Tuesday, December 11, 2018

YOUR THE LIVING TESTIMONY/WEWE NI USHUHUDA UNAO ISHI.

Habari.
Mungu akubariki sana kwa kuendelea kuamini katika mfumo wa mabadiliko na mapinduzi ya fikra.

Mtu anae amini katika uwezo wake bila kujali mazingira, watu wanaomzunguka, hali ya kimaisha, Kielimu, kiimani na kadhalika mara nyingi mtu wa namna hii hufanikiwa sana kwenye maisha.

Mara nyingi huishi kwenye ndoto yake, malengo yake bila kujali amefikia ndoto na malengo hayo akiwa kwenye umri upi mwanzo kati au mwisho.

Mtu wa namna hii huwa hawaogopeshwi na hali yake, mazingira ila anachokiamini ni ule uwezo ulio ndani yake na kuamini kupitia uwezo huo ndiyo sababu ya yeye kuishi ndoto zake.

Sababu kubwa inayomfanya awe hivyo ni kuamini kuwa hakuna mtu aliumbiwa kuishi maisha ya hali fulani milele (uduni) na wengine kuwa na hali nzuri za kimaisha (utajiri).

Kupitia changamoto anazopitia humjengea shauku na imani kubwa ndani yake, kwamba kama wazazi wangu walishindwa kusapoti taaluma yangu kwa sababu ya Maisha duni,  umasikini wa kutisha basi, soluhisho la kuachana na hali hii duni, nikutumia uwezo mkumbwa ndani yangu kama daraja halisi la kunivusha hapa nilipo leo kwenda hatua bora zaidi ya kimaisha.

Hakuna kitu kizuri kama kuamini uwezo wako bila kujali wangapi wanakuona unajifurahisha, huwezi kufika popote  pale.

kuna watu wanavipaji katika maeneo tofauti tofauti ambao walipitia changamoto za kudharauliwa na kuonekana si chochote lakini kwa sababu waliamini walichonacho basi walipambana leo hii imebaki historia vijijini kwao na kuwaacha waandika historia za watu wakiendelea kujinasibu kuwa wanawajua sana huku wao wakila vyuku na bata mijini.

UMEWAHI KUJIULIZA UNA UWEZO GANI ?
Hili ni swali nyeti sana na muhimu kujiuliza hasa kwenye kipindi hiki cha ulimwengu kuamka na kutaka kila mtu kufanikiwa.
Mungu ameniumba mimi nikiwa na uwezo fulani, wewe pia...lakini je umeshatambua ?

Historia huandikwa na wengi lakini sababu ya historia kuandikwa na wengi kama hujua basi jua leo kuwa ni wewe.
Waandishi, marafiki ndugu  majirani na taifa kwa ujumla wanatamani kukusubilia wewe kwenye viwanja cha ndege vya  KIA au Julius k. Nyerere ukitoka nchi fulani ughaibuni kuiwakilisha nchi kwenye kwenye mashindano  fulani na hapo hapo una medani ya mashindano  hayo.

Ninachokijua na kukiamini ni kwamba kila jambo linawezekana kuandikwa kwa kusema wewe ni mshindi na mshindi ni yule ambae alitambua na kutumia uwezo wake ipasavyo.

Wewe ni ushuhuda unaoishi amini hivyo na jambo la msingi la kufanya ni wewe kujitafuta na kugundua uwezo wako uko kwenye eneo gani.

Kuandika, kucheza mpira, kuimba, kuigiza, kuongoza, kuongea, kucheza, kushauri, kushawishi, kuchora, kutawala eneo lolote, kufanya kazi na kufanya jambo la uwezo wako ni maeneo ambayo unaweza wekeza nakujitambulisha duniani kuwa wewe ni nani.

Wakati dunia ikimjua Bwana Samatta, Thomas ulimwengu, Diamond, Ally Kiba, Paul Clement, Joel Lwaga, Joel Nanauka, Eric Shigongo, Donie Moen, Mr Bin, Steven kanumba na jamii kutengeneza shauku ya kuwatazama basi hawa ndugu wanatengeneza fedha na utajiri wa kutisha sana.

Nini ulichonacho je unakijua je umepata njia ya kuiambia dunia kuwa wakati Mungu anaruhusu uje duniani alikupa uwezo fulani kwa ajili ya wanadamu kupata sababu ya kukupa fedha wakikutazama,  wakihangaika na mitandao kugugo ili wajue leo umefanya nini, nakinunua magazeti ili tu wajue una nini ?.....swali kubwa na muhimu sana kujiuliza.

Bado nina nafasi, bado una nafasi kaa chini jitathimini jiulize je umetumia kipaji chako kwa manufaa yako.
Nilipokuwa nikisoma historia ya Mwandishi Joel Nanauka na Eric Shigongo ndiyo mahali ambapo nilijua unaweza kuwa The living testimony kama ukijua thaman yako.

Nilikuwa nasoma tena na kusikiliza jitihada za Diamond, Mbwana Samatta, Watoto au wachezaji kutoka America ya kusini na wengine wengi ndipo nilipojua kuwa hakuna mtu ambae hana uwezo wa asili au (Natural ability) ambayo inaweza badilisha maisha yake.

