Thursday, August 2, 2018

Madhara ya kufikiri muda mrefu

Kiumbe binadamu ni kiumbe  aliyeumbwa  kipekee sana ukilinganisha na viumbe wengine kama mimea wadudu na wanyama wa aina zote.
Binadamu amepewa uwezo na utashi unaomfanya kuwa na uwezo wa kufanya mambo yake kwa weledi na kwa ufanisi na kujisimamia.
Amepewa utashi wa kutambua jema na baya kama vitabu vya dini vinavyotuambia.
Binadamu huyu tangu aumbwe amekuwa na maisha yenye mchanganyiko Fulani ambao unamfanya wakati mwingine atenge muda wake kwa ajiri ya kufikiri ili mambo yake yakae sawa.
Hebu tutazame mambo machache ambayo mtu anaefikiri sana yaweza kumpata ( matokeo hasi)
1. Kuchelewa kuchukua maamzi na wakati mwingine kusababisha madhara
2. Huwa ni ngumu sana kufikia malengo yao hasa kibiashara na kimahusiano kwa sababu muda wote anaofikiri
  . huona changamoto nyingi kuliko njia za kutatulia hizo changamoto hasa kwa suala zima la biashara na kazi
. wakati mwingine hupata msongo wa mawazo kwa sababu anaweza akachukua muda mwingi kufikiri jambo Fulani na akaona matokeo makubwa kabla hajaweka utekelezaji anapokuja kufanya kwa vitendo na isifikie mahali alitazamia basi kwake huwa anaumia sana
.Huzeeka kabla ya umri wao
. Hukosa fursa
. Huwa sio rahisi kukubali kama wanaweza kukosea.
Note
Hujashauriwa kuacha kufikiri ila jaribu kuwa na kiasi