kwa njia rahisi kesho utashindwa na utaanguka na kukata tamaa na kufa kabisa.

Dhahabu haiwezi kuwa dhahabu safi bila kupita kwenye moto, moto unaifanya ing'ae na thamani yake kupanda na kila mtu kuihitaji kwa gharama yoyote ile. Ndivyo ilivyo hata kwenye maisha yetu kama binadamu.

Tunakuwa vizuri zaidi kwenye maeneo ya kazi zetu, kwenye matumizi ya vipaji vyetu pale tu inapotokea umepambana sana kufikia mahali ambapo ulitamani kuwa hapo kabla.

Mapambano ya muda mrefu ambayo ulikutana nayo njiani, ndiyo sababu ya wewe kuthamini kazi uliyo nayo, kipaji ambacho wengine wanacho ila bado hawajafika pale ulipo wewe Leo na wanatamani siku moja wawe hapo lakini bado wako mbaaali sana.

Kwa hiyo usikatishwe tamaa na vikwazo vichache vilivyopo njiani, pambana hakikisha focus yako iko klia isiyoyumbishwa na pepo za kiangazi ambazo zina mwisho na masika yaja.

Usiyumbishwe na kelele za watu hasa ambao wamefanikiwa na kushindwa, maana kila mtu anamtazamo na mawazo yake, hivyo ukiwasikiliza utapotea maana miruzi mingi humpoteza mbwa asie na mmiliki bali mbwa anaemjua bwana wake huitambua sauti ya mruzi wa bwana wake, kwa hiyo usie mbwa mwitu asie na bwana wake.

Maamzi ya kufika mbali kihuduma, kibiashara na kwenye eneo lolote ulilopo iko mikononi mwako, hakuna mtu anaweza kuyaamua maisha yako yaweje kesho isipokuwa wewe mwenyewe, sio mazingira, sio Sera za nchi sio changamoto yoyote bali ni wewe.

>Maamzi yako ndiyo dira yako
>Malengo yako ndiyo dira yako
>Kichwa chako ndo dira yako
>uwazavyo ndivyo unavyoiamua kesho yako.
>Uwezo na kipaji ndani yako ni urithi wa Mungu.

Mwisho
Jitathimini na kujipambanua kama unaona kuwa unapita kwenye njia sahihi ya kuifuluzia ndoto yako

Moses Zephania Mgema
0755632375/0715366003
mgemamoses@gmail.com
www.mosesmgema12.blogspot.Com
Dar es salaam, Tanzania