Tuesday, September 25, 2018

WAZAZI NA WAZAZI MNAOKUJA AMKENI SIKU ZIMEBADILIKA

PARENTS AND UPCOMING PARENTS WAKE UP DAYS HAVE CHANGED:
Nimshukuru sana Mungu kwa kuniwezesha kuwa mzima na mwenye afya tele kufikia sasa.
Nitoe pole kwa ndugu jamaa marafiki na wanamwanza na Tanzania kwa ujumla kwa msiba mkubwa ambao umelikumba Taifa letu siku ya Alhamis Tarehe 20/09/2018 kwa Meri ya Mv nyerere kuzama katika ziwa victoria.
Yote kwa Yote mola anapo ruhusu haku na wa kupinga. Zaidi ya yote Tumshukuru Mungu.

Leo napenda sana tujifunze mambo machache ambayo kwa hakika ni muhimu sana kuyajua.
Dunia tunayoishi inakwenda kwa speed sana na hakika mambo yamebadilika sana katika karne hii tuliyo nayo
ongezeko la maendeleo ya Teknolojia na utandawazi umechukua hatamu kwa wingi.
Maendeleo haya ya sayansi na Teknolojia yameweza kurahisisha sana njia za mawasiliano na utendaji kazi pia ukilinganisha na huko tulikotoka.
mambo ambayo yangeweza faywa na watu kumi leo watu watatu wanaweza kuhatekeleza kwa ufanisi wa hali ya juu sana na wakati sahihi.

Mahali ambapo ilitupasa kusafiri kupeleka mizigo au kupeleka habari fulani leo hatufanyi tena.
umekaa kwenye kiti unaratibu kila kitu hapo hapo na kila kitu kinafanikiwa kwa ufanisi ule ule ulioutaka
Express=Digital Age period ni muda ambao tunaishi.
Maendeleo haya yamekuja na matokeo Yote yaani
matokeo chanya  (positive results)
Matokeo hasi  (Negative results)
Tumeona kwa uchache matokeo chanya hapo juu japo sio yote ila tunaweza ongeza zaidi na zaidi

MATOKEO HASI  (NEGATIVE RESULTS)
Baada ya maendeleo haya kuchukua nafasi watu wengi wamekosa ajira
Idadi ya watu ambao wangehitajika kuajiliwa mahali fulani kama ni 10 sasa wanahitajika wawili au watu wakati mwingine mmoja tu.
Jiulize swali hawa wengine tisa nane na saba wako wapi?
posta ilikuwa na madereva lundo na posta ilikuwa active. Jiulize baada ya simu na matumizi ya scanning, Email simu calling sms nk. kuchukua hatamu wako wapi waliokuwa waajiliwa posta na maeneo mengine.
Baada ya hapo dunia imejikita katika ujasiriamali  (Entrepreneurship) kila mmoja barabarani na maeneo mengi watu wanafanya business.
Lakini bado sijajua kama watu wanachukua tahadhali ya kuwa kama ajira zilikuwa nyingi enzi hizo na leo ni changamoto je mambo ya ujasiriamali hayatafika mahali yabane iwe ilimradi watu wanafanya business.
Kiufupi ni kwamba biashara hazitakoma hata kama watu watakuwa wanaigana lakini bado watu wataendelea kufanya biashara.
Faida Je hilo ni swala lingine la kusubiri.

Kuna jambo muhimu sana kizazi cha leo lazima tuyajue lakini pia kuyafanyia kazi kwa haraka na kuwekeza nguvu kwa nguvu zote kuanzia rasilimal nafasi tulizo nazo ushauri nk kwa watoto wetu.
Mungu atabaki kuwa Mungu kabla ya misingi ya dunia aliyajua yote haya ndiyo maana akamwezesha kila mtu kitu cha pekee sana ndani yake.
Kipaji ni zawadi na hii zawadi ni zawadi ambayo hakuna anaweza kuigawa mzazi anaweza mpa mtoto wake kila kitu elimu fedha na mahitaji yote lakini kipaji ni Mungu pekee.
Dunia ya kwanza yaani nchi zilizoendelea Nchi za ulaya Kama England, German France nk. zinafurahia faida kubwa kutokana na vipaji vya watoto wao kuanzia kwenye soka mziki, Kikapu wasemaji wa hadhara  (Public speakers) waandishi wasimuliaji washauri wa masuala ya biashara, saikolojia, kudansi kupiga mziki, kuchora, kuchekesha na kila aina ya vipaji.
wenzetu walishituka mapema wakawekeza sana kwenye kile mtoto anakipenda lakini pia alicho na uwezo nacho.
Wanachofanya wanatoa elimu ili kumwezesha mtoto kujua Thamani ya kile kitu alicho nacho na namna ya kukitumia na kumletea manufaa.

kupitia njia hizo hakika dunia imeweza kushuhudia burudani mbalimbali kutoka kwa watu mbalimbali ambao waliweza na wanaoendelea kutumia vipaji vyao.
Mfano dunia ya soka imeshuhudia watu wengi waliozaliwa kwenye familia masikini na fukara wakibadilisha sura na maisha ya familia zao.
Iko mifano mingi ya vijana kutoka Amerika ya kusini kwenye nchi kama
Argentina, Brazil chile Uruguay peru Ambao  ni kina Alexes Sanchez, Ronaldo, Leo Messi, Ronaldinho Gaucho, Angel Di maria na wengine wengi  na baadhi ya nchi za Afrika magharibi  amabao ni Nwango kanu Didie Drogba Samwel Eto'o na Afrika mashariki kidogo Mbwana Ally  Samatta, Donald mariga na ndugu yake Victor wanyama toka nchini kenya kwa hakika wengi na baadhi yao walizaliwa kwenye kaya fukara sana lakini leo ni mamilionea na mabilionea wa kutupwa sababu kubwa ni vipaji.

