Thursday, October 22, 2020

Dr. Paul book

Aliweza kununua kiwanja maeneo ya mtaa wa kindai Mkoani Singida na kuanza kazi ya kufyatua tofauli na kuanza ujenzi kwa mikono yake mwenyewe  kwa sababu alijigunza ujuzi wa kujenga nyumba, hivyo kwa kushirikiana na Mke pamoja na watoto wake waliweza kujenga nyumba ambayo ipo katika mtaa wa kindai mkoani Singida.
Maamzi ya Dr. Paul ya kuamua kujenga nyumba yake na kuondoka kwenye nyumba ya kanisa pamoja na kwamba haikupokelewa vyema na baadhi ya wachungaji na waumini wa kanisa kutokana na utamaduni ambao ulikuwa umezoeleka tangu awali kwamba makazi ya mchungaji yalipaswa kuwa kanisani, lakini Dr. Paul alisimamia malengo na sababu za kutoka kwenye nyumba ya kanisa sababu ili kuwa ni (.............)
Miaka michache baadae watumishi wa Mungu walimwelewa kwa nini alichukua uamzi huo, na kupitia maono yake ya kuhakikisha mchungaji anajitenga na kanisa kwa maana ya sehemu ya kuishi umeleta manufaa kwa watumishi wa Mungu na kujenga heshima kuanzia kwa mchungaji na familia kwa ujumla.
Pamoja na kwamba yeye alijenga nyumba yake, lakini pia amekuwa mstari wa mbele kuwahamasisha wachungaji wote kuwa na nyumba zao ili kujenga heshima ya utumishi wao kwa kanisa lakini pia kwa familia zao, baadhi ya juhudi zake kwa wachungaji kuwa na nyumba zao ni pamoja na hamasa aliyoitoa kwa Mchungaji Boniface Ntandu kujenga nyumba yake pamoja na Mchungaji Philipo Sospeter ambae aliweza kujenga nyumba yake pia katika mtaa wa jineri na wachungaji mbalimbali wamekuwa wakifanya hivyo na kuondokana na mtazamo wakuishi kwenye nyumba za kanisa.