Usikatishwe tamaa kuna wakati unapambana kwa bidii lakini mazingira sio rafiki,umasikini lakini mwisho wa siku Mungu hubariki sana mikono yenye bidii hasa kwenye eneo la kusudi lako.
Mbwana Samatta amelala sana kinesi, Uhuru stadium yote haya aliyafanya akiwa mbagala na alikuwa anawahi sana toka nyumbani ili program ya mazoez ya simba asikose hata point leo imebaki records kwenye vitabu ila yeye yuko ulaya.

Diamond, Harmonize na wengine wengi wamepambana sana kuwa mahali walipo leo jiulize wao waweze wana nini na wewe ushindwe una nini......Your the living Testimony jitambue.

Unaweza jiulize mimi nina nini.....ntakujibu mimi ni Ushuhuda unao ishi mwishoni mwa mwaka ujao utajua bila kusimuliwa kwa nini mimi ni The living testimony.

Hata wewe unaweza jipambanue, unaweza kuwa fulani kupitia kipaji chako, kazi unayofanya, biashara, kilimo na eneo lolote lile ulilopo ukishajitambua tu na kutambua thamani ya kile umekibeba ndani yako...
Mazingira, marafiki hukarii aina fulani fulani ya maisha, hapo ulipo unaweza nyanyuka vizuri kabisa acha visingizio pambana ongeza maarifa ujuzi na kupata wingi wa maarifa kwa kuendelea kusoma ili usiwe nje ya track.
Mgema Moses
P.o.box 166....
0755632375

Sunday, December 2, 2018

HONGERA SAMSON ERNEST KWA KUWA MFANO KWETU

Hongera katibu kwa uthubutu ambao hakika bado inatupa changamoto vijana wengine.
Chepeo ya Wokovu imeanza kama utani lakini leo ni moja ya website inayokuwa kwa kasi sana.
Kidogo kidogo leo umekuja na notebook, calendar kesho kitu kingine
Maisha yanahitaji sana, maamzi, bidii na juhudi, kujituma na kufanya kile ambacho unahisi ni sahihi kwa wakati sahihi, nidhamu, maarifa sahihi lakini ya kutosha, socialization. Juu yote haya Mungu lazima awe mbele kabisa maana ndo anahesabu kila hatua ya kila mtu.
Wakati najiunga na kundi la chepeo ya wokovu Facebook lilikuwa ni kundi dogo sana lakini leo ni kundi kubwa sana.

kila jambo lina vikwazo vyake kama vile  kukatishwa tamaa, watu kukuambia wewe huwezi, walikuwa kina fulani wakashindwa ije iwe wewe wapi..... vitu kama hivyo ni changamoto kwenye njia ya kila mtu lakini mwisho wa siku lazima uitambue focus na nia yako ni nini hapo ndipo unaweza thubutu na ukafanya kwa vitendo na vitendo vikaonekana kwenye matokeo.

Kalenda, Notebook vinaweza onekana ni vitu vidogo sana kwa Mtazamo wa watu wengi lakini kiufupi hili ni jambo kubwa sana ambalo kila mwenye akili anapaswa kulipongeza angawa kupongeza au kutokupongeza ni uamzi wa mtu Binafsi.
Vijana wezangu ni wakati wa kuamka na kutumia kila fursa inayopatikana Mbele yetu au kwenye mazingira yetu ili tuweze kuondoka kwenye maisha tuliyonayo kwa sasa.
Wakati wa kukaa tu, kulaumu, kuponda na kudharau na kujiona mwenye hadhi fulani huwezi kufanya mambo fulani umepotea na wakati ukiendelea kukaa kwenye mtazamo huo utajikuta unabaki mwandika historia za watu, kwamba huyu amekuwa tunamwona,tumesoma nae, amesoma hapahapa au amekuja akiwa hivi huku wenzako wameshasepa na maisha yao yako juu tayari.

Katibu ni somo kubwa sana kwangu, alinieleza alikoanzia mpaka alipo leo hakika ni mfano wa kuigwa sana ni mtu mpanaji asie kata tamaa, anafanya kazi sana, ana nidhamu sana kazini lakini ni mtu mwenye malengo makubwa, anaamini katika kile kidogo anapata ndicho kinaweza kumfanya akawa na kikubwa kesho.

Huwezi kuwa fulani kesho kama unakosa uthubutu, bidii, nidhamu katika kile kidogo unachopata, lakini bila malengo na nia ya dhati toka moyoni.
Kila mtu ana fursa kila mtu ana muda sawa na mwingine lakini namna ambavyo tunaweza kutumia huo muda.

Fedha watu tunapata lakini namna ya mgawanyo na matumizi ya hiyo fedha wapi unawekeza ni changamoto nyingine ambayo inatukumba vijana wengi, jitahidi kuheshimu kila kile kido unachopata ili kikufanye uwe na uwezo wa kusogea kesho huku ukijua kuwa hakuna siku utakuja kuwa na pesa nyingi kiasi kwamba utaanza kung'aa juu kwa juu ila katika vichache tunachopata ndicho chaweza kuleta kikubwa
Samson Ernest ni darasa kubwa sana kwa vijana wa Fpct Singida Mjini hakuna ubishi wala mashaka. Najua wapo wengi wamefanikiwa lakinikwangu mimi huyu ni mfano kwa vijana wengi
Tabua Thamani yako, tumia muda penda kujifunza ili kuongeza maarifa na ujuzi kwa ajili ya kuendelea kuwa bora