Vile vile kwenye music,waigizaji iko mifano hai ya watu wanaovuna pesa kwa sababu ya music na uigizaji na uchekeshaji mifano hai:Mr Bin waimbaji Boyce Michael Jackson na wengine wengi hata hapa nyumban kidogo kina diamond Ali kiba kwa uchache angalau mifano ipo.
Wazazi wengi tunajaribu kukariri maisha sana Kitabu cha Rich dad and poor dad kinagusia sana kwa habari ya kijana ambae aliona elimu ya darasani kwake haikuwa much paid kwa sababu ni kama aliona wazazi wake wanafanyia kazi maisha ya kulipa kodi na mafao ya uzeeni ndipo mama ake alipogundua kuwa wao kama wazazi walikuwa wamekariri mfumo wa maisha ambao wazazi wao waliutumia hapo awali na hakujua kuwa dunia tayar ilikuwa nje ya kile alikuwa akikisshi.
Ndiyo wazazi wengi tulivyo hata sio kwamba tunasema watoto wasiende shule hapana lazima watoto waende shule lakini lazima tuwe namna nzuri ya kufanya vipaji vya watoto vinakuwa na manufaa kwao sana
Ajira kwa sasa hakuna lakini pia mtu anaetumia kipaji chake vema hakika hakuna mfanya kazi anaweza mgusa kiuchumi na kifedha mifano angalia diamond Ali kiba  lady Jdee Harmonize  Mbwana Samatta kwa hapa nyumban na wengine wengi
Majuu
Cristiano Ronaldo Leo Messi David Beckham Ronaldo delima LeBron James nk  ni watu matajiri wa kupindukia kwa sababu ya vipaji vyao
Lazima wazazi tushituke tuache kuishi kwa mazoea tusitumie nafasi zetu za uzazi kudidimiza na kuua vipaji vya watoto
wewe kama mzazi onya elekeza shauri na tekeleza hitaji la mtoto ili afanye jambo anapenda kwa uhakika kwa moyo na kwa upendo na kwa manufaa yake na kwako pia.
kwa leo tuishie hapo itaendelea......next time
Moses zephania Mgema
mwandishi
mgemamoses@gmail.com
0755632375/ 0678355394

Friday, September 14, 2018

Brand yourself

*CHAGUA UNATAKA KUWA BORA KWENYE NINI?*

Kila jambo lina bingwa wake, kama unakumbuka Michael Jackson alikuwa Bingwa wa Muziki wa Pop Duniani, Michael Jordan alikuwa ni bingwa wa mchezo wa kikapu.

Vivyo hivyo Pelle, Mike Tyson, Diana King na wengine kibao. Ukija Bongo kwenye Muziki wa Taarab, Malkia wa Mipasho, Khadija Kopa anakaa, Mfalme Mzee Yusuph anachukua kwa wanaume, Kina  diamond Ali kiba  na wengine wengi na ndivyo ilivyo kwa wengine na wengine.

Nimetolea mfano vitu hivyo vichache lakini kuna vitu vingi sana vinahitaji bingwa au bora wa kuviongoza au kuvifanya. Je, leo hii wakiita bingwa wa jambo fulani mtaani kwako utatoka au na penyewe hautaweza kuonesha uwezo au ubora wako?
Kuna watu wao huwa nyuma kwa kila jambo yaani ile kujifanya nyuma nyuma kwa kila kitu na hii imechangia watu wengi sana kupoteza karama vipaji vyao kwa sababu ya kuwa nyuma nyuma kwa kila jambo.
Jiulize una uwezo gani wewe kama wewe au wakati Mungu anakuumba kitu gani aliweka ndani yako na ili iweje aweke kwako na sio kwangu au kwa yule kiufupi unagundua kuwa
Mungu alikuamini
alijua wewe pekee ndo unaweza kukitendea haki kitu hicho
hivyo basi jaribu kukitumia kwa ajili yako na kikutambulishe kuwa mtu akihitajika kwa jambo fulani basi iwe ni wewe
Leo dunia ina mfahamu Tyson Diamond,Eric Shigongo, c.Ronaldo, Leo Messi.
Jay z Beyonce, Bob Marley na wengine wengi ambao walijipambanua na kutumia vipawa vyao mpaka leo hata kama wengine wamekufa lakini bado kazi zao zinaishi
Jiulize Mimi nitakumbukwa na nini  ?

Jifunze au jitengeneze kuwa bigwa wa Jambo Fulani kama Mungu alikuamini na kukuumba na akakupa uwezo fulani tumia nafasi ya uwezo huo au kipaji hicho kujitanbulisha na kutambulika kwenye jamii kwa manufaa yako au manufaa ya kazazi chako ninacho
Muda wa kuwaandalia watoto wako maisha mazuri ni leo kwa kutumia kile ulicho nacho kama ni kipaji au kazi na biashara uliyo nayo
work hard

MUANDALIE  MAZINGIRA MWANAO  ULIYENAYE AUAJAYE.

0719110760
Email mgemamoses@gmail.com
Moses zephania Mgema.
Instagram: Mo_mgema