Sunday, April 18, 2021

Nimekuwa ni mtu mwenye ndoto na maono makubwa tangu nilipokuwa mtoto mwenye rika lakujitambua, shauku yangu nikuona kuwa nafikia mambo fulani kwenye maisha yangu duniani.
Pamoja na changamoto nyingi ambazo zinaweza kuwa zinajitokeza kwenye safari yakufikia maońo, uvivu wakati mwingine, kuchukulia kawaida, kuchoka, kutokufikia malengo kusudiwa ndani ya muda fulani bado naamini kwamba, hakuna njia nyepesi inayoweza kukupeleka kwenye mafanikio na malengo yenye kutimiza maono yako/yangu.
Maono ni picha kubwa na nzito sana, haibebwi na watu legevu, inahitaji watu shupavu, makini, wenye mtazamo mpana na uwezo wa kuona pasina kutumia upeo halisi wa macho yakawaida bali upeo wa macho ya ndani ya akili na fikra.