Sunday, December 13, 2020

JANA SIO MWAMZI WA KESHO YAKO.

Usiichukie jana kwa sababu ya mapito uliyopitia, machungu,maumivu makali, kukataliwa kunyanyaswa na kuonekana hufai, umeonyesha juhudi nyingi ukitafuta kuwa wewe halisi, lakini pamoja na juhudi unazofanya lakini hazijakupa matokeo na matarajio sawa na nguvu ambazo umekuwa ukitumia muda wote....

Umefika mahali umeyachukia maisha, umesikia maneno ya walimwengu kuwa riziki ni mafungu saba, umeyabeba nakuyakiri kwenye moyo wako na akili imepokea na kujenga picha kwamba wewe uko upande wa fungu la kukosa.

Umefika mahali juhudi za jana ambazo hazikukupa matokeo uliyotarajia zimekufanya uichukie jana na kuamini kuwa haiwezekani tena, Umekaa chini umesońoneka, huzuni imejaa moyoni, huoni tumaini tena wala mwanga na mwelekeo mpya wa kesho yako, umejiinamia kwa uchungu na uchovu mwisho umelia umechoka

Ushauri wangu kwako.............
Kesho yako usikubali iamuliwe na jana, jana imepita, ifanye kuwa darasa, ujifunze kuwa pamoja na juhudi yawezekana kuna mahalï nimekosea, au nilipatia ila kuna eneo nilïkuwa sifanyi kwa usahihi, fanya Tathimini yako binafsi, jikague kwa uaminifu baada ya evaluation yako ya uhakika, majibu utakayopata usiyapindishe, yakubali halafu yafanyie kazi.

Penye udhaifu wako kubali halafu aanza kupafanyia kazi, penye uimara wako jitahidi kuongeza jitihada mara dufu, jiboreshe zaidi.......

Baada ya hapo simama chukua hatua ya imani, anza upya kwa nguvu kubwa, ikanyage jana kawa jiwe la kuvukia mto, tembea mbele, tazama kesho kwa kujenga msingi imara leo.

Bora kesho msingi wake ni leo, jana imepita, haiwezi kufutwa ila inaweza kufanyiwa masahihisho leo, nakuleta matokeo tarajiwa kesho....

Wote tunapitia changamoto lakini tunakabiliana nazo kwa kuamini kiĺa jambo hutokea maisha for a reason not otherwise.
Moses zephania Mgema

Tuesday, December 1, 2020

BE POSITIVE

Changomoto huimalisha uwezo wa akili na namna ya kuwaza na kufikiri hasa ukichukulia kila jambo kwa namna ya mtazamo chanya. Bila kujali ugumu, hali ya jambo lilivyokuja iwe umetendewa kwa makusudi au kwa bahati mbaya, au unapitia hali fulani ambayo hujawahi kuitegemea hapo kabla, bado inakupa nafasi ya kuzichulia changamoto hizo katika mlengo chanya.

Chanya huonyesha wepese, huleta kupumua, kulilax, kujipa muda na kuonyesha hatua, njia na mlango wakutatulia au kukabiliana na changamoto iliyoko mbele.

Chanya huleta courage na nguvu ya ziada ndani yako, huleta imani kuanzia ndani ya uwezekano, hujenga ujasiri na hali ya kujiamini bila kujali ukubwa au mlima ulioko mbele..

Hivyo ni vyema kuchukulia kila jambo katika mwelekeo chanya, yakutukwaza na kutuumiza ni mengi, yetu binafsi ya ndugu, rafiki, na mifumo ambayo huendesha maisha yetu,
Hivyo ni vyema kuchukua kila hatua kwa mlengo chanya ili kuweza kuishi maisha ya furaha na afya ya akili, nafsi mwili na roho.
Relax
Be positive, 
Focus